Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Habari zilizonifikia toka jimbo la Bukoba mjini zinasema mgombea Udiwani kwa tiketi ya chama cha CUF kata ya Hamugembe aliyejulikana kwa jina moja kama "Kenyanya" na ambaye amekuwa katika kiti hicho kwa miaka kumi na sasa ameomba kupitia chama chake kutetea tena kiti chake, jana alihudhuria mkutano wa Kampeini wa Chama cha Chadema uliokuwa ukifanyika katika eneo la Omukishenye Hamugembe, na kukaribishwa meza kuu kama mgeni.
Alipopewa nafasi ya kusalimia wahudhuriaji wa mkutano huo wa kampeini, kwa mshangao, diwani huyo aliomba huku akinadi wananchi wa kata hiyo wamchague kwa kura zao zote mgombea wa Chadema Ndugu Peter Rugemarila. Akionyesha kuwa anasema kile alichokusudia, alibainisha kuwa mgombea huyo wa Chadema ni mgombea anayekubalika katika kata yao na hata yeye atampatia kura yake na kura zote ambazo wananchi wa kata hiyo wanakusudia kumpatia yeye badala yake wampe mgombea huyo wa Chadema pamoja na mbunge wa Chadema ndugu Lwakatare.
Habari ndiyo hiyo.
shabiki wa chadema Bukoba mjini akiwa katika vazi alilojitengenezea.
Alipopewa nafasi ya kusalimia wahudhuriaji wa mkutano huo wa kampeini, kwa mshangao, diwani huyo aliomba huku akinadi wananchi wa kata hiyo wamchague kwa kura zao zote mgombea wa Chadema Ndugu Peter Rugemarila. Akionyesha kuwa anasema kile alichokusudia, alibainisha kuwa mgombea huyo wa Chadema ni mgombea anayekubalika katika kata yao na hata yeye atampatia kura yake na kura zote ambazo wananchi wa kata hiyo wanakusudia kumpatia yeye badala yake wampe mgombea huyo wa Chadema pamoja na mbunge wa Chadema ndugu Lwakatare.
Habari ndiyo hiyo.
shabiki wa chadema Bukoba mjini akiwa katika vazi alilojitengenezea.