William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
Kaka mengine sema lakini hili ni uongo na uzandiki wa hali ya juu. Si kila kinachosemwa kwenye magazeti ni kweli na haswa kinachosemwa na "anayejiita" SAID KUBENEA. Tunathamini mchango wake na ni muhimu kuulinda lakini ukweli wa kazi yake unajulikana.
BENO MALISA sio chaguo la MAFISADI maarufu lakini hilo jungu la kumhusisha nao limepikwa muda mrefu sana. Kama angekuwa mtu wao si angechukua mamilioni waliyotaka kumpa wakati wa uchaguzi wa halmashauri kuu kama walivyofanya wenzake wengi vijana kwa wazee waliokubali kujidhalilisha kupanga foleni kwa yule nyang'au wa LOWASA. Ni Beno ndiye niliyekutana naye katika mabasi akisafiri mikoani kutafuta kura wakati wenziwe walikuwa wakipishana na mashangingi. Hivi sasa inabidi ategemee gari la baba yake kujiandaa na uchaguzi lakini mafisadi wamezusha kuwa wamempa gari ilo kama walivyowapa wengine ambao tunawafahamu.
Kaka semeni mengine lakini hili la uswahiba BENO na ROSTAM LOWASSA and Company si la kweli. Labda nipate habari zingine tofauti na nilizonazo.
Kuhusu RIDHWAN kusafiri ni uzandiki mwengine. Fuatilia ujue kama amefichwa kama usemavyo wewe ama ameenda masomoni. Sasa kaka kama utaona kwenda masomoni ni kumficha mtoto na ndio ushahidi wa kuwa Kikwete ameshtukia mwanaye anatumiwa then hapo kuna tatizo kaka...
Tafuteni mengine lakini sio hili kaka....
Tanzanianjema
Mkuu TZnjema,
Between wewe na Kubenea, ninamuamini Kubenea kwa 100%, na hizi notes za mkutano wa Morogoro, ambazo hata Kubenea hana lakini tutampa, hazikuandikwa na Kubenea,
Ninaliyoyasema ni maneno yaliyojibiwa na Kubenea, kwenye barua aliyoijibu serikali kama alivyoulizwa kueleza ni kwa nini anasema mtoto wa rais anatumwia, na Kubenea sio wa wa kwanza kuandika habari hii, imetolewa toka last weeek na nipashe, sasa mbona hukuwajibu wao kuwa ni waongo?
Kama una tatizo lako lingine na Kubenea, uliweke hapa lakini usichanganye mambo mkuu, wewe unajua kua hivi majuzi at one point Lowassa na Ridhiwani walikuwa pamoja US walikuwa wanafanya nini? Kwa maneno yako ninakuelewa wazi kuwa una something to do na huyo Beno au Lowassa, lakini sisi tumeamua kulikomboa taifa letu hatuogopi mtu wala maneno makali ambayo ni hewa tupu!
Punguza jazba bro! Kubali ukweli kuwa haya either huyajui au unataka kudanganya umma hapa JF kuwa-cover mafisadi, hii habari unayoililia iliandikwa Nipashe last week, Kubenea ame-etxend tu!