Mgomo wa Madaktari na wanaharakati wetu

Hivi unapomwita mkuu wa nchi kilaza unajisikiaje? Tena unamlinganisha na mwanae; hivi ungetendewa wewe hivyo ungejisikiaje. Usimtendee mwenzako usilopenda kutendewa wewe. Hata kama ana makosa ziko lugha za kuongea kama great thinkers sio kama kijiweni. Alichokosea ni nini? Je haki ya mwanadamu ni kifo au uhai? Ina maana ni sahihi madaktari kufanya madai yao kwa gharama za uhai wetu? Au wewe hujawahi kuuguliwa? Je unajua madaktari wanalipwa kiasi gani ukilinganisha na watumishi wengine wa umma? Je wao ndio wenye haki tu ya kulipwa fedha hata kama ni za bajeti yote na watumishi wengine waendelee kufa njaa? Let us be serious and realistic!!!!!!!!!!! Unapochangia jambo tafuta ukweli wa upande wa pili. Hebu fanya utafiti kidogo madaktari wanalipwaje ukilinganisha na watumishi wengine wa Serikali. Linganisha Scale yoyote ya madaktari uilinganishe na scale ya watumishi wengine wa serikali k.m. walimu, polisi, wahasibun.k. Uone jinsi ambavyo mishahara yao ni kama mara karibu tatu ya hao wengine. Sikatai kwamba wana haki ya kudai haki zao lakini si kwa gharama ya maisha ya watu na kwa kuzingatia kile wanacholipwa sasa na ukweli kwamba serikali ilishapokea madai yao.
Hivi madaktari wakipewa malipo wanayotaka na wahasibu nao wakagoma nao wadai kulipwa kama madaktari, wao watalipwa na nani? Au polisi wakigoma itakuwaje? Wote hatuwezi kuwa madaktari, uhasibu au ulinzi ungefanywa na nani ili wao waweze kufanya kazi zao? Sisi tu mwili mmoja kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake hakuna ambaye peke yake anaweza kufanya kila kitu peke yake. Tuache ubinafsi kila mmoja anahitaji maisha mazuri.:lock1::decision::attention:

nimefatilia hoja zote za huu uzi ila nimeona hoja yako haistahili kuwepo hapa, jifunze kuwajibika na uiondoe maana haina maana na haileti motisha kwa wasomaji. Unasema eti kila fani ikigoma eti itakuwaje? Fani ya kutibu wagonjwa na kuuguza unafananisha na uhasibu? Damn siamini kama ulifikiri kabla ya kupost hii hoja yako.
 
Sikonge,
Mkuu wangu, hakuna anayepinga kuboresha hali ya hospital zetu, lakini huwezi kutaka kuboresha Hospital zetu kwa kuua baadhi ya wagonjwa makusudi ikiwa hatua za majadiliano yenyewe zinawekwa vipingamizi visivyokuwa na maana kabisa..Hii ilikuwa sinema... Ni sawa kabisa na hostage taking ambayo ktk sinema utamuona mtu akidai hawezi kuongea na watu wengine isipokuwa fulani tu. Na huyo anapokuja anadai kwanza aletewe mtu fulani kubadilishana aidha mtu huyo aliua ndugu yake au alisababisha huyo Hostage taker kufanya kitendo kile. Hivyo hata kama yule alosababisha ni mkosa, lakini kile kitendo cha kuwaweka wananchi ktk mashaka ya Uhai wao, kuhatarisha usalama na uhai wa wananchji wote kwa jumla na kuwatumia wao kama ngao ya madai ni kosa vile vile... Hapa Madaktari walitumia Udokta wao kama SILAHA ya kupambana na serikali na sio NYENZO ya kuwawezesha wao kuponyesha maisha ya watu - ELIMU SIO SILAHA BALI NI NYENZO.
 
Naona watu wote mnahalalisha kila kitu sasa kwakuwa tu GVT yetu ni hovyo kitu ambacho kimsingi sina matatizo nacho na nakubaliana kwa hilo
Lakini mimi hapa na naangalia pia upande wa pili wa shilingi ambao hamtaki kuuangalia, kama utahukumu kwa mabaya ya gvt tu bila kuangalia na role za watu wengine katika kupigania haki za wananchi kama wanavyojiita wenyewe dhidi ya madai mengine yasiyo na tija nasema sio haki pia
Kuhalalisha kila hoja zenu kwa mifano ya ufisadi wa gvt tu wakati mwingine kunakosa nguvu kama swala linakuwa kuna watu wanaumia pasipo sababu za msingi za watukushinikiza maamuzi ya kisiasa ndio iwe hoja kuu huku wengine wasio na hatia wakipotea na wanaharakati kujifanya hawalioni hilo

Mkuu wangu, binafsi sijataka sana kuchangia post yako #1 sababu hoja yako imekuwa na matundu kadhaa,
Pia members wamekuonyesha mfano Bigirita...
Kaka Paulss huo upande unaojaribu kurudisha kuungalia, labda umesahau mbona ndio yamekuwa maisha ya watz ya kila siku??

Kuiamini serikali yao, kuamini katika majdiliano hadi tunaitwa watu blah blah, tumekuwa watu wa kuishi kwa mazoea huku tukifunikwa na uoga na uvumilivu tulivyovivika jina la "amani"
Paulss, ndugu yangu lazima tukubali kuwa muda unaenda na nyakati zinabdili hali....

Lakini pamoja na yote hayo jamii yetu bado imekuwa hodari wa kutamani kubakia katika namna ile ile..... Huku ikitamani kuwa jamii bora katika hali zote, kitu ambacho hakiwezekani!

Labda niiweke hii katika mfano wa suala husika.
Wewe unaelewa vizuri sana mgogoro huu wa madrs na gvt, zaidi sana unaielewa kwa kiasi fulani sekta yetu ya afya....
Lakini sana sana unaelewa aina ya watawala tulionao na namna wanavyotumia katika kuongoza na kusimamia masuala ya WATU...

Paulss tusijisahaulishe kuwa hali ya mabadiliko ya dunia katika suala la taarifa na hali ya nchi zingine kuwa litatuacha tubaki kama tunavyotamani...Haiwezekani kabisa...

Kama sisi vijana tulio katika nafasi ye kuelewa mambo kwa mwanga wa kulinganisha na historia yetu na mwendo wa dunia wa sasa tutakuwa ni wapu-uzi kama wapu-uzi wengine kwa kutaka kujiaminisha kuwa eti tutafanya mabadiliko tunayoyatamani huku jamii hii ikibaki kama ilivyo....

Hamna namna historia itatuacha salama kwa kutaka kudogosha (kulifanya dogo) suala la UFISADI.... hilo ni suala linalotakiwa kuwa ndio moyo wa Taifa, na kama watawala watalichezea hasi utawala huo unatakiwa ulaanike kwa kila namna na itoshe tu kwa hilo utawala huo uanguke...

Hivyo kama unadhani wote tunaozichukia serikali za serikali za CCM kwa sababu ya ufisadi ni wanoko tu tulio na gubu basi inabidi ujiulize tena unachosimamia......

Watu kufa.... sawa sio sahihi kushabikia watu kufa ila kuna wakati katika historia ya taifa lolote watu hufa na hiyo mara zote inatakiwa ibaki kuwa changamoto kwa wanaobaki hai ni namna gani wanaenzi vifo hivyo, na kuvifanya vifo hivyo kuwa na thamani hasa katika kusimamia vile ambavyo ndio walivyofia.....

Nje ya hapo ni kuvifanya vifo hivyo kuwa watu hao walikufa for nothing....

Mfano mgogoro huu wa madaktari ulivyomalizwa ni wazi kuwa waliokufa wamekufa for nothing, sababu vifo vyao havijatupa tafakari ya kitaifa katika kujenga hasa mfumo bora wa afya...

Vifo vitaendelea , je imetufaa nini??

Wakati unafunga mjadala huu kwa lawama juu ya sie tuliogoma kabisa kuielewa serikali hii katika suala hili na masuala mengine, pia tafakari huo upande unaotaka turudi tena kuungalia.....

Dunia inasonga mbele, na namna ya kuhoji uhalali wa masuala fulani ni lazima ubadilike..
Ni muhimu kama vijana tujikite kuijenga jamii hii katika kubadilika kuliko hali ya sasa ambapo bado ni nzito kupokea mabadiliko na wakati huo huo wanatarajia mabadiliko makubwa ya kijamii "eti maisha bora"!!
 
Mkuu, Hospital siyo WORKSHOP ya kuwa ukishaweka Drilling Machine bazo mchezo umekwisha bila kujali unasafisha au husafishi. Hospital ni sehemu ambayo inatakiwa kuwa katika hali ya usafi mkubwa ukiachia vifaa vyenyewe.

Sasa niambie baba yako afanyiwe upsasuaji na mwisho aje kulazwa kwenye wodi hii hapa chini.

Kuna tofauti gani Madokta wakitibu na mgonjwa akafa kwa kuambukizwa au kukosa Oxygen au akaachwa ajifie?

mhimbili.jpg

419799_318693151515179_129370793780750_963632_158016554_n.jpg

432098_318693854848442_129370793780750_963652_381356718_n.jpg


Labda mie nazeeka vibaya kwa kutokukuelewa :(
Sijui....ama hunielewi au hutaki kunielewa
Sijawahi kusema kwamba hali hiyo ni sahihi hata kidogo, kwa bahati mbaya mimi sina picha ya marehemu waliofariki kwaajili ya mgomo huu kwa kukosa huduma walau kama uliyoipost kwenye picha zako

 
Jaribu kujua maana ya uwanaharakati kiundani ndipo utaweza jua kwanini Wanaharakati wale waliwa-support Madaktari! Hao wanaharakati hutoa ripoti za study nyingi juu ya mapungufu ya serikali na wanajua kuliko unavyodhani wewe unafahamu zaidi! hoja ya msingi pale ilikuwa usalama wa madaktari na wauguzi mahospitalini na maslahi kuboreshwa ili mwananchi wa kawaida atibiwe ipasavyo! Sasa sijaona ubaya wao kuishurutisha serikali kutoka kwenye kuzembea kwake! Hapa huyo Rais wako ndiye aliyechemka kuingiza siasa kwenye madai ya wafanyakazi wa serikali!
 
Tatizo siyo Marehemu waliofariki wakati wa mgomo.

Mie naweza kukuletea pia za Marehemu waliofariki KABLA YA MGOMO. Mfano ni Marehemu dada yangu na Mumewe walifariki kwa sababu tu mashine ya kusafisha damu pale Muhimbili kwa miaka mingi haipo au ni mbovu. Mashine ambazo hata si za bei mbaya.

Hata kwenye Biblia imeandikwa kuwa ili upate mahindi punje mia zaidi, basi kubali hiyo punje moja uipande kwanza, kuombea kuwa haitaliwa, itakuwa na mwisho kuzaa hizo punje 100. Katika process, wengine wanakufa. Hili limesemwa sana na wamekuwa hawajali. Nina imani sasa linawakera sana na kutokuwapa usingizi. Kama si Mgomo................

To be, or not to be, that is the question.

Sijui....ama hunielewi au hutaki kunielewa
Sijawahi kusema kwamba hali hiyo ni sahihi hata kidogo, kwa bahati mbaya mimi sina picha ya marehemu waliofariki kwaajili ya mgomo huu kwa kukosa huduma walau kama uliyoipost kwenye picha zako
 
Watu msiojua mazingira ya hospitali zetu ni rahisi sana kuongea, watu msiojua watu wangapi wanapoteza maisha kila siku pasipo sababu za msingi ni rahisi sana kumsifia Raisi. Hauhitaji kusubiri migomo ndipo uboreshe mazingira na mishahara ya wafanyakazi wako. Serikali isiyofahamu wajibu wake huwa inashtushwa toka usingizini na migomo. Hao madaktari hata wakirudi kazini wakakaa hata masaa 24 bila uboreshaji hamna outcome yoyote inayopatikana. Tofauti tu ni kwamba kutakuwa na silent deaths, kila familia italia kwa msiba kivyake vyake na hamna lawama ya mgomo.

Waswahili walisema heri wachache wetu tupoteze maisha ili wenzetu wengi wapone. Lakini kilichofanyika ni kwamba vifo vitakuwa vya kimya kimya, wananchi badala ya kuinuka na kuunga mkono wanachopigania wataalamu ati vibabu vinaenda kupiga makofi halafu kesho yake kinaamkia hospitali ya serikali akiambiwa mzee dawa hamna anakunja uso. Mtu akikunyima elimu amekunyima na uhai moja kwa moja, na hili ndio tatizo sugu linalotusumbua, serikali hii haiwezi kuwaongoza watu waliosoma hata kwa wiki moja, patachimbika.
 
Naona wanaharakati ndo wamekuwa scapegoat wa uzembe wa taasisi nyingine.. Kosa lao nini hawa..? ni kufunga barabara kulazimisha Serikali iwacikilize madaktari..? Kupaza sauti zao kutaka Madaktari walipwe stahili zao na kuboreshewa vitendea kazi..? Hivi kuna yeyote anaeweza kuja na ushahidi hapa ambao unaonyesha wanaharakati wakiwashawishi madaktari wagome..? Mbona sasa uongo umekuwa ni sehemu kuu ya serikali hii..? Nadhani JK anataka kutuhamisha kwenye kiini cha tatizo..
 
Tatizo siyo Marehemu waliofariki wakati wa mgomo.

Mie naweza kukuletea pia za Marehemu waliofariki KABLA YA MGOMO. Mfano ni Marehemu dada yangu na Mumewe walifariki kwa sababu tu mashine ya kusafisha damu pale Muhimbili kwa miaka mingi haipo au ni mbovu. Mashine ambazo hata si za bei mbaya.

Hata kwenye Biblia imeandikwa kuwa ili upate mahindi punje mia zaidi, basi kubali hiyo punje moja uipande kwanza, kuombea kuwa haitaliwa, itakuwa na mwisho kuzaa hizo punje 100. Katika process, wengine wanakufa. Hili limesemwa sana na wamekuwa hawajali. Nina imani sasa linawakera sana na kutokuwapa usingizi. Kama si Mgomo................

To be, or not to be, that is the question.
Mkuu hata mimi naweza kukuweka picha za watu kibao waliopona kutokana na hospitali hizi hizi kabla ya mgomo, mmoja wapo nikiwa mimi mwenyewe nilipelekwa hoi bin taabani:focus:

Mkuu kwanza naomba unielewe sipo hapa kuitetea GVT hapana, nipo hapa kuangalia pia nini wajibu wa hawa DRs juu ya dhamana ya afya zetu, Mkuu Mkandara amelijengea hoja vizuri sana hili.
Iweje uhai wetu uwe ndio dhamana ya madai yao, na kibaya zaidi wamekubaliana mambo ya msingi yatafanyiwa kazi lakini wao wanasema hayo ya vifaa vya hospitali na huduma bora weka kando kwanza, ili turudi kazini toa kwanza waziri na naibu vinginevyo acha watu ajifie...... hili sita kaa nilielewe kamwe
Kama serikali ilikuwa imeisha fanya upumbavu wa kupuuzia madai ya msingi na baadae ikajirudi kulikuwa na sababu ya ndugu yangu kufa kwasababu mponda bado ni waziri? hapa ndipo tunalazimika kuangalia na upande wa shilingi je role yao katika hili ilikuwa vipi?
 
Nafikiri kama unakwenda kwa Waziri wa Usafiri na Uchukuzi na kuwambia Tanzania kuna shida ya usafiri (Malecela) na yeye anakujibu "anayesema Tanzania kuna shida ya usafiri, he can go to hell." Hivi mtu kama huyu ndiyo uendelee kukaa naye meza moja? Hivi kweli huyu atashughulikia madai yako?

Tatizo lilianza kwa majibu OVYO ya hao Wahusika wote. Pinda badala ya kujibu hoja, anaenda Bungeni na kuanza kumshambuli kiongozi wao vitu vya uongo. Hawa ndiyo ukae nao meza moja?

Jana umesikia hotuba ya Rais eti madaktari wanadai Milioni 17 kwa mwezi, lohhhh...... Huyu ndiyo ummpe muda ashughulikie matatizo yako, are you kidding me?

Mwisho, mie naweza kukuletea picha za waliopona bila hata ya kwenda HOSPITAL. Mfano ni mie nilinunua mwenyewe dawa Pharmacy.
Mkuu hata mimi naweza kukuweka picha za watu kibao waliopona kutokana na hospitali hizi hizi kabla ya mgomo, mmoja wapo nikiwa mimi mwenyewe nilipelekwa hoi bin taabani:focus:

Mkuu kwanza naomba unielewe sipo hapa kuitetea GVT hapana, nipo hapa kuangalia pia nini wajibu wa hawa DRs juu ya dhamana ya afya zetu, Mkuu Mkandara amelijengea hoja vizuri sana hili.
Iweje uhai wetu uwe ndio dhamana ya madai yao, na kibaya zaidi wamekubaliana mambo ya msingi yatafanyiwa kazi lakini wao wanasema hayo ya vifaa vya hospitali na huduma bora weka kando kwanza, ili turudi kazini toa kwanza waziri na naibu vinginevyo acha watu ajifie...... hili sita kaa nilielewe kamwe
Kama serikali ilikuwa imeisha fanya upumbavu wa kupuuzia madai ya msingi na baadae ikajirudi kulikuwa na sababu ya ndugu yangu kufa kwasababu mponda bado ni waziri? hapa ndipo tunalazimika kuangalia na upande wa shilingi je role yao katika hili ilikuwa vipi?
 
Mkandara:

To be, or not to be, that is the question.
We ain't making a play scene!
Mkapa hakutuambia sisi tuna wivu wa kike na hatuna elimu na bado leo ndio mnasema Kiongozi bora kuliko wote? mbona dharau hizi za viongozi zipo miaka yote na mnaendelea kuwachagua kama wabunge wetu..Unajua fika kabisa kwamba viongozi wetu wapo juu ya sheria halafu mnataka hao hao watoe hukumu. Kesi ya Ngedele kumpelekea Nyani, tofauti mnachagua nyani gani anayefaa. Yet bado mnashindwa kuelewa sisi tumesimama wapi? Ama kweli usistaajabu ya Mussa...
- *Unajitolea mfano wa kupona bila kwenda Hospital kama kigezo mkuu wangu?... Dah! haya sasa madaktari wa nini? basi tusiwalipe kabisaa hawana maana.
 
Nafikiri kama unakwenda kwa Waziri wa Usafiri na Uchukuzi na kuwambia Tanzania kuna shida ya usafiri (Malecela) na yeye anakujibu "anayesema Tanzania kuna shida ya usafiri, he can go to hell." Hivi mtu kama huyu ndiyo uendelee kukaa naye meza moja? Hivi kweli huyu atashughulikia madai yako?

Tatizo lilianza kwa majibu OVYO ya hao Wahusika wote. Pinda badala ya kujibu hoja, anaenda Bungeni na kuanza kumshambuli kiongozi wao vitu vya uongo. Hawa ndiyo ukae nao meza moja?

Jana umesikia hotuba ya Rais eti madaktari wanadai Milioni 17 kwa mwezi, lohhhh...... Huyu ndiyo ummpe muda ashughulikie matatizo yako, are you kidding me?

Mwisho, mie naweza kukuletea picha za waliopona bila hata ya kwenda HOSPITAL. Mfano ni mie nilinunua mwenyewe dawa Pharmacy.
Mkuu utafanya nikuletee picha za waliopona kwa babu sasa........lol

Lakini mkuu wewe unadhani ni kwanini Drs wameamua kumaliza mgomo?
Au unaamini wataendesha mgomo wa kimya kimya(chinja chinja) kukomoa watawala? just asking
 
P mara nyingi huwa nashangaa unachoongeaga ni tofauti na hil6 tabasamu lako. Au unatabia ya mamba?
Ha Haaaaaa............ at least you made my day dada jane, sijacheke toka asubuhi
BTW naongea maneno ya kikatili?
 
Sikonge,
Mkapa kasema hivi huko Arumeru - "Wapinzani ni wajinga na hawana Adabu". Sasa mtamfanya nini huyu mzee, mtagoma uchaguzi hadi avuliwe uanachama wa CCM?.
 
Mimi huwa najiuliza mbona haend pale mlimani ili baada ya hotuba wamswalike maswali kadhaa!!Mkuu wa kaya anajua jinsi ya kujisafisha kwa kutumia media,pale sauti yake ilikuwa inasikika nchi nzima,ya wanaharakati ilishazimwa kwenye media kitambo.sasa upotoshaji utafanyika na ukweli utafifishwa,rejea pia majibu ya mtoto wa mkulima hoja ya AR.bungeni dhidi ya mh. Lema. Wanaharakati walitaka serikali ichukue hatua kuhusu mgomo ule,kumbuka mtoto wa mkulima alizira na kwenda bungen dom baada ya kutoelewana na maDR. kuhusu ukumbi wa mkutano!Kwa ujumla mgomo ulikuwa unaendelea na hakukuwa na jitihada za wazi toka serikalini za kumaliza mgogoro huo.,ilikuwa lazima jamii ionyeshe hisia zake kuhusu msimamo huo wa serikali ambao haukuwa na maslahi kwa nmma.Wanaharakati walifanya hilo kwa niaba ya jamii.
 
..hivi kwanini nchi hii madaktari bingwa wanalipwa mshahara mdogo kuliko wabunge?
 


Lakini mkuu wewe unadhani ni kwanini Drs wameamua kumaliza mgomo?
Au unaamini wataendesha mgomo wa kimya kimya(chinja chinja) kukomoa watawala? just asking

Mkuu.. Hivi unadhani Madaktari walikuwa wanafurahia huo mgomo..? Au unafikiria Madaktari ni wakatili na hawana huruma hata kidogo..? Hii ndo dhana ambayo inalazimishwa kwa jamii kwamba Madaktari ni katili..! Unfortunately na ww kwa makusudi au bahati mbaya unasaidia kuisambaza hii dhana.. Ningependa Paulss uombe kwamba Serikali i-meet Doctors' demand halfway.. Badala ya kuendelea kujaribu kuwa-portray vbaya Doctors..
 
..hivi kwanini nchi hii madaktari bingwa wanalipwa mshahara mdogo kuliko wabunge?
Hii ndiyo vita kubwa tulokuwa nayo na binafsi sidhani kama maisha ni magumu kiasi kwamba Wabunge wachukue mishahara, posho, magari, na incentive kibao ambazo kwa ujumla wake ni kubwa kuliko mbunge wa Marekani au hata Daktari wa Marekani ni aibu tupu. Inakuwaje mbunge wa Ukerewe apewe malipo sawa na Mbunge wa Ubungo wakitumia wote kigezo cha ugumu wa maisha!..

Kwa nini mbunge asiwe mkazi wa sehemu alogombea?... haya yote ni maamuzi ambayo yanatakiwa kupunguza gharama kwa wananchi. Na nina hakika tukitumia kigezo cha MAKAZI na UZALENDO kwa wabunge basi utaona jinsi watakavyo kimbia mamlaka haya.

Lakini pia hatuwezi wachukulia wao kama kipimo cha mshahara unaowafaa madaktari wetu, walimu wetu na kadhalika. Kwanza tupigane na mfumo FISADI kuuondoa madarakani kisha tutazame kipimo safi cha maisha nchini maana utasikia tuna unemployment sijui 20% hii hesabu wameipata vipi? ikiwa hatuna utaratibu wa job search, total work force na kadhalika.
 
Back
Top Bottom