Mgombea UDIWANI kata ya mwawaza ni mwizi - BABA YAKE mzazi

huyu mzee ni gamba hana lolote. Kama mwanae hana ajira sasa hafikiri kama akipata huo udiwan atatulia? Sasa anachomwaribia nini? Aendelee kuwa mwizi. Halafu ni ngumu faza wako kukuharibia kwenye issues kama hizi.
 
vitu vingine jaribu kujiongeza hakuna baba wa aina hiyo babako hata uweje hawezi kukuchafua hadharani wakati akijua lolote likikupata yeye ndie anaeuza ng'ombe akutoe!!
kwanini asifurahi kuwa mwanae anaenda kuwa diwani?
ili ng'ombe wake wasalimike!!?
mzee katumika kisiasa na ametumika vibaya.
ccm walikuwa kwenye ufunguzi wao.
haya ya mgombea wa CDM yakatoka wapi!?
na yule mzee alipewa nafas kama nani ndani ya huo mkutano!!?
siasa bhana sihasa!!!.
Ukweli ni kwamba hata kama ni mwizi vp kama amemadilika,
tunakaa na wahalifu wengi na wengine walikuwa wahalifu na wamebadilika tatizo liko wapi!?
haya ndo yakusema mtoto huyu wakati anamiaka 2 alikuwa kikojozi huu si upumbavu, jana alikuwa mwizi na sasa amebadilika!
 
Huyo baba hamnazo kabisa! Kwani yeye ni mgombea? Na alikuwa anafanya nini kwenye kampein ya magamba
 
CHAPAAA CHAPAAA SABUNI YA ROHO! CHAPAA ILIMUUZA YESU!!! CHAPAA ILIMNUNUA YULE SHEHE WA IGUNGA AKATOA TAMKO KUWA FATUMA KIMARIO ALIDHALILISHWA KIDINI WAKTI SIVYOOO!!! CHAPAA MWENYE CHAPAA SIYO MWENZIO.

KAMA YUDA ISKARIOTI ALIMKANA MWALIMU NA BWANA WAKE AMBAYE NI MWOKOZI SHAURI YA CHAPAA, ITASHINDIKANA NINI KWA HUYU BABA ALIYEPEWA CHAPAA NA CCM LABDA 200,000 AMBAYO HAJAWAHI KUIHESABU KUMKANA MWANAWE?
INANIKUMBUSHA jamaa yangu mtoto wake alipewa mimba na mzee mmoja, akalalama akatuita tukafanya vikao lukuki kumtetea bintiye mwanafunzi dhidi ya fedhulu yule. baadaye wakakutana kiaaaaina na mtuhumiwa mzee akaktiwa nasikia laki 5, kikao kichofuata yeye ndo alikuwa anendeleza mashambulizi kwa bintiye... malaya huyu, matoka wapi kuwaweka majaribuni watu wa rika langu? hiyo mimba ni haki yake, mwache, alee mimba akome.....chapaaaaaaaaaaa waku wangu msimlaumu baba wa watu kumwona mwanawe ni mwizi kwenye kampeni.
 
Tunapojadili vitu tuwe na hakika na kile tunachojadili kama ndiyo haswa kinatakiwa kujadiliwa tusije tukawa tunajadili kisicho mjadala. Hivi ni baba yake huyo kijana ndiye kaleta humu hiyo hoja kwamba mtoto wake ni mwizi, au bandiko hili limeletwa na mtu anayejiita rais wa migomo?

Sasa kama hata hilo hulioni unajadili nini sasa?


Asante kwa angalizo, ni kweli nimekosea kumlaumu baba mtoto kwa mada iliyoletwa jf na member mwenzetu, lakini bado wehu wa baba bado haufutiki, kwa nini akalalame kwenye mkutano wa kampeni na si kabla ya hapo?
 
Huyu baba anasema aliuza g'ombe wake kwenda kumuokoa mtoto wake Polisi siku chache zilizopita, cha ajabu ni kwamba ilikuwaje mpaka leo hii anagombea udiwani na huku alikamatwa na silaha? Au tuseme alihonga Polisi wakamuachie? hivi huyu mzee anaelewa anachosema au katumwa na mafisadi wammalize kwa njia hiyo. Hebu TAKUKURU wamkamate huyu mzee na awaonyeshe hao polisi walivyomuachia mwizi wa kutumia silaha.
Vinginevyo siamini kama ni kweli maana hata huyo baba yake anampenda mwanae mpaka akamtoa Polisi na sidhani kama kafanya hivyo na huku anahutubia mambo kama hayo. Mgombea wa CDM ajibu mapigo hayo kwa nguvu zote maana kuna walikini katika habari hiyo.
Demo.


