M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Lile sakata la muda mrefu juu ya matumizi ya maji ya mto Nile baina ya Misri na Sudan dhidi ya nchi za maziwa makuu limeendelea kuchukua sura mpya baada ya nchi tano za maziwa makuu ikiwemo Tanzania kusaini mkataba mpya wa matumizi ya maji ya mto huo unaolenga pia kuanzisha taasisi moja itakayoratibu matumizi ya maji ya mto Nile na wakati huohuo nchi ya Misri ikitoa msimamo kuwa itatumia nguvu za kijeshi ili kulinda monopoly yake ya matumizi ya maji hayo iliyotokana na mkataba uliosainiwa na kuratibiwa na serikali ya kikoloni tarehe 7 Mei 1929.
Kinachonishangaza ni kwamba hawa wamisri wana akili timamu kweli kutaka kuhodhi matumizi ya maji ambayo chanzo chake ni katika nchi hizi za maziwa makuu, hata kama wao wana matumizi nayo zaidi hawaoni kuwa maji ni resource muhimu sana kwa uhai wa kila kiumbe, au wao ndio wanajiona viumbe bora zaidi?.,kweli sisi tufe kwa ukame wakati maji yanatiririka kwetu yakielekea Misri na Sudan, si itakuwa ni uzembe wetu wenyewe?.,nionavyo mimi kama ni vitani twende tu maana naamini nchi zote tano zitaungana dhidi ya Misri na Sudan na hapo ndipo watakapojua kuwa pamoja na unyonge wetu, tunaweza kusimama pamoja na kutetea maslahi yetu.
Kinachonishangaza ni kwamba hawa wamisri wana akili timamu kweli kutaka kuhodhi matumizi ya maji ambayo chanzo chake ni katika nchi hizi za maziwa makuu, hata kama wao wana matumizi nayo zaidi hawaoni kuwa maji ni resource muhimu sana kwa uhai wa kila kiumbe, au wao ndio wanajiona viumbe bora zaidi?.,kweli sisi tufe kwa ukame wakati maji yanatiririka kwetu yakielekea Misri na Sudan, si itakuwa ni uzembe wetu wenyewe?.,nionavyo mimi kama ni vitani twende tu maana naamini nchi zote tano zitaungana dhidi ya Misri na Sudan na hapo ndipo watakapojua kuwa pamoja na unyonge wetu, tunaweza kusimama pamoja na kutetea maslahi yetu.