Mgomo wa Madaktari: Serikali Yasalimu Amri! Yaomba Mazungumzo Upya!

Serikali haikusita kuongea na Madaktari, madaktari ndio waliosita kuongea na Serikali. Hata Pinda alisema waziwazi milango ya maongezi iko wazi. Kwanini mnapenda kusema uongo?

Serikali ya Kikwete ni sikivu kuliko Serikali yoyote ile. Ni nani asiyelijuwa hilo? Tumeona kina Mbowe na Slaa hata walipo susa Rais akawaambia mtakuja tu, na walipokwenda akawapokea na kuwapa Juisi kwa mkono wake. Jee, nani asiyeyajuwa hayo?
kauli ya kuwatisia iltoka wapi ili hali serikali ni sikivuuuuuuuu

Hapo mwisho lengo lako ni kubadli ladha ya UZI
 
Serikali haikusita kuongea na Madaktari, madaktari ndio waliosita kuongea na Serikali. Hata Pinda alisema waziwazi milango ya maongezi iko wazi. Kwanini mnapenda kusema uongo?

Serikali ya Kikwete ni sikivu kuliko Serikali yoyote ile. Ni nani asiyelijuwa hilo? Tumeona kina Mbowe na Slaa hata walipo susa Rais akawaambia mtakuja tu, na walipokwenda akawapokea na kuwapa Juisi kwa mkono wake. Jee, nani asiyeyajuwa hayo?

I pity you!!!!

Na viongozi tuliowapa dhamana ya kutuongoza wakifanya mchezo, tutawafuata huko huko walipo!!!! Waka muulize Gadhafi kilichomtokea!!!.


I pity pity u uuuuuu!!!!!!!!

Why do you love your Vasco Da Gama who has brought us nothing but humiliation! burden of problems! unaccountability!!!
What is going on between you and Vasco Da Gama "JK"
 
Serikali haikusita kuongea na Madaktari, madaktari ndio waliosita kuongea na Serikali. Hata Pinda alisema waziwazi milango ya maongezi iko wazi. Kwanini mnapenda kusema uongo?

Serikali ya Kikwete ni sikivu kuliko Serikali yoyote ile. Ni nani asiyelijuwa hilo? Tumeona kina Mbowe na Slaa hata walipo susa Rais akawaambia mtakuja tu, na walipokwenda akawapokea na kuwapa Juisi kwa mkono wake. Jee, nani asiyeyajuwa hayo?

Serikali imejaa wababaishaji wengi, na hilo ndilo linalomkwamisha mh. Raisi, ni kweli mh. Raisi ni sikivu lakini je anatekeleza anachoambiwa au ndio kinaishia mezani? Laiti kama wangekuwa wasikivu leo hii madaktari wangekuwa kazini hata kama matakwa yao yangekuwa hayajatekelezwa, tatizo ndani ya watendaji wa serikali kuna viongozi wanaotaka kuleta ubabe usio na maana, matokeo yake ni haya ya kuhatarisha maisha ya watanzania wasio na hatia.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Hatimaye serikali imesalimu amri, yatafuta mazungumzo upya na madaktari.

Source ni Waziri wa Afya akizungumza na BBC Swahili jioni hii.

More to follow!

kanjanja bana.....zile saa zako zimeishia wapi?
 
Usijifanye kuwa hujui yaliyojiri, Pinda alikwenda Karimjee, ambao hawakwenda kwa maongezzi ni hawa madaktari uchwara, na Pinda aliamuru warudi kazini lakini alisema wako tayari kukaa na kuwasikiliza wakati wowote. Msizuwe.
kweli nimeamini ulimpenda mume hata akiunguruma tu na kukohoa unatabasamu ....
 
Ati hali ya utoaji huduma afya Muhimbili inarudi kuwa ya kawaida: jamani madaktari 15 wa jeshi kweli wameweza kukavaa pengo la madaktari waliogoma? Propaganda hii mbaya sana. Serikali wanaona ni sawa kulinda image yao kwa public ilhali wagonjwa bado wanateseka.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, ni kipi ambacho Kikwete hakifanyi? huyu Rais akiondoka tutamkumbuka kama tunavyomkubuka Mwinyi aliyetutoa kwenye lindi la umaskini.
utamkumbuka wewe..usitake kunitapisha sasa hivi....
 
Huo sio ukweli, hawa madaktari uchwara wanaochochea hii migomo wanajulikana agenda zao za siri na kina nani wanaowachochea, Serikali inafanya kila njia isiwape mwanya, lakini mwenye lake hakosi kulitafuta.

Ukweli ni nani asioujuwa?
ff funguka!mchochezi ni nani?blandina,njelekela,pinda,vyombo vya habari,chadema au ulimboka?usitaje jina tu,toa sababu.
 
Huo sio ukweli, hawa madaktari uchwara wanaochochea hii migomo wanajulikana agenda zao za siri na kina nani wanaowachochea, Serikali inafanya kila njia isiwape mwanya, lakini mwenye lake hakosi kulitafuta.

Ukweli ni nani asioujuwa?

Agenda zao za siri zipi? Za kusema waboreshewe mazingira yao ya kazi au mnafikiri wanataka kuiondoa serkali madarakani maana ndio wasiwasi wa serikali legelege hapa duniani.
 
Nway ishu hapa si mazungumzo issue ni..............kufell kwa vitisho na tingiza kiberiti ya serikali. Ile kuwaamuru warudi makazini kama wanavyowatishiaga nyau wanafunzi wa chuo. Pinda asingeitoa ile kauli yake ya asiyerudi kazini atapoteza ajira. Hili liwe funzo kwa serikali kuwa just because umeniajiri haikupi wewe madaraka ya kunizuia kwa vitisho na kunidindishia jisauti lako haki yangu ya kudai ninachoamini ni haki yangu. Mimi ni mtu mzima mwenzio na wakumbuke vyeo ni dhamana tu.
 
Usijifanye kuwa hujui yaliyojiri, Pinda alikwenda Karimjee, ambao hawakwenda kwa maongezzi ni hawa madaktari uchwara, na Pinda aliamuru warudi kazini lakini alisema wako tayari kukaa na kuwasikiliza wakati wowote. Msizuwe.

Leo hii madaktari wetu wamegeuka uchwara? Na wewe upo zile orodha za matibabu India? Usidharau taaluma za watu wanachodai ni haki yao ya kimsingi, tatizo ni hawa wanasiasa wetu.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Ati hali ya utoaji huduma afya Muhimbili inarudi kuwa ya kawaida: jamani madaktari 15 wa jeshi kweli wameweza kukavaa pengo la madaktari waliogoma? Propaganda hii mbaya sana. Serikali wanaona ni sawa kulinda image yao kwa public ilhali wagonjwa bado wanateseka.
mkuu hiri ri nchi bana.....kila kitu kinaamliwa na watu wakiwa klabu ya mbege.....
haya sasa naangalia sasa hiv walimu wa handeni nao wamegoma kufunindisha mpaka walipwe mshiko wao.....na hapa wanajeshi waende na huko...
 
Mbona sielewi kwani serikali ilikataa mazungumzo na madaktari au madaktari ndio walikataa mazungumzo na viongozi wa wizara ya Afya wakimtaka waziri mkuu?.. Sasa haya mazungumzo mapya yanahusu kitu gani kinyume cha yale yaliyotangulia!

Kaka, serikali haikuwa na lengo la kutatua mgogoro; walichotaka ni kulazimisha hoja ziishe kwa sababu wao wana dola. Wangeweza kabisa kufanya mazungumzo haya kwa kuonesha unyenyekevu na kukaa chini lakini wakataka madaktari waende kuwabembeleza kwenye viti vyao vya enzi! Hivi unafikiria kama ungekuwa mwaka wa uchaguzi serikali inge react hivi? Sasa hivi serikali imetambua kuwa "hiari yashinda utumwa"; wametambua serikali haina support kwa wananchi kwenye hili. Sasa, pa kuanzia ni kuwafuta kazi Waziri, Katibu na Mganga mkuu kwanza kuonesha kweli wameyapa uzito madai ya madaktari kutoka hapo mambo mengine yanzungumzika tena kwa haraka kweli.
 
My Take
Kumbe serikali bado iko tayari kuendeleza mazungumzo!. Sasa kwa nini Pinda aliharakisha kuutoa msimamo ule ile Jumapili ilhali ingesubiri mpaka Jumatatu ndipo wangeyamaliza!.

Kurejea kwenye meza ya mazungumzo ni uthibitisho mwingine wa serikali legelege dhaifu na ya waoga kama kunguru!.

Kwa serikali sasa kuwapigia magoti madaktari, Mhe. Pinda nae sasa awajibike kwa aibu!. Afadhali ya Lowassa aliwajibika ili kusave faces, Pinda awajibike kwa aibu ya mwaka kujidai kuchukua maamuzi magumu wakati uwezo hana!.

Oh poor government!.

Aibu!.

Pasco, unaamini sana serikali. Huishuku, unaipa benefits of the doubt na kwa kweli kabisa usipoangalia ni rahisi sana kuifuata kokote inakoelekeza. Kama raia katika nchi ya demokrasia jukumu lako la kwanza ni kuishuku serikali.
 
Mkandara the whole saga ni vulu vulu. Serikali ikisema nyundo madaktari wanasema maziwa ili mradi mambo hayajakaa sawa. Lakini nahisi mzizi wa kutoelewana kati ya serikali na hawa madaktari ni wajumbe/washauri toka ofisi ya waziri mkuu. Kuna tabia (ya muda mrefu) kwa watu wanaowazunguka viongozi wakuu kupindisha mambo! Sijui kwa nini? Pia wakubwa nao wamekuwa na tabia ya kuto-cross check kile wanachoombiwa. Matekoe yake unakuta viongozi wanatoa matamko kwa mambo ambayo sivyo.

Kwa mfano madaktari walisema kabisa hawawezi kuonana na waziri mkuu Jumapili kwa sababu timu ilikuwa haijatimia, sasa kwa nini Waziri mkuu alienda Karimjee? Watu wake walimwambia nini baada ya madaktari kuwaambia categorically kuwa Jumapili haiwezekani? Au walifiri madkatari wana tania? Wapi skills za negotion? Na kama wakubwa wetu wanashindwa ku-negotiate mambo madogo kama kukutanisha Waziri mkuu na madaktari wanawezaje ku-negotiate mambo mazito kwenye ulingo wa kimataifa ambapo wajanja wanatumia kila mbinu kupata kile wanataka?
Mkuu wangu nijuavyo mimi madaktari ndio wanatuchezea wananchi. Huu mgogoro baina yao na serikali hauwezi kuwa mtaji wa kugharamia maisha ya wananchi kwa sababu Waziri mkuu anaposema tukutane Jumapili, wewe mwajiriwa huwezi kupanga siku yako uitakayo. Huu ni ufedhuli na ukosefu wa heshima na kama unataka kunambia Pinda haheshimiki tena hapo nitakukubalia. Pengine tumefikia mahala nchi imekuwa haitawaliki..

Nimewahi kusema huko nyuma unakumbuka Ijumaa walikuwa wakizungumzia kuhusu Ukumbi? Ofisi ya waziri mkuu wakikataa kwenda Starlight kwa sababu ya Usalama wake na wao madaktari wakitaka mkutano ufanyike Hapo hapo na sio sehemu nyingine... Sasa hii taarifa wanayoisema leo ni taarifa gani ya kutokuwa na wajumbe!... walipogoma na kumtaka waziri mkuu siku ya kwanza walikuwa tayari vipi tofauti na Jumapili...Wewe huoni ujinga wa madai kama haya?.. haya nasikia tena leo kwamba MAT na madaktari hawakuwashirikisha TUCTA ktk kuongoza madai ama mgomo wakati hiki ni chombo cha watumishi wote wa serikali. WHY?...Je, haya ni madai ya madaktari wenye shahada kubwa na kujinadi wao kuwa wabora zaidi ya watu wote au?..

Uamuzi wa mgomo yameandaliwa na kina nani maana mara nisikie viongoziw a MAT ni madaktari wa Private Hospitals..Kitu gani haswa hapa kinatokea na kaa ni mageuzi ya kisiasa yanaanza na madaktari kwa nini wasiwashirikishe wananchi ktk madai ambayo yatawahusu wananchi wote na sio wao pekee?..
 
Back
Top Bottom