Elections 2010 Mgombea Mwenza Dr Slaa

Hivi dr salim anaogopa nini kugombea? angekuwa mgombeA UPANDE WA CHADEMA AU HATA MGOMBEA MWENZA
 
Tukiwa bado katika dukuduku ya kuteuliwa Dr Slaa kugombea urais kwa kupitia Chadema swali najiuliza ni yupi anafaa kuwa mgombea mwenza wake, ukitilia maanani kuwa kwa mujibu wa katiba yetu huyu inabidi atokee Zanzibar. Ingekuwa vyema sana kama Chadema na CUF wangeshirikiana kwenye hili (nilishawahi kutoa hii hoja na baadhi ya WanaJF wanaaafiki na wengine kukataa i.e MM) na kumruhusu Hamad Rashid Mohammed au Fatma Maghimbi kuwa wagombea wenza wa Dr Slaa. Vilevile ingekuwa bora kama CUF wasimsimamishe Dr Lipumba na badala yake wamsapoti Dr Slaa kama ambavyo Chadema walivyofanya 1995 na 2000, maana tayari Lipumba kashagombea mara tatu. Haya ni maoni yangu. Hayo ni majina mawili tu ambayo yaminijia kwa haraka, lakini nina uhakika wapo wengine wenye uwezo...

Nawakilisha

WaMzizima,

Uko spot-on ..... tiketi ya ushindi ni Dr Wilbroad Slaa na Hamad Rashid Mohamed .... hiyo combination ni kiboko. Kama ulivyoshauri, ingekuwa vema kama CUF wangekubali kumuondoa Profesa Lipumba ktk kugombea uraisi
 
Here is where that part of constitution which is unconstitutional rules. Mgombea mwenza oyeeeeeee! Mtikila can help on how to go through this paradox
Mwambie Mtikila akamsaidie Mrema na TLP yake.
 
Wachangiaji wengi wamependekeza team ya Slaa na Hamad lakini wamesahau
kuwa wote hao ni wa vyama tofauti. Sheria za vyama hairuhusu miungano ya vyama kama
ilivyo kwa nchi kama ya Kenya. Si jambo rahisi kwa Hamad ambaye ni mmoja wa
waanzilishi kwa CUF kuingia CHADEMA wakati huu tukielekea katika uchaguzi mkuu.
Kwa maoni yangu hawa CHADEMA wangetafuta mgombea mwenza mtu mwengine
ambaye ni msomi na nayekubalika katika jamii, na sidhani kwama watamkosa huko
Zanzibar kwani wapo Wazanzibari wengi tu wenye sifa na ambao hawajajitokeza katika
mambo ya siasa.
 
Hoja yako ni muafaka kabisa.Ila kwangu mimi Hamadi Rashidi ananafaa sana.He seems to be serious and more committed to the wananchi.
 
Wachangiaji wengi wamependekeza team ya Slaa na Hamad lakini wamesahau
kuwa wote hao ni wa vyama tofauti. Sheria za vyama hairuhusu miungano ya vyama kama
ilivyo kwa nchi kama ya Kenya. Si jambo rahisi kwa Hamad ambaye ni mmoja wa
waanzilishi kwa CUF kuingia CHADEMA wakati huu tukielekea katika uchaguzi mkuu.
Kwa maoni yangu hawa CHADEMA wangetafuta mgombea mwenza mtu mwengine
ambaye ni msomi na nayekubalika katika jamii, na sidhani kwama watamkosa huko
Zanzibar kwani wapo Wazanzibari wengi tu wenye sifa na ambao hawajajitokeza katika
mambo ya siasa.
Hatujasahau kuwa ni vyama tofauti ila tunaona kuwa ideally ni 'good team'. tatizo na kikwazo ni hilo swala la vyama na tafsiri ya katiba. Technically inawezekana, Hamad akahamia Chadema kwa ajili ya uchaguzi tu...Haya ni maombi yangu kwake, basi kama wakishindwa atarudi Cuf na sidhani kama Cuf watamkatalia, labda kama Lipumba ang'ang'anie kama alivyotangaza nia yake ya kugombea na kisha kumchagua Hamad kama Mwenza wake, hatujui.
Cha msingi mi niliona kwa vile Dr Slaa ametangaza nia nia ya kugombea huu ni wakati muafaka kwa vyama vikuu vya upinzani (Cuf, Nccr, Udp,Tlp n.k) kumuunga mkono na kuwatoa wagombea wao wa urais, hii ni nadharia kwa vitendo sidhani kama watakubali, tusubiri tuone...
 
Kama ambavyo JF ilimchagua mgombea wa urais ("Padre Slaa") hivyo hivyo itamchagua "Mnafiki fulani" mchumia tumbo uhakiki ukishafanywa na pengo na secretariate yake...of course jina la mnafiki huyo liko kanisani kwenye mchakato maalum na wanatafuta bei yake hapa JF...good try!

Si ajabu atakuwa sikonge atajidai ametoka znz ..endeleni kuwa vipofu.
Tumain kama Watanzania hawadanganyiki tena, hata ukimwaga sumu, haitasambaa, haina mashiko tena, the wind of change is sweeping across Tanzania, Soma makala ya M.M.Mwanakijiji kwenye Tanzania Daima ya leo.
 
Back
Top Bottom