Baba amwumbua mtoto wake anayegombea udiwani

Jumatatu, Octoba 15, 2012 06:27 Na Sam Bahari, Shinyanga

*Amtangaza hadharani kuwa ni mwizi, hana sifa
MGOMBEA udiwani wa Kata ya Mwawaza Manispaa ya Shinyanga, Anthony Peter (CHADEMA), juzi aliumbuka baada ya baba yake mzazi kumtangaza katika mkutano wa hadhara, kuwa hana sifa za kuwania nafasi hiyo kwa madai kuwa ni mwizi.

Hali hiyo ilijitokeza katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni katika uchaguzi mdogo, ambao umeitishwa baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo Charles Magina, kufariki dunia kwa ajali ya pikipiki.

Katika mkutano huo, mzazi wa mgombea huyo mzee Peter Molla (62), aliwaacha hoi wananchi waliohudhuria mkutano huo pale alipomshambulia kijana wake akisema kuwa, hafai kuwa kiongozi.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa, Molla alisema pamoja na kuwa mwanaye huyo hapendi kufanyakazi, licha ya kuwa na umri mkubwa na kwamba muda mwingi amekuwa akizurura kwa ndugu zake kijijini bila ya mafanikio.

Molla alisema, hivi karibuni aliuza ng’ombe zake kwa ajili ya kwenda kumuokoa mgombea huyo, baada ya kukamatwa na polisi usiku kwa kosa la kukutwa na bunduki kinyume cha sheria.

“Mimi sikujua nilidhani nimezaa mtoto wa kiume ambaye atakuja kunilea na kunitunza uzeeni, kumbe hakuna kitu, amenitelekeza hapa mnaniona na umri huu nimebaki napata shida.

“Siyo siri mwanangu amekuwa mwizi, hawezi kukaa sehemu moja anatangatanga ovyo na makundi ya vijana wenzake anaozunguka nao huku wakimshauri mambo machafu, hao jamaa zake nao ni wezi,” alisema.

source wavuti na magazeti ya jana (mtanzania).

MY TAKE; IMEKUWAJE CHAMA KINASIMAMISHA MGOMBEA WA NAMNA HII BILA KUMCHUNGUZA KWANZA???
 
Asante kwa angalizo, ni kweli nimekosea kumlaumu baba mtoto kwa mada iliyoletwa jf na member mwenzetu, lakini bado wehu wa baba bado haufutiki, kwa nini akalalame kwenye mkutano wa kampeni na si kabla ya hapo?
Ni aina ya siasa za kijinga tunazoziendekeza badala ya kujadili masuala tunajadili watu!!
 
ukisoma habari hii, kama una hekima japo kidogo tuu utajua kuwa ni uwongo mkubwa sana aidha wa chombo cha habari au chanzo chenyewe, kwani kama ni mwizi na alishikwa na bunduki kesi hii wapi? anasema aliuza ng'ombe mbili kwenda kumtoa halafu analalamika kuwa mwanawe hamtunzi, sasa kama yeye ana uwezo zaidi ya mwanawe kwanini alalamike kuwa hatunzwi ? kama alieleza hivyo inaonekana si baba yake kama ni baba basi ni baba asiye na hekima, na kama hana hekima ni rahisi kwake ni mwongo na mwenye njaa.
 
Huyo baba wa ki-china, kilio chake ni kuterekezwa sio wizi aufanyao mwanae, hivyo angekuwa mwizi lkn hajamterekeza asingelaumu.....masikini namuonea huruma gamba huyo alivyotumika vibaya kwenye mkutano wa magamba.
 
Kuna tatizo kubwa sn hapo!!!Mbona hayo mafisad papa wazaz wao hawayasem hayo jukwaani?Kadaaaaa huyoooo
 
Kuna tetesi Mzee ameshakula za magamba na kawageuka, sasa anataka kuzungumza live leo jioni.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom