Mgomo wa Madaktari na wanaharakati wetu

You are very wrong, unajua analysis zinazotolewa na wanaharakati kipindi cha budget?
Ever heard of Budget analysis? Umeshawahi kumsikia Irenei Kiria akuwa na team yake wakiongelea swala la allocation ya budget ya Afya? how small it is, and what are the key i=areas ambazo haziguswi kila siku?

Mkuu, wakati hawa wanaharakati wakiwa wanapambana na serikali katika level hiyo, wewe na wengine wetu huwa hatuoni kazi yao.
sasa hapa unakuja kutuambia eti vi-NGO vyao?
Wakati Wanaharakati wa haki za binadamu wakitoa taarifa za mauaji ya raia ambayo serikali haijachukua hatua yoyote, wakati wakisema this government should act firmly on the issues surrounding deaths of citizens in the gold mines, the right to live as a fundamental human right is to be protected by the regime........wewe hukuona kwamba wanafanya kazi?

Tuacheni porojo, watazania tutatawaliwa na hawa wahuni mpaka mwisho wa dahari!!.......kwa mwendo huu!!!.duh!!

Wanaharakati hawakwenda kuwa-support Drs, walikwenda kuiambia Serikali iwajibike kwa kushindwa kutoa huduma za afya na hatimae kusababisha vifo!!,

Ni kazi ya serikali kuhakkisha huduma za afya zinatolewa no matter what, wanaharakati waliona mgomo, wakasema madaktari wanahoja, lakini ni kazi ya serikali kutatua swala lao. baada ya kuona huduma za afya hasa kwenye hospitali za rufaa zimedorora, wao wakaema. no, we cannot have a government that does not act!

Paulss, jipange tena, apa umechemka mbaya!
Mkuu pamoja na ubovu wote wa JK na gvt yake lakini kwenye ukweli pasemwe basi
Bandiko langu hakuna sehemu nimesema gvt ilikuwa sahihi, HAPANA, nilicho sema mimi ni kuwa kama haki yangu ya kwanza ni kuishi na DRs wamegoma je hawa wanaharakati hawaoni kuna haja pia ya kuwatetea Wananchi ambao ni wahanga wa mpambano huu? hivi nidhambi kwa wanaharakati kutaka DRs warudi kazini wakati wakiishinikiza serikali kutimiza matakwa ya DRs

Nimehoji je wanaharakati ni watu wa matukio kwa maana sijawahi kusikia wanaibua hoja yoyote, hiyo bajeti unayo sema wewe ikitoka si wanaharakati tu ni watu wote watasema maana ni tukio kubwa
Nitajie lini na hoja gani hawa jamaa wameibua, ukisema mauaji watasubiri yatokee ndio waite media sipo hapa kusema hawafanyi kazi nzuri, nipo hapa kusema kwamba hata kama gvt haiku act inavyotakiwa ilikuwa ni jukumu la wanaharakati kuikemea serikali at the same time kuhakikisha pia DRs wanahududmua wananchi maana ndio wanao watetea
 
So unataka WANAHARAKATI waendelee kusupport ukosefu wa vifaa vya kutendea kazi mahospitalini?

Mbona MKWERRE hakuongelea kabisa ukosefu wa mikasi na gauze mahospitalini?..takwimu zile alizosoma zinasaidia nini kwa mgonjwa aliyewasili OPD?

U should be joking meen!

Idadi ya wa tz wanaokufa kwa kukosa huduma zinazotokana na mazingira mabaya ya kazi ni kubwa mno mgomo utatusaidia maana mkulu mgomo ulikuwa ukiendelea yeye anakenua tu
 
