Mgomo wa Madaktari (Leo): Kiburi cha Blandina Nyoni

Hapa ndipo madaktari wanapokosea kama mtizamo wao ndio huu wa Zimmerman. Hapa unachotafuta ni Daktari awe na mshahara mkubwa kuliko watumishi wengine wote au maslahi yaendane na kazi? Hebu mfikirie rubani anayeongoza ndege yenye abiria 480, there is no room for error, hakuna cha kusema ati nurse alimix mafaili, one mistake half a thousand people are dead! mfikirie mtu anayetreat maji tunayotumia dar es Salaam kutoka mto Ruvu, no room for errors, mix-up of chemicals my dear the whole city is dead! Kwa hiyo hiyo arragance uliyo/mliyonayo is a grave mistake. Nchi nyingine zilizoendelea unazozitolea mifano, mishahara iko very close hamna tofauti kubwa kati ya dereva wa basi hata na daktari, wote wanatoa huduma muhimu kwa jamii. Sema mishahara inakidhi mahitaji. Madaktari wanayo baadhi ya madai ya msingi kabisa, suala la posho ni la msingi.

Kwa upande wa pili, madaktari nao wana matatizo makubwa sana na ndio maana naona baadhi ya watu wanaandika kwa hisia hapa. Nadhani kila mmoja wetu ameshatendwa in one way or another na wafanyakazi wa sekta ya afya. Na hii kwa kiasi kikubwa inatokana na arrogance waliyonayo kuwa they are the best, most important professionals, which is not true at all, kila mtu na fani yake ana umuhimu kwa jamii, you need to look it from the system perspective na sio kama units. Fani ya udaktari imeoza, purely rotten, wengi wana majina ya udaktari but ni wababaishaji wakubwa, hakuna kitu, empty headed enjoying being called with all sweet prefixes in the street, Dr, Dr! Madaktari wa leo hawana ethics, na mwili wa binadamu wanauchukulia kama wa mnyama tu, they dont care at all. Nasema wengi ni wababaishaji, lakini wapo wazuri na makini, wanaopenda kazi yao.

Mwisho, system nzima ya afya inahitaji complete overhaul, haiwezekani mgonjwa atoke Amana anafikishwa Muhimbili ati anapokelewa na Intern, ni upuuzi mtupu huu. Hospitali ya Rufaa inageuka ya kujifunzia tena? mgonjwa aliyezidiwa anaonwaje na daktari mwanafunzi kama sio uwendawazimu huu! nchi gani inafanya huu upuuzi? Hospitali za rufaa zinatakiwa 24 hours zina specialists, za kwetu ati zina interns. Akili za wapi hizi? Wagonjwa wengi naamini zaidi ya nusu wanafariki sio kwa maradhi yanayowasumbua, hapana wanakuwa mismanaged. Hili linajulikana, mara intern mara mwanafunzi wa masters mara nurse mara huyu, mpaka mtu anakata roho anafanyiwa mizaha tu.

kweli uhuru wa kulalamika unautumia vizuri kaka, mala Amana, mala intern, mala pilot, tunaposema hili ni jukwaa la greater thinker hatumaanishi kuandika text ndefu iliyojazwa na mitizamo ya hisia, next time jipange kaka.
 
Hapa ndipo madaktari wanapokosea kama mtizamo wao ndio huu wa Zimmerman. Hapa unachotafuta ni Daktari awe na mshahara mkubwa kuliko watumishi wengine wote au maslahi yaendane na kazi? Hebu mfikirie rubani anayeongoza ndege yenye abiria 480, there is no room for error, hakuna cha kusema ati nurse alimix mafaili, one mistake half a thousand people are dead! mfikirie mtu anayetreat maji tunayotumia dar es Salaam kutoka mto Ruvu, no room for errors, mix-up of chemicals my dear the whole city is dead! Kwa hiyo hiyo arragance uliyo/mliyonayo is a grave mistake. Nchi nyingine zilizoendelea unazozitolea mifano, mishahara iko very close hamna tofauti kubwa kati ya dereva wa basi hata na daktari, wote wanatoa huduma muhimu kwa jamii. Sema mishahara inakidhi mahitaji. Madaktari wanayo baadhi ya madai ya msingi kabisa, suala la posho ni la msingi.

