Kuna habari kwamba kuna basi la Buffalo linalofanya safari zake kutoka Dar es salaam kupitia Lindi, Mtwara Mpaka Tunduru lilikamatwa mwaka jana (2011) Masasi likiwa na Meno ya Tembo. Baada ya kukamatwa inasemekana kesi ilifunguliwa pale Masasi (Mtwara) na baadae kuhamishiwa Mtwara.
Taarifa ambazo zimesambaa kwa wakazi wa Masasi hivi sasa ni kwamba, askari walifanya makosa kukamata basi hilo kwa kuwa hayakuwa meno ya Tembo bali yalikuwa makopa (mihogo iliyokaushwa kwa ajili ya kusaga unga).
Kutokana na hilo, serikali inatakiwa kulipa hasara yote iliyopatikana kutokana na basi hilo kusimama kufanya kazi.
Vinavyowachanganya wakazi wa masasi ni hivi:
1. Askari wameshindwa kabisa kutofautisha meno ya Tembo na Mihogo(makopa)!
2. Basi limekaa muda mrefu sana kituo cha polisi, bado wasijue wameshikilia mihogo (makopa) badala ya meno ya tembo!
mwisho wa siku hawajaelewa .......
Note: si rahisi kutaja chanzo cha habari, ila fika masasi uliza wakazi, fika kituo cha polisi uliza basi la buffalo linafanya nini kituoni, fika mahakamani uliza kesi ya meno ya tembo katika basi la buffalo,- ilikuwa ni katika uongozi wa Nape Nauye (DC Masasi)
Taarifa ambazo zimesambaa kwa wakazi wa Masasi hivi sasa ni kwamba, askari walifanya makosa kukamata basi hilo kwa kuwa hayakuwa meno ya Tembo bali yalikuwa makopa (mihogo iliyokaushwa kwa ajili ya kusaga unga).
Kutokana na hilo, serikali inatakiwa kulipa hasara yote iliyopatikana kutokana na basi hilo kusimama kufanya kazi.
Vinavyowachanganya wakazi wa masasi ni hivi:
1. Askari wameshindwa kabisa kutofautisha meno ya Tembo na Mihogo(makopa)!
2. Basi limekaa muda mrefu sana kituo cha polisi, bado wasijue wameshikilia mihogo (makopa) badala ya meno ya tembo!
mwisho wa siku hawajaelewa .......
Note: si rahisi kutaja chanzo cha habari, ila fika masasi uliza wakazi, fika kituo cha polisi uliza basi la buffalo linafanya nini kituoni, fika mahakamani uliza kesi ya meno ya tembo katika basi la buffalo,- ilikuwa ni katika uongozi wa Nape Nauye (DC Masasi)