Elections 2010 Mgaya wa TUCTA kugombea Muheza?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Kule Muheza mmojawapo wa watu wenye kutaka kugombea kule ni Balozi Andrew Daraja na Mbunge wa sasa Herbert Mntangi. Lakini siku chache zilizopita (kuanzia hii tarehe 19 Mei) kuna tetesi kuwa Katibu wa TUCTA Yusuph Mgaya ambaye alijiwa juu na Rais Kikwete anampango wa kupeleka mapambano yake ya wafanyakazi ndani ya Bunge kwa kugombea huko Muheza kwa tiketi ya Chadema. Kuna vipeperushi inadaiwa vimeenezwa vikimwaga sifa zake huko na wenye nchi yao wanashtuka.

Hata hivyo, kwa sasa Bw. Mgaya hajakiri moja kwa moja kuwa kweli anataka kugombea zaidi ya watu wengine kuwa na wasiwasi huo kwa sababu tu alienda kusalimia nyumbani kwao na kuondoka mapema na hivyo tetesi hizi kuanza.

Stay tuned.
 
Kama ni kweli, jamaa atakuwa amejifunga goli la kisigino. Unapotetea maslahi ya wafanyakazi, jiepushe na siasa maana wanasiasa wakikujua watakumaliza wewe pamoja na wafanyakazi unaowatetea.
 
Ni
Taarifa ya habari chanel 10 Mgaya kakanusha, kasema kwanza yeye siyo mwanachama wa chadema.

Kukanusha ktk vyombo vya habari mara nyingi ni step ya kwanza kuelekea ktk tendo halisi. Yeye si mwanasiasa angekaa kimya tuli.

Na huyu jamaa akigombea JK atashinda kwa kishindo
 
Kama ni kweli, jamaa atakuwa amejifunga goli la kisigino. Unapotetea maslahi ya wafanyakazi, jiepushe na siasa maana wanasiasa wakikujua watakumaliza wewe pamoja na wafanyakazi unaowatetea.


Sidhani kama mtazamo huu ni kweli.

Kwani kama ni hivyo akina Rashid Kawawa, Bruno Mpangala, David Hollela, Peter Kisumo, Barongo, Margreath Sitta na wengine waliopitia katika mgongo wa wafanyakazi (Zambia Chiluba, Kaunda,...... Afrika Kusini Steve Biko, Walter Sisulu,......Poland Wence V, Urusi Lenin, Stalin,.......Germany Karl Max, ..........etc) na kupanda hadi siasa za kitaifa/kimataifa, wangekuwa wamemalizwa siku nyingi na wafanyakazi waliokuwa wakiwatetea pia.....
 
Sidhani kama mtazamo huu ni kweli.

Kwani kama ni hivyo akina Rashid Kawawa, Bruno Mpangala, David Hollela, Peter Kisumo, Barongo, Margreath Sitta na wengine waliopitia katika mgongo wa wafanyakazi (Zambia Chiluba, Kaunda,...... Afrika Kusini Steve Biko, Walter Sisulu,......Poland Wence V, Urusi Lenin, Stalin,.......Germany Karl Max, ..........etc) na kupanda hadi siasa za kitaifa/kimataifa, wangekuwa wamemalizwa siku nyingi na wafanyakazi waliokuwa wakiwatetea pia.....

Maeneo tofauti
Sio kilakitu kina apply, hizi fikra zako pia nafikiri ndo zinaturudisha nyuma
 
Kule Muheza mmojawapo wa watu wenye kutaka kugombea kule ni Balozi Andrew Daraja na Mbunge wa sasa Herbert Mntangi. Lakini siku chache zilizopita (kuanzia hii tarehe 19 Mei) kuna tetesi kuwa Katibu wa TUCTA Yusuph Mgaya ambaye alijiwa juu na Rais Kikwete anampango wa kupeleka mapambano yake ya wafanyakazi ndani ya Bunge kwa kugombea huko Muheza kwa tiketi ya Chadema. Kuna vipeperushi inadaiwa vimeenezwa vikimwaga sifa zake huko na wenye nchi yao wanashtuka.

