Mgomo mwingine wa madaktari hautakubalika!

wewe hiyo serikali yako unayosema inafanya kazi kwa utaratibu wake nani aliwaambia watoe ahadi Wakijua hawatatekeleza??si wangeomba muda mrefu siku waliyotuomba turudi kazini?its ppl like you who choose stupid leaders kama hawa tulionao....
 
Hatua yoyote ile ya kugoma kutoa huduma kwa WATANZANIA wasio na hatia haitakubalika. Kwa sasa watanzania tutalaani na kupinga action yoyote kwa madaktari wanayokusudia kuchukua. Hatua hiyo ni kama uhaini kwa kukusudia kuua raia wema wanaokamuliwa kodi kwa kusomesha na kuwalipa mishahara wataalamu. Tunaamini bado kuna nafasi ya kukaa na kupata muhafaka kupitia meza ya majadiriano bila kuilazimisha, kuisulutisha na kuiwekea mashariti ya kuidhalilisha serikali eti kwa kwa kigezo ni kada muhimu. Serikali ina utaratibu wake ambao inapaswa uheshimiwe na watu wote kwa mujibu wa katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Pia tunatoa mwito kwa serikali kuheshimu taaluma za wataalamu wetu kwa kuwapatia vitendea kazi na maslahi yanayokidhi taaluma husika. Suala la kada ya afya lishughulikiwe kwa ujumla wake kwa kuzingatia wataalamu wote waliopo katika kada hiyo bila kuwabagua maana wanategemeana bila kusema Daktari ni bora zaidi, kinyume na hapo ni kuzalisha Crisis nyingine ndani ya kada ya Afya kwa kusababisha chuki kati yao na mgomo baridi utakaoleteleza kuzorotesha huduma ya Afya. Hatua kwa hatua na kwa kasi, Serikali iboreshe maslahi kwa watumishi wake, maana tukisema Sekta ya Afya ni muhimu zaidi, je Walimu wanaopigana kuondoa ujinga na kuzalisha hao wataalamu wa Afya wao si ni bora zaidi? SERIKALI ISIJIINGIZE KATIKA MTEGO WA KUONA KADA NYINGINE NI BORA ZAIDI KWA MAANA KADA ZOTE ZINATEGEMEANA! Mfanyakazi wa TRA si bora zaidi, kuliko mtaalamu wa Afya za Mazingira, Mkemia au mhandisi, Mwanajeshi si bora zaidi Kuliko Daktari, na wala Daktari si bora zaidi kuliko Mwalimu, na Wala WABUNGE si bora kuliko watu wengine. Na kinyume chake ni hivyo hivyo. Tofauti inayoweza kujitokeza, madharani ni kwa kuhamasisha wanafunzi wengi wapende masomo ya Sayansi, hivyo ili linaweza kufanyika kwa wataalamu wa sayansi kupewa motisha na hata ikibidi nje ya mishahara yao. lakini suala la mishahara lazima liwe na kanuni ya uwiano.
Changamoto ninayoitoa kwa serikali kwa siku za mbeleni na kwa hatua za haraka zaidi, pelekeni kwa wingi wataalamu wa kada ambazo zina impacts za moja kwa moja kwenye maisha ya binadamu katika vyombo vya usalama kama vile jeshini, usalama wa Taifa, police na vinginevyo kwa ajili ya emergency wakati wa dharula. Lakini pia maslahi ya wataalamu wetu lazima yaboreshwe.

Nasilisha kwa maslahi ya Taifa

This is the problem of drinking red wine or beer with breakfast instead of milk - Ukikua utaacha
 
Kbindi unaifanya JF windvane?
Usikute hujuma wanazofanyiwa madaktari wewe kwako faida!
 
Nyinyi mshambulieni huyo Kibindi left and right, lakini mimi nauliza hivi hawa madaktari si wamesomeshwa kwa fedha zetu sisi walipa kodi wa nchi hii?

Nyinyi munaoshangiria mgomo nyote ndiyo munaokwenda hospitali za binafsi kwa hivyo hamuathiriki na huo mgomo hata ukiendelea kwa mwaka mzima.

Ila musiwasahau wale waliokufa kwa kukosa huduma.
 
nyinyi mshambulieni huyo kibindi left and right, lakini mimi nauliza hivi hawa madaktari si wamesomeshwa kwa fedha zetu sisi walipa kodi wa nchi hii?

Nyinyi munaoshangiria mgomo nyote ndiyo munaokwenda hospitali za binafsi kwa hivyo hamuathiriki na huo mgomo hata ukiendelea kwa mwaka mzima.