Hivi unapomwita mkuu wa nchi kilaza unajisikiaje? Tena unamlinganisha na mwanae; hivi ungetendewa wewe hivyo ungejisikiaje. Usimtendee mwenzako usilopenda kutendewa wewe. Hata kama ana makosa ziko lugha za kuongea kama great thinkers sio kama kijiweni. Alichokosea ni nini? Je haki ya mwanadamu ni kifo au uhai? Ina maana ni sahihi madaktari kufanya madai yao kwa gharama za uhai wetu? Au wewe hujawahi kuuguliwa? Je unajua madaktari wanalipwa kiasi gani ukilinganisha na watumishi wengine wa umma? Je wao ndio wenye haki tu ya kulipwa fedha hata kama ni za bajeti yote na watumishi wengine waendelee kufa njaa? Let us be serious and realistic!!!!!!!!!!! Unapochangia jambo tafuta ukweli wa upande wa pili. Hebu fanya utafiti kidogo madaktari wanalipwaje ukilinganisha na watumishi wengine wa Serikali. Linganisha Scale yoyote ya madaktari uilinganishe na scale ya watumishi wengine wa serikali k.m. walimu, polisi, wahasibun.k. Uone jinsi ambavyo mishahara yao ni kama mara karibu tatu ya hao wengine. Sikatai kwamba wana haki ya kudai haki zao lakini si kwa gharama ya maisha ya watu na kwa kuzingatia kile wanacholipwa sasa na ukweli kwamba serikali ilishapokea madai yao.
Hivi madaktari wakipewa malipo wanayotaka na wahasibu nao wakagoma nao wadai kulipwa kama madaktari, wao watalipwa na nani? Au polisi wakigoma itakuwaje? Wote hatuwezi kuwa madaktari, uhasibu au ulinzi ungefanywa na nani ili wao waweze kufanya kazi zao? Sisi tu mwili mmoja kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake hakuna ambaye peke yake anaweza kufanya kila kitu peke yake. Tuache ubinafsi kila mmoja anahitaji maisha mazuri.:lock1::decision::attention:

Lini utahitimu upadri?
 
nadhani wanaharakati ambao miongoni mwao ni wanasheria, walipoteza dira pale waliposhindwa kuwashauri vizuri madaktari jinsi ya kukabiliana na likely legal action i.e.kama vile amri ya mahakama kuzuia mgomo etc
 
Jana wakati Rais JK anaongea na wazee wa DSM aliligusia hili la wanaharakati wetu jinsi walivyoshiriki katika mgomo huu, ingawaje kwa walio wengi ambao walisapoti Drs hili wataliona ni moja ya porojo alizokuwa anazipiga Mzee wa Kaya.
Wakati ule wanaharakati walipo ingilia kati kwa kusapoti DRs kwa asilimia mia moja wenye akili timamu tulihoji,
tulihoji kuwa kweli wanaharakati hawaoni na upande wa pili kuwa wananchi wanaowasimamia katika harakati zao wanaumia kwa vita ya GVT vs DRs, kwa bahati mbaya hatukueleweka

Nadhani hii ni changamoto kubwa kwa wanaharakati wetu kuangalia upya kile wanacho kitetea kwa maslahi ya mwanachi wa chini kabisa
Kwenye mgomo huu Ingawaje DRs walikuwa na madai yao ya msingi ambayo GVT ilionyesha nia ya kuyatekeleza wanaharakati hawa walikuwa kimya hadi pale DRs walipotaka viongozi wa kisiasa wawajibishwe kwanza ndio maswala mengine yafuatie ama sivyo mgomo moja kwa moja
Hapa sasa waliibuka from no where na kuanza kushinikiza mawaziri wawajibishwe na kuunga mkono mgomo uendelee hadi watolewe mawaziri.

Binafsi nilijiuliza sana kwamba ni kweli DRs wanasuguana na GVT kuhusu madai yao na hapa wanao umia ni wananchi, je wanaharakati ni lazima walalie upande mmoja wa DRs na kuacha wananchi wakitaabika, hivi walifanya juhudi gani kuhakikisha wanatetea maslahi ya mwanachi wa kawaida anayeuza vitumbua na maji akakuta Drs wamegoma na mfukoni ana pesa ya kumudu gharama za hospitali za serikali tu.

Kweli walimfikiria mwananchi huyu au walifikiria JK ni mgumu kuwajibisha wateule wake na sasa watumie mwanya huo kushinikiza bila kujali athari kwa wananchi wano watetea?

Je wanaharakati wetu ni ma opportunist wanao subiri tukio ndio waonekana kwenye media "kutetea" wananchi?
To be frank sijawahi kusikia wanaharakati wetu hawa wameibua hoja na kuivalia njuga zaidi ya kusubiri matukio pamoja na kuwa wanafanya kazi nzuri kiasi

Je kuwa mwanaharakati ni nini? nikuwa againt GVT muda wote hata kama kufanya hivyo ni kuumiza wananchi wasio na hatia kwa mambo yasiyo na ulazima

Mtazamo wangu nadhani ni vizuri wanaharakati hawa wakaangalia maslahi ya wananchi kwa ujumla hasa linapokuja swala la uhai wa watu, nilitarajia wanaharakati wangekuja na msimamo wa kuitaka GVT itimize matakwa ya DRs haraka huku wanaharakati hao wakiwataka DRs kurudi haraka kazini kuokoa maisha ya wananchi wano watetea wakiwa kama wanaharakati, vinginevyo uwana harakati wao itakuwa ni kupinga serikali tu na si maslahi kwa umma

analysis yako hapa ni ya kitoto sana alafu uko biased sana....kama alichokisema kikwete against activists umeona ni sahihi basi we have a very serious problem.ningekuwa na muda ningejaribu kukuonesha shida ulonayo wewe,kikwete na serikali yake.itoshe tu kusema this gvt is awful,a disaster ever!
 
