Amoeba
JF-Expert Member
- Aug 20, 2009
- 3,289
- 781
Salam,
Nafahamu kuwa una majukumu chungu mzima, lakini vilevile nafahamu kuwa JF ni kijiwe chako, hivyo hauishi kuchungulia humu na kuona wadau wana mpya gani, hasa baada ya Ujumbe wa CHADEMA kukutana na kuzungumza na Mh. Kikwete kuhusu mapendekezo ya SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, 2011. Nimesoma walaka huo uliojaa mapendekezo mwanana yaliyoshiba maslahi tele kwa taifa. Ni jambo lililo wazi kabisa kuwa masikio ya Watanzania wengi yalikuwa wima kuskiliza Raisi na Jopo lake watajibu nini katika hoja hizo nzito zinazotuhusu moja kwa moja sisi kama Watanzania, mmoja mmoja, na hakika tulitegemea baada ya kikao kilichosheheni watu muhimu kabisa tunaowaamini katika taifa hili kuwa watakuja na maafikiano na majibu yaliyo fafanufu na yaliyoshiba maslahi ya taifa (ikizingatiwa kuwa kodi zetu zilitumika kugharimia kikao hicho), kinachosikitisha na kuchanganya ni kupata "taarifa" yenye ukurasa mmoja tu na vipengele viwili tu vya makubaliano, ambayo haina anwani, utambulisho, wala mhuri wowote, "tangazo" lililosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa upande mmoja, na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa upande mwingine!!! Baada ya maelezo, naomba kuuliza maswali kadhaa ya msingi, ili uweze kututoa kizani kama kuna mambo ya muhim yaliyotupita;
Natanguliza shukrani zangu, na nakutakia kila la heri katika kujenga TANGANYIKA HURU ILIYOJAA HAKI NA USAWA!
People's Power,
Amoeba Mdudu.
Nafahamu kuwa una majukumu chungu mzima, lakini vilevile nafahamu kuwa JF ni kijiwe chako, hivyo hauishi kuchungulia humu na kuona wadau wana mpya gani, hasa baada ya Ujumbe wa CHADEMA kukutana na kuzungumza na Mh. Kikwete kuhusu mapendekezo ya SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, 2011. Nimesoma walaka huo uliojaa mapendekezo mwanana yaliyoshiba maslahi tele kwa taifa. Ni jambo lililo wazi kabisa kuwa masikio ya Watanzania wengi yalikuwa wima kuskiliza Raisi na Jopo lake watajibu nini katika hoja hizo nzito zinazotuhusu moja kwa moja sisi kama Watanzania, mmoja mmoja, na hakika tulitegemea baada ya kikao kilichosheheni watu muhimu kabisa tunaowaamini katika taifa hili kuwa watakuja na maafikiano na majibu yaliyo fafanufu na yaliyoshiba maslahi ya taifa (ikizingatiwa kuwa kodi zetu zilitumika kugharimia kikao hicho), kinachosikitisha na kuchanganya ni kupata "taarifa" yenye ukurasa mmoja tu na vipengele viwili tu vya makubaliano, ambayo haina anwani, utambulisho, wala mhuri wowote, "tangazo" lililosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa upande mmoja, na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa upande mwingine!!! Baada ya maelezo, naomba kuuliza maswali kadhaa ya msingi, ili uweze kututoa kizani kama kuna mambo ya muhim yaliyotupita;
- TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI, ambayo nimeambatanisha hapa ni nyaraka halali?
- Hayo makubaliano, kama yanavyosomeka katika TAARIFA KWA VYOMBO vya habari ndiyo mazao ya mjadala uliogharimu masaa mengi na fedha nyingi za walipa kodi, mjadala uliokutanisha vichwa vyenye kuwaza kwa mapana kuhusu ustawi wa Tanzania ya leo na kesho, Ndiyo majibu ya waraka wa CHADEMA wenye kurasa 17?
- CHADEMA iko tayari kuweka hadharani nyaraka na makubaliano halali za kikao kati ya Rais na wajumbe wa CHADEMA?
- Naamini kuwa CHADEMA kukutana na kujadili suala la katiba na Rais ni moja ya masuala ya msingi kabisa mwanamapinduzi yeyote anaweza kufanya kwa niaba ya wananchi wenzake, Je Ulishiriki mazungumzo hayo? na kama haukkuhudhuria na kushiriki ni kwa nini?
Natanguliza shukrani zangu, na nakutakia kila la heri katika kujenga TANGANYIKA HURU ILIYOJAA HAKI NA USAWA!
People's Power,
Amoeba Mdudu.