Mgomo wa walimu na maamuzi ya Serikali, Mahakama

Wanafunzi wa shule kadhaa za msingi huko Mbagala wameandamana leo kwenda kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya kupinga walimu wao kutokuonekana darasani kufuatia mgomo wa walimu ambao ulikuwa umeanza jana.

Hata hivyo mahakama ya kazi jana usiku ilitoa amri ya walimu kusitisha mgomo huo kwani kuna kesi ya msingi. Rais wa CWT ametoa wito kwa walimu kurejea madarasani hadi kesi hii itakapoamriwa.

Wakati huo huo mikoa mbalimbali imeanza kupokea fedha za malipo ya malimbikizi ya madai ya walimu.

Huko Moshi, Chuo Shiriki Ushirika leo kimewasimamisha masomo wanafunzi wa mwaka wa pili na watu ambao waligoma leo kuunga mkono wenzao wa mwaka wa kwanza waliosimamishwa masomo jana!
 
Haya bana, huyu mtu ambaye alikuwa anashangiliwa na kila mtu, hadi watoto wadogo, leo serikali yake inagomewa na kila mtu hadi watoto wa shule!!
 
Mi nakwambia Titanic linazama, halafu kuna watu wanakwambia "it is unsinkable".

Yaani ni kudra tu na docility yetu ndiyo inatufanya tuendelee kuwa na "amani" mpaka leo, vinginevyo watu wangeshafanya ma guillotine kitambo tu.

Wewe unasema na choo cha passport size, chumba mbavu za mbwa umande unapita usiku wakati mtu ana dud kama la ma star wa Beverly Hills na Malibu huko?

Halafu bado watu wanajichekesha chekesha kwenye hotuba tu, kila siku kutupiana mipiara, mara tume ya kuchunguza tume ya tume, mara Saidi Mwema kampasia Hosea aliyempasia DPP, ili mradi sarakasi kupita Vegas!

Hawa wanafunzi wa shule za msingi ndio waliomtoa Jean Bedel Bokassa mfalme wa Ubangi, hata kitabu kizuri kimeandika what has been hidden from the wise and the prudent is revealed to the babe and the suckling"

Labda pressure kutoka kwa madogo itasaidia.
 
Mi nakwambia Titanic linazama, halafu kuna watu wanakwambia "it is unsinkable".

Yaani ni kudra tu na docility yetu ndiyo inatufanya tuendelee kuwa na "amani" mpaka leo, vinginevyo watu wangeshafanya ma guillotine kitambo tu.

Wewe unasema na choo cha passport size, chumba mbavu za mbwa umande unapita usiku wakati mtu ana dud kama la ma star wa Beverly Hills na Malibu huko?

Halafu bado watu wanajichekesha chekesha kwenye hotuba tu, kila siku kutupiana mipiara, mara tume ya kuchunguza tume ya tume, mara Saidi Mwema kampasia Hosea aliyempasia DPP, ili mradi sarakasi kupita Vegas!

Hawa wanafunzi wa shule za msingi ndio waliomtoa Jean Bedel Bokassa mfalme wa Ubangi, hata kitabu kizuri kimeandika what has been hidden from the wise and the prudent is revealed to the babe and the suckling"

Labda pressure kutoka kwa madogo itasaidia.

I'm sure most of the kids protested just for fun but some people in high places should be ashamed by this.
Pundit unaona hicho kitabu kizuri kilivyo-cover kila sehemu ya maisha ya binadamu? Na bado unasema hakuna Mungu?You know quite a bit for a non believer, r u a retired Christian?
 
Hivi hawa madenti wa shule ya msingi wanaelewa wanachokifanya kweli?[/QUOTE]

Hawaelewi ndo maana walijikuta wakifika Ofisi za Mkuu wa Wilaya badala ya kwenda feri kushangaa kama walivyokuwa wameambizana awali.
"A Grain Of Wheat" na Ngugi wa Thiong'o.
 
Labda nao wanatumiwa na wapinzani. Si umesikia ni storm in a teacup?

hahaha Js umenichekesha haswaaa, mimi naanza kufikiria hii migomo inawezekana kabisa wapinzani hawausiki na ninachoanza kukihisi ni wenyewe kwa wenyewe wanasumbuana, unakumbuka ile thread ya Mzee mwana Kijiji ya JENDA 21?? mwenye macho na apate kuona na asiyena macho basi tutamuadisia
 
Mhadhiri asema migomo nchini Tanzania ishara ya wananchi kuzinduka
Na Geofrey Nyang'oro (Mwananchi)

MHADHIRI Msaidizi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Duce), Haruna Makandi amesema migomo inayoendelea nchini inadhihirisha kuwa amani iliyodumu tangu uhuru ilitokana na watu kunyimwa haki ya kuzungumza.

Makandi alisema hayo alipokuwa akizungumza na Mwananchi nje ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke, mkoani Dar es Salaam alipokwenda kushuhudia maandamano ya wanafunzi wa shule tatu za msingi waliofika ofisini hapo kuishinikiza serikali iwalipe walimu madai yao.

