Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Mgonjwa wa akili ailiyeua wenzake kortini tena
Na Pauline Richard
MGONJWA wa akili, David Denge (21), ambaye anadaiwa kuua watu wawili na kujeruhi wengine wanne ambao walikuwa wanapatiwa matibabu katika wodi ya wagonjwa wa akili Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), jana amefikishwa kwa mara nyingine katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam ambako kesi yake imetajwa kwa mara ya pili.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa katika mahakama hiyo saa 2.45 asubuhi akiwa kwenye gari la mahabusu aina ya Isuzu yenye namba STK4310 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari magereza.
Mgonjwa huyo, alipelekwa katika gereza la keko ambako anaishi ili upelelezi wa kesi hiyo ukamilike.
Mara baada ya kufikishwa katika mahakama hiyo, mshitakiwa aliteremshwa ndani ya gari hilo huku akiwa amefungwa pingu na kupelekwa moja kwa moja kwa Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Joyce Minde .
Mtuhumiwa huyo alivaa shati la rangi ya kahawia na suruali yenye michirizi meusi na alionekana kuwa mpole na kutetemeka kana kwamba alikuwa anajisikia baridi, tofauti na mara ya kwanza alipofikishwa katika mahakama hiyo.
Awali wakati anafikishwa katika mahakama hiyo, Denge alionekana kuwa msumbufu kwa askari waliokuwa wanamlinda.
Baada ya kutajwa kwa kesi yake ya mauaji inayomkabili, Mwendesha mashitaka mkuu wa Polisi Naima Msangi aliiomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa madai kuwa upelelezi haujakamilika.
Mahakama iliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 10, mwaka huu itakapotajwa tena, mtuhumiwa amerudishwa mahabusu na upelelezi wa kesi yake unaendelea.
Baada ya tarehe hiyo kutajwa, alirudishwa ndani ya gari akiwa mnyonge na kutulia kwenye kiti alichokuwa amekaa mpaka gari hilo, lilipoondoka eneo la, mahakama saa 3.15 ili kumrudisha mtuhumiwa huyo katika gereza la Keko
Mwananchi lilishuhudia mtuhumiwa huyo akiwa amekaa kiti cha mbele karibu na dereva wa gari hilo akiwa ametulia, huku akiwa anaongea sauti ya chini na kutetemeka hali ambayo haikuwa rahisi kubaini alikuwa anaongea nini.
Muda mfupi baada ya mtuhumiwa huyo kurudishwa gereza la keko, watu wengi walimiminika mahakamani hapo kwa ajili ya kumuona Denge.
Awali ilidaiwa katika mahakama hiyo kuwa Agosti 11, mwaka huu, saa 1.45 usiku mtuhumiwa huyo, alidaiwa kumuua Paulo Maganga na Abdukadir Abed ambao walikuwa wanapatiwa matibabu katika wodi ya wagonjwa wa akili Muhimbili.
Mtuhumiwa huyo kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Agosti 13 mwaka huu na alisomewa shitaka hilo la mauaji mbele ya Hakimu Samel Maweda wa mahakama hiyo.
Siku ya kwanza mtuhumiwa huyo mara baada ya Mwendesha mashitaka Mkuu Naima Msangi kumsomea shitaka hakutakiwa kujibu lolote, lakini cha kushangaza mshitakiwa huyo, alimjibu akisema,'' Ushindwe kwa jina la Yesu''.
Na Pauline Richard
MGONJWA wa akili, David Denge (21), ambaye anadaiwa kuua watu wawili na kujeruhi wengine wanne ambao walikuwa wanapatiwa matibabu katika wodi ya wagonjwa wa akili Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), jana amefikishwa kwa mara nyingine katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam ambako kesi yake imetajwa kwa mara ya pili.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa katika mahakama hiyo saa 2.45 asubuhi akiwa kwenye gari la mahabusu aina ya Isuzu yenye namba STK4310 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari magereza.
Mgonjwa huyo, alipelekwa katika gereza la keko ambako anaishi ili upelelezi wa kesi hiyo ukamilike.
Mara baada ya kufikishwa katika mahakama hiyo, mshitakiwa aliteremshwa ndani ya gari hilo huku akiwa amefungwa pingu na kupelekwa moja kwa moja kwa Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Joyce Minde .
Mtuhumiwa huyo alivaa shati la rangi ya kahawia na suruali yenye michirizi meusi na alionekana kuwa mpole na kutetemeka kana kwamba alikuwa anajisikia baridi, tofauti na mara ya kwanza alipofikishwa katika mahakama hiyo.
Awali wakati anafikishwa katika mahakama hiyo, Denge alionekana kuwa msumbufu kwa askari waliokuwa wanamlinda.
Baada ya kutajwa kwa kesi yake ya mauaji inayomkabili, Mwendesha mashitaka mkuu wa Polisi Naima Msangi aliiomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa madai kuwa upelelezi haujakamilika.
Mahakama iliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 10, mwaka huu itakapotajwa tena, mtuhumiwa amerudishwa mahabusu na upelelezi wa kesi yake unaendelea.
Baada ya tarehe hiyo kutajwa, alirudishwa ndani ya gari akiwa mnyonge na kutulia kwenye kiti alichokuwa amekaa mpaka gari hilo, lilipoondoka eneo la, mahakama saa 3.15 ili kumrudisha mtuhumiwa huyo katika gereza la Keko
Mwananchi lilishuhudia mtuhumiwa huyo akiwa amekaa kiti cha mbele karibu na dereva wa gari hilo akiwa ametulia, huku akiwa anaongea sauti ya chini na kutetemeka hali ambayo haikuwa rahisi kubaini alikuwa anaongea nini.
Muda mfupi baada ya mtuhumiwa huyo kurudishwa gereza la keko, watu wengi walimiminika mahakamani hapo kwa ajili ya kumuona Denge.
Awali ilidaiwa katika mahakama hiyo kuwa Agosti 11, mwaka huu, saa 1.45 usiku mtuhumiwa huyo, alidaiwa kumuua Paulo Maganga na Abdukadir Abed ambao walikuwa wanapatiwa matibabu katika wodi ya wagonjwa wa akili Muhimbili.
Mtuhumiwa huyo kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Agosti 13 mwaka huu na alisomewa shitaka hilo la mauaji mbele ya Hakimu Samel Maweda wa mahakama hiyo.
Siku ya kwanza mtuhumiwa huyo mara baada ya Mwendesha mashitaka Mkuu Naima Msangi kumsomea shitaka hakutakiwa kujibu lolote, lakini cha kushangaza mshitakiwa huyo, alimjibu akisema,'' Ushindwe kwa jina la Yesu''.