Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Jamani hii nimeipata live kutoka kwa swahiba wangu aliye Shinyanga. Anasema mgombea ubunge wa CCM jimbo la Shinyanga mjini aliyemtaja jina la Steven Masele hatakiwi na wana_CCM kwa sababu siyo mtu wa pale.
Swahiba yangu huyo anasema wana-CCM Shinyanga wanashangaa katokea wapi huyu kwani hana makazi pale na anaishi gesti. Kila siku anabadilisha gesti kwani watu humfuata na kumpigia kelele aonyeshe makazi yake.
Inasemekana mtu huyu alikuwa anafanya kazi TIGO, kanda ya Ziwa na hadi sasa haijulikani kwao ni wapi, kwani hata hilo jina la Masele ingawa ni la Kisukuma kuna wasiwasi alijipachika tu kwani hajui hata Kisukuma vizuri!
Wadau, nashindwa kuzithibitisha hizi habari kutoka kwa mtu mwingine lakini naomba mwenye habari zaidi kuhusu huyu bwana atuwekee hapa.