Mkuu pamoja na ubovu wote wa JK na gvt yake lakini kwenye ukweli pasemwe basi
Bandiko langu hakuna sehemu nimesema gvt ilikuwa sahihi, HAPANA, nilicho sema mimi ni kuwa kama haki yangu ya kwanza ni kuishi na DRs wamegoma je hawa wanaharakati hawaoni kuna haja pia ya kuwatetea Wananchi ambao ni wahanga wa mpambano huu?
hivi nidhambi kwa wanaharakati kutaka DRs warudi kazini wakati wakiishinikiza serikali kutimiza matakwa ya DRs

Mkuu, wewe sijui hutaki kuelewa au una agenda yako, Wanaharakati walikuwa wanaishinikiza serikali itatue mgogoro wa Drs na GVT, kumbuka wanaharakati wakisema Drs rudini kazini haisaidii. This is very simple, BAKWATA walisema, still Drs didnt rect, Mgaya na chama cha wafanyakazi walisema still Drs didint react.
Kwa hiyo, issue unayoisema wewe ni kwamba, Wanaharakati wangesema, ''Drs rudini kazini'' so what?


Nimehoji je wanaharakati ni watu wa matukio kwa maana sijawahi kusikia wanaibua hoja yoyote, hiyo bajeti unayo sema wewe ikitoka si wanaharakati tu ni watu wote watasema maana ni tukio kubwa
Nitajie lini na hoja gani hawa jamaa wameibua, ukisema mauaji watasubiri yatokee ndio waite media

Nafikiri inabidi kuelewa kuwa mwanaharakati maana yake ni nini!!!

sipo hapa kusema hawafanyi kazi nzuri,
nipo hapa kusema kwamba hata kama gvt haiku act inavyotakiwa ilikuwa ni jukumu la wanaharakati kuikemea serikali at the same time kuhakikisha pia DRs wanahududmua wananchi maana ndio wanao watetea

Sasa mkuu, wewe ulikuwa unataka wanaharakati wahakikishe vipi Drs wanarudi kazini kuwahudumia wananchi? wahakikishe kwa kuwachapa viboko au waandamane kulazimisha warudi? at the same time waandamane kuwashinikiza serikali kuwasikiliza Drs?
Very contradicting indeed!
Ni jukumu la serikali kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa raia, serikali isipofanya hivyo, either kwa kuwa inagombana na Drs au kwasababu yoyote ile, ni kazi ya wananchi na wanaharakati kuiambia serikali, whatever your problems with the Drs are, we want service, resolve your problems, sisi tunataka huduma, that is what Wanaharakati was telling this government ambayo ilichukua more than one weak to react!
Mkuu, naona lawama zako hazipo valid hata kidogo!
 
analysis yako hapa ni ya kitoto sana alafu uko biased sana....kama alichokisema kikwete against activists umeona ni sahihi basi we have a very serious problem.ningekuwa na muda ningejaribu kukuonesha shida ulonayo wewe,kikwete na serikali yake.itoshe tu kusema this gvt is awful,a disaster ever!
Mkuu sio JK na GVT wala sio Drs waliokuwa sahihi katika hili, na hata tukisema GVT ndio walichemka lakini je hao Activists upeo wao wa kutete roho zisizo na hatia kwenye mgogoro huu ilikomea kwenye kusapoti mgomo? je walitafakari role ya Drs juu ya dahamana waliyo nayo kwa afya zetu
unajua tukivaa ubaya wa JK na gvt tu na kusahau wajibu wa DRs juu ya afya zetu tutakuwa hatutendi haki watu waliopoteza maisha yao au kupata madhira kwa mgomo huu
 
Mkuu, naona lawama zako hazipo valid hata kidogo!
Mkuu, wewe sijui hutaki kuelewa au una agenda yako, Wanaharakati walikuwa wanaishinikiza serikali itatue mgogoro wa Drs na GVT, kumbuka wanaharakati wakisema Drs rudini kazini haisaidii. This is very simple, BAKWATA walisema, still Drs didnt rect, Mgaya na chama cha wafanyakazi walisema still Drs didint react.
Kwa hiyo, issue unayoisema wewe ni kwamba, Wanaharakati wangesema, ''Drs rudini kazini'' so what?

Mkuu hoja sio wakiambiwa watafanya au hawatafanya hoja ni wao kuseama kinachopaswa kusema, nadhani unajua zaidi ya asilimia 90 ya waliyosema hayajafanywa na sio kwenye issue hii tu, mambo mengi tu.

Sasa mkuu, wewe ulikuwa unataka wanaharakati wahakikishe vipi Drs wanarudi kazini kuwahudumia wananchi? wahakikishe kwa kuwachapa viboko au waandamane kulazimisha warudi? at the same time waandamane kuwashinikiza serikali kuwasikiliza Drs?
Very contradicting indeed!
Ni jukumu la serikali kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa raia, serikali isipofanya hivyo, either kwa kuwa inagombana na Drs au kwasababu yoyote ile, ni kazi ya wananchi na wanaharakati kuiambia serikali, whatever your problems with the Drs are, we want service, resolve your problems, sisi tunataka huduma, that is what Wanaharakati was telling this government ambayo ilichukua more than one weak to react!

Nafikiri inabidi kuelewa kuwa mwanaharakati maana yake ni nini!!!
Mkuu wewe ndio unajichanganya jukumu la wanaharakati ni kupaza sauti, kwani walipoiambia gvt ihakikishe huduma bora walitumia nini, kwanini vivyo hivyo wasitumie the same way kuwaambia DRs
Au kuwaambia DRs ni kuwalazimisha na kuwaambia gvt ndio sahihi,

Walifanya vyema kupaza sauti kuhusu gvt kutimiza wajibu wake lakini tunahoji kwanini hawakupaza sauti wakati walala hoi wanakufa na wenye dhamana na hilo wanataka tu fulani lazima awajibishwe kwanza ndio warudi kazini?wajibu wao ni kuhakikisha haki za wananchi zinatimizwa
 
Nafikiri wewe, Mkandara na wengine wengi ndiyo mlikuwa mnalilia warudi kazini kwa usemi wa Bora Dokta na si Dokta Bora.

Sasa mlichokitaka mtakipata. Kama ni mauwaji, sisi sote tumefanya kwani hatukuwaunga mkono.

Acha tufe sana tu ndiyo tutatia adabu maana akili zetu hazina akili.

Ni UUWAJI kutafuta mchawi wakati Mchawi ni wewe mwenyewe/mimi mwenyewe........

Anyway, AIDS itasaida ikishirikiana na malaria kupungiza Watanzania.

Acha liende hadi ligotaGE.

Kwa kadri nijuavyo mimi madaktari kuendeleza mgomo baridi ni kuendelea kuua wananchi pasipo na sababu ya msingi
Kama wakiamua ni bora watangaze mgome na wasiende kabisa kazini ili serikali ijue nini cha kufanya kuliko kwenda na kuacha wtu akijifia.....huu ni uuaji live kabisa

Mkuu, utatafuta sana wachawi wa kuusukumiza mzigo huu ila ukweli unajulikana. Waliokufa huko waliko ninaamini roho zao zitashuka na kuanza kulipa kisasi. Nyie wote mliohusika kuifikisha Tanzania hapa ilipo na hao wote waliosababisha mgomo wa kijinga, MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI.

Kuna siku itafika hata kama akina Nyoni watakuwa na miaka 70 au 80, itabidi wapandishwe Mahakamani kama Mubarack huko Egypt aliyeletwa kitandani ili asomowe mashitaka. Watoto wao wote watakamatwa na mali zao kutaifishwa.
 
Jana wakati Rais JK anaongea na wazee wa DSM aliligusia hili la wanaharakati wetu jinsi walivyoshiriki katika mgomo huu, ingawaje kwa walio wengi ambao walisapoti Drs hili wataliona ni moja ya porojo alizokuwa anazipiga Mzee wa Kaya.
Wakati ule wanaharakati walipo ingilia kati kwa kusapoti DRs kwa asilimia mia moja wenye akili timamu tulihoji,
tulihoji kuwa kweli wanaharakati hawaoni na upande wa pili kuwa wananchi wanaowasimamia katika harakati zao wanaumia kwa vita ya GVT vs DRs, kwa bahati mbaya hatukueleweka

Nadhani hii ni changamoto kubwa kwa wanaharakati wetu kuangalia upya kile wanacho kitetea kwa maslahi ya mwanachi wa chini kabisa

Kwenye mgomo huu Ingawaje DRs walikuwa na madai yao ya msingi ambayo GVT ilionyesha nia ya kuyatekeleza wanaharakati hawa walikuwa kimya hadi pale DRs walipotaka viongozi wa kisiasa wawajibishwe kwanza ndio maswala mengine yafuatie ama sivyo mgomo moja kwa moja
Hapa sasa waliibuka from no where na kuanza kushinikiza mawaziri wawajibishwe na kuunga mkono mgomo uendelee hadi watolewe mawaziri.

Binafsi nilijiuliza sana kwamba ni kweli DRs wanasuguana na GVT kuhusu madai yao na hapa wanao umia ni wananchi, je wanaharakati ni lazima walalie upande mmoja wa DRs na kuacha wananchi wakitaabika, hivi walifanya juhudi gani kuhakikisha wanatetea maslahi ya mwanachi wa kawaida anayeuza vitumbua na maji akakuta Drs wamegoma na mfukoni ana pesa ya kumudu gharama za hospitali za serikali tu.

Kweli walimfikiria mwananchi huyu au walifikiria JK ni mgumu kuwajibisha wateule wake na sasa watumie mwanya huo kushinikiza bila kujali athari kwa wananchi wano watetea?


Je wanaharakati wetu ni ma opportunist wanao subiri tukio ndio waonekana kwenye media "kutetea" wananchi?
To be frank sijawahi kusikia wanaharakati wetu hawa wameibua hoja na kuivalia njuga zaidi ya kusubiri matukio pamoja na kuwa wanafanya kazi nzuri kiasi

Je kuwa mwanaharakati ni nini? nikuwa againt GVT muda wote hata kama kufanya hivyo ni kuumiza wananchi wasio na hatia kwa mambo yasiyo na ulazima

Mtazamo wangu nadhani ni vizuri wanaharakati hawa wakaangalia maslahi ya wananchi kwa ujumla hasa linapokuja swala la uhai wa watu, nilitarajia wanaharakati wangekuja na msimamo wa kuitaka GVT itimize matakwa ya DRs haraka huku wanaharakati hao wakiwataka DRs kurudi haraka kazini kuokoa maisha ya wananchi wano watetea wakiwa kama wanaharakati, vinginevyo uwana harakati wao itakuwa ni kupinga serikali tu na si maslahi kwa umma



Mimi wewe sijakuelewa kabisa! Raisi alisema wana harakati waliwachochea Drs wagome ili wauwe watu. Wewe unasema wana harakati walisubiri Drs wagome ndipo wakaibuka na kusema. Wana harakati wangeibuka na kusema kabla ya madakitari kugoma na kisha hao Drs wakagoma Wangelaumiwa sana na kusema ndio wamechochea mgomo, kutokana na kauli ya Raisi. Wewe unasema wana harakati wanasubiri liibuke jambo ndio waseme, harafu unasema wanaharakti wliunga mkono mgomo wa Drs na kuipinga serikari! Unajua unapo andika habari yoyote usiandike tu maadam huwapendi wana harakati unaandika na uongo ili kuwadanganya watu. Watu wanfuatilia mambo sana na wana uelewa mkubwa. Mimi nilivyo soma hii habari yako nilichokigundua ni kuwa wewe una chuki na wana harakati na ndiyo maana ukaandika mambo ya uongo. Unasema ulitarajia wanaharakati waje na msimamo wa kuitaka Serikari itimize matakwa ya Drs na kuwataka Drs warudi haraka kazini kuokoa maisha ya wananchi. Ndiyo maana nasema unaandika maneno kwa ushabiki, Ungelikuwa umewasikiliza matamshi yao wana harakati usingesema ulitarajia!! Maneno uliyotarajia ndiyo waliyo yasema. Serikari ifikie Muafaka na Drs na Drs warudi kazini ili wananchi wasinyimwe haki yao ya msingi ya afya. Au wewe uliwaskiliza wana harakati wa wapi! Usiandike maadamu umeandika kwa kusikia maneno na huna uhakika. Kwa mtazamo wako serikari ikifanya madudu isifiwe tu. Acha kuwadanganya watu kama habari huna uhakika nayo usidandie tu eti kwa kuwa JK kasema. Jibuni haja sio kuongea vitu visivyo elewaka
 
Hivi unapomwita mkuu wa nchi kilaza unajisikiaje? Tena unamlinganisha na mwanae; hivi ungetendewa wewe hivyo ungejisikiaje. Usimtendee mwenzako usilopenda kutendewa wewe. Hata kama ana makosa ziko lugha za kuongea kama great thinkers sio kama kijiweni. Alichokosea ni nini? Je haki ya mwanadamu ni kifo au uhai? Ina maana ni sahihi madaktari kufanya madai yao kwa gharama za uhai wetu? Au wewe hujawahi kuuguliwa? Je unajua madaktari wanalipwa kiasi gani ukilinganisha na watumishi wengine wa umma? Je wao ndio wenye haki tu ya kulipwa fedha hata kama ni za bajeti yote na watumishi wengine waendelee kufa njaa? Let us be serious and realistic!!!!!!!!!!! Unapochangia jambo tafuta ukweli wa upande wa pili. Hebu fanya utafiti kidogo madaktari wanalipwaje ukilinganisha na watumishi wengine wa Serikali. Linganisha Scale yoyote ya madaktari uilinganishe na scale ya watumishi wengine wa serikali k.m. walimu, polisi, wahasibun.k. Uone jinsi ambavyo mishahara yao ni kama mara karibu tatu ya hao wengine. Sikatai kwamba wana haki ya kudai haki zao lakini si kwa gharama ya maisha ya watu na kwa kuzingatia kile wanacholipwa sasa na ukweli kwamba serikali ilishapokea madai yao.
Hivi madaktari wakipewa malipo wanayotaka na wahasibu nao wakagoma nao wadai kulipwa kama madaktari, wao watalipwa na nani? Au polisi wakigoma itakuwaje? Wote hatuwezi kuwa madaktari, uhasibu au ulinzi ungefanywa na nani ili wao waweze kufanya kazi zao? Sisi tu mwili mmoja kila mmoja ni kiungo kwa mwenzake hakuna ambaye peke yake anaweza kufanya kila kitu peke yake. Tuache ubinafsi kila mmoja anahitaji maisha mazuri.:lock1::decision:
Tatizo ni utendaji wa serikali yetu umekuwa wa kigoigoi sana ndio maana inafika mahali watu wanapandwa na hasira wanatukana, hebu fikiria kipindi cha mgomo wa madaktari rais yeye alikuwa anatalii njee ya nchi ikiwemo kuhudhuria sherehe za chama kule Botswana wakati watanzania wanateketea. kama angekuwa rais mtendaji angerudi na kulisimamia mara moja ili kuepusha vifo zaidi lakini alipuuza mpaka juzi ndio anakuja kujitokeza. swala la mishahara kwa wafanyakazi mbalimbali serikalini serikali inatakiwa kuliangalia upya hasa ya walimu na madaktari na hili linawezekana kwa serikali kuacha kuishi kitajiri wakati nchi masikini, isimamia vizuri ukusanyaji wa kodi, ipunguze matumizi yasiyo ya lazima hasa ya magari ya kifahari , safari za kula bata zisizo na tija, isimamiae vizuri rasilimali zetu, ishughulikie wala rushwa. ifike mahali basi tusikie mishahara ya mawaziri imechelewa au hawajalipwa posho miezi kadhaa...siyo kila siku kwa walimu na madaktari tuu.... na tukisikia ****** kawafunga richmond,epa,kagoda nakuwafukuza watendaji wabovu kama Mponda,kawambwa na wengineo hakika hutasikia mtu kamtukana mwere humu. :attention:
 
Nani hasa asiyekuwa na huruma kwa wananchi/wagonjwa, Kikwete kwa kushindwa kuendesha vizuri serikali,ikiwemo wizara ya afya;ukosefu wa vifaa vya kutolea huduma,kwa maana ya mazingira magumu ya kufanyia kazi kwa watumishi wa sekta ya afya,huku fedha za wananchi zikiishia mifukoni mwa mafisadi,safari za nje zisizo na tija,warsha,semina kama za Ngurdoto kule Dodoma,kukabidhi rasilimali za taifa kwa wawekezaji(sekta ya madini,maliasili nk) ambao hata hivyo hawalipi kodi kulingana na mali wanayopora(rejea tukio la wazalendo wenye uchungu kuvamia ndege iliyokuja bubeba dhahabu yenye thamani ya sh bilioni 43 na serikali kuambulia kodi ya sh.bilioni 1(moja) kule Mgodi wa Geita AU madaktari waliogoma kwa niaba ya wagonjwa na Watanzania kwa ujumla kudai uboreshaji wa huduma za afya na wanaharakati kumkumbusha Rais juu ya ukweli huo?
Yawezekana wewe unaona ubaya wa wanaharakati kama Rais wetu una interest isiyokuwa na manufaa kwa umma na hivyo share interest hizo na magamba na sasa ni rahisi tu kuonana na mabosi wengi wa MAGAMBA kwani wako kule Arumeru wakipanga namna ya kuwanunua wapiga kura ingawa hata hivyo wana Arumeru mashariki wako macho this time round!
 
Naona watu wote mnahalalisha kila kitu sasa kwakuwa tu GVT yetu ni hovyo kitu ambacho kimsingi sina matatizo nacho na nakubaliana kwa hilo
Lakini mimi hapa na naangalia pia upande wa pili wa shilingi ambao hamtaki kuuangalia, kama utahukumu kwa mabaya ya gvt tu bila kuangalia na role za watu wengine katika kupigania haki za wananchi kama wanavyojiita wenyewe dhidi ya madai mengine yasiyo na tija nasema sio haki pia
Kuhalalisha kila hoja zenu kwa mifano ya ufisadi wa gvt tu wakati mwingine kunakosa nguvu kama swala linakuwa kuna watu wanaumia pasipo sababu za msingi za watukushinikiza maamuzi ya kisiasa ndio iwe hoja kuu huku wengine wasio na hatia wakipotea na wanaharakati kujifanya hawalioni hilo
 
Nafikiri wewe, Mkandara na wengine wengi ndiyo mlikuwa mnalilia warudi kazini kwa usemi wa Bora Dokta na si Dokta Bora.

Sasa mlichokitaka mtakipata. Kama ni mauwaji, sisi sote tumefanya kwani hatukuwaunga mkono.

Acha tufe sana tu ndiyo tutatia adabu maana akili zetu hazina akili.

Ni UUWAJI kutafuta mchawi wakati Mchawi ni wewe mwenyewe/mimi mwenyewe........

Anyway, AIDS itasaida ikishirikiana na malaria kupungiza Watanzania.

Acha liende hadi ligotaGE.



Mkuu, utatafuta sana wachawi wa kuusukumiza mzigo huu ila ukweli unajulikana. Waliokufa huko waliko ninaamini roho zao zitashuka na kuanza kulipa kisasi. Nyie wote mliohusika kuifikisha Tanzania hapa ilipo na hao wote waliosababisha mgomo wa kijinga, MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI.

Kuna siku itafika hata kama akina Nyoni watakuwa na miaka 70 au 80, itabidi wapandishwe Mahakamani kama Mubarack huko Egypt aliyeletwa kitandani ili asomowe mashitaka. Watoto wao wote watakamatwa na mali zao kutaifishwa.
Mkuu wangu kwanza kabisa heshima mbele. Nafikiri Watanzania tuna matatizo sana ya kufikiri na kibaya zaidi ni watu ambao tumejengwa kuunga mkono upande yaani mtu hawezi kutofungamana na upande wowote.

Mgomo wa Madaktari nimeupinga kwa sababu binafsi yangu sikukubaliana na maamuzi ya serikali wala ya madaktari na nimeeleza hata sababu na solution kinyume cha hao mnaowaita WANAHARAKATI ambao kimajukumu yao wamechukua upande bila kujali hali za wananchi. Siku zote mwanaharakati hutazama haki na uhai wa wananchi kwa kutumia neno zito sana la UTU kwanza.

Sasa ikiwa wao wamechukua upande wa madaktari pasipo kuelewa uzito ama uwezo wa serikali ktk janga hilo, bila kuzingatia uwezekano wa matakwa hayo kufikiwa within time frame iliyowekwa ni Ushabiki ule ule wa Simba vs Yanga au Arsenal vs ManU ambao mimi sina. Kwanza hata nikiwa Bongo huwashangaa watu kukaa vijiweni na kubishana juu ya Arsenal na ManU kwa sababu huku majuu watu hawabishani mpira pengine huko UK, ila huzipenda na kuzishabikia team zao hata kama wanajua zina mapungufu na uwezekano wa kushindwa... U bet for a winning team hata isipokuwa team yako kwa sababu hakuna ugonvi uki bet team nyingine kuwashinda.

Kilichotokea nchini hakina chembe ya Uzalendo, watu wamekufa wakiwa hostage wa madaktari, kitendo cha kuwatumia wagonjwa kuonyesha mabavu yao kwamba wao ni muhimu kuliko kila kitu ilihali chanzo cha yote haya ni Posho za Wabunge ambao wanaharakati wote tunazipinga kwa nguvu zote...Sasa leo zihalalishwe kwa madaktari kwa sababu tu Wabunge wanapewa, hivi hii vita against Posho tutaweza kupigana nayo vipi ikiwa tunaongeza wigo la wapokeaji..Na kesho kama tutaendeleza kupambana na Posho hao madaktari hawatakuwa upande wetu..Hiyo ni given kwa sababu watatetea maslahi yao kwanza. daktari anataka kuanza mshahara kwa Mil 7.5 wengine 17.7 wakati vita yetu kubwa ni ongezeko la mashara across the board ya ajira zote nchini. hakuna mtu muhimu duniani kuliko mwingine ama mwenye kuthaminika kimaisha au kimaendeleo kuliko wengineo.. Hii ni NO! NO!

Huu ni mtazamo wangu na naomba sana uheshimiwe kimawazo na nipewe majibu yanayoridhisha kuhusiana na ongezeko la wapokea Posho zisizokuwa accounted for, sio Mkandara hivi ama vile. Sina muda wa kuzungumzia WATU bali kitendo kilichofanywa na kutugharimu uhai wa WATU, mwanaharakati yeyote hatakiwi kukiunga ikiwa maisha ya watu yapo hatarini. Leo hii huko Syria wanaharakati wanatafuta suluhu baina yao na sio kuchochea vita zaidi. Kwa yeyote anachochea mapambano haya kwa kuchagua upande dhidi ya wananchi basi sii mwanaharakati tena ni ALLIES wa upande alochagua.
 
Mkuu, Hospital siyo WORKSHOP ya kuwa ukishaweka Drilling Machine bazo mchezo umekwisha bila kujali unasafisha au husafishi. Hospital ni sehemu ambayo inatakiwa kuwa katika hali ya usafi mkubwa ukiachia vifaa vyenyewe.

Sasa niambie baba yako afanyiwe upsasuaji na mwisho aje kulazwa kwenye wodi hii hapa chini.

Kuna tofauti gani Madokta wakitibu na mgonjwa akafa kwa kuambukizwa au kukosa Oxygen au akaachwa ajifie?

mhimbili.jpg

419799_318693151515179_129370793780750_963632_158016554_n.jpg

432098_318693854848442_129370793780750_963652_381356718_n.jpg


Labda mie nazeeka vibaya kwa kutokukuelewa :(

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-hali-inavyotisha-hospitali-ya-muhimbili.html

NB: Mkandara, ujumbe wako wa juu nimeujibu hata kabla sijasoma, hapo kwenye RED. Mengine itakuwa tu kurudia. Sisi wananchi ndiyo tunataka TUFE kwa kutokuingia barabarani. Kama serikali wamefilisika basi tuone kweli wamefilisika kwa kubana matumizi na si kila siku majuu kutembeza bakuli wakati Ulaya sasa hivi wanahaha kuikoa Ugiriki huku wengine akina Spain, Portugal, Italy wako hoi bin taabani na kwa lugha nyingine, wanachechemea huku wakishaanza kutishia hata kuuvunja Muungano wao wa Ulaya.
Lawama itabebeshwa Serikali kwa uzembe wake na ikibidi ije siku watu washitakiwe kwa kusababisha hayo mauwaji. Tunaona sasa hivi Mkapa anavyobebeshwa gunia la CCM kwa kuogopa kuwa akigoma watampandisha kizimbani kwa ufisadi wake. Ila Muoshwa Huoshwa. Just a matter of time.
NALAANI POSHO ZOTE TANZANIA.

Naona watu wote mnahalalisha kila kitu sasa kwakuwa tu GVT yetu ni hovyo kitu ambacho kimsingi sina matatizo nacho na nakubaliana kwa hilo
Lakini mimi hapa na naangalia pia upande wa pili wa shilingi ambao hamtaki kuuangalia, kama utahukumu kwa mabaya ya gvt tu bila kuangalia na role za watu wengine katika kupigania haki za wananchi kama wanavyojiita wenyewe dhidi ya madai mengine yasiyo na tija nasema sio haki pia
Kuhalalisha kila hoja zenu kwa mifano ya ufisadi wa gvt tu wakati mwingine kunakosa nguvu kama swala linakuwa kuna watu wanaumia pasipo sababu za msingi za watukushinikiza maamuzi ya kisiasa ndio iwe hoja kuu huku wengine wasio na hatia wakipotea na wanaharakati kujifanya hawalioni hilo
 
Back
Top Bottom