Hata hivyo, kwa sasa Bw. Mgaya hajakiri moja kwa moja kuwa kweli anataka kugombea zaidi ya watu wengine kuwa na wasiwasi huo kwa sababu tu alienda kusalimia nyumbani kwao na kuondoka mapema na hivyo tetesi hizi kuanza.

Stay tuned.

100% Fact.
 
Duh,
kama kweli atakuwa amewatosa watumishi wa umma. Hata kama aliyokuwa anayatetea yana haki ataonekana alikuwa anatumiwa na hayana msingi. Bad timing bro!
 
Duh,
kama kweli atakuwa amewatosa watumishi wa umma. Hata kama aliyokuwa anayatetea yana haki ataonekana alikuwa anatumiwa na hayana msingi. Bad timing bro!

Atakuwa amewatosa kivipi? Nadhani akienda Bungeni ndiyo anapata platform ya kuwatetea hao watumishi.

Mama Sitta alikuwa Rais wa CWT, akagombea kupitia huko huko na akapata. Alipopewa nafasi ya Waziri wa Elimu alishindwa, maana utawaambia nini walimu wenzako ambao mlikuwa nao kwenye mapambano na serikali kwamba maombi yenu hayawezekani na ilihali ulipokuwa mwalimu ulikuwa unaona yanawezekana.

Mtu anayeshindwa kutetea maslahi ya watumishi ni yule anayeingia serikalini na siyo anaekwenda Bungeni. Wakijitokeza akina Mgaya kama 10 hivi, kunaweza kuwa na mabadiliko ya kueleweka.

Kwanini linapokuja swala la kutetea maslahi ya walalahoi huwa tunakimbilia sana swala la kutumiwa? Kama kuna kasoro mtu akae kimya tu? Madai ya nyongeza ya mshahara hayajaanza leo, ni tangu mwaka juzi. Kwa hiyo hoja ya kwamba anatumiwa, is just an excuse ya serikali.
 
Kukanusha ktk vyombo vya habari mara nyingi ni step ya kwanza kuelekea ktk tendo halisi. Yeye si mwanasiasa angekaa kimya tuli.

Na huyu jamaa akigombea JK atashinda kwa kishindo
How? una maana Mgaya asipogombea JK atashindwa, sijaona correlation yeyote ya Mgaya kugombea na JK kushinda kwa kishindo.
 
MMJ;
Hapa umesema Yusuf Mgaya, lakini mara nyingi nimekuwa nikisia jina la Kaimu Katibu wa TUCTA likiandikwa na kutamkwa kama Nicholaus Mgaya, kuna uhusiano gani hapo?
 
Sidhani kama mtazamo huu ni kweli.

Kwani kama ni hivyo akina Rashid Kawawa, Bruno Mpangala, David Hollela, Peter Kisumo, Barongo, Margreath Sitta na wengine waliopitia katika mgongo wa wafanyakazi (Zambia Chiluba, Kaunda,...... Afrika Kusini Steve Biko, Walter Sisulu,......Poland Wence V, Urusi Lenin, Stalin,.......Germany Karl Max, ..........etc) na kupanda hadi siasa za kitaifa/kimataifa, wangekuwa wamemalizwa siku nyingi na wafanyakazi waliokuwa wakiwatetea pia.....

Hao wote uliowataja waliongoza vyama vya siasa ambavyo ama vilikuwa part of the system kama akina Bruno Mpangala, David Hollela, Peter Kisumo na wengine au waliongoza mapinduzi yaani kuitoa serikali moja madarakani kama vile akina Walesa wa Poland, Chiluba nk.

Ni tofauti sana ni hii ya Mgaya. Kama ni kweli itakuwa ni very bad news kwa wafanyakazi.
 
Hao wote uliowataja waliongoza vyama vya siasa ambavyo ama vilikuwa part of the system kama akina Bruno Mpangala, David Hollela, Peter Kisumo na wengine au waliongoza mapinduzi yaani kuitoa serikali moja madarakani kama vile akina Walesa wa Poland, Chiluba nk.

