Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Global Publishers
Mauaji ya kutisha yaliyofanywa na wananchi wenye hasira dhidi ya kijana aliyejulikana kwa jina moja la Idd aliyetuhumiwa kutaka kuiba mbuzi kwenye banda eneo la Kigogo jijini Dar es Salaam, yamelaaniwa na baadhi ya wakazi wa eneo hilo.
Licha ya kijana huyo kufumwa akiiba, wananchi hao walisikitishwa na namna kijana huyo alivyoteswa hadi kuuawa.
Ilielezwa na mwanamke mmoja mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Mama Omari kuwa, mtuhumiwa akiwa na wenzake wawili walinaswa na wananchi majira ya alfajiri wakifanya jaribio la kuiba mbuzi kwenye banda la mzee mmoja (jina halikutajwa).
Alisema mama huyo aliyeshuhudia unyama aliofanyiwa Idd kwamba, wakiwa kwenye harakati za kumtwaa mbuzi huyo, mwenye mali aliwaona na kuwapigia kelele za mwizi ambapo wananchi walijitokeza na kumnasa kijana huyo, huku wengine wakifanikiwa kukimbia.
"Walipomkamata walimvua nguo, wakaanza kumkata na viwembe, kumpiga kwa mawe huku wakimtaka atubu dhambi zake kabla ya kumtoa uhai.
Baadaye walimchoma moto hadi ngozi ikatoka akawa anahangaika, watu hawakujali wakaendelea kumtesa hadi alipokata roho," alisema mama huyo kwa masikitiko.
Mwananchi mmoja mkazi wa Kigogo ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini alisema kuwa, kitendo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi kinatokana na watu kuchoshwa na vitendo vya kihalifu.
"Kwa mfano eneo letu vibaka ni wengi sana, watu wanaibiwa kila siku na wahusika wanakamatwa lakini siku mbili wanaonekana tena mitaani, ndiyo maana watu wanajichukulia sheria mkononi," alisema Hamis Juma.
Hata hivyo, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Kamanda Abdallah Msika amekuwa akiwaomba wananchi kutochukua sheria mkononi na kuwataka wawe wavumilivu wakati jeshi lake likiendelea kuweka mikakati ya kukomesha vitendo vya uhalifu nchini.
NB:
Naamini Waziri Mkuu alimaanisha kitu kama hiki. Ingawa kwenye kesi za wizi wa "mbuzi" adhabu ya kifo namna hii ni kitu cha kulaaniwa, nina uhakika kama jamii tuko tayari kuona wauaji wa albino wakipewa kibano namna hii na kuuawa papo hapo.
Kwa vile serikali imetoa kinga kwa wananchi kuchukua sheria mikononi, tusishangae kuona picha za namna hii zikidai kuwa "x ni muuaji wa albino". Waziri Mkuu ambaye alilia kuona mauaji ya albino sijui anaweza kujisikia vipi watu wakianza kutiwa moto, kupata kipigo namna hii kwa kisingizio cha "kutekeleza agizo la serikali".
Mauaji ya kutisha yaliyofanywa na wananchi wenye hasira dhidi ya kijana aliyejulikana kwa jina moja la Idd aliyetuhumiwa kutaka kuiba mbuzi kwenye banda eneo la Kigogo jijini Dar es Salaam, yamelaaniwa na baadhi ya wakazi wa eneo hilo.
Licha ya kijana huyo kufumwa akiiba, wananchi hao walisikitishwa na namna kijana huyo alivyoteswa hadi kuuawa.
Ilielezwa na mwanamke mmoja mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Mama Omari kuwa, mtuhumiwa akiwa na wenzake wawili walinaswa na wananchi majira ya alfajiri wakifanya jaribio la kuiba mbuzi kwenye banda la mzee mmoja (jina halikutajwa).
Alisema mama huyo aliyeshuhudia unyama aliofanyiwa Idd kwamba, wakiwa kwenye harakati za kumtwaa mbuzi huyo, mwenye mali aliwaona na kuwapigia kelele za mwizi ambapo wananchi walijitokeza na kumnasa kijana huyo, huku wengine wakifanikiwa kukimbia.
"Walipomkamata walimvua nguo, wakaanza kumkata na viwembe, kumpiga kwa mawe huku wakimtaka atubu dhambi zake kabla ya kumtoa uhai.
Baadaye walimchoma moto hadi ngozi ikatoka akawa anahangaika, watu hawakujali wakaendelea kumtesa hadi alipokata roho," alisema mama huyo kwa masikitiko.
Mwananchi mmoja mkazi wa Kigogo ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini alisema kuwa, kitendo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi kinatokana na watu kuchoshwa na vitendo vya kihalifu.
"Kwa mfano eneo letu vibaka ni wengi sana, watu wanaibiwa kila siku na wahusika wanakamatwa lakini siku mbili wanaonekana tena mitaani, ndiyo maana watu wanajichukulia sheria mkononi," alisema Hamis Juma.
Hata hivyo, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Kamanda Abdallah Msika amekuwa akiwaomba wananchi kutochukua sheria mkononi na kuwataka wawe wavumilivu wakati jeshi lake likiendelea kuweka mikakati ya kukomesha vitendo vya uhalifu nchini.
NB:
Naamini Waziri Mkuu alimaanisha kitu kama hiki. Ingawa kwenye kesi za wizi wa "mbuzi" adhabu ya kifo namna hii ni kitu cha kulaaniwa, nina uhakika kama jamii tuko tayari kuona wauaji wa albino wakipewa kibano namna hii na kuuawa papo hapo.
Kwa vile serikali imetoa kinga kwa wananchi kuchukua sheria mikononi, tusishangae kuona picha za namna hii zikidai kuwa "x ni muuaji wa albino". Waziri Mkuu ambaye alilia kuona mauaji ya albino sijui anaweza kujisikia vipi watu wakianza kutiwa moto, kupata kipigo namna hii kwa kisingizio cha "kutekeleza agizo la serikali".