Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kule Muheza mmojawapo wa watu wenye kutaka kugombea kule ni Balozi Andrew Daraja na Mbunge wa sasa Herbert Mntangi. Lakini siku chache zilizopita (kuanzia hii tarehe 19 Mei) kuna tetesi kuwa Katibu wa TUCTA Yusuph Mgaya ambaye alijiwa juu na Rais Kikwete anampango wa kupeleka mapambano yake ya wafanyakazi ndani ya Bunge kwa kugombea huko Muheza kwa tiketi ya Chadema. Kuna vipeperushi inadaiwa vimeenezwa vikimwaga sifa zake huko na wenye nchi yao wanashtuka.
Hata hivyo, kwa sasa Bw. Mgaya hajakiri moja kwa moja kuwa kweli anataka kugombea zaidi ya watu wengine kuwa na wasiwasi huo kwa sababu tu alienda kusalimia nyumbani kwao na kuondoka mapema na hivyo tetesi hizi kuanza.
Stay tuned.
Hata hivyo, kwa sasa Bw. Mgaya hajakiri moja kwa moja kuwa kweli anataka kugombea zaidi ya watu wengine kuwa na wasiwasi huo kwa sababu tu alienda kusalimia nyumbani kwao na kuondoka mapema na hivyo tetesi hizi kuanza.
Stay tuned.