Mfaransa ashangaa LUKUBI apatayo Maximo

Mfumwa

JF-Expert Member
Aug 29, 2008
1,456
42
Mshahara wa Maximo wamshangaza Mzambia
Michael Momburi,Kampala

KOCHA wa Zambia ambae juzi aliteta na Marcio Maximo kwenye hoteli Ivys, ameshtushwa na mshahara wa kocha huyo na ameomba namba ya simu ya TFF.

Herve Renard ambae ni raia wa Ufaransa, timu yake ilitolewa juzi katika hatua ya makundi ya kombe la chalenji baada ya kufungwa mabao 2-0 na Sudan.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, kocha huyo alisema yeye analipwa dola 7000 za Marekani, lakini aliposikia Maximo analipwa dola

15,000 akashtuka na kushika mdomo.

Herve alisema kwamba amevutiwa na Tanzania baada ya kukaa na Maximo wakateta na akamuambia kwamba Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete na serikali yake wanathamini sana michezo na ndio mabosi wake.

Kocha huyo alisema kwamba anatamani kufanya kazi Tanzania kutokana na mambo aliyoyasikia.

"Hela nyingi sana hizo analipwa Maximo inaonekana mnapenda sana michezo namna viongozi wazuri,"alisema kocha huyo kijana.

"Kwani mkataba wa Maximo unamalizika lini? Nipe na namba ya Rais wa Shirikisho lenu,Tanzania ni nchi nzuri sana."

Kocha huyo baada ya kuambiwa kwamba Maximo mkataba wake unamalizika Julai na amegoma kuongeza, aliomba namba ya Rais wa TFF, Leodegar Tenga, lakini hakutaka kuweka bayana ni ya nini.

Herve ambae timu yake ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa, alisema kwamba anaelekeza nguvu zake kwenye michuano ya CHAN mwezi ujao.
Source: Mwananchi Read News
 
...nao, si wangempa namba ya Mo' Dewji?

BTW mfumo wa uchezaji kutumia akili+mbinu wa nchi za ulaya hautufai sie wa Africa mashariki, bora huo huo wa vipaji+nguvu wa Maximo toka America kusini.
 
Duh nchi yetu bwana...we spend more on Football then we do on promoting ICT for development....aibuuuu!!!!
 
Kama kweli mahela yenyewe anayolipwa ni hayo mbona hayalingani na tija anayotupa!!!!, Afu mtu mwenyewe anatudengulia na kutikisa kiberiti cha kutoendelea kufundisha, ni bora mkataba ukiisha aondoke zake. TFF mleteni Paulo Ince baada ya Maxcimo kumaliza mkataba
 
Mbona hy iko wazi kuwa jamaa anakula kama 18m kwa mwezi ndio maana analeta kocha viungo anamlipa yeye maximo upo???lakini ni pesa ndogo sana ukilinganisha na nchi za karibu tu hapo sudan au misri
 
...nao, si wangempa namba ya Mo' Dewji?

BTW mfumo wa uchezaji kutumia akili+mbinu wa nchi za ulaya hautufai sie wa Africa mashariki, bora huo huo wa vipaji+nguvu wa Maximo toka America kusini.

+Hapa ni vice versa! Ulaya ndio vipaji + nguvu Latin America ndio akili + mbinu
 
Mbona hy iko wazi kuwa jamaa anakula kama 18m kwa mwezi ndio maana analeta kocha viungo anamlipa yeye maximo upo???lakini ni pesa ndogo sana ukilinganisha na nchi za karibu tu hapo sudan au misri

Kwa Wamisri tija inaonekana, na hata kwa Wasudani na ndo mana tulivyowapiga bao ulisikia nini kiliendelea. Sasa huyu jamaa mpaka timu ikiwa imeshatolewa (tiketi ya kombe la dunia na mataifa ya afrika) ndo inashinda, haileti ladha. Haijengi timu ikawa na consistance ndo maana waganda wakatufunga.

Mechi yetu na Uganda ilikuwa ni ngumu sana lakini inaonyesha benchi la ufundi waliiona kuwa ni rahisi na hasa yale mazoea ya kusema tunahitaji suluhu ya aina yeyote tu, afu tunacheza na Uganda ambao wameshafuzu, kumbe jamaa wana kisasi cha kuwafunga kwenye mashindano ya wachezaji wanaochezea ligi za ndani
 
Back
Top Bottom