Mchokonozi
Member
- Nov 17, 2009
- 15
- 0
Mmoja wa wagombea ubunge wa CCM aliyeshinda nafasi hiyo kwenye kura za maoni amenusurika kuuwawa na jambazi aliiyetumwa kummaliza baada ya jambazi huyo kumwambia kwamba yeye ni mtu mwema asiyestahili kufanyiwa unyama huo.
Akisimulia ndugu na jamaa zake, mgombea huyo (jina limehifadhiwa) alisema kwamba jambazi huyo alivamia nyumbani kwake wakati wa usiku, siku chache zilizopita, na alipofanikiwa kuingia ndani alimtambua mgombea huyo, ndipo alipoamua kuweka chini silaha yake na kutoa kitita cha fedha na kumwonesha akisema: "Mzee hunikumbuki, lakini wakati nilipokuwa jela ulitusaidia kwa kutupatia suruali, mashati na viatu".
"Nimetumwa na (jina limehifadhiwa) nije kukumaliza kwa kuwa unaonekana mkaidi kwao na kwamba utawaharibia ukirudi bungeni. Lakini siwezi kukuua kwa kuwa wewe ni mtu mwema. Wamenipa milioni sita (akamwonesha) lakini hata kwa milioni mia mimi sitakuua. Hustahili adhabu hii, wewe ni mtu mwema," alinukuu mgombea huyo.
Mgombea huyo ambaye amekuwa machachari kwenye bunge lililopita, alisema kwamba alimwomba muuaji huyo kutoa tamko kwenye mkanda wa video, ambapo alikubali na kusema: "Mimi siogopi kufa. Mke wangu aliuwawa majuzi akipora benki kule (jina limehifadhiwa). Kwa hiyo hata kama wakiniua, niko tayari, siogopi."
Mgombea huyo amesema kwamba anatafuta siku na muda muafaka kutoa taarifa rasmi kwa umma wa Watanzania kupitia vyombo vya habari. Amesema kwamba anahofia kwamba akitangaza mapema tukio hilo, machafuko makubwa yanaweza kutokea nchini, kwani kilichojaribiwa kwake ni dhahiri kwamba mpango huo uliwalenga watu wengine zaidi yake yeye, na tayari amekwishachukua hatua za kuwatahadharisha watu wengine ambao anadhani waliwekwa kwenye kundi moja na yeye, yaani, kundi la kuuwawa na kupelekwa mapema kuzimu.
-----------------------------------
Haya, Mchokonozi nimechokonoa tena. Sasa mjadala uanze rasmi!
Kweli, mwaka huu ni wa mabadiliko! Kama CCM wanafikia kutaka kuwauwa Watanzania wazalendo, wadilifu, ambao wanataka CCM iwe ya Watanzania wote, basi tumefika pabaya! Tusifike pabaya zaidi!
>>> Mchokonozi <<<
Akisimulia ndugu na jamaa zake, mgombea huyo (jina limehifadhiwa) alisema kwamba jambazi huyo alivamia nyumbani kwake wakati wa usiku, siku chache zilizopita, na alipofanikiwa kuingia ndani alimtambua mgombea huyo, ndipo alipoamua kuweka chini silaha yake na kutoa kitita cha fedha na kumwonesha akisema: "Mzee hunikumbuki, lakini wakati nilipokuwa jela ulitusaidia kwa kutupatia suruali, mashati na viatu".
"Nimetumwa na (jina limehifadhiwa) nije kukumaliza kwa kuwa unaonekana mkaidi kwao na kwamba utawaharibia ukirudi bungeni. Lakini siwezi kukuua kwa kuwa wewe ni mtu mwema. Wamenipa milioni sita (akamwonesha) lakini hata kwa milioni mia mimi sitakuua. Hustahili adhabu hii, wewe ni mtu mwema," alinukuu mgombea huyo.
Mgombea huyo ambaye amekuwa machachari kwenye bunge lililopita, alisema kwamba alimwomba muuaji huyo kutoa tamko kwenye mkanda wa video, ambapo alikubali na kusema: "Mimi siogopi kufa. Mke wangu aliuwawa majuzi akipora benki kule (jina limehifadhiwa). Kwa hiyo hata kama wakiniua, niko tayari, siogopi."
Mgombea huyo amesema kwamba anatafuta siku na muda muafaka kutoa taarifa rasmi kwa umma wa Watanzania kupitia vyombo vya habari. Amesema kwamba anahofia kwamba akitangaza mapema tukio hilo, machafuko makubwa yanaweza kutokea nchini, kwani kilichojaribiwa kwake ni dhahiri kwamba mpango huo uliwalenga watu wengine zaidi yake yeye, na tayari amekwishachukua hatua za kuwatahadharisha watu wengine ambao anadhani waliwekwa kwenye kundi moja na yeye, yaani, kundi la kuuwawa na kupelekwa mapema kuzimu.
-----------------------------------
Haya, Mchokonozi nimechokonoa tena. Sasa mjadala uanze rasmi!
Kweli, mwaka huu ni wa mabadiliko! Kama CCM wanafikia kutaka kuwauwa Watanzania wazalendo, wadilifu, ambao wanataka CCM iwe ya Watanzania wote, basi tumefika pabaya! Tusifike pabaya zaidi!
>>> Mchokonozi <<<