Kwa upande wa pili, madaktari nao wana matatizo makubwa sana na ndio maana naona baadhi ya watu wanaandika kwa hisia hapa. Nadhani kila mmoja wetu ameshatendwa in one way or another na wafanyakazi wa sekta ya afya. Na hii kwa kiasi kikubwa inatokana na arrogance waliyonayo kuwa they are the best, most important professionals, which is not true at all, kila mtu na fani yake ana umuhimu kwa jamii, you need to look it from the system perspective na sio kama units. Fani ya udaktari imeoza, purely rotten, wengi wana majina ya udaktari but ni wababaishaji wakubwa, hakuna kitu, empty headed enjoying being called with all sweet prefixes in the street, Dr, Dr! Madaktari wa leo hawana ethics, na mwili wa binadamu wanauchukulia kama wa mnyama tu, they dont care at all. Nasema wengi ni wababaishaji, lakini wapo wazuri na makini, wanaopenda kazi yao.

Mwisho, system nzima ya afya inahitaji complete overhaul, haiwezekani mgonjwa atoke Amana anafikishwa Muhimbili ati anapokelewa na Intern, ni upuuzi mtupu huu. Hospitali ya Rufaa inageuka ya kujifunzia tena? mgonjwa aliyezidiwa anaonwaje na daktari mwanafunzi kama sio uwendawazimu huu! nchi gani inafanya huu upuuzi? Hospitali za rufaa zinatakiwa 24 hours zina specialists, za kwetu ati zina interns. Akili za wapi hizi? Wagonjwa wengi naamini zaidi ya nusu wanafariki sio kwa maradhi yanayowasumbua, hapana wanakuwa mismanaged. Hili linajulikana, mara intern mara mwanafunzi wa masters mara nurse mara huyu, mpaka mtu anakata roho anafanyiwa mizaha tu.

Hapo kwenye red umeeleweka mkuu. Chanzo cha tatizo la madaktari kubabaisha kina mizizi yake tokea namna serikali inavyochukulia maandalizi ya taaluma yenyewe ya udaktari na uendeshaji wa taaluma hiyo. Mnalaumu kwamba madaktari ni wazembe kazini na wana upungufu wa weledi wa kazi yenyewe mlishawahi kujiuliza kwamba chanzo kinaweza kuwa ni maandalizi mabovu ya wataalamu wetu? Kwani hao madaktari wa intern vuguvugu la mgomo lilianza vipi kama siyo kubabaishiwa pesa zao za kujikimu, zenyewe kiduchu tu? Vifaa vya kujifunzia na kufanyia kazi mahospitalini je? Kwa kifupi ni kwamba maandalizi bora ya daktari yatapelekea daktari bora katika huduma. Usione vya wenzako vyaelea, wameviunda.

Sasa swali la msingi, je ni dakatri au watumishi wa afya peke yao ndio wanaostahili maslahi mazuri tu eti kwa sababu kazi yake ni high risk job? Jibu lake ni HAPANA kubwa. Kila kazi yapaswa kuheshimiwa kwa maslahi sahihi, na hasa hasa kazi zile ngumu na zinazoboresha au kulinda maisha ya mwanadamu. Lakini niambie, ni Rubani gani analipwa laki 8 na wakimkata kodi zote ikiwemo ya loan board anarudi nyumbani na laki 4 ?? Aviation Services zote wana akili, wanafahamu kwamba usafiri wa anga ni delicate and "no room for error" nikitumia kauli yako, na ndio maana wanawalipa mishahara ya ajabu hao marubani na air hostesses/hosts wao, sio kama serikali yako inampa daktari na nesi wakati mgumu kweli kweli kiasi kwamba hata hiyo huduma kidogo wanayotoa ni kwa mapenzi na wito wa kazi yao na ndo maana wamevumilia sana kuisotea tangu wakisoma na hata mazingira magumu ya kufanya kazi.

Mbunge anaweza kuvumilia posho zake za vikao? Rais anaweza kuvumilia posho zake za safari? Kwa nini ni daktari tu ndie anapaswa kuvumilia maisha magumu?

Mimi binafsi si dakatri na wala sina ndugu yangu ninayemtetea, hat kazi ninayofanya si nzuri kivile lakini naridhika na hiki kidogo nilicho nacho kwa maana kazi yangu naiconsider "not a high risk job". Hivyo mimi binafsi hata maisha yawe magumu kivipi hutanisikia najitetea eti nipandishiwe mshahara. Nitapanda tu kwa kudra za mnyaazi. Lakini kwa daktari au nesi au huyo mtaalamu wa maabara au any job that a small error will cost your life, no, hawa ni lulu zetu tunapaswa kuwatunza. Ni serikali yako tu ndio hawana akili timamu kuona hilo. Mbona wao wakiugua wanakimbilia India? Wanafahamu daktari India analipwaje?
 
kweli uhuru wa kulalamika unautumia vizuri kaka, mala Amana, mala intern, mala pilot, tunaposema hili ni jukwaa la greater thinker hatumaanishi kuandika text ndefu iliyojazwa na mitizamo ya hisia, next time jipange kaka.

Ukipenda kusifiwa na kukosolewa ukubali pia. Hisia ndio huleta thinking perspective. Great thinker anayeona kusoma paragraph tatu ni kazi nafikiri hastahili kuitwa great thinker, labda lazy thinker. Lipi la uongo hapo? au unapenda niseme unachokitamani wewe ndio uridhike, sahau kabisa hilo. La ukweli tutalisema lilivyo. Na narudia tena ili uchukie zaidi, madaktari wanayo baadhi ya madai ya msingi, lakini pia wanayo matatizo makubwa ya kiutendaji yanayowahitaji wajirekebishe.Pili system nzima ya afya ni ya kufumua ili ipangwe vizuri, referal hospital zijulikane ni referal na sio sehemu ya kwenda kufanya mazoezi, period! kama hutaki ni juu yako. Wewe ndio ukajipange sio mimi.
 
Mimi binafsi si dakatri na wala sina ndugu yangu ninayemtetea, hat kazi ninayofanya si nzuri kivile lakini naridhika na hiki kidogo nilicho nacho kwa maana kazi yangu naiconsider "not a high risk job". Hivyo mimi binafsi hata maisha yawe magumu kivipi hutanisikia najitetea eti nipandishiwe mshahara. Nitapanda tu kwa kudra za mnyaazi. Lakini kwa daktari au nesi au huyo mtaalamu wa maabara au any job that a small error will cost your life, no, hawa ni lulu zetu tunapaswa kuwatunza. Ni serikali yako tu ndio hawana akili timamu kuona hilo. Mbona wao wakiugua wanakimbilia India? Wanafahamu daktari India analipwaje?

Mimi ndio maana nasema system nzima ina mapungufu na inahitaji overhaul, ukianzia kwenye training mpk kwenye kazi yenyewe kunahitaji marakebisho makubwa sana. Madaktari wana baadhi ya madai ya msingi kabisa, atakayekataa hilo atakuwa hana akili timamu. Wizara ya afya ina matatizo pia namna inavyoiendesha sekta husika na inachangia kwa kiasi kikubwa ufanisi mbovu kwenye utendaji wa watumishi wa afya.

Na mwisho, watendaji wenyewe, madaktari, wafamasia na wauguzi nao wana matatizo makubwa pengine just to blame wengi watasema ni mazingira ya kazi, lakini pia mengine ni ya binafsi, ethics za kazi hakuna, baadhi wamesomea udaktari wakifikiri ni fani kama biashara kumbe sio. Hilo lazima tulikubali, sio tutazame upande mmoja tu.
 
Huu mgogoro upo Kwa waziri mkuu, ameahidi kulishughulikia. Tungojee majibu.

Kuhusu wanashabikia serikali mjua hata madaktari wakiamua kufanya kazi Kwa kulazimishwa mtakao umia nyie ambao hamna uwezo wa kutibiwa iIndia.

Mi na familia yangu tunaenda India mwezi ujao Kwa ajili ya Health Check !

Kule India sasa hivi kuna Hostel ya watanzania imechukuliwa na Wizara ya afya Kwa ajili ya watu Kama sisi na familia zetu.
 
Mimi ndio maana nasema system nzima ina mapungufu na inahitaji overhaul, ukianzia kwenye training mpk kwenye kazi yenyewe kunahitaji marakebisho makubwa sana. Madaktari wana baadhi ya madai ya msingi kabisa, atakayekataa hilo atakuwa hana akili timamu. Wizara ya afya ina matatizo pia namna inavyoiendesha sekta husika na inachangia kwa kiasi kikubwa ufanisi mbovu kwenye utendaji wa watumishi wa afya.

Na mwisho, watendaji wenyewe, madaktari, wafamasia na wauguzi nao wana matatizo makubwa pengine just to blame wengi watasema ni mazingira ya kazi, lakini pia mengine ni ya binafsi, ethics za kazi hakuna, baadhi wamesomea udaktari wakifikiri ni fani kama biashara kumbe sio. Hilo lazima tulikubali, sio tutazame upande mmoja tu.
Okay, unafavor overhaul ya sekta ya afya, kwa upande wangu nafavor overhaul ya serikali nzima inayoongozwa na chama cha mapinduzi. Hakuna sekta hata moja inayofanya vizuri. Sekta ya uongozi wa serikali juu sera zake zinaboronga zinapelekea utendaji mbovu wa waalimu wa kada zote wanaoboronga kutengeneza wataalamu wa kada zote wanaoboronga kila sehemu katika utoaji wa huduma zao.

