Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Meya Arusha aanika mikakati yake Tuesday, 28 December 2010 20:16
Happy Lazaro, Arusha
HALMASHAURI ya Jiji la Arusha limejiwekea mikakati mipya ya ukusanyaji mapato na kuhakikisha yanaongezeka kwa asilimia 80, kipindi cha miaka miwili ijayo.
Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo, alisema mkakati mkubwa ni kuhakikisha vyanzo vya mapato vinaongezeka, huku wakibuni mbinu mpya ya ukusanyaji ambayo haitasumbua wananchi.
Lyimo alisema badala ya kuwatumia watumishi wake kukusanya mapato, atakuwa wasimamizi na kwamba, watawatumia mawakala na wakusanyaji kodi ili kufuatilia kwa undani zaidi.
Tunachotaka kufanya ni kuhakikisha kuwa, ukusanyaji kodi wetu unakuwa wa kisasa zaidi ambao hautasumbua wananchi wetu na kwa njia hiyo, kila mwananchi atapenda kulipa kodi kwa hiari yake, alisema Lyimo.
Alisema lengo ni kuhakikisha kuwa ndani ya miaka miwili, jiji hilo linaweza kukusanya mapato kwenye vyanzo mbalimbali kwa umakini zaidi na kwa muda muafaka bila kusumbua wananchi.
Lyimo alisema licha ya kuweka mikakati hiyo mipya ya ukusanyaji kodi, pia atahakikisha anaongeza barabara ili kuepukana na msongamano uliopo.
Aliendelea kuwa barabara zilizopo nje ya mji zitatengenezwa kwa kiwango cha lami, huku nyingine ambazo ni chakavu zikikarabatiwa ili kuongeza hadhi ya jiji.
Lyimbo alisema kwenye mikakati ya kuongeza barabara, watahakikisha kuwa wanaongeza madaraja mengi iwezekanavyo, lengo likiwa ni kuunganisha kijiji kimoja hadi kingine ili kuboresha mawasiliano.
Pia, alisema watahakikisha wanaboresha utalii wa ndani kwa kuweka mikakati mbalimbali ya kuboresha milima ambayo ni vivutio kwa watalii walio wengi.
Kuhusu usafi wa jiji, Lyimo alisema wamejiwekea mikakati mbalimbali kuhakikisha suala la usimamizi wa mazingira linabinafsishwa kwa watu binafsi.
Alisema sheria zitatungwa kwa mtu anayetupa taka ovyo kuchukuliwa hatua kali, ikiwamo kutozwa faini.
Happy Lazaro, Arusha
HALMASHAURI ya Jiji la Arusha limejiwekea mikakati mipya ya ukusanyaji mapato na kuhakikisha yanaongezeka kwa asilimia 80, kipindi cha miaka miwili ijayo.
Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo, alisema mkakati mkubwa ni kuhakikisha vyanzo vya mapato vinaongezeka, huku wakibuni mbinu mpya ya ukusanyaji ambayo haitasumbua wananchi.
Lyimo alisema badala ya kuwatumia watumishi wake kukusanya mapato, atakuwa wasimamizi na kwamba, watawatumia mawakala na wakusanyaji kodi ili kufuatilia kwa undani zaidi.
Tunachotaka kufanya ni kuhakikisha kuwa, ukusanyaji kodi wetu unakuwa wa kisasa zaidi ambao hautasumbua wananchi wetu na kwa njia hiyo, kila mwananchi atapenda kulipa kodi kwa hiari yake, alisema Lyimo.
Alisema lengo ni kuhakikisha kuwa ndani ya miaka miwili, jiji hilo linaweza kukusanya mapato kwenye vyanzo mbalimbali kwa umakini zaidi na kwa muda muafaka bila kusumbua wananchi.
Lyimo alisema licha ya kuweka mikakati hiyo mipya ya ukusanyaji kodi, pia atahakikisha anaongeza barabara ili kuepukana na msongamano uliopo.
Aliendelea kuwa barabara zilizopo nje ya mji zitatengenezwa kwa kiwango cha lami, huku nyingine ambazo ni chakavu zikikarabatiwa ili kuongeza hadhi ya jiji.
Lyimbo alisema kwenye mikakati ya kuongeza barabara, watahakikisha kuwa wanaongeza madaraja mengi iwezekanavyo, lengo likiwa ni kuunganisha kijiji kimoja hadi kingine ili kuboresha mawasiliano.
Pia, alisema watahakikisha wanaboresha utalii wa ndani kwa kuweka mikakati mbalimbali ya kuboresha milima ambayo ni vivutio kwa watalii walio wengi.
Kuhusu usafi wa jiji, Lyimo alisema wamejiwekea mikakati mbalimbali kuhakikisha suala la usimamizi wa mazingira linabinafsishwa kwa watu binafsi.
Alisema sheria zitatungwa kwa mtu anayetupa taka ovyo kuchukuliwa hatua kali, ikiwamo kutozwa faini.