Mgomo wa TUCTA wapingwa na TIC na TCCIA

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Mgomo ulioitishwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), umeingia dosari baada ya kubainika kutokuwa na tija kwa uchumi wa nchi na ustawi wa jamii.

Ikiwa mgomo huo unaotarajiwa kuanza rasmi Mei 5, mwaka huu utafanikiwa, ni dhahiri kwamba utafanyika wakati ambapo mkutano wa kuhusu hali ya uchumi duniani (WEF) utakaoanza Mei 5 hadi 7, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo utajumuisha wafanyabiashara wakubwa, wawekezaji na taasisi za kiuchumi kutoka nchi mbalimbali duniani.

Hivyo, usumbufu utakaotokana na mgomo huo si kwamba utawaathiri raia na watu wengine wanaoishi nchini tu, bali pia washiriki wa mkutano huo kutoka maeneo mbalimbali duniani, wakiwemo wawekezaji.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Emmanuel Ole Naiko, amesema mgomo wa wafanyakazi haupaswi kufanyika kwa vile athari zake zitakuwa kubwa kwa uchumi wa nchi na Watanzania wenyewe.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Ole Naiko, alisema kufanyika kwa mkutano huo hapa nchini ni fursa muhimu itakayothibitisha kuwepo kwa mazingira bora ya uwekezaji nchini.

Ole Naiko alisema migomo ni miongoni mwa adui wakubwa katika uwekezaji, hivyo ikiwa utafanyika wakati wa WEF, kuna hatari ya kujenga hofu na woga kwa wafanyabiashara wa nje wenye nia ya kuwekeza nchini.

Mkurugenzi huyo wa TIC alisema, mabadiliko ya uchumi wa dunia yameifanya sekta binafsi kuwa mwajiri mkuu wa wananchi walio wengi, hivyo ufanisi katika kuepuka mgomo unaoratibiwa na Tucta ni jambo lenye maana kubwa.

"Kama mgomo huu utafanyika wakati wawekezaji wakiwa hapa nchini, hii ni sawa na kujenga mazingira ya kuwakimbiza (wawekezaji), hivyo kuongeza tatizo la ajira nchini," alisema.

Alisema kwa hali hiyo Taifa linapaswa kupiga hatua katika kuhamasisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi na kusema mkutano wa WEF ni moja ya fursa itakayochochea ufanisi huo.

"Kuna umuhimu wa kusaidiana, tusaidiane kama Taifa ili suala hili la mgomo lijadiliwe kwa ustaarabu," alisema.

Kwa upande wake, mmoja wa waratibu wa mgomo wa wafanyakazi, Gratian Mukoba, alipendekeza kwa serikali kuwezesha mchakato utakaofanikisha kupata suluhu ya madai ya msingi yanayosababisha hali hiyo.

Kutoka mkoani Kilimanjaro, Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA), Patrick Boisafi, alisema mgomo huo unajionyesha katika taswira ya kukidhi matakwa ya kisiasa zaidi ya maslahi ya nchi.

Alisema kwa nchi changa ikiwemo Tanzania, mgomo kama unaoitishwa na Tucta, una athari nyingi za kiuchumi na kijamii, hivyo njia pekee ni kudhibiti ili usitokee.

Boisafi alitoa mfano kuwa madai ya kupandisha kima cha chini cha mshahara kama inavyotajwa na Tucta, yanapaswa kuwiana na hali ya uchumi iliyopo badala ya `kukurupuka' kiasi cha kutokuwa na tija kwa pande zote.

Kwa hali hiyo, Boisafi alieleza kushangazwa na tamko la Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, kutangaza ongezeko la mishahara kwa sekta binafsi kufikia asilimia 100.

Habari hii imeandikwa na Mashaka Mgeta, Dar es Salaam na Salome Kitomari, Kilimanjaro

From Nipashe
 
Huyu Ole Naiko na the so called Boisafi wanamuwakilisha nani???????? Wamewahi kuvaa viatu vya watumishi wa umma i.e kulipwa 85,000 kwa mwezi as of now? In fact hii ni gd test kwa serikali kama inathamini wawekezaji na wananchi wake basi they need to find a compromise............... TUCTA songeni mbele msitishwe na watu kama Ole Naiko na Boisafi.

Huyu Boisafi alikuwa wapi TUCTA walipotoa elaboration ya ni kwa vp kima cha chioni wanachopendekeza kinawezekana?
 
Hawajui machungu ya sisi wa KCC (Kima Cha Chini) tunavyoumia lazima tugome tuuuu hata kama kuna mkutano wa malaika tutagoma tuuu mpaka haki zetu tupewe
 
Sijawahi kuona nonsense kubwa kama wanavyoonyesha viongozi wa taasisi hizi mbili -- TIC na TCCIA. Ni nonsesense kubwa kuliko hata ile ya Mrema kuhusu mgomo. hawa wametumwa na serikali ya CCM.

'Kutokuwa na tija kwa uchumi wa nchi na ustawi wa jamii' ni siasa tu kwani jamii ni hiyo hiyo inayokosa usitwai kwa kupewa punje badala ya mishahara. mambo ya migomo hayahusiani na mikutano ya kimataifa inayotarajiwa kufanyika nchini katika kipindi cha mgomo kwani wafanyakazi ndiyo wanaopanga timing yao ili kupata maximum attention kutoka serikalini kuhusu madai yao halali.

Kama serikali inajiona imeshikwa pabaya na timing ya mgomo, basi hiyo ni nishai kubwa kwa wapinga uonevu. Kwani serikali nayo hutumia kila hila pamoja na timing kuhujumu wananchi.
 
BNdugu yangu Ole Naiko ulitegemea mgomo ukifanyika unakuwa na manufaa kwa uchumi wa nchi? Ikiwa mgomo hautakuwa na athari especially kwa mwajiri basi hakuna maana yoyote ya kuuitisha.

You guys sounds like you are never serious.
 
Nafikiri huyu Ole Naika hana akili nzuri kama anadai mgomo unafanyika siku si nzuri kuna mkutano wakimataifa kuhusu hali ya uchumi duniani WEF sasa yeye alitaka mgomo ufanyike lini kabla au baada ya huo mkutano hii ni nonsense kweli, anathamini wawekezaji kuliko wafanyakazi wenye nchi. Timing ya mgomo ni pamoja na mambo kama hayo tunashuhudia maandamano ya nchi mbalimbali yakifanyika siku za mikutano ya kimataifa mfano G8 na G20 au siku Obama akiwa ziarani Uturki ndiyo waturuki wanaandamana na kuchoma bendera mbele yake ili aone ndiyo timing za migomo na maandamano zinavyotakiwa, hapa TUCTA wameishika serikali penyewe keep on keeping on.

Mwisho haya magazeti ya IPPMEDIA Nipashe, The Guardian nk wameanza kuupinga huu mgomo kwa muda mrefu sijui wanawasiwasi gani au na wao wanawalipa wafanyakazi wao mishahara kiduchu? ukifuatilia uandishi wao karibu wote ni kupinga mgomo, wanapohoji mtu mmoja wanaripoti kana kwamba taasisi nzima au watu wote wamepinga, leo wamehoji watu wawili tu lakini heading inakuwa kubwa kuliko maelezo menyewe kwani huyo Ole Naiko ndiyo leo kaanza kuyasikia matatizo ya wafanyakazi, hawa jamaa nafikiri hata leo wakinihoji mimi kesho wataandika gazetini Mgomo wapingwa this is ridiculous.
 
Yeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeees huu ndio wakati mzuri sana kwa wafanyakazi wa Tanzania kufikisha ujumbe.Tunataka hao wageni wajue kuwa nchi hii ina amani lakini wananchi wake hawana amani kama wanavyozania.TUCKA hii kitu isonge mbele tumechoka kunyanyaswa.Ole ni multimillionea hana uchungu na na shida za walala hoi anataka aendelee kutengeneza ulaji wake tu.Hureeeeeeee wafanyakazi tupiganie haki zetu.
 
Kumlipa Mtu sh 85,000 kwa mwezi, araverage ya Tshs 2,883 kwa siku hii ni dhambi, Serikali inategemea huyu jamaa aishi vipi, asomeshe watoto kwa hela ipi, afanye saving kwa hela ipi na bado huyu huyu jamaa unategemea awe na ufanisi kazini kwake?

Unapomwajiri mtu si kumsadia bali anakufanyika kazi na lazima umlipe vizuri - hili napenda liwe fundisho kwa serikali kuthamini wafanyakazi wake. hayo mambo ya propaganda za uchumi utaathirika ni ya kisiasa - hoja ya msingi ya kujibiwa ni kwamba mtu ataishije na mshahara wa sh 85,000 kwa mwezi, hata posho ya mbunge kwa siku haifiki.
 
Kumlipa Mtu sh 85,000 kwa mwezi, araverage ya Tshs 2,883 kwa siku hii ni dhambi, Serikali inategemea huyu jamaa aishi vipi, asomeshe watoto kwa hela ipi, afanye saving kwa hela ipi na bado huyu huyu jamaa unategemea awe na ufanisi kazini kwake?

Unapomwajiri mtu si kumsadia bali anakufanyika kazi na lazima umlipe vizuri - hili napenda liwe fundisho kwa serikali kuthamini wafanyakazi wake. hayo mambo ya propaganda za uchumi utaathirika ni ya kisiasa - hoja ya msingi ya kujibiwa ni kwamba mtu ataishije na mshahara wa sh 85,000 kwa mwezi, hata posho ya mbunge kwa siku haifiki.

naungana na wewe Elnino ..inatupasa kuungana na huu mgomo uwepo! nina uchungu sana moyoni juu ya hili
 
Hivi Ole Naiko anazungumzia athari za ustawi wa jamii ipi wakati asilimia 80 ya Watanzania wanaishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku na wengi hata hawajui watakula kesho watakula nini na familia zao? Hawa wenzetu wanachojali ni 'uchumi wao' na wala si uchumi wa Mtanzania wa kawaida akina KCC ambao hata siku moja hawajauona uchumi ukikua ndani ya nyumba zao tangu waajiriwe mpaka wanastaafu! Ama kweli Ubepari ni Unyama!! Ndio yale yale ya Malkia aliyedai kama wananchi hawana mkate kwa nini wasile keki?
 
Ole Naiko aliniacha hoi pale alipotetea 3% tunayopata kwenye madini akisema it is better than nothing, kwamba before that tulikuwa hatupati chochote. Huyu nilishamweka kwenye kundi la Makuhadi wa Ubepari.
 
Tangu mwanzo nimekuwa nikiunga mkono mgomo huu na bado msimamo wangu ni ule ule kwa madai yote ya TUCTa ni ya msingi kwetu sisi wafanyakazi.
Leo ninatoa mfano wa dhati katika aspect ya PAYE, nina pay slip mbili mkoni mwangu zote za mwaka huu
Mwezi X gross ilikuwa Tshs. 3.3M na vichengi kidogo na makato ya PAYE yakawa Laki 8 na changi hivi
Mwezi Y gross ilikuwa Tshs 3.9M na vichangi kidogo na makato ya PAYE yakawa Laki 9 na changi hivi
Ebu fanya projection ya mwaka mzima mimi nalipa kiasi gani cha PAYE?
Wakati huo mchango wangu wa Social Security Fund mwezi X ni Laki 3.3 na mwezi Y ni Laki3.9
Je hili nalo halituhumizi sisi Wafanyakazi? Afadhali hata hiyo fomula ya NSSF?PPF ndiyo ingekuwa hiyo inayotumika kukata PAYE ili tujiwekee akiba ya kutosha ya uzeeni
 
Tangu mwanzo nimekuwa nikiunga mkono mgomo huu na bado msimamo wangu ni ule ule kwa madai yote ya TUCTa ni ya msingi kwetu sisi wafanyakazi.
Leo ninatoa mfano wa dhati katika aspect ya PAYE, nina pay slip mbili mkoni mwangu zote za mwaka huu
Mwezi X gross ilikuwa Tshs. 3.3M na vichengi kidogo na makato ya PAYE yakawa Laki 8 na changi hivi
Mwezi Y gross ilikuwa Tshs 3.9M na vichangi kidogo na makato ya PAYE yakawa Laki 9 na changi hivi
Ebu fanya projection ya mwaka mzima mimi nalipa kiasi gani cha PAYE?
Wakati huo mchango wangu wa Social Security Fund mwezi X ni Laki 3.3 na mwezi Y ni Laki3.9
Je hili nalo halituhumizi sisi Wafanyakazi? Afadhali hata hiyo fomula ya NSSF?PPF ndiyo ingekuwa hiyo inayotumika kukata PAYE ili tujiwekee akiba ya kutosha ya uzeeni

It is just bul.................shyt!!!!!!!!!, Lakini cha kushangaza unaweza kukuta Mfanya biashara mwenye operating capital ya Tshs 100 Million halipi ushuru japo 80% ya hiyo kodi unayolipa. PAYE is the only area serikali yetu iko effective kukusanya kodi kwa sababu ya urahisi. What a shame, kuna siku nilisoma ripoti moja nilitaka kulia yaani walipa kodi TZ is only 15%.
 
Kichekesho cha tamko la Ole Naiko ni kwamba anawalaumu TUCTA kwa kufuata matakwa ambayo yeye mwenyewe anayafuata. Kauli yake imekaa kisiasa. Ole Naiko na TIC hawana lolote zaidi ya kutoa certificate of incentives tu kwa hao wanaowaita wawekezaji zenye kuwaruhsu kukwepa kulipa kodi ambayo ingesaidia hawa mabwana wanaotaka kugoma kupata ahueni kidogo ya mshahara.

Maneno kama haya ya madhara kwa uchumi yanaangalia upande mmoja tu, je wanafikiri ufanisi wa wafanyakazi hawa unakuwa vipi wakati maslahi yao hayaeleweki huku gharama za maisha zikipanda na wao kupewa ahadi hewa kila leo?

Naelewa msukumo ambayo hawa mabwana wawili wanaipata kutoka serikalini ya kuisaidia kuepusha mgomo huu ila ni vyema wakakaa kimya maana pilipili wasiyoila yawawashia nini?

Kugoma kufanya kazi ni haki ya msingi ya mwanadamu yeyote yule kama ilivyokuwa haki yake kwenda kuomba kazi
 
Mi Nauunga mkono huu mgomo. Ila kwa uzoefu inaonyesha migomo huwa inayeyuka siku za mwishoni kabisa. Hofu yangu na huu usiwe kama hiyo iliyoyeyuka katika hatua za mwisho mwisho
 
Back
Top Bottom