Mgao wa umeme: Tanesco leo wamesahau kukata au umepungua?

Ulukolokwitanga

JF-Expert Member
Sep 18, 2010
8,396
7,968
Jenereta ya jirani yangu inayoniamsha usingizini saa 12 kila siku leo haisikiki kabisa....

Salon ya nywele hapa jirani naona mayankee wanatabasamu tu meno yote nje wanakamua hela leo...

Jamaa wanochomelea mageti na welding nao wanachapa mzigo tu wako full shangwe....

Nimeona hata wauza Ice cream leo wako mtaani na madeli yao...

Mashine za Car wash ziko full pressure, magari yanaingia yanatoka vijana wanakamata hela...

Kuna mtanga mmoja hapa jirani huwa anatukamulia juice ya miwa naye anapiga kazi... Anasema leo hata muazini aliita waenda masjid sa11...

Stationery zimefunguliwa Jumapili watu wanafanya typing na madesktop yao wana make mahela....

Mwenye ratuba ya mgao wa umeme atujuze jamani tunashangaa jana na leo mambo sio mabaya ingawa jana tuliangalia game ya yanga hadi half time. Rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete, hivi hupendi watanzania hao hapo juu ambao wako kwa maelfu wakiendeleza matabasamu waliyonayo leo yawepo kesho, keshokutwa, wiki ijayo, mwezi ujao, mwaka ujao na hadi 2015 unaondoka na watu wakukumbuke kuwa ulileta umeme na sio kukumbukwa kwa kucheza Kiduku...
 
January Makamba, tunajua umeisharubuniwa kwa kupewa hela ndio maana hutaki kumlima Ngeleja barua nyingine na umekuja na stori zile zile kuwa matatizo ya Tanesko ni ya muda mrefu, eti shirika lilidumaa kusubiri kubinafsishwa. Pia tunajua kuwa wewe na familia yako hamna mgao wa umeme na majenereta ya akiba mnayo. Actually hamtegemei umeme kupata hela kwani una mshahara wa ubunge na posho umegoma kuturudishia watanzania, lakini hebu wahurumie hawa vijana wenzio wanaotegemea umeme kupelekwa mkono kinywani... Waambie Tanesco watuletee hata ratiba tu tujue umeme utakatika muda gani ili tuwapange wateja wetu, badala ya mnavyofanya sasa kutokuwa na ratiba maalum
 
Mgao kwetu upo na jana tumeweka unit 80,ilibidi leo ukatwe usiku wameubeba mchana
 
Braza Ngeleja najua pale kwenu Bitoto Sengerema hakuna umeme na umeshindwa kutekeleza ule mradi wa kupeleka umeme Buyagu Ginnery ili angalau upite kijijini kwako, wanaBitoto wanaona umewasaliti kwa kuwa pale kwa Mzee Mganga Ngeleja kuna Sollar na Genereta kubwa. Lakini jaribu pia kuwafikiria na watu wengine. Tunakujua wewe ni mbinafsi toka utotoni lakini jitahidi basi kwenye masuala yanahusu mustakabari wa nchi yetu punguza ubinafsi, piga kazi umeme uje....
 
Mgao kwetu upo na jana tumeweka unit 80,ilibidi leo ukatwe usiku wameubeba mchana
Sisi leo full shangwe, watoto wamefurahi sana wanaangalia tu maCartoon.
Wanamuangalia Mutley na Wacky races na Luninga inasema next on Boomerang is Scooby Doo...
Daaa kumbe umeme unaimarisha sana familia...
 
Mgao huu ni balaa. Kilaza Ngeleja azima hata akili kwa Mnyika utumalizie hii kadhia
 
Rais wetu wa Moyoni Dr Wilbroad Slaa, tumemiss sana maandamano. Hebu tuitishie maandamano ya kupinga bei ya umeme ili tuendelee kufaidi utetezi wako. Tulizoea ukitutetea bungeni lakini sasa tunao watetezi wengi bungeni Kama Silinde, Mnyika, Zitto na Lisu lakini wewe utetezi wako kwetu ni nje ya bunge. Itisha maandamano ya ukombozi wa kiuchumi tuukatae mgao. Kauli yako Doctor wa ukweli ni dawa ya mgao wa umeme. Mbona sukari walishusha bei ulipowapa siku nane?
 
Back
Top Bottom