Wanafunzi hao walisema kutokana na serikali kushindwa kuwalipa madai yao, walimu hao wamegoma kuingia darasani na kuwafanya kukosa haki ya kupata elimu waliyoifuata.


Alisema licha ya kutambua athari zitokanazo na migomo pamoja na njia mbadala za watu kutaka kuwasilisha madai yao baada ya njia za kawaida kushindikana, migomo iliyopo inaonyesha kukua kwa demokrasia.

"Watu wamechoka kuonewa wamekaa kimya kwa muda mrefu, lakini sasa wameamua kutumia njia mbadala kuwasilisha madai yao. Hali hii kitaalamu tunaiita (popular democracy) yaani demokrasia ya wengi ambayo huibuka ghafla na hudumu kwa muda mfupi, lakini huacha mabadiliko makubwa katika jamii," alisema Makandi.

Makandi alitolea mfano nchi ya Uphilipino ambayo alisema wananchi walipochoshwa na utawala uliokuwapo madarakani waliandamana na hawakujali mauaji yaliyofanywa na polisi waliokuwa Ikulu hadi walipokamilisha madai yao.

Aliitahadharisha serikali kama haitakuwa makini katika kushughulikia hali hii watu, wataendelea na maadnamano hayo mpaka bungeni na baadaye Ikulu hivyo kuondoa kabisa hali ya utulivu na amani iliyopo.

"Migomo inaonyesha wazi kuwa watu wamechoka kukaa kimya huku wakinyimwa haki zao, watu wamekuwa wakikosa nafasi ya kutoa malalamiko yao na pia wamekuwa wakikosa fursa za kusikilizwa, hali hiyo ya watu kutafuta njia mbadala ya kusikilizwa hudumu kwa muda mfupi, lakini huleta mabadiliko makubwa kwenye nyanja za utawala," alisema.

Alisema jibu pekee la kuituliza migomo hii inayoendelea hapa nchini ni kwa serikali kuwapa watu haki zao kadiri ya makubaliano waliyoafikiana.

Alitoa mfano wa mgomo wa walimu ulioanza juzi kwa nchi nzima wenye lengo la kuishinika serikali kuwalipa malimbikizo ya madai yao kwamba, kama serikali hatafanya hivyo mgomo huo hautatulia mpaka walimu walipwe haki zao.

Alisema kwa sasa vitisho siyo wakati wake kwa sababu dhana hiyo ya mabavu ni sehemu ya kuwashinikiza watu kukubaliana na matakwa ya serikali hata inapokwenda kinyume na haki zao.

Makandi alisisitiza kuwa, walimu hao wanaoendelea na mgomo hivi sasa inaonyesha wazi kuwa watu wamechoshwa na uonevu pamoja na vitisho na kwamba, kinachotakiwa kufanywa na serikali ni kuwalipa madai hayo haraka.
 
Imetolewa mara ya mwisho: 19.11.2008 0123 EAT

• Viongozi CWT wakamatwa

*Wadaiwa kumtusi Rais Kikwete
*Mukoba:Uhakiki umejaa ufisadi
*Atangaza rasmi kusitisha mgomo
*Ikulu 'yawasamehe' waliogoma

Na Waandishi Wetu
Majira

SIKU moja baada ya walimu mbalimbali nchini kugoma kufundisha na hatimaye jana wengi kuanza kurejea madarasani baada ya Serikali kuanza kuwalipa mafao yao, mgogoro mkubwa huenda ukaibuka tena baada ya kuwepo taarifa za kamatakamata ya viongozi wa vyama vya walimu iliyoanza katika mikoa mbalimbali.

Viongozi wengi wa Chama cha Walimu (CWT) katika mikoa kadhaa nchini wameripotiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi nchini kwa madai ya kufanya makosa mbalimbali ikiwemo uchochezi na kuhamasisha wenzao kugoma.

Kutoka Dodoma, Waandishi Wetu Rehema Lippu na Pendo Mtibuche wanaripoti kuwa viongozi kadhaa wa CWT mkoani humo walikamatwa kwa kudaiwa kufanya kosa la uchochezi na kuikashifu Serikali.

Akizungumza na majira ofisini kwake, Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Bw.Omary Mganga alithibitisha kutokea tukio hilo akiongeza kuwa viongozi hao walikamatwa majira ya saa 5.00 asubuhi.

Aliwataja viongozi hao kuwa ni Katibu wa CWT Mkoa wa Dodoma, Bw. Frateli Kwaison, Katibu CWT Manispaa, Bi. Romana Aloyce (50) pamoja na Mwenyekiti CWT Bw. Lucas Luhombo (53).

"Hawa viongozi walipita katika shule za hapa mjini wakiwashawishi walimu waliokua katika kazi kugoma ili kuunga mkono migomo inayoendelea na ndipo tulipopata taarifa na kufuuatilia na tulipogundua ni kweli tuliwakamata na kuwatia nguvuni," alisema Kamanda huyo.

Aidha amesema watu hao walifika katika shule ya msingi Amani na kukuta wanafunzi wakiwa katika mitihani ya mwisho wa mwaka na kuwarubuni walimu wa shule hiyo kugoma kitendo kilichopelekea walimu hao kufuata mkumbo na kuwafanya wanafunzi kuishia kufanya mtihani mmoja tu.

Bw. Mganga amezitaja shule ambazo walipita kwa ajili ya kushinikiza mgomo huo kuwa ni Chang’ombe,Chamwino, Chinangali, K-Ndege Mlezi, Uhuru pamoja na Kaloleni.

Pia amesema katika uchunguzi uliofanywa, watuhumiwa hao walikutwa na meseji za kashfa katika simu zao. Amesema kashfa hizo zinaihusu Serikali pamoja na Rais wa Tanzania na wapo rumande, upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Dodoma (CWT), Mwenyekiti wa Chama cha walimu Manispaa ya Dodona na Katibu wa Chama cha walimu Manispaa ya Dodoma kwa kosa la kuwashawishi walimu wa shule mbalimbali za msingi waendelee na mgomo.

Shule ambazo polisi walifika jana na kukuta walimu wakiwa wamegoma ni pamoja na shule ya Chang’ombe, Mlezi, Amani, Kaloleni, Kizota, Chamwino, Mkakole, Chinangali pamoja na shule ya Chamwino.

Naye Zuhura Semkucha, anaripoti kutoka Shinyanga kuwa uongozi wa Serikali mkoani humo umeagiza kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa baadhi ya viongozi wa CWT waliobainika kupita mashuleni na kuwatoa madarasani walimu waliokataa kuunga mkono mgomo huo.

Agizo la kukamatwa kwa viongozi CWT lilitolewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Kanali, Mstaafu Edmund Mjengwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana.

Kanali Mjengwa alisema baadhi ya viongozi wa CWT ngazi ya Mkoa na wilaya walionekana juzi wakitembelea baadhi ya shule za msingi ambako walikuwa wakiwatoa madarasani walimu wote waliowakuta wakiendelea na kazi baada ya kugoma kushiriki katika mgomo ulioitishwa na chama hicho.

Alisema mbali ya kuwatoa madarasani walimu waliogoma kushiriki mgomo pia viongozi hao waligonga kengele zilizopo shuleni na kuwaruhusu watoto wote kurejea nyumbani kitu ambacho alisema ni kinyume cha sheria.

“Tayari nimewaagiza wakurugenzi wote wa Halmashauri za Wilaya kuwachukulia hatua mara moja viongozi wote wa CWT waliotenda kitendo cha kuwatoa madarasani walimu waliokataa kuunga mkono mgomo wao, hili ni kosa la jinai, sisi tuliwaheshimu, hakuna mwalimu aliyefuatwa nyumbani kulazimishwa akafundishe, vipi wao wasiwe wastaarabu?” alihoji Kanali Mjengwa.

Wakati huo huo Serikali Mkoani Shinyanga kuanzia jana imeanza kulipa madai ya walimu wote ambao madai yao yaliishafanyiwa uhakiki.

Kanali Mjengwa alisema Mkoa wa Shinyanga ulipokea jumla ya shilingi 1,085,225,837.21 kutoka Serikali Kuu ikiwa ni malipo ya malimbikizo ya mishahara, malipo ya likizo, uhamisho, matibabu na masomo.

Hata hivyo alisema malipo yote ya malimbikizo ya mishahara yatawekwa katika mishahara ya mwezi huu ambapo malipo mengine ya likizo, uhamisho, matibabu na masomo yameanza kulipwa kupitia ofisi za wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya kuanzia jana.

Mkoani Iringa, Mwandishi Wetu Francis Godwin anaripoti kuwa walimu mkoani humo jana walianza kulipwa madai yao halali yanayofikia sh. milioni 70,476,608,00 ambayo yamekubaliwa na serikali kati ya madai ya sh. bilioni 1.5 yaliyotolewa CWT mkoa wa Iringa huku walimu wengi wakimpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kutekeleza ahadi yake.

Kwa upande wa walimu wa Manispaa ya Iringa baada ya kutangaziwa na kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Dkt. Nicholaus Mgumba kuwa malipo yao yapo tayari walionekana wenye nyuso za tabasamu huku wakiimba CCM hoyee!

Mwandishi wa habari hizi ambaye jana alitembelea shule mbali mbali za Manispaa ya Iringa na kukuta wanafunzi wakiwa pekee yao huku idadi kubwa ya walimu katika shule hizo wakiwa wamekwenda ofisi za Manispaa ya Iringa kulipwa madai yao.

Baadhi ya wanafunzi walimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa walimu wao walifika shuleni hapo majira ya saa 1;00 asubuhi ila wakiwa katika hali ya kuchangamka tofauti na ilivyo kuwa juzi wakati walipokuwa katika mgomo.

Katika hatuya nyingine, Rais wa CWT, Bw. Gratian Mukoba ametangaza rasmi kusitisha mgomo wa walimu uliokuwa umeanza nchini kote juzi kufuatia amri ya mahakama iliyotolewa juzi usiku, anaripoti Joyce Magoti kutoka jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana na waandishi wa habari akiwa pamoja na viongozi wa kitaifa wa vyama nane vya wafanyakazi akiwemo Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Bw. Nestory Ngulla, kwa lengo la kuonesha mshikamano, Bw. Mukoba aliinyooshea kidole Serikali na akisisitiza kuwa wametii amri ya mahakama lakini Serikali ifahamu mahakama si njia ya kuwariwadha walimu wenye kero nyingi, bali kutekeleza ahadi zake kwao.

"Tunawaomba wanachama wetu na walimu wote kwa ujumla waendelee kufundisha lakini Serikali itambue kuwa kukimbilia kuzuia mgomo mahakamani hakuwezi kusaidia Taifa na wala hakutafifisha juhudi za walimu kudai haki zao.

"Wakati tukitoa tamko hili tunajua walimu hawajalipwa madai yao ya likizo, matibabu, masomo na uhamisho na wengine hawajapanda madaraja," alisema Bw. Mukoba.

Bw. Mukoba alitumia nafasi hiyo kuiomba mahakama kusikiliza kesi ya msingi iliyofunguliwa na Serikali kupinga mgomo huo kama ilivyofanya juzi wakati wa kusikiliza ombi la kuusitisha ili haki iweze kutendeka.

Kuhusu uhakiki wa madai ya walimu, Bw. Mukoba alidai kwa sasa uhakiki umegeuka aina nyingine ya ufisadi kwa kile alichodai unafanyika taratibu ili wahakiki waweze kuendelea kulipwa posho.

"Kwa kipindi cha siku 90 za uhakiki umegeuzwa ufisadi, kwa sababu wanaohakiki wanajifungia ndani na kujilipa posho kubwa pengine hawapendi kazi hiyo imalizike," alidai Bw. Mukoba.

Akizungumzia viongozi wa CWT waliokamatwa mikoani, Bw. Mukoba aliitaka Serikali iwaachie mara moja.

"Tunaitaka Serikali iwaachie huru mara moja kwani mgomo huo ulikuwa ni halali kwa nini wamewakamata hao na mimi Rais wao Serikali haijanikamata ," alihoji Bw. Mkoba.

Akitoa msimamo wa TUCTA, Bw. Ngulla alisema vyama vya wafanyakazi vinatambua kuwa madai ya walimu ni halali kwa sababu yamekuwepo kwa muda mrefu ndio maana wameamua kugoma.

"TUCTA inaunga mkono walimu kogoma kwani Serikali ilipewa muda wa kutosha kutekeleza madai yao lakini haikufanya hivyo," alifafanua Bw. Ngulla.

Katika hatua nyingine Serikali 'imewasamehe' walimu wote waliogoma kufundisha kufuatia mgomo uliofanyika juzi kwa kusisitiza kuwa inaamini watarejea kazini kuungana na wenzao kuendelea na kazi hasa baada ya jana kuanza kulipwa mafao yao.

Kauli hiyo ililitolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Bw. Philemon Luhanjo iliwapongeza pia walimu walioachana na mgomo na kujitolea kufundisha hata wakati ambapo bado walikuwa na madai mbalimbali.

"Huu ni uamuzi wa busara na wa uzalendo unaojali maslahi mapana ya Taifa letu Serikali inaamini kuwa wale walimu wachache tu waliojitokeza kushiriki katika mgomo huo uliokuwa batili wataungana na wenzi wao walio wengi kuendelea na kazi yao adhimu katika jamii," alisema Bw. Luhanjo akiashiria kuwa iwapo walimu hao wataendelea kufundisha Serikali itaendelea kuwaheshimu.

Alisema kuwa Serikali inapenda kuwahakikishia walimu wito nchini kuwa inathamini na kutanbua kazi yao nyeti na muhimu kwa uhai wa Taifa.

Bw. Luhanjo aliongeza kwa Serikali itafanya kila iwezalo kutatua matatizo yanayowakabili walimu kwani wamekuwa wakifanya hivyo huko nyuma na wataendelea kufanya hivyo.

Mgomo wa juzi ni mara ya pili kwa CWT kuuitisha ili kushinikiza kulipwa madai yao, lakini wamekuwa wakikumbana na kisiki kutokana na Serikali kukimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kuomba izuie mgomo huo, ombi ambalo limekuwa likikubaliwa.

Kwa mara ya kwanza walimu hao walikuwa waanze kugoma Oktoba 15, mwaka huu baada ya kumalizika kwa notisi ya siku 60 waliyotoa kwa Serikali iwe imewalipa madai yao lakini ulizuiwa na mahakama katika uamuzi wake uliotolewa Oktoba 13 mwaka huu.

Hatua hiyo ilisababisha Bw. Mukoba kupigwa na walimu hadi kuokolewa na Polisi kwa kufyatua risasi za moto hewani baada ya kutoa tangazo la kuahirisha mgomo kwenye mkutano wa walimu na viongozi wa CWT uliofanyika Diamond Jubilee Oktoba 14, mwaka huu.

Hata hivyo Mahakama ya Rufaa Tanzania ilitengua uamuzi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kwa kuwa kifungu kilichotumika hakikuwa sahihi, uamuzi uliotoa fursa kwa CWT kuendelea na mipango ya mgomo wao ambao ulianza juzi lakini ukazuiwa tena na mahakama katika uamuzi wake wa juzi usiku.
 
Habari zaidi!
Walimu waanza kulipwa
Mlacha na Waandishi Wetu Mikoani
Daily News; Tuesday,November 18, 2008 @21:15

Wizara ya Fedha na Uchumi imepeleka zaidi ya Sh bilioni 10 kwa halmashauri 132 nchini ili kulipa malimbikizo hayo ya madeni. Katika taarifa yake Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, alisema serikali inaamini kuwa ni walimu wachache tu ndio waliojitokeza kushiriki katika mgomo huo batili na aliahidi kuwa serikali itafanya kila iwezalo kutatua matatizo yanayowakabili walimu.

“Serikali inapenda kuwahakikishia walimu wote nchini kuwa inathamini na kutambua kazi yao nyeti na muhimu kwa uhai wa taifa letu,” alisema Luhanjo. Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili mkoani Dar es Salaam, ulibaini kuwa walimu wengi walitii amri ya mahakama kwa kuhudhuria madarasani na kufundisha kama kawaida na ni baadhi ya walimu tu ambao walisaini na kuondoka bila kufundisha.

Mkoani Mbeya, halmashauri nane za mkoa huo hatimaye jana zilianza kutekeleza agizo la serikali kwa kuanza kulipa madai ya walimu. Akizungumza jana, Ofisa Elimu Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda, alisema halmashauri za wilaya tayari zimepokea fedha zilizotumwa kwa ajili ya malipo ya madai ya walimu, na mkoa huo umepokea Sh.636,507,723 kwa ajili ya kuwalipa walimu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashasuri ya Wilaya ya Chunya, Maurice Sapanjo alithibitisha wilaya hiyo kupokea Sh milioni 39,997,523 fedha zitakazotumika kuwalipa walimu 148. Ofisa Elimu wa Jiji la Mbeya, Aulelia Lwenza alisema Halmashauri ya Jiji la Mbeya imepokea Sh milioni 56.3 ambazo zitatumika kuwalipa walimu 442, wakati Wilaya ya Kyela imepokea Sh milioni 162.9 kwa ajili ya kuwalipa walimu 262.

Wakati Serikali ikiwa imeanza kulipa madeni hayo ya walimu, zaidi ya walimu 300 wa Mkoa wa Mbeya huenda wakajikuta mikononi mwa sheria baada ya kudaiwa kughushi nyaraka zilizokuwa zinathibitisha madai ya zaidi ya Sh milioni 400.
Habari kutoka Tabora zinasema kwamba Halmashauri ya Manispaa ya Tabora jana ilianza kuwalipa walimu madai yao ambayo wamekuwa wakiidai Serikali kwa muda mrefu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Hassan Mwanziku amesema kwamba tayari kazi ya kusaini hundi za malipo hayo imeshakamilika. Mwanziku ameeleza kuwa malipo hayo yanatokana na serikali kutuma pesa katika manispaa hiyo jumla ya Sh milioni 106 kwa ajili ya malipo ya walimu hao.

Amesema kwamba jumla ya walimu 519 katika Manispaa ya Tabora walitarajia kulipwa pesa zao jana na kutoa wito kwa walimu kuacha mgomo. Baadhi ya walimu hao wameishukuru serikali kwa kuwalipa mapunjo yao ya muda mrefu ambayo wengi walikuwa wameyasahau.

Akiwataka walimu kurejea kazini kutokana na amri ya mahakama Rais wa Chama hicho, Gratian Mukoba, aliwataka walimu kurejea katika vituo vyao vya kazi na kuendelea na kazi wakati CWT inatafuta suluhu zaidi ya mgogoro wao na serikali.

Alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kufuatia zuio la mgomo huo, lililotolewa juzi usiku na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi Ernest Mwipopo. “Tunatoa tamko hili huku tukifahamu kabisa kwamba bado walimu hawajalipwa madai yao ya likizo, matibabu masomo na uhamisho na wengi bado hawajapata madaraja stahiki, lakini tunaomba waendelee kufundisha kwa kuwa tunaheshimu sheria,” alisema Mukoba.

Alisema kwa mujibu wa Mahakama Kuu Divisheni ya kazi, ilitangaza zuio la walimu kuendelea na mgomo, ili kesi ya msingi iliyofunguliwa na serikali inayohusu uhalali wa hatua zilizofuatwa na CWT kutangaza mgomo isikilizwe, jambo ambalo inabidi watii hadi hatua hiyo ikamilike kwani hawawezi kukata tena rufaa.

Alisema pamoja na uamuzi huo wa kusitisha mgomo, wanaamini kuwa mahakama hiyo haitatumia muda mrefu kusikiliza shauri la msingi bali itatumia kasi kama ilivyofanya pindi serikali ilipowasilisha ombi la kuzuia mgomo huo. Aidha alisema kitendo cha serikali kukimbilia mahakamani si suluhisho la kudumu katika kutatua mgogoro huo bali ingeshughulikia kikamilifu matatizo yote yaliyoorodheshwa katika notisi ya mgomo ya siku 60.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Nestory Ngulla, alisema shirikisho hilo linaunga mkono mgomo wa CWT, kwa kuwa madai yao ni ya muda mrefu na serikali ilikuwa na muda wa kutosha kuyatekeleza.

Pia alikishutumu Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kulihusisha suala la mgomo wa walimu na siasa na kutoa tamko lao katika kipindi cha mgomo wakati tatizo hilo la madai ya walimu lilikuwapo muda mrefu na chama hicho kilikuwa kimya. “Matamko yaliyojitokeza hivi karibuni kutoka CCM yanajaribu kutishia uhuru wa wafanyakazi katika kudai haki zao kwa mujibu wa sheria, jambo hili hatulikubali na tunalipinga kwa nguvu zote na kukemea,” alisema Ngulla.

Aliiomba serikali kutambua kuwa suluhu ya mgogoro huo wa walimu ni kutekeleza madai yao ya muda mrefu na kuchukua hatua za kisheria na kiutawala kwa wale wote waliosababisha kucheleweshwa kwa malipo na si kutumia dola au siasa. Wakati huohuo, Polisi mkoani Dodoma, inawashikilia baadhi ya viongozi wa CWT Mkoa wa Dodoma kwa kosa la kushinikiza mgomo na kashfa dhidi ya viongozi wa serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dodoma, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Omary Mganga, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja viongozi hao kuwa ni Fratern Kwahson (46) ambaye ni Katibu wa CWT Mkoa wa Dodoma, Romana Aloyce (50) Katibu wa Manispaa ya Dodoma na Lucas Luhombo, Mwenyekiti wa Manispaa ya Dodoma.

Mganga alisema watu hao walipita katika shule tisa za Manispaa ya Dodoma kwa lengo la kushinikiza mgomo kwa walimu na kwamba watu hao watafikishwa mahakamani muda wowote upelelezi utakapokamilika. Alitaja shule walizopita kuwa ni Shule ya Msingi Amani ambako walikuta wanafunzi wakiwa katika mtihani wa kumaliza mwaka na kuwashawishi walimu wagome, kitendo kilichopelekea wanafunzi hao kufanya mtihani mmoja tu.

Shule nyingine walizopita ni Chang’ombe, Chamwino, Chinangali, Kiwanja cha Ndege, Mlezi Uhuru na Kaloleni. Maganga aliongeza kuwa katika uchunguzi wao waligundua katika simu za watuhumiwa hao kulikuwa na ujumbe wa simu unaomkashifu Rais na vyombo vya serikali. Wakati akitoa tamko, Rais wa CWT Mukoba, aliiomba serikali iwaachie walimu hao kwa kuwa walikuwa wakitekeleza mgomo ulio halali kabla ya amri ya mahakama kutolewa.
 
Hatimaye Waalimu wamegundua ukweli kwamba nguvu yao iko katika umoja wao. Siku nyingi wamekua wakiiomba serikali iwaonee huruma iwalipe mafao yao. Ni sasa ndio wamegundua ukweli kwamba serikali, hasa hii ya CCM, haina huruma.

Waalimu wana nguvu kubwa kutokana na wingi wao na umuhimu wa kazi yao. Wanapotaka haki yao haina budi waidai, na sio waiombe.

Sasa kuna uvunjwaji wa sheria katika kukamata viongozi wao. Kosa la "kuikashifu serikali ni lipi?" Kuna kitu kinaitwa freedom of speech. Wote tuna haki ya kusema lolote tupendalo kuhusu serikali.

Viongozi wa mikoa walioagiza viongozi wa waalimu wakamatwe ni mafisadi ya kuwekwa kwenye kumbukumbu zetu. Tutawaadabisha siku tukijikwamua kutokana na police state ambayo tumekuwa nayo siku nyingi.

Kuna kosa la wrongful arrest kwa polisi kuwakamata viongozi wa waalimu wanaopita wakizungumza na wenzao mashuleni. Nawaomba mawakili wapiganiaji haki za binadamu (eg. Tindu Lissu) wajitokeze kuwatetea waalimu walioonewa. Idaiwe fidia for wrongful arrest.

Naona serikali hii sasa imeamua kuanza kutawala kwa nguvu za maonezi. SMS mnazodai kukuta kwenye simu za waalimu zina signature? Si polisi wenu wameziweka huko wenyewe?
 
Habari zaidi!
Walimu waanza kulipwa
Mlacha na Waandishi Wetu Mikoani
Daily News; Tuesday,November 18, 2008 @21:15

Wizara ya Fedha na Uchumi imepeleka zaidi ya Sh bilioni 10 kwa halmashauri 132 nchini ili kulipa malimbikizo hayo ya madeni. Katika taarifa yake Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, alisema serikali inaamini kuwa ni walimu wachache tu ndio waliojitokeza kushiriki katika mgomo huo batili na aliahidi kuwa serikali itafanya kila iwezalo kutatua matatizo yanayowakabili walimu.

