Mgomo wa Madaktari hautaisha kwa vitisho na Dola; ni kwa Makubaliano tu!

Kwanza huu n mgomo ambao ungeweza kuepukika mapema kweli lakini hapa ulipofikia si pazuri kabisa.

Mwanakijiji,

Tupo ukurasa mmoja. Mie naona mgomo ulipofikia ndio pazuri kwani tunakaribia apex ya ukombozi wa kifikra kwa watanzania wote. Come 2015 (kama watafika maana wengine wanaweza kuwa Hague kama Gbagbo) kila kura italindwa kwa hali na mali. Kwenye kampeni inakuwa ni kuwakumbusha kuhusu ndugu zetu waliokufa kutokana na uzembe wa viongozi wao waliowaamini kwa miaka 50+.
 
RichardBrunwick
26 January 2012 2:33PM
Tanzania's Kikwete is one of the most pathetic African leaders of our times. He is a peacetime leader for a country known to be one of the richest in the world in terms of natural resources, yet he leades the world with begging. Foreign companies have known Tanzania to be a free land in which you can go in and take all you can without being asked a question. I really don't get the mind set of its leaders especially their prsident Mr. Kikwete, a Muzungu worshiper. Having worked with the UNDP in that country for 8 years, I realized how inneficient and corrupt the country's leadership is. His ministers that requested bribes from BAE have never been tried despite the damning evidence against them. British TAX payers must stop funding this man's corruptin and foreign trips. His human rights record is horrible. Mr. Kikwete had no business of going to Davos to ask for foreign aid. Already his country is the world third leading foreign Aid dependant nation. He should be embarassed to say to the world that people are poor. His people living "hand to mouth " is his own is own ignorance and stupidity.That is hiw own problem, Brits are having their own problems he must realize that. We cant bankroll his foreign trips. He should make good use of his country's wealth. Instead of letting his corrupt officials and foreigners loot his country, he needs to think before letting himself be a global loughing stock. I read in one of the regional (kenyan) publication the mockery nature related to his frequent foreign trips. Palestinian, Haiti, Lebanon, Somalia and even Rwanda economies are more robust that of Tanzania. We must question the nations that welcomes this "Joker's" request for AID. He needs to be on a "no-fly" list so he can be serious. Hopefully the billionaires questions what he has done with the Money he has received for decades. The Arab spring should turn into the African summer and get rid of the Kikwete. likes
(http://www.guardian.co.uk/discussion/comment-permalink/14344505)

Daaah..!! Haya matusi sasa!
 
Nimeisikiliza hotuba ya waziri mkuu kuhusu mgomo wa madaktari kama mtiririko wa matukio ni ule aliyoeleza waziri mkuu, waziri mkuu ame'missimage mgogoro huo.

Kasoro ya 1: yalikuwa ni makosa makubwa kukubali kuongea na madaktari zaidi ya mia nne (400) kwa sababu sio rahisi kupata suluhu ya mvutano katika mkusanyiko wa watu mia nne, yeye angekubali kuongea na wawakilishi.

Kasoro ya 2: ni kutoa majibu ya mkato tuu kuwa madai ya nyongeza ya tshs3,000,000/= hayawezekani. Nakubaliana na madai ya nyongeza ya mshahara toka tshs.900,000/= hadi tshs.3,000,000/= ni unrealistic lakini angewauliza hao madaktari wametumia vigezo vipi kufikia ongezeko la madai ya zaidi ya 300%, inawezekana madaktari walijiropokea tu, angewauliza vigezo wangejiona hawana hoja. Pia angewaeleza financial implications za madai yao kitaifa , madaktari ni watu wenye vipaji vya akili ya juu na ni waelewa wangemwelewa. Majibu yaliyotelewa ya mkato hayakuwa ya kutafuta mwanzo wa mazungumzo ya kutafuta mwafaka. Hapa pia ni upungufu wa kutafuta mwafaka.

