Mgao wa umeme: WaTanzania tuamke, tuukatae

Hivi kweli hakuna wa kutatua tatizo hili? Mgao Umepitiliza masaa 16 na bado unaendelea. Garama ya mgao huu itarudisha nyuma miaka 20. Nahisi wasimamishe michakato yote ya kujiunga katika eneo la kiuchumi la afrika mashariki. Wakati wakenya, waganda, wanyarwanda wanazalisha sie tumesimama halafu tuungane kwa lipi? Inatia hasira sana hali hii. Hivi hakuna wa kuunganisha sauti zetu kwenye hili???Naona tunalia mmoja mmoja ndio maana ngeleja na wenzie wanaendelea "burudani" kama kawa...Suala hili linahitaji uwajibikaji wa hali ya juu na sio huu tunaouona. Au ndio wanataka tuseme bora ya lowasa na Richmond yake kuliko hiki cha Pinda? Naona kuna kitu nyuma ya pazia na Raisi anafumbia macho.Hasiraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Jamani wanasiasa mbona mnatupa adhabu,vyakula vinaharibika uchumi utazidi kuporomoka eti sababu mgao wa umeme.Kuna Ma-geologist wa kutosha hapa nchini na wamegundua madini nyie wanasiasa mkaingia mikataba mibovu,leo wamegundua uranium huenda tena mkatupoteza,Huu sio mgao ni adhabu 12hrs.kweli maisha bora kwa kila mtanzania.

Mkuu sahihisha hapo kwenye red, ondoa na kuweka 'watu wa magamba.'
 
Kaka ni hasira kubwa sana halafu wenyewe wamefocus uchaguzi wa 2015 mimi naona 2zinduke kama wenzetu waarabu umefika mda kuwa sasa tunajitambua kudai haki zetu sio kuomba
 
watanzania wote ni sawa na marehemu walioko kaburini, mimi nilisepa long time baada ya kugudua hilo, wanaongea tu lakini hakuna action, shame on them, na mtakufa wote vinywa wazi, mijitu imekaa tu kama magogo, i hate you all
 
Njo na bango lako ubungo mataa tukuunge mkono!!! Kama mkweli
Mijitu mingine bana, yaani utafikiri hii topic ni ya kumchangia mtoa mada wakati inatuhusu wote,suala sio ''tumuunge mkono'', ni kwamba tuungane WOTE Mikono.Cha msingi tupange tarehe, muda mahali pa kuanzia, njia tutakayopita, mahali pa kumalizikia, ujumbe tutakaobeba.Logistics za vibali zitafuata baadae
 
Nyie watu computers hamna lolote, mnapiga kelele mkiwa humu ndan lakn hakuna anayeliweza kunji. Tokeni road tufanye vitendo. Mtaishia kusema kama tunisia, kama misri, kama senego, halafu mnabaki ndani ya computers. Majaa yanaendelea kula bila kunawa then sisi tunaambulia migawo ya umeme na maji. Tokeni tufanye kweli.
 
mkuu mimi ninashauri Wiliam Ngeleja abebe virago yvake arudi nyumbani kwao sengerema, atabakia na cheo chake cha waziri wa nishati na madini kulipwa mishahara, shangingi pia atapewa na posho zote kama kawaida ya waziri halafu tumuombe balozi wa japan nchini tanzania asimamie utekelezaji wa sekta ya nishati na balozi wa Africa ya Kusini hapa nchini asimamie utekelezaji wa sector ya madininimekuwa na maono haya kwa sababu ndugu william ngeleja amekuwa hana uzalendo na nchi ya Tanzania
acha matani, issue hii ni silias. We have to do somethng.
 
mkuu mimi ninashauri Wiliam Ngeleja abebe virago yvake arudi nyumbani kwao sengerema, atabakia na cheo chake cha waziri wa nishati na madini kulipwa mishahara, shangingi pia atapewa na posho zote kama kawaida ya waziri halafu tumuombe balozi wa japan nchini tanzania asimamie utekelezaji wa sekta ya nishati na balozi wa Africa ya Kusini hapa nchini asimamie utekelezaji wa sector ya madininimekuwa na maono haya kwa sababu ndugu william ngeleja amekuwa hana uzalendo na nchi ya Tanzania
acha matani, issue hii ni silias. We have to do somethng.
 
Nyie watu computers hamna lolote, mnapiga kelele mkiwa humu ndan lakn hakuna anayeliweza kunji. Tokeni road tufanye vitendo. Mtaishia kusema kama tunisia, kama misri, kama senego, halafu mnabaki ndani ya computers. Majaa yanaendelea kula bila kunawa then sisi tunaambulia migawo ya umeme na maji. Tokeni tufanye kweli.
 
Tuwape muda mpaka 1/8/2011 kama awana solution atukutane Mnazi Mmoja tarehe 2/8/2011 saa 10:00AM kupinga mgao wa umeme,
 
Hii ni nchi ya ajabu kweli. Giza miaka nenda rudi. Umasikini wetu umetokana na akili zetu. Watu wanaona sawa sawa, raisi naye kakaa kama zigo la pumba. Kachoka kama nini. Anaishi kwa kudra Mwenyezi Mungu. Kazi kupaa anga. Kweli tunajutia kuchagua mtu wa mwambao kwa maana kazi starehe tu.

Huyu si raisi. Ni mhuni tu wa mitaa ya kati. Hana akili vizuri. Anacheka cheka kama malaya vile. Eti tatizo la umeme limeletwa na Mungu kutukosesha mvua. Kama haitanyesha tena. Tufe? Tukae gizani miaka yote? What a stupid comment?

Viwanda vimelala, watanzania wamelogwa wako kwenye usingizi pono maana giza limewazunguka kwanini wasilale? Tutazidi kuletewa misaada, tusubiri. Poor people; Gadaffi ndio huyoooo wanataka kuhama na kichwa chake. Bora huyu Gadaffi anafanya kazi inayoweza kueleweka kuliko huyu wa kwetu ambaye haoni mbali anamwona tu mkewe.

Angekuwa ana busara hata hizi safari za nje angeziacha kabisa. Maana hazina maana kabisa kwa sasa. Safari za nini nchi inaangamia????? Eti nisingeomba nje mngekufa njaa. Watanzania tuna moyo kweli.

Nimemkumbuka Mkapa kweli. Nasema kweli ya moyoni. Hana choko choko kama hizi. Kazi kwa kwenda mbele. Japo naye lkn nafuu sana kuliko huyu anayetembeza pua na bakuli.

Mungu utuhurumie maana ni kwa makosa ya watanzani. Eti walinena ni chaguo lako lkn wamegundua kuwa siyo kweli. Na sasa wanaomba toba kwako. Baba utuhurumie. Mwalimu wetu na baba yetu wa Taifa ulisema utatuombea kwa Mungu, usisahau kutuombea maana ni wewe uliyesema hili jamaa halijakomaa lkn hukutaka kuainisha kuwa siyo kwa umri bali hana kabisa akili ya kukomaa.

Asante baba.
 
hivi kuna mgao? Maana mie naishi karibu na baraza la maaskofu kurasini umeme upo 24/7
hii ni rushwa ya bila kificho,na nd'o maana hawaongei chochote kuhusu mgao.watumishi wa siku zetu hz ni nuksi mikosi wamejitenga kabisa na kondoo wa bwana wamekuwa walafi na wabinafsi wakubwa wakisahau kabisa sisi kondoo/waumini nd'o sababu ya hiyo nguvu yao ya ushawishi wanayodaiwa kuwa nayo.ni aibu kubwa kwao kupotoshwa kusimamia haki kwa rushwa ya kijinga namna hii.nimepata majibu ya sababu ya ukimya wao katika hili.
 
basi hawa viongozi wa upposition wako wapi waongoze mapinduzi? Vijana tuamke, lets take to the streets.
tusingoje viongozi wa opposition tutakuwa tunatafuta kufeli si unaona wenyewe wako scattered.sisi wenyewe tutoke tuwe kitu kimoja kwenye hili,ndiyo tuwashirikishe lakini wakileta tofauti zao kisiasa tunawaweka pembeni kisha tunasonga mbele.
 
Watanzania tunaupenda mgao wa umeme japo unatuathiri kiuchumi. Kelele zinazosikika ni za kushangilia tukio hili ambalo waziri wake ameliita janga la taifa(JK). Tunaupenda mgao, wasioupenda mgao senegal wameshachukua hatua japo tatizo lao ni la muda mfupi. Watz tumekuwa na tatizo hili kwa muda mrefu tumelifurahia na kulishangilia tatzo hilo. Watz waoga wa kutenda lakn ni wajasiri wa kusema. Hii haitatusaidia na hatutalisaidia taifa. Kinachouma zaidi wale wanaonufaika na tatzo hilo wao hawana mgao. 24/7 wana umeme.
Sasa tufanyeje? Jf kiwe chombo cha kutuunganisha. Nawahimiza wanajf wote wawe chachu ya mabadiliko. Tuache kuwa watu computers na badala yake tuwe watu halisi na tusimame imara kupinga dhulma hiyo. Wanajf tufungue id ndani ya jf ambazo zitatumika kuunganisha wananchi na hivyo kushinikiza kuondoshwa kwa matatizo. E.g najitolea kufungua id yenye jina la mgomo shy na wanajf wa mikoa mingine wafungue e.g mgomo mbeya n.k. Tujaribu tunaweza.
 
naunga mkono hoja!ukiona jambo baya zuia kwa mikono yako,au kemea kwa mdomo ikishindikana chukia matendo hayo mabaya!watanzania hatujachukua hatua!
 
Nchi hii tuna kila kitu ila viongozi wetu hawana mipango endelevu ya kuendeleza rasilimali kama gesi,makaa ya mawe, maporomoko ya maji n.k. wamekaa wakihofia maandamano ya CDM.
 
Tatizo kubwa la Watanzania ni waoga wa kudai haki zao za msingi suala umeme limechangiwa kwa kiasi kikubwa na woga wetu tujilaumu wenyewe ,haki ya mtu haimbwi bali inatafutwa .sasa ni muda muafaka wa kuitafuta haki yetu Watanzania tubadilike jamani .wanaoumia ni sisi wananchi sio vingozi hima watanzania twendeni tukadai haki ya kupata umeme masaa 24
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom