Mengine ya Upinzani yana Ukweli... Polisi wanatumiwa

kweli polisi muda mwingine wanatumiwa hadi wewe Zomba mzee wa saigon wamekutosa, au hawakujua kama wewe ni mzee wa saigon!
 
zomba kwanza namshukuru mungu amekuonesha uonevu unaofanywa na serikali yako.sasa bas upo tayari kufanya kazi na mimi ya kutetea wanyonge?kama upo tayari ni-pm twende wote mpaka wazo,tufatilie kumbukumbu number za mastaka yao,then twende kwa rpc,ikishindika ndani ya masaa saba twende tukawaone nchimbi,mwema,na wanaharakati wa haki za binadgamu,mdee na wandishi wa habar tuone huyo badr kama ananguvu
 
Last edited by a moderator:
Leo Zomba kawa kundi moja na sisi tunaolalamikia dhuluma za polisi? Ndio anayaona leo? Kumbuka usemi wa Father Martin Niemoller wa Ujerumani, tafuta kwenye google ujue aliongea nini!
 
Hunisomi vizuri, rejea posts zangu, "Ntasema kweli daima, uongo kwangu ni mwiko".

ili uamini ulichokiandika leo ni tofauti na siku zote, ni hii heading ambayo inajitambuisha kuwa zamani uliona wapinzani wanapoyonga tu lakini sasa umekubali kazi yao
[h=2]Mengine ya Upinzani Yana Ukweli...Polisi wanatumiwa.[/h]
 
Iwe isiwe, kuna malalamiko mengine mengi ya upinzani yana ukweli ndani yake.

Nasema hili kwa kuwa nimeshuhudia dhulma zinazofanywa na Serikali kwa macho yangu. Ukweli ubaki kuwa ukweli.

Kuna mtu kaja kunihadithia juzi, kuwa kuna vijana watatu na mzee mmoja wamekamatwa kwa tuhuma ya wizi na wako Polisi kituo cha Wazo Hill na wamekataliwa dhamana kwa sababu tu, tajiri aliyewashtaki amesema wasipewe dhamana.

Sikuamini nilivyoambiwa hayo, ikanibidi jana nitengeneze safari ya kwenda kituo cha Polisi cha Wazo Hill. Naam, nikawakuta kweli hawa watu wameshikwa na wapo ndani kwa wiki nzima sasa na wamenyimwa dhamana. Cha kushangaza zaidi ni kuwa wizi wenyewe wanatuhumiwa si wa kupora wala kunyang'anya, ni wa shoti iliyotokea kituo cha mafuta cha BP Boko, ambacho hakiuzi hata mafuta ya uwiano wa millioni 20 kwa siku.

Nilipofika kituo cha Polisi OCD akakataa kabisa kuniona wala kunisikiliza nilipomona nje ya kituo nikamueleza huku anatembea, kuwa "nakuja kuulizia kuhusu waliokamatwa kwa wizi wa millioni 80". Akanitazama, hakunijibu ndee wala sikio.

Katika kuwaulizia ndugu na jamaa wa "wafungwa" nikaoneshwa kikundi cha kina mama upande mmoja na kina kaka upande mwingine, nikaenda kuwajulia hali na kuwauliza kulikoni? Kisa walichonipa kinanifanya leo hii nikiri kuwa hii Serikali ina mambo inayoyafanya bila sheria na kwa dhulma.

Wale kina mama walinieleza kuwa wameongea na Kova, wameongea na Kenyela lakini swala lao wamekuwa wakipigwa danadana na wote hao. Kisa na sababu kwa kuwa aliyeshitaki ana fedha nae si mwingine bali ni kijana anaesemekana kuwa kaiweka Serikali mkononi kwa fedha zake kwa jina la Badr, mmiliki wa vituo vya GBP.

Cha kusikitisha na kushangza zaidi nilipoongea na wale kina kaka, mmoja wao akasema "mimi nafanya kazi kwa Badr" nimekuja kufatilia namna ya kumwekea dhamana Mzee ambae ni dereva wa gari la mafuta, lakini nimekataliwa, na sijui kinaendelea nini na OCD hataki kuongea na mtu".

Akazidi kunielezea kuwa huyu "Badr" anatumia Polisi kuhalalalisha amma alipwe Insurance kwa kusuka nao hizi kesi za wizi amma huwa anatumia hizi kesi kukwepa kodi. "hii siyo kesi ya kwanza, kama unabisha kamchunguze uone huko nyuma ameshawabambikia wangapi kesi kama hii" alisema huyo kaka, akifikiri mie ni mwandishi wa habari.

Kenyela, Kova, Mwema, Nchimbi, Kikwete. Haya hamuyaoni?

Hivi ni sheria gani inayoweza kumuweka kifungoni mtu ambae hajaua, na kumyima dhamana bila kumfikisha hata mahakamani kwa siku 8 mfululizo?

"Badr" ana ukaribu na hao mapolisi wakubwa wote akiwemo na Mwema, kwa mujibu wa huyo anaefanya kazi kwake ambae kaja mtafutia dhamna dereva aliyepo ndani.

Mawakala wa Badr wanaokwenda na kurudi huko Polisi mmoja anaitwa Mzee Nassor (Nasa) mmoja anaitwa Musa, wamewaambia hawa ndugu jamaa na marafiki, kuwa "nyie nendeni hata kwa Kikwete, sie tunatumia fedha, tuone fedha au kujuana ndio kutashinda".

Natamani majibu ya haya, kutoka kwa wanasiasa na wana harakati wa haki za binaadam, Mdee upo? sio kwako huko? Dili hilo.

Zomba,km serikali ndo inafanya haya unafikiri Mdee atafanya nn?better umejua km upinzani wanaongea ukweli
 
Aliongea mengi, hukuwa na sababu ya kumrefer bila kusema kitu alichokisema.
 
Kinana ndio amewakumbusha? zomba polisi wa Tanzania ya leo wapo free kufanya wanayotaka kama vile hawana sheria zinazoongoza kazi wanayofanya, wala uongozi. What is the problem?
 
kiswahili lugha ya taifa, mtu anaandika jinsi anavyotamka. Unaweza kosea matamshi lakini ukawa makini kwenye maandishi.
 
Leo Zomba kawa kundi moja na sisi tunaolalamikia dhuluma za polisi? Ndio anayaona leo? Kumbuka usemi wa Father Martin Niemoller wa Ujerumani, tafuta kwenye google ujue aliongea nini!

Its about the way power exchange hands...sis sote dugu moja. Inategemea at that particular time umesimamia upande gani.
 
zomba ni mnafiki,akipewa pilau ataanzisha thread mpya ya kuwasifia polisi..polisi wa tz wataendelea ktuua na hawatafanywa kitu na serikali ya magamba kwa sababu wanawahakikishia kuwepo madarakani...
 
Hayo cha mtoto ndungu zangu lakini ipo siku hawa waliopo madarakani watakuwa uraiani na watakumbana na haya haya!!!

eti Rais anawekwa mfukoni,IGP,Mawaziri yaani mtu anakutisha kabisa (ukichunguza kuna ukweli) kuwa hao wote hawawezi kunifanya lolote!

Mtu anavunja sheria akibanwa na watendaji wadogo anampigia simu "mwenye nchi" au waziri alafu ghafla unashangaa bosi wako anakuchimba mkwara utafikiri wewe mtendaji ndio umekosea na ikibidi unaambiwa kamuombe radhi grrrrrrrrrrrrrrrrrrr!!!!!!!!!!:frusty:
 
Kwa hiyo zomba unashauri tufanyeje kuondoa hili tatizo, tusubiri map aka watakosikia?
 
zomba ni mnafiki,akipewa pilau ataanzisha thread mpya ya kuwasifia polisi..polisi wa tz wataendelea ktuua na hawatafanywa kitu na serikali ya magamba kwa sababu wanawahakikishia kuwepo madarakani...

Ha ha ha,haya Zomba njoo ujibu hii
 
Back
Top Bottom