Mfanyakazi wa Bodi ya Mikopo akamatwa kwa kuingiza Majina hewa na kujipatia ulaji mil 91

Haya majitu ni majizi makubwa sema bado wengi hamjayashtukia!Hebu naomba mnisaidie wadau,ni shirika gani la ndege linalotoza one way ticket Dar to Shanghai kama final destination kwa dola 1900?Nina ushahidi wa ndugu yangu ambaye yupo huko kimasomo ticketi yake iliyogharamiwa na loan board inasomeka hivyo!Ndiyo mchezo wao haya majitu sema hili litakuwa wamelichomekea tu labda walipishana maslahi!!
 
kwa hiyo hao mkuu Kayla hapa ukisikia kuna watu wanadai mwalimu anaweza kulipwa 800,000/ - 1,200,000/- mnaambiwa hizo ni siasa!
Ukweli unakuwa unajulikana lakini kwa hilo tu mbali na utendaji mbovu (HRM wanasema kazi bila job description against job evaluation) mfanyakzi mmoja anahesabiwa hiyo, unakuta 60% ya wafanyakazi hapo wako pia lanked kwenye kiwango hichohicho cha wizi. Na hicho ni KAKITENGO kamoja kwenye cycle ya serikali, can you imagine!!!!!!??
Sio rahisi huu mfumo kujibadilisha wenyewe bali inabidi atokee nje ya system iliyopo kurekebisha haya mambo yote.

Haishangazi kuona Mzee Mwanakijiji aliwahi kutoa tena bure structue nzuri sana ya ni jinsi gani bodi hii inaweza kufanya kazi kwa ufanisi ikihudumia waoote wenye kuhitaji mikopo lakini waliolikataa hilo wazo walijua ni kwanini. Ni suala la muda tu kwa binadamu kukubaliana na ujinga wa namna hii japo kwa TZ naona huo muda wa kusubiria kufanya maamuzi umezidi mipaka.

For really, it is not an easy Task but is achievable.
Database na system nzima ya bodi ya yetu ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ni mbovu na inatoa mwanya wa kuibiwa na kuwaibia watanzania maskini waliotukopesha. Wiki iliyopita kwenye website yao wametoa majina ya wadaiwa na vitisho kibao, miongoni mwao kuna majina ya watu ambao wameshamaliza kulipa mikopo yao, kuna ambao bado tunaendelea kuwalipa lakini wao taarifa zao zinaonesha hata kuripoti na kupeleka taarifa zetu huko bado. Wizi mtupu.
 
Dah..yeye atakuwa ni kadaraja tuu....hii deal itakuwa inawahusisha wengi kuanzia ndani mpaka vyuoni...ngoja kesi ikianza ndio watatajwa...hawezi kufanikisha zoezi kubwa kiasi hicho peke yake
 
wafanyakazi wengi wa bodi ya mikopo wanamajumba na mashamba let alone magari ya kifahari
jeuri hii wanaipata wapi? namfahamu mmoja amejenga bonge la jumba tena kijijini la garama kubwa
dar ana majumba sinza na bunju,kwa cheo chake na hela hizo havilingani
wachunguzwe wote ikiwezekana wakaguliwe mali zao
wizi mtupu huyo dada hayuko peke yake ni chambo tu
wakamuaji wametulia ofisini kwao,
 
huu ndo upumbavu wa serikali yetu,mnasema hamna hela lakini mtu anaiba mpaka 90 mil.......crap
 
Maleria Sugu,acha chokochoko za udini bhana,am a muslim cpend haka ka'tabia,mbona waislam wengi wanapga sala 5 na wanakwapua mali?
 
Wanafunzi wanakosa bum ye anafisadi!! Atafunhwa mia ka miwili tu kama martyna alivyosema. Au
 
Haya majitu ni majizi makubwa sema bado wengi hamjayashtukia!Hebu naomba mnisaidie wadau,ni shirika gani la ndege linalotoza one way ticket Dar to Shanghai kama final destination kwa dola 1900?Nina ushahidi wa ndugu yangu ambaye yupo huko kimasomo ticketi yake iliyogharamiwa na loan board inasomeka hivyo!Ndiyo mchezo wao haya majitu sema hili litakuwa wamelichomekea tu labda walipishana maslahi!!

though cjawai panda ndege,ila dah dola 190O,ndo iwe naul?
 
Amekwiba kama wengi wanavyofanya. Na jamii nzima kwa kawaida tunachangia uovu huu kwani tunawashangilia wale wanaoishi kwa anasa zilizopindukia bila vipato vinavyojulikana.
 
Amesoma udsm then mastaz yake kachukulia mzumbe, mwenye kubisha aseme ukweli maana hivi vyuo ndo chimbuko la majambazi na mafisadi plus majambazi wa elimu a.k.a wenye vyeti vya kufoji. na ndo ukweli wenyewe juu ya hivi vyuo au tuwataje wenye udr wa kufoji na majambazi? wananikela na hivi vyuo vinanikela mpaka nataka kutapika! natamani vifutwe kabisa!
 
Amesoma udsm then mastaz yake kachukulia mzumbe, mwenye kubisha aseme ukweli maana hivi vyuo ndo chimbuko la majambazi na mafisadi plus majambazi wa elimu a.k.a wenye vyeti vya kufoji. na ndo ukweli wenyewe juu ya hivi vyuo au tuwataje wenye udr wa kufoji na majambazi? wananikela na hivi vyuo vinanikela mpaka nataka kutapika! natamani vifutwe kabisa!
I will be back
 
Mbuzi wa kafara huyu, ishu kama hii ina mtandao mkubwa. Wanaosaini hati za malipo wanajua na wanatamka hizo takwimu hata kwenye vikao. Kumbe kuishi kwingi kuona mengi, utawaona wanabinua midomo kumbe wanawaibia wanaowabinulia midomo.
 
ndio maana 2nd year sikupata hela yangu ya field kumbe huyu sista duu alikuwa ananunulia vipodozi!!
 
Back
Top Bottom