“Serikali inapenda kuwahakikishia walimu wote nchini kuwa inathamini na kutambua kazi yao nyeti na muhimu kwa uhai wa taifa letu,” alisema Luhanjo. Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili mkoani Dar es Salaam, ulibaini kuwa walimu wengi walitii amri ya mahakama kwa kuhudhuria madarasani na kufundisha kama kawaida na ni baadhi ya walimu tu ambao walisaini na kuondoka bila kufundisha.

Mkoani Mbeya, halmashauri nane za mkoa huo hatimaye jana zilianza kutekeleza agizo la serikali kwa kuanza kulipa madai ya walimu. Akizungumza jana, Ofisa Elimu Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda, alisema halmashauri za wilaya tayari zimepokea fedha zilizotumwa kwa ajili ya malipo ya madai ya walimu, na mkoa huo umepokea Sh.636,507,723 kwa ajili ya kuwalipa walimu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashasuri ya Wilaya ya Chunya, Maurice Sapanjo alithibitisha wilaya hiyo kupokea Sh milioni 39,997,523 fedha zitakazotumika kuwalipa walimu 148. Ofisa Elimu wa Jiji la Mbeya, Aulelia Lwenza alisema Halmashauri ya Jiji la Mbeya imepokea Sh milioni 56.3 ambazo zitatumika kuwalipa walimu 442, wakati Wilaya ya Kyela imepokea Sh milioni 162.9 kwa ajili ya kuwalipa walimu 262.

Wakati Serikali ikiwa imeanza kulipa madeni hayo ya walimu, zaidi ya walimu 300 wa Mkoa wa Mbeya huenda wakajikuta mikononi mwa sheria baada ya kudaiwa kughushi nyaraka zilizokuwa zinathibitisha madai ya zaidi ya Sh milioni 400.
Habari kutoka Tabora zinasema kwamba Halmashauri ya Manispaa ya Tabora jana ilianza kuwalipa walimu madai yao ambayo wamekuwa wakiidai Serikali kwa muda mrefu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Hassan Mwanziku amesema kwamba tayari kazi ya kusaini hundi za malipo hayo imeshakamilika. Mwanziku ameeleza kuwa malipo hayo yanatokana na serikali kutuma pesa katika manispaa hiyo jumla ya Sh milioni 106 kwa ajili ya malipo ya walimu hao.

Amesema kwamba jumla ya walimu 519 katika Manispaa ya Tabora walitarajia kulipwa pesa zao jana na kutoa wito kwa walimu kuacha mgomo. Baadhi ya walimu hao wameishukuru serikali kwa kuwalipa mapunjo yao ya muda mrefu ambayo wengi walikuwa wameyasahau.

Akiwataka walimu kurejea kazini kutokana na amri ya mahakama Rais wa Chama hicho, Gratian Mukoba, aliwataka walimu kurejea katika vituo vyao vya kazi na kuendelea na kazi wakati CWT inatafuta suluhu zaidi ya mgogoro wao na serikali.

Alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kufuatia zuio la mgomo huo, lililotolewa juzi usiku na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi Ernest Mwipopo. “Tunatoa tamko hili huku tukifahamu kabisa kwamba bado walimu hawajalipwa madai yao ya likizo, matibabu masomo na uhamisho na wengi bado hawajapata madaraja stahiki, lakini tunaomba waendelee kufundisha kwa kuwa tunaheshimu sheria,” alisema Mukoba.

Alisema kwa mujibu wa Mahakama Kuu Divisheni ya kazi, ilitangaza zuio la walimu kuendelea na mgomo, ili kesi ya msingi iliyofunguliwa na serikali inayohusu uhalali wa hatua zilizofuatwa na CWT kutangaza mgomo isikilizwe, jambo ambalo inabidi watii hadi hatua hiyo ikamilike kwani hawawezi kukata tena rufaa.

Alisema pamoja na uamuzi huo wa kusitisha mgomo, wanaamini kuwa mahakama hiyo haitatumia muda mrefu kusikiliza shauri la msingi bali itatumia kasi kama ilivyofanya pindi serikali ilipowasilisha ombi la kuzuia mgomo huo. Aidha alisema kitendo cha serikali kukimbilia mahakamani si suluhisho la kudumu katika kutatua mgogoro huo bali ingeshughulikia kikamilifu matatizo yote yaliyoorodheshwa katika notisi ya mgomo ya siku 60.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Nestory Ngulla, alisema shirikisho hilo linaunga mkono mgomo wa CWT, kwa kuwa madai yao ni ya muda mrefu na serikali ilikuwa na muda wa kutosha kuyatekeleza.

Pia alikishutumu Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kulihusisha suala la mgomo wa walimu na siasa na kutoa tamko lao katika kipindi cha mgomo wakati tatizo hilo la madai ya walimu lilikuwapo muda mrefu na chama hicho kilikuwa kimya. “Matamko yaliyojitokeza hivi karibuni kutoka CCM yanajaribu kutishia uhuru wa wafanyakazi katika kudai haki zao kwa mujibu wa sheria, jambo hili hatulikubali na tunalipinga kwa nguvu zote na kukemea,” alisema Ngulla.

Aliiomba serikali kutambua kuwa suluhu ya mgogoro huo wa walimu ni kutekeleza madai yao ya muda mrefu na kuchukua hatua za kisheria na kiutawala kwa wale wote waliosababisha kucheleweshwa kwa malipo na si kutumia dola au siasa. Wakati huohuo, Polisi mkoani Dodoma, inawashikilia baadhi ya viongozi wa CWT Mkoa wa Dodoma kwa kosa la kushinikiza mgomo na kashfa dhidi ya viongozi wa serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dodoma, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Omary Mganga, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja viongozi hao kuwa ni Fratern Kwahson (46) ambaye ni Katibu wa CWT Mkoa wa Dodoma, Romana Aloyce (50) Katibu wa Manispaa ya Dodoma na Lucas Luhombo, Mwenyekiti wa Manispaa ya Dodoma.

Mganga alisema watu hao walipita katika shule tisa za Manispaa ya Dodoma kwa lengo la kushinikiza mgomo kwa walimu na kwamba watu hao watafikishwa mahakamani muda wowote upelelezi utakapokamilika. Alitaja shule walizopita kuwa ni Shule ya Msingi Amani ambako walikuta wanafunzi wakiwa katika mtihani wa kumaliza mwaka na kuwashawishi walimu wagome, kitendo kilichopelekea wanafunzi hao kufanya mtihani mmoja tu.

Shule nyingine walizopita ni Chang’ombe, Chamwino, Chinangali, Kiwanja cha Ndege, Mlezi Uhuru na Kaloleni. Maganga aliongeza kuwa katika uchunguzi wao waligundua katika simu za watuhumiwa hao kulikuwa na ujumbe wa simu unaomkashifu Rais na vyombo vya serikali. Wakati akitoa tamko, Rais wa CWT Mukoba, aliiomba serikali iwaachie walimu hao kwa kuwa walikuwa wakitekeleza mgomo ulio halali kabla ya amri ya mahakama kutolewa.

ahahahahahahah kumbe hili liserikali bila migomo haliendi eheee, sasa itabidi FFU waandae pilipili nyingi sasa ni kugoma kwa kwenda mbele maji hamna mgomo, foleni barabarani mgomo, mpaka mtachoka,
 
Hatimaye Waalimu wamegundua ukweli kwamba nguvu yao iko katika umoja wao. Siku nyingi wamekua wakiiomba serikali iwaonee huruma iwalipe mafao yao. Ni sasa ndio wamegundua ukweli kwamba serikali, hasa hii ya CCM, haina huruma.

Waalimu wana nguvu kubwa kutokana na wingi wao na umuhimu wa kazi yao. Wanapotaka haki yao haina budi waidai, na sio waiombe.

Sasa kuna uvunjwaji wa sheria katika kukamata viongozi wao. Kosa la "kuikashifu serikali ni lipi?" Kuna kitu kinaitwa freedom of speech. Wote tuna haki ya kusema lolote tupendalo kuhusu serikali.

Viongozi wa mikoa walioagiza viongozi wa waalimu wakamatwe ni mafisadi ya kuwekwa kwenye kumbukumbu zetu. Tutawaadabisha siku tukijikwamua kutokana na police state ambayo tumekuwa nayo siku nyingi.

Kuna kosa la wrongful arrest kwa polisi kuwakamata viongozi wa waalimu wanaopita wakizungumza na wenzao mashuleni. Nawaomba mawakili wapiganiaji haki za binadamu (eg. Tindu Lissu) wajitokeze kuwatetea waalimu walioonewa. Idaiwe fidia for wrongful arrest.

Naona serikali hii sasa imeamua kuanza kutawala kwa nguvu za maonezi. SMS mnazodai kukuta kwenye simu za waalimu zina signature? Si polisi wenu wameziweka huko wenyewe?


kumbe serikali inajua umuhimu wa walimu kiasi hicho maana walivyokimbilia mahakamani haraka na kupekua vilongalonga inaonyesha jinsi ambavyo walimu ni tishio sasa inabidi muwaachie hao wenzao la sivyo watapata sababu nyingine za kugoma na hivi mnaelewa kuwa vihela vyenyewe mmewawekea kibonyo na mimazingaumbwe kibao shauri zenu mtaipata...
 
CCM oyee ,hao walimu ndio mnawaona wameshau kuwa uchaguzi bado mwaka tu ,hivyo kulipwa ni kurubuni kura zao,sasa kama walikuwa na umoja ambao umesababisha kulipwa ,waandae kuwatetea wenzao waliokuwemo au waliokamatwa kwani kama si wao kuwashawishi wasingelipata kitu na mambo yangepita kimya kimya.
Umoja ni nguvu walimu na wanafunzi kama wameanza kulipwa bado wakatae na kudai wenzao waliokamatwa warudishwe kazini na kuachiliwa na vyombo vya dola.Zaidi ya hapo watakosa viongozi kakamavu kwa siku zijazo.
 
Back
Top Bottom