Mengi VS Warioba

Status
Not open for further replies.

Spiderman

JF Admin
Jan 1, 1970
7,219
441
Waziri Mkuu za Zamani Jaji Joseph Warioba amesema anakusudia kumfungulia mashitaka ya kashfa Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP na Media Solutions, Reginald Mengi.

Jaji Warioba, aliambia Mtanzania katika mahojiano ya Simu jana kwamba pamoja na Mengi, atayashitaki magazeti ya This Day na Kulikoni, wachapishaji wake, wahariri na waandishi wa habari.

Kauli hiyo ya Jaji Warioba inatokana na habari zilizochapishwa na magazeti hayo wiki hii zikidai kwamba Warioba anahusika na Kampuni ambayo inaelezwa na magazeti hayo kuwa imesajiliwa kwa ujanja na ambayo inahusishwa na chama tawala CCM

"Huko nyumba waliandika habari kama hizi. Tukawaomba watuombe radhi. Hawakutujali Badala yake wameendelea kuandika bila hata kutupa nafasi ya kueleza upande wetu.

Sisi ni watu ambao tunaamini Mahakama kuwa ndiko ambako mtu anaweza kupata haki yake. Hivyo tumeamua kuwafungulia mashitaka. Sasa siwezi kusema tutafungua lini, lakini itakuwa ni hivyi karibuni. Nitafungua mimi binafsi na kampuni ya Mwananchi GOld Mining nayo itafungua kesi yake," alisema warioba.

Alisema si kweli kwamba kwa kampuni hiyo kuna utata wowote na kwamba kilichochapishwa katika magazeti hayo ni ugongo wa dhahiri.

"Ninachoweza kukuambia tuu ni kwamba habari hiyo ni ya uongo. Walichoandika, pamoja na kwamba hawakujali kuniuliza kabla ya kuandika, ni uongo mtupu. Lakini kwa kuwa sisi tunaamini katika Mahakama, sasa sitazungumza sana kuhusu jambo hilo kwa kuwa tayari liko mahakamani," alisema na kuongeza:

"Nchi hii inaendeshwa kwa misingi inayofuata Sheria. Mimi naheshimu Sheria, kwa kuwa kati ya mambo haya mengine yako mahakamani, siwezi kusema zaidi. Naiachia mahakama.

Kama hatimaye jaji warioba na kampuni ya Mwananchi watakwenda mahakamani, hiyo itakuwa mara ya tatu katika kipindi kifupi kwa mengi na timu yake kufikishwa huko.

Wiki iliyopita balozi wa Tanzania nchini Italia, aliyemaliza muda wake hivi karibuni, Profesa Costa Mahalu, alimshitaki Mengi, wahariri na waandishi wa magazeti yake kwa kashfa akidai fidia ya billion 12

Shitaka hilo la Profesa Mahalu lilikuwa ni la pili, likiwa limetanguliwa na lile la mfanyabiashara wa Dar es Salaam, Yusuf Manji, ambaye anamdai mengi SH. Billion 100 kwa kashfa ya magazetini.

Source: MTANZANIA
 
Nafikiri wakati umefika sasa wa kuanza kuhoji issues badala ya watu. Sidhani kama ni kukomaa kumhusisha Mengi na habari zinazotolewa na vyombo vyake. Nafikiri hapa tuanze kuhoji nini magazeti yameandika badala ya kuanza kuhoji mahusiano ya watu wawili.
 
Mafuchila,
Nakuafiki. Lakini nadhani hapa kosa waliyofanya waandishi habari ni kutokuupa nafasi upande mwingine utoe maoni yake katika hili suala kabla ya makala hiyo kuchapishwa. Ndio maana Jaji Warioba ameamua kuwa"sue."
 
Mimi nakungana kusema Media Solution ishitakiwe na si Mengi kama yeye hili ni kosa na kumtisha Mengi maana huwa hatuko huko wanako andika habari hizi. Pia Warioba nadhani kuna kasoro mahala maana anahusika mno na watuhumiwa wa mambo mbali mbali kama Mahalu na sasa Mwananchi .Mwache aende huko wote ni wana CCM tutaujua ukweli mbele kwa mbele lakini afanye kweli si kusema na kukaa kimya .
 
Kwenye kesi za madai, unaweza kumdai hata mmiliki wa vyombo hivyo! siyo tu mwandishi au shirika..lenyewe!
 