Ni tofauti sana ni hii ya Mgaya. Kama ni kweli itakuwa ni very bad news kwa wafanyakazi.
Itakuwa bad news kivipi sijakuelewa, kuwatetea wafanyakazi au kugombea.
 
How? una maana Mgaya asipogombea JK atashindwa, sijaona correlation yeyote ya Mgaya kugombea na JK kushinda kwa kishindo.

Hii kitu ipo wazi sana refer nini JK alisema akigombea tu wafanyakazi watakubali kuwa walikua steping stone. Na watakubali kabisa mgomo huo uliandaliwa na chadema na si tucta. Hiyo fact najua mtaikataa lakini
 
Hii kitu ipo wazi sana refer nini JK alisema akigombea tu wafanyakazi watakubali kuwa walikua steping stone. Na watakubali kabisa mgomo huo uliandaliwa na chadema na si tucta. Hiyo fact najua mtaikataa lakini
Kwa akili ya watanzania nitakubaliana na wewe lakini katika nchi nyingi mgomo ni haki ya mfanyakazi uwe unamsukumo wa kisiasa, upinzani au chochote kile, kinachotafutwa ni maslahi mazuri ya mfanyakazi haijalishi yameletwa na nani. Hata TANU ilitumia vyama vya wafanyakazi kufanikisha matakwa yake kama TAA, NUTA nk. Mimi nafikiri wafanyakazi hawana akili ndogo kiasi hicho kudhani kwa vile madai yao yanamsukumo wa siasa za upinzani basi wasidai tena au ndiyo sababu ya kumpa kura JK.
 
Kwa akili ya watanzania nitakubaliana na wewe lakini katika nchi nyingi mgomo ni haki ya mfanyakazi uwe unamsukumo wa kisiasa, upinzani au chochote kile, kinachotafutwa ni maslahi mazuri ya mfanyakazi haijalishi yameletwa na nani. Hata TANU ilitumia vyama vya wafanyakazi kufanikisha matakwa yake kama TAA, NUTA nk. Mimi nafikiri wafanyakazi hawana akili ndogo kiasi hicho kudhani kwa vile madai yao yanamsukumo wa siasa za upinzani basi wasidai tena au ndiyo sababu ya kumpa kura JK.

Najua unatako elekea.
Lakini hiyo haina tofauti na ROSTAM kufadhili Rais kwa pesa ili apate njia sahihi ya kunyonya kama kupe wa pori. Tatizo mkuu watanzania tunakua na kasumba ya kufanya lolote ili mradi tu tupate vyeo hili lina effect hasi. Mkama ana baki kumwinda Luteni kwenye kona ipi Luteni atafanya makosa basi mimi hapo hapo ndo nijapitie uongozi , huo ni urasimu na siasa mfilisi.

Luteni
Hii inafanana kabisa na mkasa huu, hua napenda kuurudia rudia tangu 2007, let assume wewe ni bwana na umeoa lakini siku moja ukawa una ka kijimada kangine ,kumbe mimi bwana hua namtaka mkeo sasa sera ya kumwibisha ndo inagomba. Bahati mbaya ikatokea nikagundua umetoka na kakimada kako kaleee nikamfuata mkeo na kumwambia mmeo Luteni katoka na kimanda na nikamuongoza mpaka tukakukamata ugoni na kutokana na hasira alizo nazo mkeo mie nikaanza kuchombeza.

Angalia mimi ni mwema , nimekuonyesha jinsi mmeo Luteni anavyokutenda na kumuweza Luteni na wewe bora utembee na mimi maana nitakusaidia zaidi. Mkeo kutokana na hasira kaingia mkenge pia.

Amini na kuambieni mtu wa namna hii si mwema na OLE WANGU mimi ni BORA ya LUTENI kuliko mtu wa namna ile. Na ole wao watakaopata kuwaamini watu wa namna hii
 
Back
Top Bottom