PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Wengi tulishasoma habari za Mfalme Herode wa Israel jinsi alivyoamua kuua watoto wote wachanga wa kiume, baada ya kupata habari kutoka kwa Mamajusi wa Mashariki, kuwa amezaliwa mtoto ambaye atakuwa mfalme wa Uyahudi nzima.
Herode alikuwa na wasiwasi kuwa mtoto huyo aliyezaliwa atampora nafasi yake ya Ufalme, na kumharibia heshima yake kwa jamii! Lakini pamoja na Herode kufanikiwa kuwaua watoto wote wa kiume huko Bethehemu, Yesu alisalimika baada ya wazazi wake kuonywa kupitia ndoto kuwa wakimbilie Misri wakajifiche huko.
RC wa Dodoma jana alipiga marufuku mikutano ya Kisiasa mjini Dodoma kwa kisingizio cha uwepo wa vikao vya Bunge, na hivyo anahofia wageni kuwa wengi mno Dodoma kiasi cha kushindikana kudhibitiwa.
Je mkuu huyu wa mkoa ametafiti na kukuta kuwa mikutano ya siasa inaleta wageni wangapi mjini Dodoma?
Lakini hapohapo sheria ya nchi hii inaruhusu raia yeyote kuwepo sehemu yoyote ya nchi hii, ili mradi kama hahalifu sheria. Pia mikutano ya kisiasa ni haki ya msingi ya vyama vya siasa.
Hakuna kumbukumbu zozote zilizoonyesha kuwa mikutano ya kisiasa imeshawahi kukwamisha shughuli za Bunge, maana mikutano hii inahudhuriwa na wananchi wa kawaida ambao si sehemu ya Bunge.
Ikumbukwe pia kuwa amri hii imekuja baada ya chama cha Chadena kufanya mkutano wakemkubwa leo katikA Viwanja vya Barafu Mjini Dodoma.
Je, katazo hili la Mkuu wamkoa wa Dodoma ni kama hofu ya Mfamle Herode ya kuzaliwa kwa Chama kitakachochukua madaraka ya watawala waliomweka madarakani?...tujiulize na kutafakari!
Herode alikuwa na wasiwasi kuwa mtoto huyo aliyezaliwa atampora nafasi yake ya Ufalme, na kumharibia heshima yake kwa jamii! Lakini pamoja na Herode kufanikiwa kuwaua watoto wote wa kiume huko Bethehemu, Yesu alisalimika baada ya wazazi wake kuonywa kupitia ndoto kuwa wakimbilie Misri wakajifiche huko.
RC wa Dodoma jana alipiga marufuku mikutano ya Kisiasa mjini Dodoma kwa kisingizio cha uwepo wa vikao vya Bunge, na hivyo anahofia wageni kuwa wengi mno Dodoma kiasi cha kushindikana kudhibitiwa.
Je mkuu huyu wa mkoa ametafiti na kukuta kuwa mikutano ya siasa inaleta wageni wangapi mjini Dodoma?
Lakini hapohapo sheria ya nchi hii inaruhusu raia yeyote kuwepo sehemu yoyote ya nchi hii, ili mradi kama hahalifu sheria. Pia mikutano ya kisiasa ni haki ya msingi ya vyama vya siasa.
Hakuna kumbukumbu zozote zilizoonyesha kuwa mikutano ya kisiasa imeshawahi kukwamisha shughuli za Bunge, maana mikutano hii inahudhuriwa na wananchi wa kawaida ambao si sehemu ya Bunge.
Ikumbukwe pia kuwa amri hii imekuja baada ya chama cha Chadena kufanya mkutano wakemkubwa leo katikA Viwanja vya Barafu Mjini Dodoma.
Je, katazo hili la Mkuu wamkoa wa Dodoma ni kama hofu ya Mfamle Herode ya kuzaliwa kwa Chama kitakachochukua madaraka ya watawala waliomweka madarakani?...tujiulize na kutafakari!