Ila musiwasahau wale waliokufa kwa kukosa huduma.

nimechoshwa na hizi kauli ma dr wamesomeshwa na walipa kodi!!?hivi hujui hata madactari wanalipa kodi!
 
mtaandika mtachoka! lakini watu wenye akili hawatasupport mgomo wenu! sikatai mudai maslahi yenu, lakini si kwa kutoa uhai wa Watanzania wasio na hatia na kujiona bora kuliko wengine! nyie mna vyama vyenu TMA na TUGHE ina maana vyote vimeshindwa kuzungumza na Serikali? basi anzieni hapo mviwajibishe kama havifai viondoeni! tunapashwa kuheshimu binadamu wenzetu wasiyo na uwezo wa kutibiwa Hosp za binafsi na kuepuka kuwafanya chambo. Haya ni mawazo yangu na wala sitoi mawazo kwa kufuata mkumbo hata kama nitapingwa na wachangiaji wote lakini lazima nisimamie kile ninachofikiri ni sahihi.MGOMO HAPANA NA HAPANA! TUTAWAPINGA KWA NGUVU ZOTE!
 
mtaandika mtachoka! lakini watu wenye akili hawatasupport mgomo wenu! sikatai mudai maslahi yenu, lakini si kwa kutoa uhai wa Watanzania wasio na hatia na kujiona bora kuliko wengine! nyie mna vyama vyenu TMA na TUGHE ina maana vyote vimeshindwa kuzungumza na Serikali? basi anzieni hapo mviwajibishe kama havifai viondoeni! tunapashwa kuheshimu binadamu wenzetu wasiyo na uwezo wa kutibiwa Hosp za binafsi na kuepuka kuwafanya chambo. Haya ni mawazo yangu na wala sitoi mawazo kwa kufuata mkumbo hata kama nitapingwa na wachangiaji wote lakini lazima nisimamie kile ninachofikiri ni sahihi.MGOMO HAPANA NA HAPANA! TUTAWAPINGA KWA NGUVU ZOTE!

Inabido tu serikali itumie akili kwani kuwafukuza kazi Mponda na Nkya kuna athari gani mpaka kuwe na mashinikizo kiasi hicho.
 
nimechoshwa na hizi kauli ma dr wamesomeshwa na walipa kodi!!?hivi hujui hata madactari wanalipa kodi!

Wewe choka lakini ndiyo ukweli ulivyo. Kwanza nyinyi munapewa misamaha kibao ya kodi. Pili hiyo kodi yenu munayolipa inaweza kusomesha wangapi wengine bila ya kuchanganywa kwa asilimia kubwa na ya kwetu munaotunyanyasa?

Ndiyo hasara ya 'bure' hiyo lazima usumbuliwe. Ingekuwa sote tunalipia elimu tusingewasema kwa hilo
 
Siwaungi mkono madaktari..

Siwaungi mkono madaktari...kabisa

Watafute njia mbadala na siyo kususa kuhudumia mgonjwa ambaye hana hatia..

Daktari kwa taalum anamtibu hata gaidi akifika hospitalini itakuwa akina mama, watoto, na yatima?

Tsh. ngapi itatosha tuwalipe??? (tutawapa milima ya dhahabu binadamu hatosheki)

Swala si pesa ni professionalism period
 
Nyinyi mshambulieni huyo Kibindi left and right, lakini mimi nauliza hivi hawa madaktari si wamesomeshwa kwa fedha zetu sisi walipa kodi wa nchi hii?

Nyinyi munaoshangiria mgomo nyote ndiyo munaokwenda hospitali za binafsi kwa hivyo hamuathiriki na huo mgomo hata ukiendelea kwa mwaka mzima.

Ila musiwasahau wale waliokufa kwa kukosa huduma.

Sote tunatumia Hospitali za Serikali, yaani huduma ni mboovu, mazingira ni machafu, hakuna dawa.

Nchi yetu ina uwezo wa kutoa huduma za afya nzuri na hakuna sababu ya kupeleka wagonjwa nje ya nchi, ikiwa na sisi tuna Hospitali zenye wataalamu.

Tatizo ni kwamba Serikali haijali kuboresha hospitali zake kwa sababu viongozi hawatumii hospitali hizi wao wakiumwa hata mafua au malaria wanaenda kutibiwa nje ya nchi hivyo hawaoni umuhimu wa kuboresha huduma. hizi Hospitali zimekuwa kwa ajili yetu walalahoi. Yaani hauna thamani ndani ya nchi yetu.

Wewe unayetetea Serikali ni kwamba tatizo lako huangalii pande zote za shilingi. Mgomo wa Mdakitari haupo kwa ajili ya kudai masilahi yao tu, bali kama Serikali ikifuatilia madai yao ni pamoja na kuboresha huduma katika hospitali. je huduma zikiboreshwa nani atakayenufaika?????

Watanzania baadhi yetu tunadanganywa na hoja kuwa mgomo ni kwa ajili ya kudai maslahi kitu ambacho ni tofauti kwani Serikali haisemi ukweli kama kawaida yake kuficha ukweli.

ACHENI NISEME HATA MKINI........ ACHENI NISEME, SERIKALI ACHENI KUCHANGANYA SIASA NA UHALISIA WA MAMBO KWA MASILAHI YA TAIFA. TIMIZA AHADI SIYO KULETA SIASA KWA KUTOA AHADI HEWA.

VINGINEVYO NAUNGA MKONO MGOMO KWANI SERIKALI IMEKIUKA MAKUBALIANO YA KIKAO.




MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
hivi ni kwanini kila mtu anayepinga mgomo wa madaktari anang'ang'ania issue ya maslahi tu?mliambiwa madaktari wamegoma kwa sababu ya mishahara/posho ndogo tu? kwanini hamvitaji vitu vya msingi wanavyopigania maktari kama uboreshwaji wa mazingira yao ya kazi,upungufu mkubwa wa vifaa/dawa mahospitalini n.k
kwanini hamvishughulishi vichwa vyenu kujiuliza ni wagonjwa wangapi wanafia mikononi mwa madaktari kwa kwa ukosefu wa dawa/vifaa tena vingine vya bei rahisi tu?
yaani serikali inapoteza mabilioni kwenye mambo ya anasa na ufisadi halafu ikishinikizwa iwajali wananchi kwa kuboresha huduma za afya wewe unakuja hapa na kupinga hilo? kimsingi unasema wananchi wa wandelee kufa kwa sababu ya ukosefu wa huduma bora...ndugu yangu serikali hii legevu haiwezi kufanya kitu cha maana bila kupewa mashinikizo...!
 
Wewe choka lakini ndiyo ukweli ulivyo. Kwanza nyinyi munapewa misamaha kibao ya kodi. Pili hiyo kodi yenu munayolipa inaweza kusomesha wangapi wengine bila ya kuchanganywa kwa asilimia kubwa na ya kwetu munaotunyanyada?

Ndiyo hasara ya 'bure' hiyo lazima usumbuliwe. Ingekuwa sote tunalipia elimu tusingewasema kwa hilo

Ieleweke kuwa si wote tunaosomeshwa na Serikali, kuna vyuo vingi ambavyo ni binafsi. NAOMBA TUONDOE HII KAULI HAINA MANTIKI KABISA NA KUONYESHA KUWA HUJUI KITU UNACHOONGEA.

Chukua mfano chuo cha IMTU pale Mbezi DSM; je, wanafunzi wanalipiwa na Serikali???? Na vyuo vingi tu ambavyo vinatoa taaluma kwa gharama za mtu binafsi.

Pia fuatilia uone ni wanafunzi wangapi katika vyuo vikuu hata mikopo hawapewi, nini kusomeshwa bure!!!!!!! HIVYO UKIONGEA KUHUSU KUSOMESHWA NA SERIKALI INAONYESHA JINSI GANI ULIVYO MBUMBUMBU KATIKA SUALA UNALOONGEA.

ACHENI NISEME HATA MKINI........ ACHENI NISEME KUWA SERIKALI TIMIZA AHADI YAKO KUHUSU MGOMO WA MADAKITARI.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Hata siku moja sijapata kuunga mkono mgomo wa madaktari achilia mbali wa walimu. Hata madaktari na waalimu hawajapata kutamani kugoma, wanalazimishwa na wanasiasa. Hawa ndiyo chanzo cha migomo.

Swala la kada gani bora kuliko nyingine pia linaletwa na wanasiasa. Wao wanadhani wakiwa viongozi lazima walipwe zaidi kuliko watu wengine wa kada zozote zilizopo duniani. Lakini malipo ni ujira wa kazi uliyoifanya. Wenye kupanga bei ( price) hutegemea vifaa ulivyotumia, muda wa kazi ongeza na kfaida kidogo. Hapo pima muda wa daktari linganisha na muda wa mbunge anaotumia kuupata ubunge na rasilimali anazotumia.

Nadharia hii ndiyo inayowasukuma madaktari kujiona bora kuliko wabunge na hata mawaziri.

Pili umuhimu unakuja kwa kukosekana. Je mbunge akigoma (jambo ambalo ni vigumu kufikirika) na daktari akigoma, wapi kunaathari kubwa? Jibu ni wazi. Mgomo wa madaktari una athari kubwa. Katika hali ya kawaida hakuna mtu anajipangia mshahara. Wanasiasa wanajipangia walipwe kiasi gani. Ruksa ya kujipangia ni ruksa ya kujipendelea. Sasa madaktari nao pia wanataka kujipangia mshahara wanaotaka kwa kuwa wanasiasa wanafanya hivyo bila kudhibitiwa na yeyote. Serkali inataka kuwadhibiti watumishi wa umma tu inawaogopa wanasiasa

Lakini viongozi serious wangalijua mapema kuwa kujilimbikizia mafao manono kwa mali za umma ingalikuja kuleta shida baadaye kwa kuwa rasilimali hizo si zao ni za umma. Zingalitumika vizuri zingali boresha huduma za jamii kama hospitali na shule.


Kabla hatujawalaumu Madaktari kugoma tuwalaumu waliotufikisha hapo tulipo kwa kujilimbikzia marupurupu mfano posho za vikao, nyumba, magodoro, mashuka nguo nk. Kama kweli wana uchungu watangaze kupunguza matumizi yasiyo ya lazima
 
wewe choka lakini ndiyo ukweli ulivyo. Kwanza nyinyi munapewa misamaha kibao ya kodi. Pili hiyo kodi yenu munayolipa inaweza kusomesha wangapi wengine bila ya kuchanganywa kwa asilimia kubwa na ya kwetu munaotunyanyada?

Ndiyo hasara ya 'bure' hiyo lazima usumbuliwe. Ingekuwa sote tunalipia elimu tusingewasema kwa hilo
kwanza,niliamini pengine unaongea hivyo kwa kuwa hukua unajua ukweli,lakini sasa nimejua pamoja na kutokujua au kwa makusudi umeamua kupotosha ukweli!una kila dalili za mtu mbinafsi mwenye wivu na kufikilia kwa mafupi na kuzungumza vitu kwa kulukia bila kujua undani wake.hivi kweli unaweza thubutu kusema dactari anakunyonya!!??
Hivi unajua ni kwa nini ilipendekezwa kuwa ma injinia,madactar na walimu wapewe grant na serkl??kwa kuwa sina uhakika kama unajua,nitakujuza!kwanza si kweli kuwa serkal imefanikiwa kufanya hivyo maana bado wako madact,ma injinia na walimu ambao hawajasomeshwa na hizo kodi zako!!pili hizo unazodai ni bure na misamaha,vinaitwa ni motisha ili angalau tuongeze idadi ya watu wa kada hizo hapa nnchini ili angalau kuongeza watu wanao chagua masomo ya sayance.sina uhakika nawewe unatoka kada gani[taaluma]ila nadhani mtu yeyote anaweza kukisia kutokana na unavyochangia.no offence,kama hukukimbia umande,na kama ulibahatika kusoma na watu ambao wali kuja kuwa ma injinia,madactari,au wana sayansi kwa ujumla,walikuwa ni wanafunzi wa upeo gani kwa kumbukumbu zako?
Tatu ktk nchi zote unazojua wewe zimeendelea ni matokeo ya sayance kupewa kipaumbele!embu imagini umepata kitu kinaitwa ints obst,ambayo nadhani ni dharula,unakimbizwa m/nyam,generator haina mafuta umeme unakatika wakati wewe umelala usingizi,hao unaowananga wanahangaika kwa simu tochi kuokoa maisha yako,unapona,unakwenda wodini dripu na vifaa tiba hakuna,ndugu zako waambiwa kuleta vifaa wanadai ma dr wameuza hvyo vifaa kwenye maduka yao!!?unaemwambia hivyo alijichoma wakati anakufanyia opertn na alipokucheki damu yako tayari wewe ni mwathirika,serikali yako, inatangaza kila kitu sasa ni bure kila kitu ni swari.mmmh,hata kama wewe ni failure embu usuhurishe kidogo ubongo wako mkuu!hivi unajua hao watu wasance wanauwezo wa kuhamia kada ingine yoyote kama yako na wakafanya mazuri kuliko ufanyavyo?fikili..nasubi majibu yako ili nikuelimishe bila tuition fee.
 
Huu ni uvivu wa kufikiri,madaktari wana hoja ya msingi mkuu!

Acha uwe uvivu wakufikiri nadhani hata madaktari furaha yao nikuona masikini tunakufa kwa kukosa huduma, tutafute mbinu zingine tafadhali hata kwakutaka wananchi tuwasaidie kwa maandamano!
 
Back
Top Bottom