Mengine ya Upinzani yana Ukweli... Polisi wanatumiwa

Zomba siku zote I believed that siku kisu kinafika mfupani utasema yes here we are uembwabwaja baada ya kibanawa vilivyo CCM yako imekulipa haki stahili through jamaa yenu.Siku zote I said mnaofaidi ni wachache Ila ndugu zenu wanapata cha moto leo umeshuhudia.

Kuna Polisi ambae ni CCM na Chadema? funguka kidogo, usiwe punguani.
 
Nadhani serikali ya ccm ndiyo serikali inayoongoza Afrika kama sio duniani kwa kuweka mfukoni na kila mwenye fedha. Mambo yataendelea hivi mpaka lini? Mabadiliko ni lazima ili kuweka utawala utakaoheshimu sheria na usio dhaifu kama huu tulionao. Ningejisikia vizuri zaidi kama mtoa mada (Zomba) ndiye angekuwa amefikwa na madhila haya ili akome kutetea upumbavu wa serikali na vyombo vyake vya dola. Next time it might be you Zomba, mabadiliko ni lazima.
 
Iwe isiwe, kuna malalamiko mengine mengi ya upinzani yana ukweli ndani yake.

Nasema hili kwa kuwa nimeshuhudia dhuluma zinazofanywa na Serikali kwa macho yangu. Ukweli ubaki kuwa ukweli.

Kuna mtu kaja kunihadithia juzi, kuwa kuna vijana watatu na mzee mmoja wamekamatwa kwa tuhuma ya wizi na wako Polisi kituo cha Wazo Hill na wamekataliwa dhamana kwa sababu tu, tajiri aliyewashtaki amesema wasipewe dhamana.

Sikuamini nilivyoambiwa hayo, ikanibidi jana nitengeneze safari ya kwenda kituo cha Polisi cha Wazo Hill. Naam, nikawakuta kweli hawa watu wameshikwa na wapo ndani kwa wiki nzima sasa na wamenyimwa dhamana. Cha kushangaza zaidi ni kuwa wizi wenyewe wanaotuhumiwa si wa kupora wala kunyang'anya, ni wa shoti iliyotokea kituo cha mafuta cha GBP Boko, ambacho hakiuzi hata mafuta ya uwiano wa millioni 20 kwa siku.

Nilipofika kituo cha Polisi OCD akakataa kabisa kuniona wala kunisikiliza, nilipomuona nje ya kituo nikamueleza huku anatembea, kuwa "nakuja kuulizia kuhusu waliokamatwa kwa wizi wa millioni 80". Akanitazama, hakunijibu ndee wala sikio.

Katika kuwaulizia ndugu na jamaa wa "wafungwa" nikaoneshwa kikundi cha kina mama upande mmoja na kina kaka upande mwingine, nikaenda kuwajulia hali na kuwauliza kulikoni? Kisa walichonipa kinanifanya leo hii nikiri kuwa hii Serikali ina mambo inayoyafanya bila sheria na kwa dhulma.

Wale kina mama walinieleza kuwa wameongea na Kova, wameongea na Kenyela lakini swala lao wamekuwa wakipigwa danadana na wote hao. Kisa na sababu kwa kuwa aliyeshitaki ana fedha nae si mwingine bali ni kijana anaesemekana kuwa kaiweka Serikali mkononi kwa fedha zake kwa jina la Badr, mmiliki wa vituo vya GBP.

Cha kusikitisha na kushangaza zaidi nilipoongea na wale kina kaka, mmoja wao akasema "mimi nafanya kazi kwa Badr" nimekuja kufatilia namna ya kumwekea dhamana Mzee ambae ni dereva wa gari la mafuta, lakini nimekataliwa, na sijui kinaendelea nini na OCD hataki kuongea na mtu".

Akazidi kunielezea kuwa huyu "Badr" anatumia Polisi kuhalalalisha amma alipwe Insurance kwa kusuka nao hizi kesi za wizi amma huwa anatumia hizi kesi kukwepa kodi. "hii siyo kesi ya kwanza, kama unabisha kamchunguze uone huko nyuma ameshawabambikia wangapi kesi kama hii" alisema huyo kaka, akifikiri mie ni mwandishi wa habari.

Kenyela, Kova, Mwema, Nchimbi, Kikwete. Haya hamuyaoni?

Hivi ni sheria gani inayoweza kumuweka kifungoni mtu ambae hajaua, na kumyima dhamana bila kumfikisha hata mahakamani kwa siku 8 mfululizo?

"Badr" ana ukaribu na hao mapolisi wakubwa wote akiwemo na Mwema, kwa mujibu wa huyo anaefanya kazi kwake ambae kaja mtafutia dhamna dereva aliyepo ndani.

Mawakala wa Badr wanaokwenda na kurudi huko Polisi mmoja anaitwa Mzee Nassor (Nasa) mmoja anaitwa Musa, wamewaambia hawa ndugu jamaa na marafiki, kuwa "nyie nendeni hata kwa Kikwete, sie tunatumia fedha, tuone fedha au kujuana ndio kutashinda".

Natamani majibu ya haya, kutoka kwa wanasiasa na wana harakati wa haki za binaadam, Mdee upo? sio kwako huko? Dili hilo.

Latest Development;

Nimeongea na mmoja wa ndugu wa watuhumiwa kwa simu mudaa huu huu, anasema walikwenda leo hii Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wakiambatana na wakili, walipofika huko wameambiwa hilo faili la hao watuhumiwa lilikwenda kwao na toka jana waliwaeleza Polisi kuwa hao watuhumiwa hawana kesi ya kujibu na waachiwe.

Polisi inaendelea kuwashikilia dhidi ya maagizo hayo kwa kuwa tu bwana mkubwa Badr hajasema waachiwe.

Latest Update:

Watuhumiwa 3 wamewachiwa leo kwa dhamana, mtuhumiwa mmoja hana mashtaka ya kujibu, kawachiwa huru.

Kesi imebadilishwa badala ya Millioni 80 imekuwa Elfu 80!.

OCD wa Wazo Hill kahamishwa kituo.

RPC Kinondoni na RCO wabishana kuhusu hili sakata!


Nimeongea kwa simu na mmoja kati ya ndugu wa watuhumiwa, anakuja kunielezea kwa kirefu jinsi hii nyuzi ilivyosaidia. Nikipata habari kamili ntakuja ifungulia nyuzi.


Zomba,leo ndio umeona polisi wabaya kwasababu ya kuwanyima haki ya msingi jamaa zako, wangelalamika wapinzani (cdm) ungewaponda
 
Si kila jambo lazima liwe ni la kisiasa bana! khaaaaa! Huo ni utendaji mmbovu wa hao ma ocd, ma rpc na sijui wengine. Kwani mmefuatilia huyo tajiri aliyemwaga pesa ili hawa wa-tz wenzetu wasitolewe ni wa chama gani???
Kisha kwanini wasichukuliwe hatua hao polisi wahusika kutokana na kukiuka sheria kwa maksudi kabisa. Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai unasema wazi kabisa mtuhumiwa lazima apelekwe mahakamani ndani ya muda wa saa 24. Hasa kama mtuhumiwa hajawekewa zamana. Kumhamisha tu haitoshi labda wamshushe cheo maana ataenda kuongoza sehemu nyingine na kuwafanyia watanzania wenzetu tena ufisadi huo.
 
Back
Top Bottom