Mgomo wa wafanyakazi wasitishwa kwa muda

Subira huvuta heri. lakini ngoja ngoja uumiza matumbooooooooooooo!!!!!!!!!Chelewa chelewa utakuta mwana si wako................. sasa tufanyeje?????????
 
mipango mipya..............tunaanza ku-scratch tena!! mpaka 2015 tena!!!

mkubwa wangu nimeishiwa manaeno ngoja nikajipe raha, maisha yenyewe magumu, mafupi agrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!!!!!!!!!!!!!!

Siwalaumu TUCTA, inawezekana wamefanya strategic withdrawal. Inaruhusiwa katika uwanja wa mapambano. Ila kama wamesitisha kwa sabab ya kuogopa plasta basi ni hatari.

Mimi nimefurahi sana kwani ni hatari kwenda vitani wakati makamanda hawajui kwa nini wanapigana na mbinu gani za kushinda vita. Ndo maana wahadhiri na ujanja wao wote wa kunyaka vijana wamepigwa tobo! Kunji siyo mchezo, linataka wanaume wa shoka; na siyo kila kikojozi anaweza kuongoza kunji!

Nenda kapate Juice ndugu yangu. Nirushie bill nitalipa tu!
 
Bajeti yangu kwa mshahara wa 130000
1-Asubuhi natembea kwa mguu hadi ninapofanyia kazi na jioni pia kwa mguu
2-nimepanga chumba kwa 10000 kwa mwezi mie na mke wangu na watoto 3 chumba kimoja tumetenganisha na panzia
3-watoto wanasoma shule ya jirani hawaitaji school bus wala kupanda daladala ninawapa 100 kila mmoja kwa ajili ya kununua kipande cha muhogo cha shilingi hamsini na maji ya shilingi hamsini wakirudi chakula ni saa kumi jioni hadi siku ya pili=9000 + 10000 =19000
4-kwa siku namuachia mama watoto 3000 kwa ajili ya chakula=3000 x 30 = 90000 + 1900 = 109000
ukitoa 130000 - 109000 = 21000
5-Nacheza mchezo wa kupeana kila mwezi 5000 hiyo kama SACCOS yetu hapo mtaani
Nabakia kama 16000
 
Jamaa anajua na alikwisha sema Watanzania asilimia 70? ni bendera fuate upepo. Pia Watanzania wengi ni waoga sana, maneno mengi, vitendo hamna. Wewe kama ni mwajiliwa angaliia hapo ofisini kwenu, kwenye lunch watu wanaongea sana lakini kwenye staff meeting kimyaaaaaa!
 
Mgaya amefanya maamuzi ya busara sana, kuliko angeingia kwenye marumbano na mwenye nchi.... Ila yana mwisho haya wazungu wanasema the end justfy the means
 
Ndo hivyo mdogo wangu. Ila nasikia Mgaya anashangaa kwa nini Rais ameamua kung'ang'ania mkutano wa tarehe 8 May wakati hoja mbili zilikuwa tayari zimepata maamuzi (i.e kima cha chini na pensheni.. walikuabaliana kutokubaliana) na kilichokuwa kimebaki ni suala la kodi kwenye mishahara. Mgaya amesema kuwa watu waende kazini na mipango mipya itatolewa baada ya mkutano huo.

Wallah uhai ni mtamu sana. Yaani jinsi JK alivyotishia kumshusha mtu ngiri sioni ajabu kwa TUCTA kuchomoa!
Mgaya umetusaliti?
Mgomo ulipaswa kuendelea sambamba na mazungumzo; makubaliano yakiwepo mgomo unasitishwa yasipokuwepo mgomo unaendelea. Sasa kama katika masuala ya msingi kama kima cha chini na pensheni mlishakubaliana kutokubaliana na jana umemsikia JK akisema hata mkigoma miaka 8 hamuwezi kupata hizo 315,000/=, sasa unategemea hiyo tarehe 8 may mzungumze nini?
Ulipaswa kutorudi nyuma; na kwa kweli umedissapoint wafanyakazi wengi, umeonyesha woga kuliko hata JK aliouonyesha jana. Nina wasiwasi kuwa ukiitisha mgomo mwingine hutapata wafuasi!.
 
Solidarity forever
Solidarity foreeever
Solidarity foreeever
Tanzania zaidi ya uijuavyooooooooo

Ah kumbe naota tu!! Nyama ya mbavu!!:brick:
 
Je itakuwaje kama hata hao FFU wa JK nao watajiunga kwenye mgomo wakidai maisha mazuri kama ya wenzao kule Mwenge??????
 
Mgaya umetusaliti?
Mgomo ulipaswa kuendelea sambamba na mazungumzo; makubaliano yakiwepo mgomo unasitishwa yasipokuwepo mgomo unaendelea. Sasa kama katika masuala ya msingi kama kima cha chini na pensheni mlishakubaliana kutokubaliana na jana umemsikia JK akisema hata mkigoma miaka 8 hamuwezi kupata hizo 315,000/=, sasa unategemea hiyo tarehe 8 may mzungumze nini?
Ulipaswa kutorudi nyuma; na kwa kweli umedissapoint wafanyakazi wengi, umeonyesha woga kuliko hata JK aliouonyesha jana. Nina wasiwasi kuwa ukiitisha mgomo mwingine hutapata wafuasi!.


