Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
CCM wamvaa Mgeja
na Bakari Kimwanga
WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Shinyanga wamemjia juu mwenyekiti wao wa mkoa, Khamis Mgeja, wakisema anatumiwa na kundi la mafisadi kujinufaisha kwa maslahi yake binafsi. Katika taarifa yao waliyoituma kwenye vyombo vya habari, wanachama hao walisema wanashangazwa na hatua ya kiongozi huyo kuanzisha malumbano na viongozi wa chama na serikali.
Wanachama hao walikuwa wakirejea hatua ya mwenyekiti wao huyo ya kuanzisha malumbano na Waziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta na Mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela.
Wanachama hao walisema kitendo kinachofanywa na Mgeja ni aibu na fedheha kwa chama kwani anachotakiwa kukifanya hivi sasa ni kuitisha kikao cha kufanya tathmini ya kina kwa nini kata na majimbo mengi katika mkoa wake yamekwenda upinzani.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Juma Maganga kwa niaba ya wanachama wenzake toka wilayani Kahama alisema itakuwa vema mwenyekiti huyo akatangaza kujiuzulu uenyekiti wa CCM wa mkoa huo.
Hata hivyo Maganga alisema kuna umuhimu kwa viongozi wa CCM Taifa kumtafari kwa kina Mgeja na kumuuliza nini nia yake.
Hivi karibuni Mgeja alinukuliwa na vyombo vya habari kuhusu azma yake ya kuwasilisha hoja binafsi katika kikao cha Halamshauri Kuu ya CCM, juu ya kauli ya Waziri Sitta, kuhusu msimamo wake dhidi ya ushindi wa kampuni ya kufua Umeme ya Dowans kulipwa na Tanesco sh 185 bilioni.
Hali hiyo imeibua malumbano na kufufua kile kinachoitwa pande mbili zinazohasimiana ndani ya CCM.
na Bakari Kimwanga
Wanachama hao walikuwa wakirejea hatua ya mwenyekiti wao huyo ya kuanzisha malumbano na Waziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta na Mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela.
Wanachama hao walisema kitendo kinachofanywa na Mgeja ni aibu na fedheha kwa chama kwani anachotakiwa kukifanya hivi sasa ni kuitisha kikao cha kufanya tathmini ya kina kwa nini kata na majimbo mengi katika mkoa wake yamekwenda upinzani.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Juma Maganga kwa niaba ya wanachama wenzake toka wilayani Kahama alisema itakuwa vema mwenyekiti huyo akatangaza kujiuzulu uenyekiti wa CCM wa mkoa huo.
Hata hivyo Maganga alisema kuna umuhimu kwa viongozi wa CCM Taifa kumtafari kwa kina Mgeja na kumuuliza nini nia yake.
Hivi karibuni Mgeja alinukuliwa na vyombo vya habari kuhusu azma yake ya kuwasilisha hoja binafsi katika kikao cha Halamshauri Kuu ya CCM, juu ya kauli ya Waziri Sitta, kuhusu msimamo wake dhidi ya ushindi wa kampuni ya kufua Umeme ya Dowans kulipwa na Tanesco sh 185 bilioni.
Hali hiyo imeibua malumbano na kufufua kile kinachoitwa pande mbili zinazohasimiana ndani ya CCM.