Madaktari ni nafuu. Kama madaktari wangeharibu kama sekta zingine za nchi basi wote hapa tungekuwa hoi au maiti tayari. Asilimia 99.99 ya watanzania wanazalishwa, wanachanjwa, wanapimwa magonjwa yote, wanatibiwa, kwenye zahanati zetu hizi hizi na hospitali zetu hizi hizi. Kitendo cha sisi kuwepo hapa, tukiwa hai, tunadunda tu, ni kitendo cha kumshukuru Mungu kwa huduma ya madaktari ingawa wanafanya kazi mazingira magumu.

Sekta zingine wanaharibu mpaka basi tu. Wengine wanavujisha mitihani huko wizarani mpaka ni kawaida sasa, wengine wanasheria na wanaongwa na mafisadi, wengine sekta ya fedha huko kwa Mkulo wamechoka kweli kweli. Wengine wapo kwenye madini lakini ndege zinaruka zimejaa vitofali vya dhahabu visivyojulikana idadi yake. Wengine wanasindikiza maliasili hai za nchi kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa zikotoroshewa ughaibuni. Wengine sijui hata wanafanya kazi gani hasa. Hivi hapo Ikulu, mkulu anafanya kazi gani hasa kwa hali ya maisha ilivyo?
 
Huyu mama ana matatizo sana. Sasa hivi hata wafanyakazi wake pale Wizarani wamechoka hadi wamechakaa. Anawafanyisha kazi hadi saa mbili usiku akiambiwa awalipe Extra duty allowance hataki anasema Wizara haina hela wakati yeye, wakurugenzi wake, Naibu Waziri na Waziri wanajilipa Utilities kila mwezi.

Siri imefichuka kumbe wanampikia majungu huyu mama kwa vile anawafanyisha kazi na wao wanataka wapate mshahara bila kufanya kazi!! Mama Nyoni usilegeze kamba kaza buti; lakini hakikisha hao Interns wanalipwa haki yao Hazina wanapotoa mgao!!
 
Ndugu zangu,

Hoja ya madaktari haina mshiko. kwa nini hawataki kufanyia mazoezi Singida, Mtwara, Kigoma, Lindi, Rukwa. Kwa nini wanakosa uzalendo kwa sababu za kijinga kabisa?? Halafu tunawatetea? Daktari wa uzoefu wa miaka kadhaa hawezi kum-mentor intern? Hii ni kweli? Wanataka wananchi tuwaelewe hivo kweli. Nadhani tufike mahali tuambiene ukweli, na siyo kusupport kila kitu ili muradi tu kiko kinyume na serikali. Siyo lazima Intern afundishwe practicing na specilist pekee anaweza kufundishwa kazi kivitendo hata na medical assistant ili muradi ana uzoefu wa kutibu wagonjwa.

Tatizo la wazi hapa ni kuwa madaktari hawataki kuja kuhudumia huku mikoani wanatunyanyapaa, kila daktari anataka afanye kazi hapo Dar es salaamu tu.

Tuamke tuwe wazalendo jamani.
 
kweli uhuru wa kulalamika unautumia vizuri kaka, mala Amana, mala intern, mala pilot, tunaposema hili ni jukwaa la greater thinker hatumaanishi kuandika text ndefu iliyojazwa na mitizamo ya hisia, next time jipange kaka.

We una tatizo nini? By Pax katoa hoja zenye mshiko. Tasnia ya afya na tiba ina matatizo makubwa sana Tanzania. Madaktari pamoja na kudai mambo wanayodai tunawaomba watende kile walichokisomea. Madaktari wengi wanafanya upuuzi sana, hawatendi wajibu wao na wakitenda wanataka malipo kwa wagonjwa. MOI tunalipa lakini bado kumwona daktari ni mbinde kuna hadi madalali wa madaktari pale. Sasa tunalipa kwa nini? Wacha kutetea uozo kwenye jamii.
 
Huyu mama si yule aliyewahi kuwa Ubalozini Canada? ni mhasibu huyu.

Iweje wizara ya Afya katibu wake mkuu kuwa Mhasibu? Je hakuna watu wa afya walioweza kushika wadhifa huo?

Poleni sana

inashangaza sana, hata mie nimejiuliza bila majibu
 
We una tatizo nini? By Pax katoa hoja zenye mshiko. Tasnia ya afya na tiba ina matatizo makubwa sana Tanzania. Madaktari pamoja na kudai mambo wanayodai tunawaomba watende kile walichokisomea. Madaktari wengi wanafanya upuuzi sana, hawatendi wajibu wao na wakitenda wanataka malipo kwa wagonjwa. MOI tunalipa lakini bado kumwona daktari ni mbinde kuna hadi madalali wa madaktari pale. Sasa tunalipa kwa nini? Wacha kutetea uozo kwenye jamii.
JF ni home of great thinkers.
Zebu tujiulize maswali yafuatayo:
Tz imeshatrain drs wangapi wa mifupa?
Wangapi wanafanya kazi hapa tz?
Hao wanaotibu wabotswana na wanamibia ni Kwa nini wameenda huko?
Nani mzalenda zaidi ni yule anayedai mshahara wake wa halali ambao uko kwenye mkataba au ni Yule anayeondoka kimya akiwaacha mkipigania wagonwa mamia kumwoma dr mmoja?
Kwa mtindo wa kuwaandalia nchi za nje drs ni lini drs Tanzania watatosha?
Nani anayeumia na Hali hii,je ni mwananchi wa kawaida, viongozi wa Wizara au drs ktk trend hii?
Vp kuhusu drs ambao wameona kazi hiyo hailipi na sasa wanafanya shughuli zingine Kama biashara,NGO etc Kwa mafanikio makubwa?
Je kila mtu anaweza kuwa dr, so long anataka au inabidi uwe na kauwezo kidogo ka kushika mambo kichwani?
 
Ile issue ilikuwa ni bifu la manesi na dactari manesi wakamchanganyia ma file ... Kazi ya surgeon ni kusoma file na kufanya upasuaji pale file inaposema afanyiwe .. wa Tanzania na waandishi wa habari uchwara mkambebesha lawama dactari ...

Mkuu huu ulioandika hapa hapa ni upupu kabisa!
 
Lula wa Ndali Mwananzela
Msiposimama pamoja, mtaangamia mmoja mmoja
TUKIO la hivi karibuni la Serikali kuamua kuwafukuza madaktari wanafunzi waliokuwa wanadai mafao yao mbalimbali na nyongeza za mafao hayo, linahitaji kulaaniwa na kuoneshwa kuwa ni la kibabe. Madaktari wa Tanzania yawezekana ndio madaktari wanaofanya kazi katika mazingira mabovu zaidi wakitarajiwa kuhudumia maisha ya wananchi huku wanasiasa wa nchini wakiishi maisha ya juu zaidi, wakijiaminisha kuwa wanastahili zaidi! Tujadili suala hili katika maeneo mahsusi kama ifuatavyo.

Tiba nchini India

Mojawapo ya vitu ambavyo vinaonesha dharau na kukosekana kwa heshima ya hadhi ya madaktari wetu ni hili la kupeleka wagonjwa India, kwa matibabu ambayo yangeweza kufanyika hapa nchini. Niliandika juu ya hili miezi michache iliyopita lakini yafaa nirudie.

Ningependa kujua kama viongozi serikalini wamewahi kukaa chini na kujiuliza swali jepesi (wengine wanaweza kuliita la kizushi) la ni kwa nini tunapeleka wagonjwa India na siyo kutibiwa hapa hapa nchini?

Jibu la swali hili lina pande mbili – upande wa kwanza wapo wanaodai kuwa gharama ya kutibiwa India ni nafuu zaidi kuliko nchini. Sijui kama kuna ukweli wa hili na ni nani aliyewahi kufanya utafiti wa kupima hili.

Ni kweli gharama ya nauli ya ndege kwenda na kurudi, chakula na malazi na mapumziko huko India ni ndogo kuliko kutibiwa hapa nchini?

Binafsi sitaki sana kuamini hili kwa sababu gharama inasababishwa na vitu mbalimbali, je, Serikali yetu imeshindwa kabisa kufikiria namna ya kufanya gharama ya afya kuwa nafuu hapa nchini? Na ni kitu gani kinafanya gharama iwe juu Tanzania ambacho hakiwezi kuangaliwa na kushughulikiwa?

Upande wa pili ni lile linalodaiwa ni ubora wa madaktari wa India. Wapo ambao wanaamini kuwa India ina madaktari wenye ujuzi mkubwa kuliko madaktari wetu. Watu wengi hawajui kuwa daktari wa Tanzania ili awe daktari kamili, anasomea kwa miaka saba wakati yule wa India anasomea miaka 5!

Madaktari wa Marekani nao wanasomea miaka saba! Na nchi nyingine zina tofauti ya kati ya miaka mitano hadi saba, huku hadi kuwa Bingwa inakuwa ni miaka karibu tisa ya mafunzo. Sasa ubora wa madaktari wa India unatokana na nini ambacho Tanzania haiwezi kukifanya?

Binafsi ningependa sana kuona chombo huru au taasisi huru kama walivyofanya watu wa taasisi za HakiElimu au Tunaweza, kwenye masuala ya elimu kupitia na kufanya ulinganifu wa madaktari wetu kulinganisha na India.

Nadharia yangu ni kuwa karibu vitu vyote vinavyofanywa India vinaweza kabisa kufanywa Tanzania. Watu wanapenda kwenda India kwa sababu zaidi ni hisia ya kuwa wanaenda “nje” kutibiwa.

Lakini nyuma ya hili ninaamini kuna hisia kuwa madaktari wa Tanzania hawaaminiki. Kuwa hawana uwezo – japo wanaweza kuwa wamesoma vizuri na hata kuzidi wale wa India na vile vile kuwa kutokana na maslahi yao duni hujikuta wakiendekeza taasisi zao binafsi zaidi kuliko kufanya kazi kwa weledi katika taasisi za ajira zao.

Hili la mwisho laweza kuwa na ukweli zaidi kwani wapo watu ambao wamewahi kujikuta wanaambiwa waende hospitali ya dokta kwa uangalizi zaidi. Lakini kwenye nchi ambayo maslahi ya daktari ni duni sana, daktari huyo afanye nini zaidi ya kujipatia kipato chake cha ziada pembeni?

Namfahamu Daktari mmoja (sasa Marehemu) ambaye alisomeshwa na fedha za Watanzania lakini baada ya kujitahidi kujitolea sana kufanya kazi ya udaktari aliona kuwa hailipi na matokeo yake alianzisha biashara yake ya baa na maduka na hadi anafariki, alikuwa ni Daktari wa cheo tu akikataa kabisa kurudi hospitali kutoa huduma. Wapo madaktari ambao udaktari ni sehemu tu ya kazi zao lakini wanapotengeneza fedha zaidi ni kwenye miradi yao mbalimbali.

Kutoboresha maslahi yao*ni kejeli kwa utu wetu

Ndugu zangu, ni kweli walimu ni muhimu (sitaki kuingia mjadala wa ‘nani bora kati ya daktari na mwalimu’) lakini katika kujenga taifa la kisasa na lenye watu wenye afya bora hakuna nafasi ya pekee kama ya madaktari.

Ni wao ndio wanatupa nafasi ya kuishi na kutumikia taifa tukiwa na afya bora zaidi. Ni watu ambao kutokana na ujuzi wa kazi zao na vipaji walivyojaliwa na Mwenyezi Mungu hujikuta wakiokoa maisha yetu (iwe katika ajali, magonjwa au dharura fulani).

Ni watu muhimu sana kiasi kwamba katika Wagiriki na Wayahudi wa kale uponyaji ulikuwa ni sifa ya kimungu. Waebrania walimuita Mungu Yehova Rapha (yaani Bwana Anayeponya) wakati Wagiriki walikuwa na mungu aitwaye Askelpias ambaye alikuwa ni mungu wa tiba na uponyaji. Kati ya mabinti zake mmoja aliitwa Hygeia (tunapata neno la Kiingereza Hygiene – usafi) na Panacea yaani “tiba ya magonjwa yote”. Ile fimbo yenye nyoka hujulikana kama fimbo ya Asklepias. Hivyo basi, madaktari si watu wa kudharauliwa au kufanywa duni.

Serikali inawaafanya madaktari wetu duni

Sizungumzii suala la kufukuzwa kwa hawa madaktari wanafunzi tu, nazungumzia jinsi tunavyowaangalia madaktari na kuwatendea. Ni kweli hatuwezi kuwalipa sana lakini ukweli ni kuwa kutokana na idadi yao, madaktari wanastahili kulipwa zaidi kwa ajili ya kuwavutia zaidi lakini vile vile kuwafanya wafanye kazi yao ambayo ni wito wao kwa kweli.

Unajua watu wengi hatuna wito wa kukaa na kufumua miili ya wanadamu, kuona uchafu wao na madamu yao na kuwapo pale kuwasaidia kurudi kwenye uzima au kuwasaidia wanapoelekea mauti. Ni wito wa ajabu sana ambao tusipoonekana kuuelewa tutaona kama “ajira nyingine tu”.

Daktari wa Tanzania anayeingia kwenye ajira tu asingelipwa chini ya mshahara wa kama dola 5,000 hivi kwa mwezi pamoja na mafao mengine. Ni lazima tumtoe huyu daktari kutoka kwenye miradi yake ya nyumbani na vibarua na kumhakikishia usalama wa maisha yake.

Hatuwezi kuwa na madaktari ambao ili wawahi hospitali kutoa huduma inabidi wadandie daladala au kununua gari mkweche. Haiwezekani leo tunajenga majumba ya wanasiasa lakini hatujawa na programu ya uhakika ya kuwajengea madaktari wetu nyumba za kudumu.

Hivi katika miradi yote ya Jiji la Dar es Salaam ni wapi wana mpango wa kujenga nyumba za makazi kwa madaktari? Huko mikoani ni wapi ambapo wana miradi ya kujenga nyumba za madaktari karibu na hospitali au kwenye maeneo ya kisasa ambayo yatawapa nafasi ya kupumzika na kutulia na kujifunza kabla hawajarudi kukimbia kuokoa maisha ya wananchi wetu?

Hivi watu wamewahi kujiuliza kuwa Tanzania ina madaktari wangapi? Katika Tanzania yetu hii ambayo watu wanaamini ina neema tuna daktari mmoja kwa kila watu kama 30,000 hivi. Marekani ina dokta mmoja karibu kwa kila watu 400 hivi. Sasa kweli tunaweza hata kufikiria kusimamisha madaktari wanafunzi zaidi ya 200 kwa sababu za kipuuzi – kwamba wamedai kuboreshewa maslahi yao? Kweli? Ni taifa gani ambalo tunajenga?

Yaani, wanasiasa wanaweza kujiongezea posho bila kuhojiwa na yeyote tena kwa asilimia zaidi ya 300, lakini hawa madaktari wetu hata ‘kiduchu’ wanachodai imekuwa ni nongwa? Hivi, kuna mwanasiasa wa CCM anayeweza kusimama na kutuambia akiwa na macho makavu kuwa madaktari wa Tanzania wanalipwa vizuri na mazingira yao ni bora?

Huyu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (wa CCM) aliyedai kuwa wamejiongezea posho kwa sababu maisha ni magumu Dodoma alikuwa hafikirii kuwa huko Dodoma nako kuna madokta? Nani atawapigania madaktari wetu?

Naomba nitoe taarifa mbaya - madaktari wa Tanzania hawatopiganiwa na wanasiasa wetu! Wanajidanganya wale madaktari waliokaa Wizara ya Afya na ambao wanaishi maisha ya furaha kwa sababu wanakula na wakubwa! Hawa madaktari waliotupwa porini huko Katavi, Bukoba, Mbeya na sehemu nyingine waishi kwa kuombea kudura (kudra) tu! Hawana mtetezi. Na bahati mbaya sana hata vyama vyao haviwezi kuwatetea.

Kuna wakati, madaktari lazima wasimamie maslahi yao kwani kwa kufanya hivyo watasimamia maslahi ya wagonjwa wao na wale watumishi wa afya wa kada nyingine. Na kuna namna moja tu ambayo italazimisha watawala wetu kuangalia maslahi ya madaktari na kuwarudisha mara moja wale wanafunzi na kuhakikisha kuwa madaktari wa Tanzania wanapewa heshima na hadhi wanayostahili – mgomo.

Mimi si shabiki wa migomo ya aina hii lakini tulipofika sasa inaonekana hoja hazitoshi kuwashawishi watawala kufikiri. Mgomo siyo wa kukataa tu bali pia wa kudai kile kinachowezekana.

Kama taifa linaweza kutenga posho ya karibu bilioni 28 kwa watu 350 hivi na wakahalalisha inawezekana, nina uhakika taifa hilo hilo lina uwezo wa kutenga kiasi kikubwa tu cha fedha kuboresha mishahara na posho za madaktari karibu 2,000 tu ambao tunao!

Mgomo ni njia pekee na sahihi ya kutuma ujumbe wa kisiasa ambao umeshindikana kupokewa kwa njia za kidemokrasia na mazungumzo. Mazungumzo yamefanywa miaka nenda rudi lakini bado watawala wetu wanaona kama wanasumbuliwa na ‘madai’ ya madaktari.

Nasema madaktari hamna cha kupoteza isipokuwa utu wenu na hadhi yenu kama waponyaji. Mtaendelea kudharauliwa, kunyanyasika na kudhulumiwa huku na ninyi mkitamani muwe wanasiasa!

Si mmewaona madaktari wenzenu walivyoingia siasa wanavyonona. Hamna mtetezi wala wa kuwapigania isipokuwa ninyi wenyewe! Tangazeni mgomo na simameni pamoja mtasikilizwa. Msiposimama pamoja, mtaangamia mmoja mmoja!

Source: Raia mwema.
 
Wizarani anaitwa Asha Ngedere. Alivyostukia hilo jina akaitisha kikao cha wafanyakazi wote akapiga mkwara wa kufa mtu. Akaweka ma spy wake kumpa udaku.

Technic zake za uongozi ni za kizamani sana. anabana matumizi kwa wenzake wakati yeye anatumbua. Anaendekeza majungu, ubabe usio na msingi, hashauriki. Mchana hizurula na anaingia ofisini saa 12 jioni na kuwaweka watu hadi aondoke. Anaweza kukupigia simu saa 2 usiku urudi ofisini anakuhitaji. ukifika anakuuliza kitu ambacho wala hata siyo urgent.

Ana frustration za maisha, nyumbani kwake hakukaliki. Aliivuruga maliasili hadi ikapoteza mwelekeo.

Wewe inaonekana ni mtumishi wa Wizara ya Afya alafu ni mvivu wa kufanya kazi ila ni mpenda posho. Mama nyoni anafahamika kwa kupiga kazi. Kama bosi wako yupo ofisi mpaka usiku kwann ww kidampa uondoke nyumbani? Acha majungu ww.
 
Mkuu,

Labda ungesema hao ni ma surgeons wa Tanzania tu na hata hivyo bado nina mashaka na majibu yako.

Mfano yule Dr.Masau wa THI ni cardiosurgeon, sivyo? Kwahiyo Dr. Masau yeye hana shughuli nyingine,isipokuwa ni kupokea watoto ambao tayari wanakuwa diagnosed na heart defects na kuwafanyia upasuaji tu.Dr.Masau hajasomea kujua dalili wala kumfanyia uchunguzi mtoto aliyezaliwa na ugonjwa wa moyo na wala hapaswi kufanya hivyo maana yeye kazi yake ni kusoma file la mgonjwa na kupasua tu.

Dr.Masau akiletewa mtoto mwenye tatizo la moyo,hana sababu ya kuchukua historia na kumfanyia uchunguzi kwanza ili kujua tatizo hasa ni nini,isipokuwa yeye hukubaliana tu na report ya daktari aliyemu attend yule mtoto na ku recommend upasuaji wa moyo.

Sitaki kuamini kuwa hivi ndivyo wanavyofanya kazi ma surgeons wetu. Vinginevyo basi tuna tatizo, tena kubwa sana!

Mkuu big up, umemjibu vizuri huyo njiwa, inaonekana hajui anachoongea kabisa. Anavyoelezea kana kwamba surgeon ni kama mchinjaji tu!
 
JF ni home of great thinkers.
Zebu tujiulize maswali yafuatayo:
Tz imeshatrain drs wangapi wa mifupa?
Wangapi wanafanya kazi hapa tz?
Hao wanaotibu wabotswana na wanamibia ni Kwa nini wameenda huko?
Nani mzalenda zaidi ni yule anayedai mshahara wake wa halali ambao uko kwenye mkataba au ni Yule anayeondoka kimya akiwaacha mkipigania wagonwa mamia kumwoma dr mmoja?
Kwa mtindo wa kuwaandalia nchi za nje drs ni lini drs Tanzania watatosha?
Nani anayeumia na Hali hii,je ni mwananchi wa kawaida, viongozi wa Wizara au drs ktk trend hii?
Vp kuhusu drs ambao wameona kazi hiyo hailipi na sasa wanafanya shughuli zingine Kama biashara,NGO etc Kwa mafanikio makubwa?
Je kila mtu anaweza kuwa dr, so long anataka au inabidi uwe na kauwezo kidogo ka kushika mambo kichwani?

Mkuu hayo mengine inawezekana ukawa na hoja yenye msingi,lakini hapo nilipo bold umekosea.Uzalendo haupimwi kwa kuishi Tanzania au nje ya Tanzania.Naamini kuna wengi tu wanaishi nje ya Tanzania lakini ni wazalendo wakubwa na wana mchango mkubwa katika ujenzi wa taifa hili.Naamini pia kuna wengi tunaishi Tanzania lakini hatuna uzalendo wowote na ndiye tunaoiharibu hii nchi na kufanya wengi wasinufaike na rasilimali na malighafi tulizojaaliwa
 
Back
Top Bottom