Nimeshindwa kumuelewa Warioba, pamoja na udhoefu wake wa sheria anashindwa kutengeneza kesi, ukimshtaki Mengi eti amekukashfu ni rahisi sana kushindwa hiyo kesi udhibitisho wake utakuwa mgumu sana lazima uonyeshe kama Mengi alitumia madaraka yake kumshawishi Mhariri mkuu kuandika hiyo habari pia lazima mjue mengi hahusiki na kitu chochote na habari zinazotolewa kwenye magazeti yake kwa hiyo ni vigumu sana kumhusisha moja kwa moja hata kama kweli anahusika. Kesi kama hizi huwa ni ngumu sana kwani kuna jambo la kudhibitisha madhara uliyoyapata kwa hiyo habari. Ukimshtaki mwandishi ni kupoteza muda, wao siyo wanayoiweka habari kwenye gazeti. Mhariri mkuu ndiye anayepitisha habari zitoke. Katika mazingira ya namna hiyo inakuharibia sana kujenga kesi kwa kuwaingiza watu ambao hawahisi. Mazingira kama haya unatakiwa umshtaki Mhariri mkuu au gazeti kwa ujumla wao watajua ni nani anahusika. Ukimuiingiza mengi itakuwa rahisi sana kwakwe kuibadilisha anaweza akaifanya iwe na sura ya kisiasa kitu ambacho kitamuongezea Warioba ugumu kushinda hii kesi.
 
Sam,
Kushtakiwa kwa Mengi ni technical. Yeye kama owner wa gazeti kwa lugha nyingine anaitwa publisher. Yeye ndiye anayeshika mkoba wa IPP Media. Sasa ukimshtaki editor peke yake bila kumshirikisha tajiri wake umeachia nafasi kubwa kwa kampuni nzima kutowajibika. Nadhani Warioba kama mwanasheria analijua sana hilo. Unakumbuka kule Kenya kesi ya Biwott? Alishtaki duka lililouza kitabu, mwandishi na mchapishaji wa kitabu kilichoelezea kuwa alihusika katika mauaji ya Ouko.
 
Jasusi
nakubaliana na wewe na wala simlaumu Warioba kwa kufanya hivyo, lakini ukimwingiza Mengi kwenye kesi hiyo kesi, unaweza ukamshtaki lakini kushinda kesi ya namna hiyo itakuwa ngumu sana hasa ukiangalia yeye ni nani kwenye IPP Media. Mengi ni mkurugenzi mtendaji wa IPP Group na siyo IPP Media, IPP Media ni kampuni lililopo chini ya IPP Group na ina mkurugenzi wake. Ndiyo unaweza kumshtaki lakini itakuwa vigumu sana kumuhusisha na kushinda hiyo kesi. Kwenye IPP Group, mengi siyo publisher wa IPP Media. Ni sawa na kumshtaki Steve Ballmer ambaye ni CEO wa Microsoft ukitegemea utashinda kesi dhidi ya Microsoft au Bill kama founder au mtu mwenye hisa nyingi kwenye Microsoft. Sina nia ya kufananisha IPP Group na Microsoft lakini is the same type ya kesi.
 
Tunapotoka na kuacha mada yenyewe ama ni mimi napotoka ? Warioba ana hamaki kwamba yaliyosemwa ni uongo basi mwache aende Mahakamani yatajulikana huko.Ila najua kwamba This Day na kulikoni ni magazeti ya wana Mtandao Mengi katumika kama kivuli wacha waumane sisi tuone nani mwenye meno makali .Lakini sasa Warioba afanye kweli asiishie kusema ukweli uje nje hapa .Siasa hizi jamani duh!!!!!!!!
 
Tulisema siku nyingi kuwa huyu Warioba, ni mnafiki na ni corrupt kama wengine anaowapigia kelele, ndio maana hakwenda Elimu na sayansi kwa Mahalu, baadaye akawa patner naye kwenye Law Firm!

Sasa mambo yanaanza kutoka pole pole, tena sio peke yake na moto umeanza huo, kuna mzee Maguifuli ambaye mtandao sasa wamepania kumuondoa, stay tuned more yanakuja...............!
 
Mzee ES,

Magufuli wanataka kumuondoa ? safi sana huyu mtu ni mbaya sana kazi yake ni kutunyanyasa sisi wanyonge anatunyanganya viwanja vyetu pale mbezi , Hati ya kujenga kwa miaka mingi wamekuwa wakitunyima sasa wameamua kutunyanganya tuu!
 
