Kuna mfanyakazi mmoja alikabidhiwa ofisi ya umma. Ndani ya miaka 2 akawa amepata shoti ya shillingi milioni 3, na alipoitwa na menajimenti akakiri kutenda kosa hilo na yupo tayari kurejesha fedha kwa kukatwa kwenye mshahara wake wa kila mwezi. Lakini hatua ya kwanza alitolewa kwenye kile kitengo. Na hata baada ya muda wa miezi 6 hayajafanyika makato yoyote ikabidi mkuu wa idara amwandikie barua ya kujieleza ni kwanini hatua za kinidhamu zisichukulie dhidi yake kwa kutumia mali ya umma kwa manufaa yake binafsi. Akajielezea kwa maandishi kuwa mbona alikwisha onyesha ushirikiano kwa kuruhusu makato kwenye mshahara wake isipokuwa ni muajiri tu ndio hajaanza kukata. Baada ya barua hiyo kumekuwa na kimya cha muda kidogo na sasa jana ameandikiwa notisi ya siku 14 atoe maelezo namna fedha hizo zilivyotumika.
Sasa swali langu ni kuwa anaweza kujitetea vipi katika suala hilo.
Sasa swali langu ni kuwa anaweza kujitetea vipi katika suala hilo.