Elections 2010 Mgombea Ubunge wa Chadema avamiwa, mmoja auawa, wana CCM washikiliwa

Hata yule wa Maswa walimuua wenyewe ili kuipakazia Chadema, kama walivyomuua Marehemu Chacha Wangwe ili kuipakazia Chadema. MWISHO WA UBAYA NI AIBU NA MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI. CCM ni wauaji kweli kweli Kumbukeni hata ya H. Kolimba.
 
wafuasi watano wa chama cha mapinduzi akiwemo mdogo wa mbunge wa jimbo la kibakwe wilayani mpwapwa wametiwa mbaroni na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mfuasi mmoja wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) yaliyotokea katika kijiji cha pwaga wilayani humo.
Tukio hilo lilitokea siku ya alhamisi tarehe 28/10/2010, inadaiwa katika tukio hilo wafuasi wa chadema walikuwa wakitoka kwenye mkutano wao na wakapita karibu na eneo ambalo ccm pia walikuwa wakifanya mkutano, kisha ccm kuona wafuasi wa chadema wanashangilia wakaanza kuwashambulia na katika tukio hilo mtu mmoja aliyekuwa amepanda powertiller alivutwa na kuanguka kisha akaanza kushambuliwa na wafuasi wa ccm mpaka mauti yalipomkuta

watuhumiwa wametiwa mbaroni na upelelezi kamili juu ya tukio hilo unaendelea

ikumbukwe jimbo la kibakwe upinzani kati ya ccm na chadema ni mkali mno.



habari leo wanataarifa hizi???? Manake ingekua kinyume ndo ingepamba ukurasa mzima wa mbele
 
CCM chama changu kinatupeleka kubaya watanzania... shime viongozi mlioko madarakani msiingize nchi katika uadui...
 
Ee bwana kama hali ndo hii naamuru sasa hivi kama Hwa vibaraka wa CCM kiravu na wenzake walivyofanya kwa shibuda mara moja wafanye na kwa huyo mbunge wa kibakwe kupitia CCM SIMBA CHAWENE.Hii nchi ni ya Watanzania na siyp ya Chama caha mafisadi.

mungu najua nani atamtumia Juma pili kuvusha watu wake katka kisiwa hiki kicho fura kwa ufisadi.
 
CCM chama changu kinatupeleka kubaya watanzania... shime viongozi mlioko madarakani msiingize nchi katika uadui...
Mimi pia ni mwanaccm ila kwa haya wayafanyayo ccm hata wakiniita msaliti sawatuuu, UFISADI, UUWAJI, KUTOWAJIBIKA, UFAMILIA, duuuuuuu mmezidi viongozi wetu mnapeleka wapi nchi hiii! hii nchi ni ya wote jamani.
 
na bariadi kwa chenge the samething happen kwa mgombea wa UDP mwanachama wake amepigwa yuko hoi wafuasi saba wa kijani na njano waliokuwa na gari ya matangazo ya chenge wako ndani na kathibitisha RPC Daud Siasi
 
muda huu TBC wanamhoji mgombea wa chadema labda watatoa nkwenye taarifa ya saa mbili usiku
 
Back
Top Bottom