Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
Thursday, 30 September 2010 19:57 0diggsdigg
Brandy Nelson, Mbeya
MGOMBEA ubunge Jimbo la Mbeya mjini kupitia CCM, Benson Mpesya amewasihi wakazi wa jimbo hilo wamchague kwa mara nyingine kwani ndiye aliyeleta Telesheni ya TBC1 na Star TV katika uongozi wake wa kipindi kilichopita.
Akizungumza katika moja mikutano yake ya kampeni juzi katika eneo la Uhindini jijini Mbeya alisema anashangazwa na watu wanaosema kuwa katika kipindi cha uongozi wake hakuna alichokifanya huku kukiwa na mambo mengi ambayo ameyafanya.
Nataka niwaeleze mambo niliyoyafanya katika kipindi cha miaka 10 kwamba ni mengi, lakini kikubwa nimeweza kuwaletea televisheni ya TBC na Star TV kwani huko nyuma hivi vitu havikuwepo,alisema.
Mpesya alisema pamoja na kuleta televisheni hizo ameweza kujenga ukumbi wa kisasa wa Benjamini Mkapa ambapo mmiliki wa ukumbi huo ni Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Mbunge huyo alisema mambo ambayo amefanya katika kipindi hicho,ni pamoja na kubadilisha Chuo cha Ufundi Mbeya (MTC) na kuwa Taasisi ya Sayansi na Tekonolojia (MIST) na kujenga Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo tayari amemuomba Mgombea urais Jakaya Kikwete kujenga wodi tatu katika hospitali hiyo.
Aidha mgombea huyo alionyesha kumbeza mgombea wa ubunge kupitia Chadema, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu.
Alisema kuwa atawashangaa wakazi wa Jimbo la Mbeya kama watamchagua mtoto ambaye ni mwanafunzi wake na anavaa kata kei na heleni wakati yeye ameweza kuwafanyia mambo mengi na kielimu amemzidi kwani mpaka sasa ana shahada mbili.
source: Mwananchi
Mpesya, uwe unaangalia maneno ya kuwaambia wapiga kura wako, unakili kuwa joseph mbilinyi ni mwanafunzi wako na anavaa kata kei na heleni!! nani alimfundisha? Wewe si ndiyo mwalimu wake? Kama mwanafunzi anavaa heleni na kata kei si mwalimu wake itakuwa zaidi maana mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu.
Brandy Nelson, Mbeya
MGOMBEA ubunge Jimbo la Mbeya mjini kupitia CCM, Benson Mpesya amewasihi wakazi wa jimbo hilo wamchague kwa mara nyingine kwani ndiye aliyeleta Telesheni ya TBC1 na Star TV katika uongozi wake wa kipindi kilichopita.
Akizungumza katika moja mikutano yake ya kampeni juzi katika eneo la Uhindini jijini Mbeya alisema anashangazwa na watu wanaosema kuwa katika kipindi cha uongozi wake hakuna alichokifanya huku kukiwa na mambo mengi ambayo ameyafanya.
Nataka niwaeleze mambo niliyoyafanya katika kipindi cha miaka 10 kwamba ni mengi, lakini kikubwa nimeweza kuwaletea televisheni ya TBC na Star TV kwani huko nyuma hivi vitu havikuwepo,alisema.
Mpesya alisema pamoja na kuleta televisheni hizo ameweza kujenga ukumbi wa kisasa wa Benjamini Mkapa ambapo mmiliki wa ukumbi huo ni Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Mbunge huyo alisema mambo ambayo amefanya katika kipindi hicho,ni pamoja na kubadilisha Chuo cha Ufundi Mbeya (MTC) na kuwa Taasisi ya Sayansi na Tekonolojia (MIST) na kujenga Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo tayari amemuomba Mgombea urais Jakaya Kikwete kujenga wodi tatu katika hospitali hiyo.
Aidha mgombea huyo alionyesha kumbeza mgombea wa ubunge kupitia Chadema, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu.
Alisema kuwa atawashangaa wakazi wa Jimbo la Mbeya kama watamchagua mtoto ambaye ni mwanafunzi wake na anavaa kata kei na heleni wakati yeye ameweza kuwafanyia mambo mengi na kielimu amemzidi kwani mpaka sasa ana shahada mbili.
source: Mwananchi
Mpesya, uwe unaangalia maneno ya kuwaambia wapiga kura wako, unakili kuwa joseph mbilinyi ni mwanafunzi wako na anavaa kata kei na heleni!! nani alimfundisha? Wewe si ndiyo mwalimu wake? Kama mwanafunzi anavaa heleni na kata kei si mwalimu wake itakuwa zaidi maana mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu.