Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukweli ni kwamba hata kama ni mwizi vp kama amemadilika,vitu vingine jaribu kujiongeza hakuna baba wa aina hiyo babako hata uweje hawezi kukuchafua hadharani wakati akijua lolote likikupata yeye ndie anaeuza ng'ombe akutoe!!
kwanini asifurahi kuwa mwanae anaenda kuwa diwani?
ili ng'ombe wake wasalimike!!?
mzee katumika kisiasa na ametumika vibaya.
ccm walikuwa kwenye ufunguzi wao.
haya ya mgombea wa CDM yakatoka wapi!?
na yule mzee alipewa nafas kama nani ndani ya huo mkutano!!?
siasa bhana sihasa!!!.
Tunapojadili vitu tuwe na hakika na kile tunachojadili kama ndiyo haswa kinatakiwa kujadiliwa tusije tukawa tunajadili kisicho mjadala. Hivi ni baba yake huyo kijana ndiye kaleta humu hiyo hoja kwamba mtoto wake ni mwizi, au bandiko hili limeletwa na mtu anayejiita rais wa migomo?
Sasa kama hata hilo hulioni unajadili nini sasa?
Baba amwumbua mtoto wake anayegombea udiwani
Jumatatu, Octoba 15, 2012 06:27 Na Sam Bahari, Shinyanga
*Amtangaza hadharani kuwa ni mwizi, hana sifa
MGOMBEA udiwani wa Kata ya Mwawaza Manispaa ya Shinyanga, Anthony Peter (CHADEMA), juzi aliumbuka baada ya baba yake mzazi kumtangaza katika mkutano wa hadhara, kuwa hana sifa za kuwania nafasi hiyo kwa madai kuwa ni mwizi.
Hali hiyo ilijitokeza katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni katika uchaguzi mdogo, ambao umeitishwa baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo Charles Magina, kufariki dunia kwa ajali ya pikipiki.
Katika mkutano huo, mzazi wa mgombea huyo mzee Peter Molla (62), aliwaacha hoi wananchi waliohudhuria mkutano huo pale alipomshambulia kijana wake akisema kuwa, hafai kuwa kiongozi.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa, Molla alisema pamoja na kuwa mwanaye huyo hapendi kufanyakazi, licha ya kuwa na umri mkubwa na kwamba muda mwingi amekuwa akizurura kwa ndugu zake kijijini bila ya mafanikio.
Molla alisema, hivi karibuni aliuza ngombe zake kwa ajili ya kwenda kumuokoa mgombea huyo, baada ya kukamatwa na polisi usiku kwa kosa la kukutwa na bunduki kinyume cha sheria.
Mimi sikujua nilidhani nimezaa mtoto wa kiume ambaye atakuja kunilea na kunitunza uzeeni, kumbe hakuna kitu, amenitelekeza hapa mnaniona na umri huu nimebaki napata shida.
Siyo siri mwanangu amekuwa mwizi, hawezi kukaa sehemu moja anatangatanga ovyo na makundi ya vijana wenzake anaozunguka nao huku wakimshauri mambo machafu, hao jamaa zake nao ni wezi, alisema.
source wavuti na magazeti ya jana (mtanzania).
MY TAKE; IMEKUWAJE CHAMA KINASIMAMISHA MGOMBEA WA NAMNA HII BILA KUMCHUNGUZA KWANZA???
Ni aina ya siasa za kijinga tunazoziendekeza badala ya kujadili masuala tunajadili watu!!Asante kwa angalizo, ni kweli nimekosea kumlaumu baba mtoto kwa mada iliyoletwa jf na member mwenzetu, lakini bado wehu wa baba bado haufutiki, kwa nini akalalame kwenye mkutano wa kampeni na si kabla ya hapo?
CCM inawahonga sana na Chadema inapenda kuhongwaHuyu mzee kapewa hela na CCM ili aende aseme uongo