Kasoro ya 3: madaktari pia walitaka walipwe risk allowance, hili lingeweza kutolewa ufumbuzi, wangeambiwa wa classify hizo risks kwa sababu siyo wote wana risk zinazofanana, kukubali hili lingewapa muda wa kutafakari na pia lingeweza kuwagawa na kupunguza makali, hapa sielewi ilipataje kigugumizi . madaktari pia walitaka walipwe hardship allowance hili pia halina utata, mbona wafanyakazi wengine wanaopelekwa mfano kasulu, kibondo n.k wanalipwa kwanini isiwe madaktari? Hapo waziri mkuu amewapotosha wananchi.

Kasoro 4: madaktari walitaka wapewe au wakopeshwe magari, hapa sioni utata. Serikali ingewakopesha kwa awamu na wengine wangelipwa transport allowance, kuna mashirika ya Umma karibu yote hapa nchini yanatoa transport allowance kwa wafanyakazi wao kufuatana na vigezo mbali mbali.

Kasoro ya 5: waziri mkuu ameshindwa kutoa majibu ya madai ya nyumba kwa madaktari. Naamini madaktari sio vichaa, siamini wangetegemea wapewe nyumba siku ya pili yake. Wangepewa housing allowance ambazo mashirika mengi ya umma hapa nchini wanatoa kwa wafanyakazi wao. Sidhani km ingekuwa mgogoro.

Kasoro ya 6. Kwamba madaktari walitaka madai yao yatekelezwe mara moja. Hii tafsiri kwa waziri mkuu ni kama AMRI au DHARAU, madaktari walitaka makubaliano sio utekelezaji ufanyike siku hiyohiyo moja, au wajenge nyumba siku hiyo hiyo, hili lingeweza kuongelewa bila viongozi kujiona wamedhalilishwa.

Kasoro ya 7: waziri mkuu kugusia maslahi binafsi ya madktari kama yalivyoainishwa kwenye madai yao bila hata kugusa mazingira ya kazi na vitendea kazi kama walivyoainisha kwenye madai yao, hapo waziri mkuu alikuwa na lengo la kuwagombanisha madaktari na wananchi.

Mwisho kabisa ni kuwapiga marufuku wasikutane popote. Serikali imewafukuza kazi hii inatosha, wasikutane popote hii inatoka wapi na kwenye katiba ipi, huu ni ufashist.
 
kwenye heading nilitaka niweke MGOGORO WA MADAKTARI-WAZIRI MKUU AMETELEZA, mods mnaweza mkanisaidia.
 
Mods unganisha hii thread ya madaktari na zingine zimeishakuwa nyingi.
 
Jamii, Mbuge ni mtu yeyote ambaye hana hanafani yeyote, ila kwa swala la madaktari hawa sio watu wa ovyo ovyo lazima awe na UJUZI,So ina kuaje wabunge waongezewe mshahara na watu wanaoshika vinyes,mikojo ,damu na hata wanao jali afya zetu,hawaongezewi risk allawance na mambo mengne kama hayo.
 
Jamii, Mbuge ni mtu yeyote ambaye hana hanafani yeyote, ila kwa swala la madaktari hawa sio watu wa ovyo ovyo lazima awe na UJUZI,So ina kuaje wabunge waongezewe mshahara na watu wanaoshika vinyes,mikojo ,damu na hata wanao jali afya zetu,hawaongezewi risk allawance na mambo mengne kama hayo.
kinachokosekana kwa viongozi wetu ni busara, wao kila kitu wanaingiza siasa, wanakurupuka kutoa majibu mepesi kwenye maswala mazito yanayohusu uhai wa mtanzania.
 
Nimeisikiliza hotuba ya waziri mkuu kuhusu mgomo wa madaktari kama mtiririko wa matukio ni ule aliyoeleza waziri mkuu, waziri mkuu ame'missimage mgogoro huo.

Kasoro ya 1: yalikuwa ni makosa makubwa kukubali kuongea na madaktari zaidi ya mia nne (400) kwa sababu sio rahisi kupata suluhu ya mvutano katika mkusanyiko wa watu mia nne, yeye angekubali kuongea na wawakilishi.

Kasoro ya 2: ni kutoa majibu ya mkato tuu kuwa madai ya nyongeza ya tshs3,000,000/= hayawezekani. Nakubaliana na madai ya nyongeza ya mshahara toka tshs.900,000/= hadi tshs.3,000,000/= ni unrealistic lakini angewauliza hao madaktari wametumia vigezo vipi kufikia ongezeko la madai ya zaidi ya 300%, inawezekana madaktari walijiropokea tu, angewauliza vigezo wangejiona hawana hoja. Pia angewaeleza financial implications za madai yao kitaifa , madaktari ni watu wenye vipaji vya akili ya juu na ni waelewa wangemwelewa. Majibu yaliyotelewa ya mkato hayakuwa ya kutafuta mwanzo wa mazungumzo ya kutafuta mwafaka. Hapa pia ni upungufu wa kutafuta mwafaka.

Kasoro ya 3: madaktari pia walitaka walipwe risk allowance, hili lingeweza kutolewa ufumbuzi, wangeambiwa wa classify hizo risks kwa sababu siyo wote wana risk zinazofanana, kukubali hili lingewapa muda wa kutafakari na pia lingeweza kuwagawa na kupunguza makali, hapa sielewi ilipataje kigugumizi . madaktari pia walitaka walipwe hardship allowance hili pia halina utata, mbona wafanyakazi wengine wanaopelekwa mfano kasulu, kibondo n.k wanalipwa kwanini isiwe madaktari? Hapo waziri mkuu amewapotosha wananchi.

Kasoro 4: madaktari walitaka wapewe au wakopeshwe magari, hapa sioni utata. Serikali ingewakopesha kwa awamu na wengine wangelipwa transport allowance, kuna mashirika ya Umma karibu yote hapa nchini yanatoa transport allowance kwa wafanyakazi wao kufuatana na vigezo mbali mbali.

Kasoro ya 5: waziri mkuu ameshindwa kutoa majibu ya madai ya nyumba kwa madaktari. Naamini madaktari sio vichaa, siamini wangetegemea wapewe nyumba siku ya pili yake. Wangepewa housing allowance ambazo mashirika mengi ya umma hapa nchini wanatoa kwa wafanyakazi wao. Sidhani km ingekuwa mgogoro.

Kasoro ya 6. Kwamba madaktari walitaka madai yao yatekelezwe mara moja. Hii tafsiri kwa waziri mkuu ni kama AMRI au DHARAU, madaktari walitaka makubaliano sio utekelezaji ufanyike siku hiyohiyo moja, au wajenge nyumba siku hiyo hiyo, hili lingeweza kuongelewa bila viongozi kujiona wamedhalilishwa.

Kasoro ya 7: waziri mkuu kugusia maslahi binafsi ya madktari kama yalivyoainishwa kwenye madai yao bila hata kugusa mazingira ya kazi na vitendea kazi kama walivyoainisha kwenye madai yao, hapo waziri mkuu alikuwa na lengo la kuwagombanisha madaktari na wananchi.

Mwisho kabisa ni kuwapiga marufuku wasikutane popote. Serikali imewafukuza kazi hii inatosha, wasikutane popote hii inatoka wapi na kwenye katiba ipi, huu ni ufashist.

yaani PM hataki kujua kitu inaitwa freedom of assembly,ambapo kwa kufanya hivyo anapingana kabisa na human rights
 
Hii thread ikiunganishwa na nyingine watu watashindwa kupata huu uchambuzi mzuri!!!

Ukweli ni kuwa madaktari wameanza na 3,000, 000 ili wakienda kwenye bagaining walau wanaweza kupata 1.5 m. Sasa serikali inaanza kupoliticise huu mgomo kwa vile wanajuwa ukuiendelea sana unaweza ukabadilika na kuwa wa kisiasa. Kumbuka Tunisia revolution ilianzishwa na machinga moja tu.

Twist nyingine inakuja, serikali inajua kuwa kama itakubali madai yote ya madaktari ............ next watakuwa nurses.................... then Lecturers na baada ya hapo makunguru (Waalimu). Kwa hiyo serikali itakomaa na kujaribu kuwamaliza nguvu taratibu. Nafikiri by the end of next week Rais atakuwa ameshawaita wazee wa CCM kupiga propaganda.

All in all posho ya wabunge imezua mambo!! Pamoja na madai ya madaktari kuwa ya msingi.... Je serikali ina pesa za kumudu hivyo viwango??
 
Mzee MMNakushukuru kwa ulivyojitahidi kuweka mpangilio Mzuri wa hii mada. Nakuomba iwekwe kwa Mwanahalisi kama hajafunga. Nilishasema. Pinda is a govt boy. For all his life amezoea kutoa amri kwa Askari wa chini yake. Umefika muda wa kuondoka hata Kenya wamevumilia mgomo wa Madaktari for almost 2weeks na hawakuwafukuza. Hatuna Madaktari sasa ukifukuza hata hao 200 interns ni wengi. Nashauri mazungumzo! Hao wanajeshi wanalipwa shillingi ngapi?
 
I agree with your points. You are a real great thinker . You are over Jk and Tha son of the farmer.
 
Nianze kwa kusema: Ninaogopa sana kama kweli madactari watarudi kazini kwa vitisho kwa necha ya taaluma yao na kazi wanayoifanya kwa sababu moja tu ya “hofu ya kupoteza kazi” Hili likitokea Madactari hawa watakuwepo kazini lakini morali yao ya kufanya kazi itakuwa imepotea kabisa na hili linaweza kupelekea “Mgomo baridi” ambao kwangu nauona ni hatari zaidi kuliko mgomo unaoendelea sasa.


Athali za matumizi ya ubabe katika mambo ya msingi Tumeona mfano mara baada ya kuzuwia kwa vitisho kwa mgomo wa waalimu hapa nchini, matokeo yake ni kwamba walimu wanakwenda shuleni kama wajibu lakini hawatekelezi kazi ipasavyo na kimsingi huu ni mgomo baridi ambao bado unaendelea matokeo yake wanafunzi wanamaliza elimu ya msingi lakini hawajui kusoma, kuandika wala kuhesabu. Wapo wanafunzi wa darasa la tano lakini hawawezi kujibu mtihani wa darasa la pili. Utafiti uliofanywa na Uwezo Tanzania Uwezo.net


Serikali imechukua hatua gani juu ya tatizo la kufeli kwa wanafunzi? Naamini wote hapa ni wafuatiliaji wazuri wa habari, zifuatazo ni baadhi ya hatua ambazo serikali imezichukua ambazo si kati ya kelo zinazolalamikiwa na walimu:


1. 1. Matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi yamepigwa marufuku
2. 2. Waziri wa elimu anasema wanafunzi waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza watapimwa tena kabla hawajaanza sekondari na atakayefeli mkuu wake wa shule atawajibishwa
3. 3. Mtihani wa kidato cha pili umerejeshwa
4. 4. Michango ya masomo ya ziada imepigwa marufuku

NOTE:

Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2010 kati ya wanafunzi 353840 waliofanya mtihani huo ni wanafunzi 40,388 tu ndio waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu.


Kwa upande wa Madactari Sasa tujiulize, kama madactari nao watarudi kazini na kuendesha mgomo baridi watanzania tutakuwa kwenye wakati gani? Ni bora ya sasa kila mtu anajua wamegoma hivyo anakwenda kwenye hospitali binafsi lakini katika mgomo baridi hatutajua madactari wanaweza wakawepo na wakatupa matibabu tofauti yatakayopelekea athari mbaya kwa wananchi. Lakini pia Tanzania haina madactari mbadala wa kujaza nafasi za madactari hawa ikiwa wataondolewa kazini kama inavyosemwa. Siamini kama matumizi ya mabavu yatalete suluhu katika jambo hili na mwisho wa siku wanaokuja kuumia ni masikini waliopewa jina “WATANZANIA WA KAWAIDA”
 
Serikali inakwenda kuiua kabisa sekta ya afya kama walivyoiua sekta ya elimu, Elimu ya Tanzania ilishakufa na sababu ni hizi hizi za kutoa vitisho kwa watumishi. Matokeo yake ni wanafunzi kumaliza la saba hajui hata kusoma na kuandika. Sasa janga hilo linaenea hadi sekta ya afya, watakuja kugundua baadae. Hapa ni wananchi kubadiri fikra zao wakati wa kuchagua viongozi, wasifanye kwa mazoea, lasivyo wataendelea kuteseka huku viongozi wao wakistarehe.
 
sasa nimeanza kuamini.the only way foward ni kwa serikali kushuka na wala haitamaanisha imeogopa,maana yake itatafsrika kuwa serikali inasikiliza wananchi wake.
 
Madaktari nanyi tuambieni mmetumia vigezo gani kufikia hiyo 3,000,000 plus other fringe benefits ambazo mwisho wa siku sitafikia karibu 5,000,000/=
1. Hamuoni kuwa Polisi nao wanastahili kupata mshahara kama huo maana wao wanahatarisha maisha yao binafsi na maisha ya wale wanaolindwa na hao askari?
2. Hamuoni askari magereza nao wanahitaji mshahara kama huo maana kazi wanayofanya kulinda wahalifu ni hatari na inawafanya wafanane na hao wafungwa?
3. Hamuoni walimu nao wanahitaji mshahara kama huo maana uhuru wao wa kuomba rikizo muda wanaotaka kama ninyi mfanyavyo wamenyang'anywa kwa kigezo kwamba wakienda kipindi cha madarasa wanafunzi hawatapata elimu?
4. Hamuoni kuwa uhamiaji nao wanahitaji mshahara kama wenu maana wanafanya kazi hatari ya kuhakikisha nchi hii haipati wageni wasio rasmi hivyo kukulinda wewe na wenzako dhidi ya wageni wa aina hiyo?
.
.
.
.
.
Kitendo walichofanyiwa interns si cha kiungwani. Ingekuwa vema kama mngeendelea na hoja zenu za kushinikiza Mponda, Nkya, Nyoni na Mtasiwa wafukuzwe. kwa kufanya hivo mngeonyesha usomi na weledi!! ila mambo mnayodai ni ubinafsi ambao hauna tofauti na ule ubinafsi wa Wabunge!!!
Kwanza mnaposema kazi na kutibu mgonjwa ni hatari kwa afya yako nami ntasema kazi wa kuwasha mtambo wa kahansi au kulinda majambazi gerezani ni hatari. Lakini hatari hizo zoote nlizozitaja zinaondolewa na mafunzo nyote mlopata kwa kazi husika kwa hiyo msije na visingizio vya hatari!!!
BADALISHENI MAUDHUI YA MGOMO WENU AU RUDINI KAZINI!!!!!!!!!!!!
 
Mzee Mwanakijiji,
Niseme mathlan unakubaliana na madai ya madaktari..mimi siyajui vizuri zaidi ya yale yaliyowekwa hapa JF..nakuomba wewe kama serikali au waziri mkuu ni yapi utakubaliana nayo na yapi hutakubaliana nayo na kwa kufanya nini?. Ili madaktari warudi kazini ni mazingira gani ya kazi utayabadilisha kulingana na madai yao.
 
Back
Top Bottom