Kwa jinsi This Day na Kulikoni walivyoandika ile habari nivigumu kuamini kwamba ni uongo. Hawa bwana inaonekana wana credible sources of information. Huyu Warioba anajikosha tu na anatujua fika hamna kesi ya yeye kushinda pale. Tunashukuru tumeanza kupata rangi halisi za Warioba, amejificha kwa muda mrefu kwenye ngozi isiyoyake. Hatimaye sasa tunaanza kumjua. He is has no intergrity as he has always tried to portray himself.
 
Mzee Rufiji,

Huyo mzee Magufuli, wabongo pole pole wameanza kumshitukia kama nilivyosema siku nyingi zilizopita kuwa hana tofauti na Keenja, kazi ya Billioni moja wao wataifanya kwa billioni Tano na kuwadanganya wananchi na viongozi wenzao wasiojua kitu kuwa ni wachapakazi hodari,

Mtu wa kwanza kunishitua kuhusu Keenja na Magufuli, alikuwa mzee Mkama, aliyechukua nafasi ya Keenja kule Halmashauri ndiye aliyenushitua kuwa hawa wawili ni magirini hawa, tena akanionyesha mpaka mahesabu ya Keenja, ambayo baadaye yalipelekwa kwa Mkapa, lakini hakuna hatua iliyochukuliwa maana Keenja ameoa nyumba moja na rafiki mkubwa wa Mkapa, mzee Sumaye!

Kuna mjumbe mmoja mpya wa kamati ya bunge ambayo zamani ilikuwa ujenzi, na sasa ni Miundombinu, anasema kuwa huko kuna ushahidi wa kutosha kuwafunga maisha mzee Mkapa pamoja na Magufuli, kwa hiyo pole pole utaona vitu vinatolewa mapaka atoke!
 
Polepole vitu vitatolea hadi atoke je nini nafasi ya CCM baadaye kwenye kampeni ama watasema wanasafisha Nchi kwa kuwaondoa wala rushwa maana najua JK na CCM yake ikifikia kwenye maslahi ya CCM wanakuwa macho zaidi maslahi ya Taifa .Sijaona wala kusikia PhD feki ziko wapi ? Zimeishia ? Au bado DCI anafanay uchunguzi ? Au ni kiini macho sasa ???
 
Editorial Comment: Mwananchi Gold: The truth shall set you free

Finally, Mwananchi Gold has come out of its shell of secrecy and spoken - loudly- against stories published by THISDAY and its sister paper - KULIKONI. According to a statement of the company published in several local dailies, what we have been saying is a pack of lies and should be ignored and the company has been so advised by those ’close to it’ It is a commendable move but one that begs a lot of questions.

Mwananchi Gold Company, which was formally inaugurated by the immediate former resident Benjamin William Mkapa in 2005 has not been known to be one that is transparent and that is a fact that we have, time and again, brought to the fore. The reason for this is paradoxically simple and complicated at the same time: the Bank of Tanzania has been bankrolling a project that the law does not allow it to be in.

We have stated the facts and cited the opinion of legal experts and it all points to one fact: the project leaves a lot to be desired in the way it was conceived, structured and funded. We are talking about billions of shillings belonging to Tanzanians here which we feel a cheeky few are trying to use for personal gain. As it does not wash with us we had to speak for the voiceless.

We must state categorically that the statement by the company has not addressed a number of issues which we think must be thoroughly explained. We understand that as a company it is the money that matters and not those who brings it. However, given the high social standing that those who are ’the body and soul’ of the company have, transparency is vital. This is not OPM (Other People’s Money) but Tanzanians’.

The statement by Mwananchi Gold is, in our considered opinion, meant to mislead the public by avoiding the real issues and resorting to simplifying matters which should not be treated so. We have addressed the illegality of the Bank of Tanzania involving itself in the project only to be told by Mwananchi Gold that its involvement ’in the development of the gold refinery is associated with the tradition that links gold refineries with central banks’ Only one example has been cited - that of the Reserve Bank of zimbabwe owning a gold refinery.

The point that Mwananchi Gold has missed here is that we are not talking about tradition but the law that governs the operations of the BoT. Expert opinion says that the old and the new Bank of Tanzania principal legislation does not allow the Bank to involve itself in commercial or industrial undertakings unless it is for the sole reason of recovering debts owed to it.

We dare Mwananchi Gold not only to deny that it is both, a commercial and industrial undertaking, but also to give the correct legal position lest we have faltered.

Mwananchi Gold has dared us to go to CCM while have stated that we have been there. We all know CCM and as its chairman President Jakaya Kikwete said, ’CCM ni vikao’ (CCM matters are decided in properly constituted meetings). Let us refresh Mwananchi Gold’s memory by stating that we quoted the immediate former Secretary General of CCM Phillip Mangula as well as Mzee Peter Kisumo, a trustee of the party.

What we said is in one of the issues that Mwananchi Gold has associated with ’the frivolous’ -us. No, we are not. We are the tellers of the truth and the truth is never frivolous.

We dare Mwananchi Gold to produce an instrument executed by CCM appointing the trustees of the Mwananchi Trust - the majority shareholders - and authorising the company (Mwananchi Trust) to purchase and hold shares in the Mwananchi Gold.

We say this as we are reliably informed that even the CCM’s Central Committee is yet to be informed about the venture - so unlike CCM. We know the ploy is to drag in CCM so that we get cold feet, but this CCM is not that of yesteryears. We invite Mwananchi Gold to closely watch the way its chairman walks his talk.

Given the massive ’investment’ in the undertaking, if Mwananchi Gold went headlong into the project without due diligence being carried out on its shareholders, it is solely responsible for getting its chestnuts out of the fire - we are not. Tell the truth Mwananchi Gold for it shall make you free.

What we see here is a situation whereby the name of the artisanal and small scale miners has been used to set into motion a project that is meant to benefit a few but putting majority in harm’s way through illegal infusion of capital .

We say, and we repeat, our law does not allow the BoT to go into ventures like this. Apparently the BoT was cajoled, whether by default or design, to bankroll a project that, four years down the line, has not shown any results but an incessant thirst for public funds. Are we supposed to bury our heads in the sand? No. Not THISDAY. We hold the truth dear and we say it - loudly and proudly.

We wish to remind Mwananchi and the like-minded that our paper is run by well-trained professionals with diverse professionals who cannot be derailed by the simple-minded. When we took it upon ourselves to tell the truth, we meant it and we are doing it. The people will absolve us. Threatened legal action is most welcome, for those who are aggrieved have that legal right.
 
PROF mahalu pia ,nafikiri na warioba walinunua kiwanda cha UBUNGO GARMENTS kikibwa tu kwa 120mil,tena wanalipa kidogo kidogo Hadi leo hakijaanza kazi na wala hakitegemei kuanza ,hii ni kunyima fursa ya wawekezaji serious ambao wangekua wameshafungua kiwanda na kuleta ajira .tatizo wanasiasa walitumia sera ya ubinafsishaji kujilimbikizia mali.

zainnadunin adamjee na wenzake walitumia fursa ya ubunge wa kawe kununua kiwanda maarufu cha nyama tena kilichotoa mchango mkubwa hadi kufilisika kipindi cha vita ,ambapo walikuwa wakipeleka beef mstari wa mbele kwa ajili ya vijana ,kilikuwa kimeajiri moja kwa moja watu 1,500 leo muwekezaji amenunua amebadilisha matumizi ya awali na anataka kujenga apartments ,hapa tunapata madhara ya kukosesha watu ajira na vilevile masoko ya ngombe wetu yaliyotegemea kiwanda hichi yanaathiriwa ....

hawa wanasiasa waliojilimbikizia viwanda bila hata kuwa na mitaji wanyanganywe!!!!!
 
IPP ni Limited company. Ingawa sijui sawaswa sheria yetu ya makampuni has limited companies. Ila ninategema kuwa makosa yote yatokananyo na biashara za kampuni hayahusishwi na wamilikaji wake unless ikithibitika kuwa wamilikaji hao walichangia kwa makusudi kufanya kampuni itende makosa hayo.
 
Let say Warioba & Co go to court and loose then what...??

Let say THISDAY is 100% right..then what??


The system is corrupt, JK & Co knows that...kwa wananchi wa Tz this is a perfect LOOSE - LOOSE situation. NOBODY will be punished for this....just another Billions wachache wameamua kujichukulia.

Mzee ES

You are...right on the money bro, somebody naughty must be behind ThisDay. May be wana-Mtandao...but bro what is their motive??? Just to embarrass Warioba???!!! That's not good enough. Any ideas???
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom