Mfumo wa kumpata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ufumuliwe

Baraghash

JF-Expert Member
Dec 18, 2012
2,713
1,786
Mfumo wetu wa kumpata Rais wa Jamhuri ya Tanzania uonekane wa kidemokrasia na halali zaidi ni kuufumua na kuja na mfumo eleweka unaozingatia haki na usawa.

Nilitafakari kwa kina uhalali wa mfumo wa uchaguzi wa Marekani na hoja ya kuchagua Rais kwa kutumia " electoral votes" badala ya " popular votes" na kubaini kuwa mfumo huo nihalali, mahiri,mzuri na wakuigwa na nchi zenye mfumo wa muungano na kuwa na Rais mmoja mtendaji.

Jamhuri ya muungano ni nchi mbili zilizoungana( Tanganyika na Zanzibar) na zina mfumo wa kuwa na Rais moja mtendaji,hivyo inapaswa Rais anaechaguliwa awe ana uhalali wa kupata ridhaa za pande zote za nchi washiriki wa Muungano.Hivyo kuondosha dhana ya mmoja mkubwa ya kumtawala mwenzake.

Kwa mfano tokea mfumo wa vyama vingi ulipoanza kutumika wakumpata Rais wa Jahuri ya muungano waTanzania hakuna awamu hata moja ambayo Rais wa Jamhuri alikubaliwa na wapiga kura wengi kutoka Zanzibar, nchi mshirika wa muungano.

Mara zote chaguo la wazanzibari limekuwa mgombea wa chama cha upinzani.Kwa vile maamuzi ya wazanzibari walio wengi hayathaminiwi hata kidogo,hali inyaleta manun'guniko upande mmoja na kumfanya hata Rais mwenyewe kutowajibika ipasavyo kuwahudumia watu ambao kwake hawana umuhimu katika uchaguzi wa uteuzi wake.

Ukiwepo mfumo ambao utalazimu mgombea urais ahalalishe ushindi wake kwa kuapata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar. Njia hii itawafanya wagombea na vyama vyao wachacharike na kuwajibika ipasavyo kuhakikisha kuwa haki za utawala zinatapakaa pande zote za muungano ikiwa kama wanataka kushika hatamu za kutawala JMT.
 
Sisi ni members wa the Commonwealth na mambo mengi yakiwamo yale ya uchaguzi yamerithiwa kutoka humo. Kwa mfano, UK ni muungano wa nchi nadhani nne hivi - England, Scotland, Wales, na Northern Ireland. Mfumo wao wa uchaguzi, kama ulivyo wa kwetu (muungano wa nchi mbili) ni "simple majority" na hakuna cha nchi hii ni ndogo au kubwa. Anayepata nyingi anabeba kila kitu. Ili tuweze kufuata huo wa Marekani, nadhani hatua ya kwanza ni kujitoa Commonwealth.
 
maoni ya mtu ya heshimiwe naunga mkono hoja lakini kuwepo na tahadhari ya wagombea kuwajibika zanji au bara tu
 
Mkuu,kura zinaendana na wingi wa watu.Huwezi kusema zanzibar yenye watu takribani Milioni Moja iwe sawa na Tanzania Bara yenye watu Takribani Milioni 50.
Marekani penyewe wanaenda na idadi ya watu ndio unapata Electroral Vote.Mfano,Alaska yenye watu wachache ina Electoral vote 3 wakati California yenye idadi kubwa ya watu ina Electoral vote 55.
 
Mfumo wetu wa kumpata Rais wa Jamhuri ya Tanzania uonekane wa kidemokrasia na halali zaidi ni kuufumua na kuja na mfumo eleweka unaozingatia haki na usawa.

Nilitafakari kwa kina uhalali wa mfumo wa uchaguzi wa Marekani na hoja ya kuchagua Rais kwa kutumia " electoral votes" badala ya " popular votes" na kubaini kuwa mfumo huo nihalali, mahiri,mzuri na wakuigwa na nchi zenye mfumo wa muungano na kuwa na Rais mmoja mtendaji.

Jamhuri ya muungano ni nchi mbili zilizoungana( Tanganyika na Zanzibar) na zina mfumo wa kuwa na Rais moja mtendaji,hivyo inapaswa Rais anaechaguliwa awe ana uhalali wa kupata ridhaa za pande zote za nchi washiriki wa Muungano.Hivyo kuondosha dhana ya mmoja mkubwa ya kumtawala mwenzake.

Kwa mfano tokea mfumo wa vyama vingi ulipoanza kutumika wakumpata Rais wa Jahuri ya muungano waTanzania hakuna awamu hata moja ambayo Rais wa Jamhuri alikubaliwa na wapiga kura wengi kutoka Zanzibar, nchi mshirika wa muungano.

Mara zote chaguo la wazanzibari limekuwa mgombea wa chama cha upinzani.Kwa vile maamuzi ya wazanzibari walio wengi hayathaminiwi hata kidogo,hali inyaleta manun'guniko upande mmoja na kumfanya hata Rais mwenyewe kutowajibika ipasavyo kuwahudumia watu ambao kwake hawana umuhimu katika uchaguzi wa uteuzi wake.

Ukiwepo mfumo ambao utalazimu mgombea urais ahalalishe ushindi wake kwa kuapata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar. Njia hii itawafanya wagombea na vyama vyao wachacharike na kuwajibika ipasavyo kuhakikisha kuwa haki za utawala zinatapakaa pande zote za muungano ikiwa kama wanataka kushika hatamu za kutawala JMT.
Sema upendavyo, Urais wa Muungano utanda na Zanzibar kama Urais wa Zanzibar vile vile utakaribisa waTanganyika.
Otherwise forget Mzanzibari urais wa Muungano.
 
<<< Tatizo Umasikini Wa kipato kwa WASIMAMIZI >>>rushwa inahusika JECHA sasa Anaishi Kama KING anakula Fadhila >>
 
Si kila kitu kinafaa kuiga japo jambo zuri ni vizuri kuiga pia. Ni wapi duniani zaidi ya marekani mfumo wa electoral votes" unatumika??? na unajua kwa nn marekani wameweka mfumo huu??? kumbuka marekani inamajimbo 50 sasa wakiweka kura za wananchi ndo znachagua rais unadhani kuna ulazima wa wagombea kupiga kampeni nchi nzima?? wakati wanaweza tu kwenda kwenye majimbo wenye watu wengi tu mfano
California 38,332,521
Texas 26,448,193
New York 19,651,127
Florida 19,552,860
Illinois 12,882,135 so ukijiakikishia ushindi kwa majimbo hayo nani anauwezo wa kukuzuia???? na yale majimbo madogo yasingekuwa na nguvu ya kuchagua raisi ndo maana wakaweka watu kama 538 ambao wamegawanywa kimajimbo so ina mlazim mgombea kuzunguka mpaka kwenye mjimbo madogo kutafuta kura kwa ajiri ya kuzipata hizo Electoral College kwani hzo ndo zinafanya mtu aingie ikulu si kura za wananchi
 
Ni wazo zuri ila nikikumbuka ile ya kenya...mashine ni mpya na ndo ilikuwa kazi yake ya kwanza ila bado zikaharibika....daaah nagundua Africa kuacha kuiba kura ni sawa na kumiliki shamba la miwa karibu na primary school...ngojea pombe 2020 uone
 
Haahaha baada yakuona uchaguzi wa US ndo umekuja na hii issue?? Katiba mpya yenyewe mgogoro hivi hili wazo lako ndo unadhani hata wataliwazia?? Hii nchi ina maajabu hii si mchezo.
 
Sisi ni members wa the Commonwealth na mambo mengi yakiwamo yale ya uchaguzi yamerithiwa kutoka humo. Kwa mfano, UK ni muungano wa nchi nadhani nne hivi - England, Scotland, Wales, na Northern Ireland. Mfumo wao wa uchaguzi, kama ulivyo wa kwetu (muungano wa nchi mbili) ni "simple majority" na hakuna cha nchi hii ni ndogo au kubwa. Anayepata nyingi anabeba kila kitu. Ili tuweze kufuata huo wa Marekani, nadhani hatua ya kwanza ni kujitoa Commonwealth.
Ni kweli kama tungebaki na mfumo wa ufalme/Malkia kama huo wa UK, rai yako iko sahihi lakini Tanzania haina mfumo wa (monarchy) wala federation. Nitajie muungano wa nchi mbili ambao kumpata Rais kunatumika "simple majority".

Tanzania ina mfumo usioeleweka, ni wa kipekee dunia nzima. Mfumo wa Mkubwa kumtawala mdogo kwa mabavu. Kama hakuna cha nchi hii ni ndogo au kubwa, basi uwepo mfumo wa kupokezana nafasi ya urais.

Tupiganie tume huru za uchaguzi, hayo mengine yoooote yatanyooshwa
Tume huru ya uchaguzi milele haipatikani ikiwa Mkuu wa Mjeshi atabaki kuwa ni mwenyekiti wa CCM wakati uchaguzi ukifanywa!
Sema upendavyo, Urais wa Muungano utanda na Zanzibar kama Urais wa Zanzibar vile vile utakaribisa waTanganyika.
Otherwise forget Mzanzibari urais wa Muungano.
Naubaliana na wewe, kwa hilo ndio hasa sera ya CCM na ndio maana "forget mgombea urais kutoka CCM kama atapata kura za kumshinda mgombea urais wa chama cha upinzani Zanzibar Daima milele"
Mkuu,kura zinaendana na wingi wa watu.Huwezi kusema zanzibar yenye watu takribani Milioni Moja iwe sawa na Tanzania Bara yenye watu Takribani Milioni 50.
Marekani penyewe wanaenda na idadi ya watu ndio unapata Electroral Vote.Mfano,Alaska yenye watu wachache ina Electoral vote 3 wakati California yenye idadi kubwa ya watu ina Electoral vote 55.
USA ni muungano wa mataifa zaidi ya 50,yaliounganishwa kwa mtutu wa bunduki.Sisi muungano wetu wa hiari (tunavyoambiwa)na ni wa mataifa mawili yaliokuwa huru,hakuna teka wa vita,hivyo hoja ya idadi ya watu hapa haisimami. Ndio maana Zanzibar ina wabunge karibu 70 wanawakilisha watu hao miloni uliosema (mbunge mmoja anawakilisha takriban watu 14,000 tu).Idadi ya watu bado si hoja kwani mlikuwa mnajua kuwa Zanzibar ina idadi ndogo ya watu ukilinganisha na Tanganyika. Rai ya mgombea urais, bila kujali anatoka wapi lazima ashinde kwa kupata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar na halikadhalika bara. Vinginevyo ni sawa na ukoloni mambo leo na sawa kuiambia Zanzibar iendeleze harakati zake za kudai uhuru, mara hii kutoka Mkoloni Tanganyika.
Hata JK alipata KURA chache Zanzibar mwaka 2005? Sidhani mkuu
Pro.Lipumba ndio alikuwa kiboko wa mgombea Rais wa CCM mara zote isipokuwa 2015 wakati Lowassa alipoziba nafasi na kuchukua chapuo na kumchapa mgombea urais Kwa tiketi ya CCM
Huyo wakufumua ndo simuoni!
Rasimu ya Katiba ya Warioba!
Tatizo Zanzibar wachache.
Uchache wa wazanzibari ndio iwanaotaka mfumo huu kandamizi ufumuliwe. Uchachwa wa wazanzibari haukuanza jana wala juzi.Ulijuulikana siku ya mwanzo uliopandikizwa muungano. " Unless their is an ulterior motive, the system must be restructured"
 
USA ni muungano wa mataifa zaidi ya 50,yaliounganishwa kwa mtutu wa bunduki.Sisi muungano wetu wa hiari (tunavyoambiwa)na ni wa mataifa mawili yaliokuwa huru,hakuna teka wa vita,hivyo hoja ya idadi ya watu hapa haisimami. Ndio maana Zanzibar ina wabunge karibu 70 wanawakilisha watu hao miloni uliosema (mbunge mmoja anawakilisha takriban watu 14,000 tu).Idadi ya watu bado si hoja kwani mlikuwa mnajua kuwa Zanzibar ina idadi ndogo ya watu ukilinganisha na Tanganyika. Rai ya mgombea urais, bila kujali anatoka wapi lazima ashinde kwa kupata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar na halikadhalika bara. Vinginevyo ni sawa na ukoloni mambo leo na sawa kuiambia Zanzibar iendeleze harakati zake za kudai uhuru, mara hii kutoka Mkoloni Tanganyika.
Kitendo cha kukiri kwamba Zanzibar inawakilishwa na wabunge karibu 70 kati ya takribani wabunge 250 wa Bunge la Muungano ni ushahidi tosha kwamba hoja ya nusu kwa nusu haipo na haiwezekani.
 
Mfumo wetu wa kumpata Rais wa Jamhuri ya Tanzania uonekane wa kidemokrasia na halali zaidi ni kuufumua na kuja na mfumo eleweka unaozingatia haki na usawa.

Nilitafakari kwa kina uhalali wa mfumo wa uchaguzi wa Marekani na hoja ya kuchagua Rais kwa kutumia " electoral votes" badala ya " popular votes" na kubaini kuwa mfumo huo nihalali, mahiri,mzuri na wakuigwa na nchi zenye mfumo wa muungano na kuwa na Rais mmoja mtendaji.

Jamhuri ya muungano ni nchi mbili zilizoungana( Tanganyika na Zanzibar) na zina mfumo wa kuwa na Rais moja mtendaji,hivyo inapaswa Rais anaechaguliwa awe ana uhalali wa kupata ridhaa za pande zote za nchi washiriki wa Muungano.Hivyo kuondosha dhana ya mmoja mkubwa ya kumtawala mwenzake.

Kwa mfano tokea mfumo wa vyama vingi ulipoanza kutumika wakumpata Rais wa Jahuri ya muungano waTanzania hakuna awamu hata moja ambayo Rais wa Jamhuri alikubaliwa na wapiga kura wengi kutoka Zanzibar, nchi mshirika wa muungano.

Mara zote chaguo la wazanzibari limekuwa mgombea wa chama cha upinzani.Kwa vile maamuzi ya wazanzibari walio wengi hayathaminiwi hata kidogo,hali inyaleta manun'guniko upande mmoja na kumfanya hata Rais mwenyewe kutowajibika ipasavyo kuwahudumia watu ambao kwake hawana umuhimu katika uchaguzi wa uteuzi wake.

Ukiwepo mfumo ambao utalazimu mgombea urais ahalalishe ushindi wake kwa kuapata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar. Njia hii itawafanya wagombea na vyama vyao wachacharike na kuwajibika ipasavyo kuhakikisha kuwa haki za utawala zinatapakaa pande zote za muungano ikiwa kama wanataka kushika hatamu za kutawala JMT.
Kwanza zuia wizi wa kura na utaona mfumo wetu ni bora kuliko wa marekani
 
Kitendo cha kukiri kwamba Zanzibar inawakilishwa na wabunge karibu 70 kati ya takribani wabunge 250 wa Bunge la Muungano ni ushahidi tosha kwamba hoja ya nusu kwa nusu haipo na haiwezekani.
hiyo hoja ya nusu kwa nusu umeitoa wapi. Mimi nazungumzia njia kumpata Rais ambae atalazimika kuwajibika pande zote za muungano kwa kikamilifu. Hata hivyo lipi haliwzekani.Mfano rahisi kwa mtoto wa chekechea; Wabunge 70 kutoka Zanzibar, mbunge anawakilisha watu 14,000 na wabunge 250 kutoka bara, mbunge anawakilisha watu 200,000. Sasa huoni hilo ni zaidi ya nusu? Mfano mwengine mgumu kidogo,2015 angeshinda uchaguzi Lowassa uchaguzi,hili ninalolizungumzia lingekuwa limeshafikiwa.Lowassa amepata kura nyingi zaidi ya mgombea mwingine Zanzibar na bara angeshinda basi Lowassa angekuwa ametimiza masharti kuwa Rais anaekubalika Tanzania nzima. Isitokee watu wa zanzibar wakaanza kuimba "You are not my president"
 
hiyo hoja ya nusu kwa nusu umeitoa wapi.

Jibu linatoka kwako.

Ukiwepo mfumo ambao utalazimu mgombea urais ahalalishe ushindi wake kwa kuapata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar.
Hata hivyo umesema;
Lowassa amepata kura nyingi zaidi ya mgombea mwingine Zanzibar na bara angeshinda basi Lowassa angekuwa ametimiza masharti kuwa Rais anaekubalika Tanzania nzima. Isitokee watu wa zanzibar wakaanza kuimba "You are not my president"

Ukweli ni kwamba kuimba hakubadili uchaguzi uliohuru na haki kama kweli ulikuwa huru.
Ni sawa na wale jamaa wa pale USA wanaojitia hamnazo kwa kumpinga Trump.
 
Ni kweli kama tungebaki na mfumo wa ufalme/Malkia kama huo wa UK, rai yako iko sahihi lakini Tanzania haina mfumo wa (monarchy) wala federation. Nitajie muungano wa nchi mbili ambao kumpata Rais kunatumika "simple majority".

Tanzania ina mfumo usioeleweka, ni wa kipekee dunia nzima. Mfumo wa Mkubwa kumtawala mdogo kwa mabavu. Kama hakuna cha nchi hii ni ndogo au kubwa, basi uwepo mfumo wa kupokezana nafasi ya urais.

Tume huru ya uchaguzi milele haipatikani ikiwa Mkuu wa Mjeshi atabaki kuwa ni mwenyekiti wa CCM wakati uchaguzi ukifanywa!

Naubaliana na wewe, kwa hilo ndio hasa sera ya CCM na ndio maana "forget mgombea urais kutoka CCM kama atapata kura za kumshinda mgombea urais wa chama cha upinzani Zanzibar Daima milele"

USA ni muungano wa mataifa zaidi ya 50,yaliounganishwa kwa mtutu wa bunduki.Sisi muungano wetu wa hiari (tunavyoambiwa)na ni wa mataifa mawili yaliokuwa huru,hakuna teka wa vita,hivyo hoja ya idadi ya watu hapa haisimami. Ndio maana Zanzibar ina wabunge karibu 70 wanawakilisha watu hao miloni uliosema (mbunge mmoja anawakilisha takriban watu 14,000 tu).Idadi ya watu bado si hoja kwani mlikuwa mnajua kuwa Zanzibar ina idadi ndogo ya watu ukilinganisha na Tanganyika. Rai ya mgombea urais, bila kujali anatoka wapi lazima ashinde kwa kupata zaidi ya nusu ya kura halali au za juu zaidi za kura ziliopigwa Zanzibar na halikadhalika bara. Vinginevyo ni sawa na ukoloni mambo leo na sawa kuiambia Zanzibar iendeleze harakati zake za kudai uhuru, mara hii kutoka Mkoloni Tanganyika.

Pro.Lipumba ndio alikuwa kiboko wa mgombea Rais wa CCM mara zote isipokuwa 2015 wakati Lowassa alipoziba nafasi na kuchukua chapuo na kumchapa mgombea urais Kwa tiketi ya CCM
Rasimu ya Katiba ya Warioba!
Uchache wa wazanzibari ndio iwanaotaka mfumo huu kandamizi ufumuliwe. Uchachwa wa wazanzibari haukuanza jana wala juzi.Ulijuulikana siku ya mwanzo uliopandikizwa muungano. " Unless their is an ulterior motive, the system must be restructured"
Unatujazia server bure, huko kwenu tu hakiekeweki, sembuse kuja Tanganyika?
Mlivyowajinga Maalim na gubu lake hata kutia mkono tu shida!
 
Unatujazia server bure, huko kwenu tu hakiekeweki, sembuse kuja Tanganyika?
Mlivyowajinga Maalim na gubu lake hata kutia mkono tu shida!
Badilisha maharage ya kuganga njaa,uliokula jana .Yana onekana yanakupa shida kidogo ya kufikiri!
 
Back
Top Bottom