Ambitious
JF-Expert Member
- Dec 26, 2011
- 2,144
- 875
Gazeti la Mwananchi,
Tuesday, 06 March 2012 20:51
MBIO za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki zimefikia patamu, baada ya mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Democratic (DP),Mohamed Abdalah Mohamed kukamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), akituhumiwa kutoa rushwa ya Sh500.
Kukamatwa kwa mgombea huyo kumekuja wakati mchakato wa uchukuaji fomu za kuwania jimbo hilo ukiwa unaendelea baada ya mgombea wa sita ambaye ni Siyoi Sumari wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kujitokea kuchukua fomu hizo. Wakati uchukuaji fomu ukiendelea jana,habari zilizolifikia gazeti hili zilisema mgombea huyo wa DP na Katibu wa Uenezi na Mipango Taifa wa chama hicho Abdul Mluya walikamatwa eneo la Maji ya Chai wakati akitafuta watu wa kumdhamini.
Vyanzo hivyo vilifafanua kwamba mgombea huyo alikamatwa jana mchana wakati akimpa kiasi cha fedha mmoja wa wapambe wake, ili akachukue kitambulisho nyumbani kwa ajili ya kumdhamini.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, tukio hilo lilitokea saa 7:00 mchana baada ya maofisa hao wa Takukuru waliokuwa wamevalia nguo za kiraia kufika eneo hilo, kuwakamata na kupeleka katika Kituo cha Polisi cha Wilaya kilichopo Usa River kwa mahojiano zaidi.
Mtuhumiwa akisimulia mkasa huo Mohammed alisema, Tukio hilo liliwaathiri kisaikolojia kwa kiwango kikubwa kwani litagharimu hata harakati zao kuendelea kuwatafuta wadhamini katika mchakato huo wa uchaguzi.
Hata hivyo, alisema baada ya mahojiano ya saa kadhaa kituoni hapo na kujieleza kuwa alikuwa katika harakati za kutafuta wadhamini.
Mkuu Polisi wa wilaya hiyo, aliwaruhusu kuendelea na mchakato huo wa kutafuta wadhamini baada ya kuchukua maelezo yao. Nikiwa kituoni wakiwa wameshikilia nyaraka zetu tulizokuwa tunazitumia kutafutia wadhamini, OCD aliwasiliana na
Msimamizi wa Uchaguzi, Trasias Kagenzi kuthibitisha kama kweli mimi ni mgombea, ndipo niliporuhusiwa kuendelea kutafuta wadhamini, alisema Mohamed.
Msimamizi huyo wa uchaguzi alithibitisha kukamatwa kwa mgombea huyo na kueleza sababu zake kuwa ni taarifa za raia wema waliopiga simu Takukuru baada ya kuona mtu akipewa fedha. "Baada ya kuongea na mgombea,aliniambia kuwa baada ya kumpata mtu wa kumdhamini katika eneo hilo,alimwambia kadi yake ya kupigia kura iko nyumbani, hivyo mgombea alitoa Sh500 ya Bodaboda ili aifuate ndipo alipokamatwa na Takukuru, alisema Kagenzi.
Hata hivyo, kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Wilaya ya Arumeru,Zawadi Ngailo alisema hakuwa amepata taarifa za kukamatwa kwa mgombea huyo hadi tunaenda mitamboni.
Tuesday, 06 March 2012 20:51
MBIO za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki zimefikia patamu, baada ya mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Democratic (DP),Mohamed Abdalah Mohamed kukamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), akituhumiwa kutoa rushwa ya Sh500.
Kukamatwa kwa mgombea huyo kumekuja wakati mchakato wa uchukuaji fomu za kuwania jimbo hilo ukiwa unaendelea baada ya mgombea wa sita ambaye ni Siyoi Sumari wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kujitokea kuchukua fomu hizo. Wakati uchukuaji fomu ukiendelea jana,habari zilizolifikia gazeti hili zilisema mgombea huyo wa DP na Katibu wa Uenezi na Mipango Taifa wa chama hicho Abdul Mluya walikamatwa eneo la Maji ya Chai wakati akitafuta watu wa kumdhamini.
Vyanzo hivyo vilifafanua kwamba mgombea huyo alikamatwa jana mchana wakati akimpa kiasi cha fedha mmoja wa wapambe wake, ili akachukue kitambulisho nyumbani kwa ajili ya kumdhamini.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, tukio hilo lilitokea saa 7:00 mchana baada ya maofisa hao wa Takukuru waliokuwa wamevalia nguo za kiraia kufika eneo hilo, kuwakamata na kupeleka katika Kituo cha Polisi cha Wilaya kilichopo Usa River kwa mahojiano zaidi.
Mtuhumiwa akisimulia mkasa huo Mohammed alisema, Tukio hilo liliwaathiri kisaikolojia kwa kiwango kikubwa kwani litagharimu hata harakati zao kuendelea kuwatafuta wadhamini katika mchakato huo wa uchaguzi.
Hata hivyo, alisema baada ya mahojiano ya saa kadhaa kituoni hapo na kujieleza kuwa alikuwa katika harakati za kutafuta wadhamini.
Mkuu Polisi wa wilaya hiyo, aliwaruhusu kuendelea na mchakato huo wa kutafuta wadhamini baada ya kuchukua maelezo yao. Nikiwa kituoni wakiwa wameshikilia nyaraka zetu tulizokuwa tunazitumia kutafutia wadhamini, OCD aliwasiliana na
Msimamizi wa Uchaguzi, Trasias Kagenzi kuthibitisha kama kweli mimi ni mgombea, ndipo niliporuhusiwa kuendelea kutafuta wadhamini, alisema Mohamed.
Msimamizi huyo wa uchaguzi alithibitisha kukamatwa kwa mgombea huyo na kueleza sababu zake kuwa ni taarifa za raia wema waliopiga simu Takukuru baada ya kuona mtu akipewa fedha. "Baada ya kuongea na mgombea,aliniambia kuwa baada ya kumpata mtu wa kumdhamini katika eneo hilo,alimwambia kadi yake ya kupigia kura iko nyumbani, hivyo mgombea alitoa Sh500 ya Bodaboda ili aifuate ndipo alipokamatwa na Takukuru, alisema Kagenzi.
Hata hivyo, kwa upande wake Kamanda wa Takukuru Wilaya ya Arumeru,Zawadi Ngailo alisema hakuwa amepata taarifa za kukamatwa kwa mgombea huyo hadi tunaenda mitamboni.