Hapana Mkuu. TUCTA wametumia busara na akili sana. JK na serikali walitumia nguvu nyingi kwa hiyo hapa ingekuwa hatari. Kwa hiyo naamini TUCTA wamefanya jambo la busara.

Hata hii hatua ya kufanya JK aongee kama jana siyo ndogo. Hapo tayari tuko hatua moja mbele.
 
Mgaya amefanya maamuzi ya busara sana, kuliko angeingia kwenye marumbano na mwenye nchi.... Ila yana mwisho haya wazungu wanasema the end justfy the means

Wenye nchi ni watanzania.kwanza JK naye alivokua anajigamba jana kwamba yeye ndiye muajiri wao mkuu..alisahau kuwa yeye ndiye aliyeajiriwa na wananchi.Huu ni udikteta wa aina yake,jamaa aliyeingia in power na 80% anaongea kama vile,kweli Demokrasia ni haramu Afrika.

Tena Rais aliwatukana wale wazee wa jana ila kwa kuwa nao ni fuata upepo walikuwa tu wanacheka cheka ovyo..wazee wale wanatuharibia taifa na future huku wakijua kuwa hawatakuwemo na hawajui watendalo anyways
 
Je itakuwaje kama hata hao FFU wa JK nao watajiunga kwenye mgomo wakidai maisha mazuri kama ya wenzao kule Mwenge??????

FFU (na JWTZ) hawawezi kuingia kwenye mgomo kirahisi wakati maboss wao wanashinda Ikulu wakila kuku. Ni vigumu kuyashawishi majitu yaliyoko jeshini kwani siku yakikubali kazi inakuwa imeisha. Siyo kitu rahisi.
 
yaani rais alisimama akamwaga radhi ,watu wamekua wapole namna hiyo?

Kweli tanzania watu ni wabinafsi,kwa hali hii hata ccm wataendelea kujikita madarakani.huku ni kujidhalilisha,poor us.wanamapinduzi tuko wapi?hivi kweli hakuna watu wenye uzoefu na migomo ktk kulazimisha maslahi yao yatiliwe maanani?yaani vitisho alivyotoa jk vinafanana na vitisho alivyokuwa anatutolea headmaster wa shule moja,lakini tuligangamana mpaka tukapata haki yetu na kukomesha udikteta wa kishenzi kwenye ile shule. Ati ffu watawapiga mkigoma?kivipi yaani?

Yaani jinsi rais alivyoongea jana bila busara,anaweza kubadilisha misimao ya watu wenye busara?
definition of fear is forget everything and run away, this is for tanzania mainland, and
definition of fear is face everything and recover, this is zanzibar. Check out where do your next generation going ?
 
Mimi sioni shida mgomo kusitishwa kidikteta..maana nasikia alikuwapo Mkuu wa majeshi, IGP (wanaoa nyumba moja), etc. Kinachofuata ni kuwahi asubuhi ofisini, lamba wino kwenye register ya maudhurio, vuta kiti, soma email, pata kikombe cha chai, soma email, pata lunchi, angalia saa, kama ni saa tisa...wahi mama watoto mpange namna ya kupata pesa ya mlo wa siku na watoto kwenda shule. Mgomo huu hanipati FFU, JWTZ au Immediate supervisor! Believe me!!
 
Eti ubalozi wa RWANDA uko wapi hapa nchini? nasikia kuna nafasi za KAZI.
 
Siwalaumu TUCTA, inawezekana wamefanya strategic withdrawal. Inaruhusiwa katika uwanja wa mapambano. Ila kama wamesitisha kwa sabab ya kuogopa plasta basi ni hatari.

Mimi nimefurahi sana kwani ni hatari kwenda vitani wakati makamanda hawajui kwa nini wanapigana na mbinu gani za kushinda vita. Ndo maana wahadhiri na ujanja wao wote wa kunyaka vijana wamepigwa tobo! Kunji siyo mchezo, linataka wanaume wa shoka; na siyo kila kikojozi anaweza kuongoza kunji!

Nenda kapate Juice ndugu yangu. Nirushie bill nitalipa tu!

Maneno ya busara sana Mkuu. TUCTA hapa imefanya kama Wanyarwanda ambao huwa hawaendi vitani kama hawana uhakika watashindwa. Hii ya Ku-RETREAT ni aina moja muhimu sana vitani. Zamani ilikuwa ukirudi nyuma basi unapigwa RISASI. Wengine wangelitaka sana kifanyike hiki. Ila hiyo ni ya zamani. Inabidi warudi na wajipange upya kwa kufahamu kuwa KIKWETE yuko tayari kutumia vyombo vya dola ili TUCTA kwenda mezani na mabandeji kichwani kama siyo kwenye majeneza. Dawa sasa ni kumsubiri na wakati wa kampeni ndiyo kumuanzishia varangati la nguvu na hapo tuone atakavyouwa watu.
 
Duh sikutegemea kwa kweli...........yaani HAKUNA MGOMO!!!!

Mhhh,

kwani wewe huogopi virungu? Na siyo virungu tu, jamaa karuhusu hao hawani (FFU) kuua kwa kutumia mfano wa Nyerere na Wazee wa Kilombero. Naanza kupata hisia kuwa TUCTA sasa kuna wapambanaji. Shida sasa itakuja baada ya kuwaingiza kwenye dili za EPA part 2. Jamaa wakishatupa chawa na kunguni, basi huo ndo utakuwa mwisho wa TUCTA. JK atapeta hadi 2015 bila kelele yoyote!
 
Back
Top Bottom