Message ya kugomea sensa

Ni muhimu kipengele cha dini kiwepo ili kama taifa lisilo na dini iweze kuwatambua kati ya wananchi wake ni wangapi wapagani,wakristo,waislamu ni wangapi.Huu uwoga wa baadhi wa watu sijui wa nini
 
kwani waislam wanataka nini ili washiriki?kama ubwabwa si wapikiwe!? ila ndizi waje nazo....
 
Watakaolala bar wataesabiwa vipi? na Night club. Naomba majibu. Sensa ni nzuri kwa wanaojua maana yake
 
Mkuu Petrol, zoezi la sensa ni la lazima sio option kama uchaguzi, its a must hakuna room ya kusema anayetaka!.

Mimi nawaunga mkono ndugu zetu Waislamu ili kikiongezwa hicho kipengele cha dini na cha kabila tutakipenyeshea hapo hapo angalau tujue wale Wahdzabe waliokuwa 250 sasa wamebaki wangapi. Miaka ya 80 iliwachukua kinguvu watoto wao 4 na kuwasomesha boarding mpaka la 7 hakuna aliyefaulu, lakini wote wanne wakapelekwa Pugu na kusomeshwa mpaka form four, wote walipata Div. 0!. Wakarudishwa kwao msituni ili kupeleka civilization kwa ndugu zao ikiwa ni pamoja kuwajengea nyumba za kisasa na kupewa nguo na vifaa vya kisasa!. Baada ya mwezi mmoja serikali ilirudi kuwatrace ilikuta vile vitu vyote walivyowapa viko pale pale walipoviacha na yale makazi yakiwa kama yalivyo na more surprising hata zile nguo za wale wasomi 4 nazo walizivua na kuziacha!.

Hivi tutaendelea kuwategemea wazungu mpaka lini?. Wazungu watuhesabie tembo wetu, Mama Jane Goodhall atuhesabie sokwe wetu!, sasa hata makabila yetu nayo ndio tusuburi wazungu watuhesabie?!.

Tulipopata uhuru tulikuwa na makabila milioni 12 na makabila 120, kwa wastani wa watu laki moja kila kabila, sasa tunaenda milioni 50 kwanini tusijue na makabila!.

Mfano wangejua kabila linaloongoza kwa procreation ni kabila gani ili elimu ya uzazi wa mpango iwe concetrated huko na makabila gani yana hatari ya kufutika ili yaingizwe kwenye 'endagered species' ili kuyalinda!.

Wangapi kati yenu mnajua Watindiga wamebaki wangapi?, Wahadzabe, Wasandawi, Wataturu Wabalungi, Wakonongo etc. etc.

Kuna ubaya gani kujua tunawapagani wangapi, Hindu, Budha, Bahai, Baniani, Waislamu wa Ahamadiya, Waislamu wa Shia, Waislamu wa Sunni, Waislamu wa Ismailia, Waislamu Makadiani etc?. Kuna ubaya gani?.

Kama rais wa kwanza wa Tanzania alikuwa Mkatoliki, Mkapa nae ni Mkatoliki, Membe, Dr. Slaa na Magufuli nao ni Wakatoliki wanaosubiria kupangishwa pale nyumba nyeupe!, kuna ubaya gani tukiwajua wako wangapi, na Anglicana wangapi, Walutheri, Waadvetisti Wasabato, Memonite, Walokoke etc. etc. Hivi kuna ubaya gani?.
Mkuu Pasco, idadi ya watu ikiongezeka na makabila yao nayo yanaongezeka?
 
Kaka kama sentensi yako ilivyoanza basi nawe umeteleza. Ustawi wa jamii unahitaji kujua idadi ya watu kwa mujibu wa itikadi zao otherwise wanavyopima viwanja wasingepima maeneo ya kufanyia ibada. haiingii akilini wewe kama mtaalam upime eneo la kuweka kanisa mfano AGP uweke sehemu ya kuabudu wafuasi wa AGP 30 nawakati wao wenyewe wako 400. jamani mbona elimu zetu mbona hazitubadilishi? tatizo ni nini
Acha kupotoka kama sio kupotoshwa .Idadi ya watu huendana sambamba na eneo ya mraba wanapoishi hivyo si kweli kwamba kujua waisilamu/wakristo wakijulikana ni wangapi eneo fulani itasaidia kujua ukubwa wa msikiti/kanisa.mfano eneo ya 100000 m[SUP]2 [/SUP]linatarajiwa liwe na watu 100 na kuwepo na huduma za jamii zinazoendana na idadi ya watu hao.

Watu wanapoongezeka makazi yanapanuliwa ndio maana kuna kuwa na upimaji wa viwanja vipya kila kukicha sambamba na makadirio ya idadi ya watu kwa eneo la mraba.

Usichanganye mambo hayo unayoaanisha ni athari za mlundikano wa watu sehemu moja. Huduma za jamii na miundombinu lazima ziwe finyu.

Funguka ,tumia elimu yako kubwa kuliko yangu kufikirisha ubongo zaidi.
 
Yaani wewe ni mweupe kichwani sijapata kuona, si kila lisemwalo na waislam basi wewe upinge hata kama huna hoja.
soma hii sensa ya india iliyoweka na dini, soma matokeo yake kisha nambie je, hauhitaji kufanya intervention kwa baadhi ya maeneo, kielimu, kiafya, kiuchumi ili kuwainua wananchi wa taifa kiujumla?
http://censusindia.gov.in/Ad_Campaign/drop_in_articles/04-Distribution_by_Religion.pdf

Kaishi india basi na wewe mwenye akili nyingi na uelewa wa juu zaidi.

Matatizo ya India wewe huyajui ndio maana unakurupuka kutetea jambo usilolijua .Zungumzia adhari za kuorodhesha watu kidini kwa mazingira ya tz acha kukwepa hoja ya msingi.

Hao wanaotoa haya matamko wameshatoa matamko mengi sana yenye mrengo wa kibaguzi kuwaona wenzao hawana maana kuwa wao wanaonewa.Hao si waisilamu hata siku moja ni watu wenye ajenda zao za siri wanatumia kivuli cha uisilamu ,waisilamu tunaishi nao mitaani na tunajua tabia zao na ustaarabu wao,hao ni wahuni ambapo hata kwenye dini ya /kikristo wapo.

Hivi nchi hii kila kikundi kikiwa kinatoa tamko la kuishurutisha serikali tutafika kweli!!!?. Huwezi wewe ukataka kuwa Lawyer/Engineer wakati unaipuuzia elimu dunia.
 
Kaka msg umeisoma ukiwa na mtizamo hasi, na hili ni tatizo siyo kwako tu bali hata kwa wenzako wengi. Msg haichochei kitu isipokuwa ni taarifa ya kiimani inayowahusu waislam, wewe kama siyo muislam hiyo msg haikuhusu na wewe jipange kuendelea na sensa. madai ya waislam ni ya kimsingi na hakuna hoja ya kuyafanya yaonekane kama hivyo unavyodhani. acha msg serikali imesha pewa taarifa ya kimaandishi kuwa kama sensa haitoweka vipengele muhimu basi mhesabiane nyinyi wenyewe wengi wakristo. Ni aibu kubwa sana kwenu kwani mitandao yenu mnajitangaza mko wengi sasa mwahofia nini kwa kipengere cha dini kuwekwa? Mrudieni Mungu, otherwise mtapotea.

namshukuru mungu wangu mimi sio muislam, huko ninako abudu sipewi vitisho wala kulazimishwa, nafundishwa tu kwambą nifanye yampendezayo mola.

sasa mnaanza kusema atakayeshiriki sensa atakiona mbele za Allah... mmeongea naye lini?
 
Hawa watu wangefanya mgomo wa kuishinikiza serikali iwajengee shule za kutosha ili kuondoa ukungu uliojaa vichwani mwao,ama sivyo hawa watu watatupa shida sana. Hii tabia ya kushinda kwenye nyumba za ibada siku nzima inawaharibu sana
 
ni uoga tu wa serikali inayoendekeza udini,kimsing sion tatiozo la kuongeza kipengele cha dini katika dodoso za sensa, viongozi wetu bwana,walitumia dini kuingia madarakani leo wanaiogopa shit!!!!
 
Hivi kweli bado kuna msomi wa kiwango cha JF anayeamini sensa inaweza kuwasaidia CCM kupanga maendeleo ya Nchi hii?
 
Kaka msg umeisoma ukiwa na mtizamo hasi, na hili ni tatizo siyo kwako tu bali hata kwa wenzako wengi. Msg haichochei kitu isipokuwa ni taarifa ya kiimani inayowahusu waislam, wewe kama siyo muislam hiyo msg haikuhusu na wewe jipange kuendelea na sensa. madai ya waislam ni ya kimsingi na hakuna hoja ya kuyafanya yaonekane kama hivyo unavyodhani. acha msg serikali imesha pewa taarifa ya kimaandishi kuwa kama sensa haitoweka vipengele muhimu basi mhesabiane nyinyi wenyewe wengi wakristo. Ni aibu kubwa sana kwenu kwani mitandao yenu mnajitangaza mko wengi sasa mwahofia nini kwa kipengere cha dini kuwekwa? Mrudieni Mungu, otherwise mtapotea.

JK Watu hawa umewalea sasa wanakutumbulia nyongo usoni. Haitakuwa rahisi tena kuongoza watu hawa. Mwanzo mlianzisha siasa za misikitini ili kupambana na Chadema. Lakini ukimfundisha mtoto kutukana wakubwa siku moja atakutukana wewe mwenyewe.
 
[h=2] Allah Promised the Land of Israel to the Jews[/h] by Tamar Yonah

Allah Promised the Land of Israel to the Jews
My weekly guest, I.Q. Al Rassooli, is an Arab originally from Iraq. Today, he lives in the West, at an unknown location to protect himself. He is an expert on the Koran, and because of this, he is no longer a Muslim. Here is what he wrote me showing that Allah promised the Land of Israel to the Jews.
----------------------------------------------------------------------
Muhammad_8.jpg

Al Israa 17: 104 And We said thereafter to the Children of Israel "Dwell securely in the land (of promise)":
*** Allah, in very clear Arabic, asserts that he fulfilled his promise to reward the People of Israel with the Promised Land, the same land that the later conquering hordes of Muhammadan Arabs claim as exclusively theirs CONTRARY to their own Quran ***
Al Baqara 2: 40 O Children of Israel! call to mind the (special) favor which I bestowed upon you and fulfill your covenant with Me as I fulfill My covenant with you and fear none but Me.
Al Baqara 2: 47 O Children of Israel! call to mind the (special) favor which I bestowed upon You and that I preferred you above the whole world
Al Baqara 2: 122 O Children of Israel! call to mind the special favor which I bestowed upon you and that I preferred you above the whole world.
Al Dukhan 44: 30 We did deliver aforetime the Children of Israel from
humiliating Punishment
31 Inflicted by Pharaoh for he was arrogant (even)
among inordinate transgressors.
32 And We chose them aforetime above all the nations
knowingly
Al Jathiyah 45: 16 "We did aforetime grant to the Children of Israel the Book (Torah), the Power of Command and Prophethood; We gave them for Sustenance things good and pure; and We favored them above all the nations"
Believers & Unbelievers, please be aware, that the Quran, in verse after verse, repeatedly and unambiguously asserts, that it was Allah & ONLY Allah who did the Choosing, contrary to the Hatemongering declarations by anti Jews, that it is the RACIST & ARROGANT Israelites and Jews who declare themselves the Chosen People ***
Al Sajda 32: 23 We did indeed aforetime give the Book (Torah) to Moses: be not then in doubt of its reaching (thee): and We made it a guide to the Children of Israel.
*** Allah is telling the followers of Muhammad that he gave the Torah ONLY to the People of Israel as a guide ***
Al Mu'min 40: 53 We did aforetime give Moses the (Book of) Guidance
and We gave the Book (Torah) in inheritance to the Children of Israel.
*** "We gave the Book (Torah) in inheritance to the Children of Israel" means to them & their generations AFTER them ***
And the last (but not least) GEM:
Al Maida 5: 21 "O my people! enter the holy land which Allah hath assigned unto you and turn not back ignominiously for then will ye be overthrown to your own ruin."
It is obvious that Muhammad did not realize that his loose-leaf notes had fully captured and preserved – though somewhat scrambled up from the more ancient accounts - actually verifying with detailed accounts, that the Israelites and the Jews had lived many centuries before him, settled and made their homeland as a nation in the very state of modern Israel & territories that have since been restored. These are the very lands that his followers absurdly deny had ever previously belonged to anyone else but themselves?
In conclusion, based upon all the above, it is crystal clear, that contrary to the untested beliefs of hundreds of millions of Muhammadan Muslims in the world today, their Quran in fact, fully supports and verifies the claims of the Jews for the land of Israel as their ancient and rightful home and nation.
Thus in a nutshell, the Quran is Zionist.
I REST my CASE!
 
kama huyo kilaza sheikh Ponda ndio kawa Allah basi ndugu waislamu wenzangu tusishiriki hiyo sensa na kama Allah ni yule alietufundisha kuheshimu mamlaka stahiki basi tumpuuzie.
 
Siwaungi mkono waislamu kugoma bali naunga mkono kipengre cha dini kiwekwe maana leo nimeamua kugoggle nikapata namba tofauti sasa najiuliza wamepata wapi hizi kama serikali yenyewe haina data yoyote ya waislamu na waikristo pamoja na wapagani. Lingine ni kuwa CIA wanadata za Tz lakini wenyewe hatuna. Katika mtandao wao nimekutana na namba hizi:

Christian 30% Muslim 35 and indigenous beliefs 35%
chanzo https://www.cia.gov/library/publications/the-world-factbook/geos/tz.html
 
[/COLOR]Mkuu Pasco hapo umeteleza ,kila jambo linafanyika kwa malengo. Jambo lolote ambalo linagharimu rasilimali kubwa (fedha na rasilimali watu) kwenye utekelezaji wake lazima malengo yake yaanishwe kwa ufasaha wa hali ya juu sana.Sensa inayofanyika inamalengo yake ,studi kwa maana ya utafiti ishafanywa na kufanya majaribio mbalimbali ya variables wanazotaka kuzitumia ili wapate majibu sahihi.Hizo takwimu za variables nyingine kama dini,kabila wameona hazitakuwa na mantiki kwa malengo ya takwimu za kimaendeleo/usatawi ya wa jamii.

Huwezi ukawa unataka majibu ya jinsi gani ya kuboresha huduma za afya ama kuongeza idadi ya shule kwa kujua waisilamu/wakristo wapo wangapi ama wapare wapo wangapi kulinganisha na wanyakyusa,huu ni ufinyu wa mawazo.Wao wameona kujua umri,jinsia ,wasiojiweza zina mantiki zaidi kiutafiti.Sensa inafanyika wakishatoa takwimu -mfano watanzania tupo milioni 60,hao wanaotaka kujua kuwa waisilamu/wakristo wapo asilimia ngapi mbona ni rahisi.Makanisa na misikiti wanautaratibu wao wa kuainisha majina ya waumini wao wa watafanya mahesabu rahisi.Sisi ambao hatuendi msikitini/kanisani idadi yetu itajulikana kwani kwenye hizo list zao misikitini/makanisani hatutaonekana.Hizo takwimu za kidini ni kwa manufaa ya waumini na wafuasi wa dini hizo.

Huu ushabiki unaofanywa na hawa baadhi ya viongozi wa dini sio wa kufumbia macho hata siku moja.Inamaana na wewe unashabikia maendeleo yaletwe na serikali kwa misingi ya udini na ukabila!!?.Kijiji nilichozaliwa kulikuwa na waisilamu na wakristo -sherehe zikifanyika iwe Idd ama Xmas watoto tulikuwa tunajuika pamoja,wazazi wetu walikuwa hawana shida na hilo.Hata katika shughuli za maendeleo mfano kujenga shule,kuchimba visima,kuchimba barabara nk. shughuli hizo zilikuwa zinafanyika kwa ushirikiano bila kujali huyu ni mwisilamu/mkristu.Siku za ijumaa waisilamu walikuwa haendi kwenye shughuli hizo na vile vile j'pili wakristo hawaendi ,hii ilitokana na misingi ya utaifa iliyokuwepo.

Leo hii wametokea watu wenye uelewa finyi wa maendeleo kwa kuweka maslahi binafsi kwa kupenyeza hizo ajenda zao kwenye taasisi za dini.Mwislamu/Mkristo haitaji kujua waislamu/wakristo wenzake wapo wangapi kwa yeye kupata elimu bora ama huduma bora za afya,anachotaka kukijua ni rasilimali za nchi yake zinamfaidishaje yeye na wanajamii wenzake kwa ujumla. Mama ntilie kilio chake ni kuona anapatiwa mahali safi pasipo na adha anapofanya biashara yake ,haitaji kujua waisilamu/wakristo ni wangapi.Huu ushabiki utatuopeleka pabaya sana,kizazi hiki kinategemewa kuwa ndio kitakacholeta mabadiliko kwenye nchi hii ,sasa kama tunageuka kuwa washabiki wa mambo kama haya napata wasiwasi.Tunatakiwa tuweke nguvu kupambana na adui yetu mkuu anayehujumu rasilimali ya nchi yetu kwa kuungana na sio kujigawa kwa misingi ya ukabila ama udini.

Mkuu Mwakalinga, with due respect, nimeuliza kuna ubaya gani kujua Watindiga wamebaki wangapi?. Kwa taarifa tuu, hivi jee unajua hadi wanyama wetu wenyewe tumefanyiwa sensa na wazungu?. Jee unajua ni wazungu ndio walijua tembo, mamba, vifaru wako kwenye hati hati ya kutoweka?. Kama mnyama tuu anahesabiwa ili alindwe, itakuwa makabila?.

Nimeuliza na please lets be genuine, put aside religious sentiments, nieleze kuna ubaya gani kujua idadi ya watu wa dini na makabila?.

Kwenye variables kuna kitu kinaitwa majority na minority, hivi unayo taarifa mpaka leo Tanzania hii, kuna makabila, hawalimi, hawapiki, wanaishi kwenye mapango na chakula chao ni matunda, mizizi na nyama mbichi?, unajua mahitaji yao ni unique?!, utajuaje kama hujawahesabu, au mpaka tusubiri wazungu waje watuambie watu wa kabila fulani ni endangered species?!.

Mipango miji wakipanga, wakatenga aneo la miskiti kwenye maeneo yenye nil muslim, huo msikiti utejengwa na kina nani and what for?!. Hao hao mipango miji, wanapaswa kutambua Muslim dorminated areas ili wareserve nafasi zaidi za misikiti!.

Naendelea kuuliza. kuna ubaya gani kujua?.
 
Back
Top Bottom