Hemed Maronda
Senior Member
- Oct 27, 2010
- 138
- 43
Mfumo unaotumika katika vyama vya siasa na Serikali Malawi ni mzuri na unaheshimu sana wapiga kura,ningependa mfumo kama huo ungetumika hapa nchini kwetu,kwa mfano Marehemu Dr Bingu wa Mutharika alipogombea Uraisi kwa mara ya kwanza alisimama kwa tiketi ya UDF lakini baada ya kupata Uraisi akatofautiana na Mwenyekiti wake wa UDF Dr Bakili Muluzi,akaona isiwe taabu akajiondoa kwenye Chama na akaunda Chama chake DPP huku bado akiushikilia Uraisi wake,kwetu sisi Watanzania isingewezekana! Makamu wake Dr Kasim Chilumpha akabaki kwenye UDF.Dr Bingu alipogombea kipindi cha pili alisimama kwa tiketi ya DPP akiwa na runningmate wake Bibi Joyce Banda,baada tu ya muda mchache akakosana pia na Makamu wake Bibi Joyce Banda,nae akaona isiwe shida akajiondoa toka DPP akaunda Chama chake PP ambacho leo hii kinaongoza Serikali baada ya kufa Dr Bingu kikiwa na Wabunge wawili tu! Demokrasia hii nimeipenda tofauti na ilivyo hapa kwetu Mbunge tu akitolewa uanachama anapoteza pia na nafasi yake ya uwakilishi kama ilivyotokea kwa Hamad Rashid wa CUF.Ningependa swala hili liwekwe wazi kwenye Katiba yetu mpya inayokuja Wanabodi mnasemaje?