Mengi VS Rostam: Where is the Government?

Hawa wote ni makada wa CCM na wamenufaika sana na ukada wao. Sitashangaa kama hawataitwa pembeni na kuambiwa waache mchezo wa kitoto. Sitashangaa kusikia kuwa Mengi na Rostam wakitoa joint statement wakisema haya yote yalichochewa na mkono wa tatu. Mengi atafuta kesi na Rostam ataondoa vielelezo vyake au Takukuru watasema tu hakuna ushahidi! Mwaka 2010 wote kwa pamoja watazunguka nchi nzima kumnadi mgombea wa chama chao! Na nyie mliotegemea makubwa mtabaki kugunia chini chini!

Amandla.......

Fundi Mchundo, mi nimejitoa ktk ushabiki huu lakini nimekuwa nikifuatilia maoni na nimeona ya kuwa unachokiandika are my thoughts on this issue. Muda umefika wa kuendelea na mjadala unaoleta maendeleo na kuachana na ushabiki. Anyway, let them have their 15 minutes of fame until the next issue comes up na tutasahau yote...
 
tunahitaji mawazo huru kama haya HONGERA SANA MKUU uchambuzi wako umekwenda shule
.
Nakubaliana na wewe Mengi nia yake ni kuwamaliza washindani wake kibiashara hana uchungu wowote wa nchi fisadi nyangumi

Tayari amewateka wengi kwa kulialia kwake na kujifanya anaonewa kumbe ni fisandi nyangumi
 
"Sasa hawa mawaziri (Sophia Simba na George Mkuchika) wanamtetea nani? Mbona wakati Mkapa na wenzake wanatuhumiwa hadi aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wawili wakajiuzulu, hakuna waziri aliyesimama kuwatetea? Serikali hii iko kwa maslahi ya nani? Kuna ambao wakiguswa Serikali na nchi inatetemeka na wengine ni mbuzi wa kafara?" alihoji mstaafu huyo..........

Hapa mstaafu alimaliza kila kitu, serikali hii ni ya kwao mafisadi.
 
Good analysis. Sasa nani apewe thanks, wewe burn au NasDaz? Anyway Burn vilevile unastahili kwani umeileta hapa. How can we thank NasDaz?
 
Kwa Mtazamo wangu, malumbano haya yana maslahi sana kwa taifa kupata true colors za nani ni nani na kewaza kutambua hswa nani ni chui ndani ya ngozi ya kondoo, fisadi-papa akijifanya kada na mfadhili mkuu wa CCM na right hand man wa JK huku akitufisidi Watanzania. na fisadi-nyangumi anayetaka kumsadia Jk ambaye ni best wa fisadi-papa, anauma huku akipulizia na wakati huo huo akitoa misaada Chadema kwa mlango wa nyuma.
Subirini tuu, hiyo ni pati gazeti, picha yenyewe ndio inakuja.
 
wewe unamjua mmoja wapo au umeshamsikia popote mtendaji yoyote?

Sijui ulikuwa unamaanisha ni mimi niliye post hii au mwandishi lakini wherever ninawajua hata mia kwa kuanza how about HE JMK
 
Ndugu tabia ya kukopi kwenye magazeti inakera? ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Inakukera wewe. Tuachie sisi tunaotaka kupata nyzi za nyumbani. Inaelekea mwenzetu uko karibu na source.................!!!!!!!

Bubu endelea, hawa jamaa wasikukatishe tamaa. Unatusaidia wengi humu kwa hizo nyuzi za magazeti kila siku.
 
Hawa wote ni makada wa CCM na wamenufaika sana na ukada wao. Sitashangaa kama hawataitwa pembeni na kuambiwa waache mchezo wa kitoto. Sitashangaa kusikia kuwa Mengi na Rostam wakitoa joint statement wakisema haya yote yalichochewa na mkono wa tatu. Mengi atafuta kesi na Rostam ataondoa vielelezo vyake au Takukuru watasema tu hakuna ushahidi! Mwaka 2010 wote kwa pamoja watazunguka nchi nzima kumnadi mgombea wa chama chao! Na nyie mliotegemea makubwa mtabaki kugunia chini chini!

Amandla.......

- Wa-Tanzania, tufike mahali tusikubali kudanganywa anytime unapoona kuna mtu au kiongozi anadai serikali au rais aingilie kati hili soo maana yake ni moja tu kwamba anataka Rostam aokolewe, ndio maana tunasema serikali na rais wakae pembeni, kwa sababu hakuna sheria iliyovunjwa so far Mzee Mengi kumtwanga Rostam na yeye kujibu, na sasa mahakama na Takukuru, ingawa ni fair kumuuliza Rostam kwa nini ameenda Takukuru badala ya mahakamani? Hili ni swali zito sana wananchi tunatakiwa kujiuliza WHY Takukuru? Kuna nini huko?

- Kuitwa pembeni it is too late, na Mengi akikubali kuitwa pembeni ajue he is done, maana the next thing watamchezea karata chafu sana kama walizomchezea DK. Salim kwenye uchaguzi wa 2005, sasa hivi Rostam na wapapmbe wake wamepagawa hawaamini, kwamba the mighty Rostam is in trouble, yes he is in trouble kwa sababu the more this war inaendelea kama ilivyo sasa ni more wananchi watajiunga na Mengi, huhitaji kuwa professor wa siasa kuelewa hili, The genius Rostam alikosea pale tu alipokubali kujitokeza Kempiski, ninasema hivi kwa mara ya kwanza toka aanze kuchanganya siasa na biashara he is in trouble tena big time, enzi zake rais angemuita Mengi na kumtuliza lakini not anymore, infact alikuwa amebanwa sana na Mengi kwamba akajaribu kuwatumia CC, huko wamemtolea nje sasa tuone kama Takukuru wana ubavu wa kumuosha, ananuka!

- Ya kuitwa pembeni Mengi asikubali ng'o! Akikubali tu ameisha na maji, Rostam hana ubavu tena, hata huko Mtandao ni Karamagi ndiye anaye-run the show anyways kwa sababu hawawezi tena ku-afford kuongozwa na a high profile na political liability kama Rostam, mambo yao huko gizani hufanikiwa wanaposhughulika bila kuonwa yaani chini ya radar, kwa hiyo hata huko sio siri nao wameshafika mwisho naye, mimi ninasema hivi ukimshika Rostam basi umekamata kichwa cha nyoka, akibanwa sana tutapata majibu ya maswali yote muhimu sana kwa mabadiliko ya taifa hili,

Huyu ndiye chanzo cha ufisadi wote nchini, majibu kama ya ufisadi wa Mkapa na Balali, yote anayo huyu, Mengi asikubali idea ya kuitwa pembeni akiendelea naye kwenye sheria, pole pole wananchi tutajiunga na hivi vita ndipo Rostam ataelewa kwamba kila chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho, na hasa ufisadi! amani ya taifa letu iko sawa sana tena kuliko wakati wowote tuwe na uhuru, hii ishu iachwe itajifungua na kujifunga yenyewe, so far haijavunjwa sheria yoyote ya jamhuri!

Respect.

FMES!

 
Mengi haitiki pembeni... kuna watu wametabika sana kuhakikisha RA anawekwa kwenye kona kabla ya 2010.. kama unavyosema Mengi akikubali kuitwa pembeni na kumaliza mjadala kinyemela na yeye atakuwa amefikia tamati..

As I said the other day.. tunachogombania ni urithi wetu.. kilicho hatarini ni zaidi ya majina, hadhi, biashara au vyeo vya hawa wawili.. the future of our nation and the destiny of our people is at stake.. if one misses that, then he/she misses the whole point..

People need to go well above the two individuals..
 
Mengi ni mfanya biashara kwanza kabla ya yote. Mengi anajua ni upande upi silesi yake imepakwa siagi. Huyu amehangaika sana kuhakikisha chama chake kinashika utamu. Mnaamini kweli ataukata mti alioukalia kwa ajili ya faraji ya muda mfupi? Mpaka sasa hakuna mahali amekosoa chama au serikali yake. Mnadhani amefanya hivi kwa sababu anaamini vyombo vyote hivi ni visafi kabisa kabisa? Halafu leo mnataka kutuaminisha kuwa ati yuko tayari kuleta ushahidi ambao unaweza kuangusha serikali ya chama chake? Thubutu!

Mzee Mwanakijiji, FMeS na wengine. Mmefunga tela kwenye gari bovu.

Amandla.......
 
- Wa-Tanzania, tufike mahali tusikubali kudanganywa anytime unapoona kuna mtu au kiongozi anadai serikali au rais aingilie kati hili soo maana yake ni moja tu kwamba anataka Rostam aokolewe, ndio maana tunasema serikali na rais wakae pembeni, kwa sababu hakuna sheria iliyovunjwa so far Mzee Mengi kumtwanga Rostam na yeye kujibu, na sasa mahakama na Takukuru, ingawa ni fair kumuuliza Rostam kwa nini ameenda Takukuru badala ya mahakamani? Hili ni swali zito sana wananchi tunatakiwa kujiuliza WHY Takukuru? Kuna nini huko?

- Kuitwa pembeni it is too late, na Mengi akikubali kuitwa pembeni ajue he is done(FINITO), maana the next thing watamchezea karata chafu sana kama walizomchezea DK. Salim kwenye uchaguzi wa 2005, sasa hivi Rostam na wapapmbe wake wamepagawa hawaamini, kwamba the mighty Rostam is in trouble, yes he is in trouble kwa sababu the more this war inaendelea kama ilivyo sasa ni more wananchi watajiunga na Mengi, huhitaji kuwa professor wa siasa kuelewa hili, The genius Rostam alikosea pale tu alipokubali kujitokeza Kempiski, ninasema hivi kwa mara ya kwanza toka aanze kuchanganya siasa na biashara he is in trouble tena big time, enzi zake rais angemuita Mengi na kumtuliza lakini not anymore, infact alikuwa amebanwa sana na Mengi kwamba akajaribu kuwatumia CC, huko wamemtolea nje sasa tuone kama Takukuru wana ubavu wa kumuosha, ananuka!

- Ya kuitwa pembeni Mengi asikubali ng'o! Akikubali tu ameisha na maji, Rostam hana ubavu tena, hata huko Mtandao ni Karamagi ndiye anaye-run the show anyways kwa sababu hawawezi tena ku-afford kuongozwa na a high profile na political liability kama Rostam, mambo yao huko gizani hufanikiwa wanaposhughulika bila kuonwa yaani chini ya radar, kwa hiyo hata huko sio siri nao wameshafika mwisho naye, mimi ninasema hivi ukimshika Rostam basi umekamata kichwa cha nyoka, akibanwa sana tutapata majibu ya maswali yote muhimu sana kwa mabadiliko ya taifa hili,

Huyu ndiye chanzo cha ufisadi wote nchini, majibu kama ya ufisadi wa Mkapa na Balali, yote anayo huyu, Mengi asikubali idea ya kuitwa pembeni akiendelea naye kwenye sheria, pole pole wananchi tutajiunga na hivi vita ndipo Rostam ataelewa kwamba kila chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho, na hasa ufisadi! amani ya taifa letu iko sawa sana tena kuliko wakati wowote tuwe na uhuru, hii ishu iachwe itajifungua na kujifunga yenyewe, so far haijavunjwa sheria yoyote ya jamhuri!

Respect.

FMES!

MKUU FMES, WEEL DONE.
Hii aNalysis yako ni kiboko, actually umenena mengi ambayo watu wengi wanaona ndio muelekeo wa hili saga la Mengi na Rostam.
Rostam is on the ropes and he is a liability, inabidi uwe mwenda wazimu kutetea position yake ya kifisadi.kwa uchaguzi wa 2010 ukiambatana na Rostam umekwisha!!
Na hilo liwe angalizo kwa TBC, Daily News na Habari leo you are doing a dis service to the wananchi-backing a losing horse-na siamini kuwa huo ndo msimamo wa serikali.
 
Mengi ni mfanya biashara kwanza kabla ya yote. Mengi anajua ni upande upi silesi yake imepakwa siagi. Huyu amehangaika sana kuhakikisha chama chake kinashika utamu. Mnaamini kweli ataukata mti alioukalia kwa ajili ya faraji ya muda mfupi? Mpaka sasa hakuna mahali amekosoa chama au serikali yake. Mnadhani amefanya hivi kwa sababu anaamini vyombo vyote hivi ni visafi kabisa kabisa? Halafu leo mnataka kutuaminisha kuwa ati yuko tayari kuleta ushahidi ambao unaweza kuangusha serikali ya chama chake? Thubutu!

Mzee Mwanakijiji, FMeS na wengine. Mmefunga tela kwenye gari bovu.

Amandla.......

ni kosa kubwa sana kutaka mtu mmoja awe vyote katika vyote ili akubalike.. asiye adui yangu yuko upande wangu.. Na unachosema pia ni kweli kwani Mengi naye ana maslahi yake binafsi ambayo ni lazima ayalinde kama vile wengine walivyonayo ya kwao. Sioni cha ajabu katika hilo.... pale yeye anapoishia wengine wanafuatia.. Mbona hata Mwakyembe, Selelii na kina mama Kilango wote kwa namna tofauti hawajaikosoa serikali au chama choa moja kwa moja (wana maslahi yao binafsi).

We should not draw a line that no one will ever reach.. I'm a realist not an idealist.. Sitarajii Mengi ili aoneshe yuko anti ufisadi aanze kumlaani JK, vyombo vya usalama n.k ili akubalike nami....vile vile sitarajii ili Dr. Slaa awe kweli ni mzalendo basi ni lazima akiumbue chama chake au kugongana na Mwenyekiti wake ili akubalike nami..

Mtu anapiga kasia kwenye maji mpaka urefu wa kasia tu.. - MM Original.
 
Mwanakijiji,
Mtu anapiga kasia kwenye maji mpaka urefu wa kasia tu.. - MM Original.
Nimependa mtazamo huu..U know what?..ndio ukweli, mashua inasonga mbele..
 
ROSTAM ni CCM na CCM ndio ROSTAM = ROSTAM ni SEREKALI na SEREKALI ndio ROSTAM ,kwa maana nyingine watu hao ni pete na chanda.poor mzee MENGI ,where are you going from here?watakuwinda hao kama vile wawindaji waliokuwemo mawindowi.I wish you the very best Good luck, only time will tell.
 
Ama kweli unafiki hautojificha milele na unafika wakati wale wanaofanyiwa unafiki wanatanabahi. Watanzania tumekuwa tukifanyiwa unafiki na kwa roho zetu za kuaminiana na kupendana tumekuwa tukifanywa mabwege na wenye akili na mikakati ya kujinufaisha.
Tulianzia na kupewa viperemende na Matajiri ambao lengo lao lilikuwa kujinufaisha zaidi kwa kulindwa kwa kisingizio cha misaada. Hawa wanafiki walitumia rasilimali zetu na Mabenki yetu kujinufaisha na kujikweza kwenye utajiri wa kutoguswa. Wanafiki hawa ha wakutosheka na kuwatumia viongozi wetu kuwalinda na wakaamuwa kuiteka Siasa. Kwa vile Siasa ya Tanzania ni kugawa kanga na viroba vya mchele na michango midogo midogo kujengea shule na vibanda vya Polisi wanafiki hawa waliiteka kirahisi siasa na siasa kuwa mchezo unaotaka Fedha ili kuchuma fedha kwenye siasa.
Hatukuishia hapo bali Chama kilichokuwa kikiaminiwa zaidi na Watanzania kikaingia madarakani kwa kutumia njia za kinafiki. Unafiki wa Chama hicho ulipaliliwa na msimamo wa pamoja wa wanachama wake waliokuwa madarakani. Wananchi walipojuwa kuwa Chama hicho kiliiingia madarakani kwa unafiki walianza kupaza sauti zao kupitia upinzani . Kama kawaida unafiki ulizidi kufichuka pale Wabunge wa Chama hicho kitukufu kuwa na msimamo mmoja dhidi ya harakati za kuwaondolea kero wananchi. Harakati na malalamiko ya wananchi vilipopamba moto ilibidi kutolewa muhanga wachache ili kunusuru unafiki wa chama.
Kuanzishwa kwa kilichoitwa vita ya ufisadi kulikuwa ni unafiki mwengine kwani haikuwa vita ya kweli bali ni njia tu ya kukinusuru Chama kilichowapa watu nafasi zinazowatajirisha. Nasema ni unafiki kwani nini hasa lengo la kuondowa ufisadi? Nafikiri lengo halisi ni kuleta hali bora kwa wananchi kutokana na kidogo kilchopo kuchotwa na wachache wajanja. Sasa inapotokea mtu anachukuwa jitihada za kufichua maovu ni wazi kuwa mtu huyo anahitaji pongezi na sio kudharauliwa na kubezwa. Wabunge wetu wanapoamuwa kuzifisadi juhudi za watu kama DR. Slaa na huku wakiimba nyimbo ya kupigana na vita ya ufisadi hao si chochote bali ni Wanafiki. Unafiki dhidi ya Watanzania unaendeshwa na hata Wapinzani kwa kuangalia maslahi ya matumbo yao. Kitendo cha Wapinzani bungeni kujiunga na wale wa chama tawala kumuandama DR. Slaa kuhusu mishahara mikubwa tafsri yake ni unafiki tu. Unafiki unajidhirisha zaidi kwa hawa wakubwa wetu kwa kudai mishahara ipandishwe huku wakijilinganisha na WATU WA NJE NA SIO KIPATO CHA MTANZANIA. Ama huu ni unafiki juu ya unafiki dhidi ya Watanzania.
Unafiki wa karibuni tunaoushuhudia hivi sasa ni huu wa watu kutaka kujipatia utajiri kwa kisingizio cha vita ya ufisadi. Najua hili litawakera wengi lakini kwa vile ni unafiki basi inabidi usemwe. Hiki kitendo cha Mzee maarufu kwa vita vya ufisadi kutaka kujipatia pato kubwa kwa kisingizio cha kupigana na ufisadi ni kitendo cha unafiki na ni kuwasaliti wale wanaomuunga mkono kwenye mapambano hayo. Watanzania wameshoshwa na kauli zinazomuhusisha Rostam Aziz na hujuma kwa maslahi ya Taifa na wangependa kuona anatokea mtu mwenye uwezo wa kutowa ushahidi wa hujuma zake na kumfikisha katika vyombo vya sheria. Hili la kutaka billioni tano na nusu kwa madai ya kukashifiwa na kuacha kile kilichotarajiwa na wananchi ni kitendo cha ubinafsi ambao mtu aliejitangaza kuwa mpiganaji wa ufisadi hakimfai kukifanya.
Reginald Mengi kama binafsi ana haki ya kujisafisha na shutuma lakini ieleweke kuwa chanzo cha yote haya ni tangazo lake la kujipa kazi ya kuongoza vita ya walio wengi, vita ya wananchi dhidi ya ufisadi na kwa hivyo hana budi kipato na tija ya mapambano hayo iwe kwa wananchi kwa ujumla wao na sio yeye binafsi kujichukulia billioni tano na nusu huku alikwishasema na kutangaza kuwa maisha yake anayaweka mikononi mwa wananchi. Pasingekuwepo unafiki kama Reginald Mengi angeamuwa kupigana vita anavyodai kuwa ni mpiganaji, angetowa ushahidi alionao uliompa ujasiri wa kumwita Rostam na wenzake kuwa ni Mapapa wa Ufisadi.
Pengine hili tunaloliona ni lile lile la kudhihirika unafiki baada ya kufanywa kwa muda mrefu. Inawezekana hiki ni kilele cha mpango mathubuti wa Reginald Mengi kuwaprovoke Wahindi ili apate pesa za urahisi. Waswahili husema mchovya asali hachovyi mara moja na Mengi kama aliweza huko nyuma kutumia vipengele vya sheria Kuiibia NBC basi alikuwa na uhakika kuwa ni mjuzi wa mchezo wa kupata pesa kwa kucheza na vipengele vya sheria. Hata hivyo hii inaonyesha namna conscious yake isivyomsuta kwani iwapo umechukuwa pesa kwa mkopo hukurudisha kwa kutumia udhaifu wa sheria itabaki kuwa zile pesa hukurudisha.
Nafikiri mbio za sakafuni huishia ukingoni na Mwenyezi Mungu huwa hamfichi mnafiki, wanafiki wote kwetu wataumbuka kama si sasa hivi basi kipindi kifupi kijacho.
 
Hizi ni athari za kunyonya maziwa ya kopo kutoka china badala ya titi la mama.

Hii kesi ya Mengi kuna vingunge nyuma yake: Mkuu wa kaya anataka kuwamaliza akina Rostamu na nduguye Lowasa:

Mchezo Wenyewe ni kwamba:
1: Mkuu wa kaya anampa tafu Mengi kusema madhambi ya Rostamu mbele ya vyombo vya habari, walijua Rostamu atakanusha na kukasilika:

2: Rostamu anapewa data fake anamwaga mbele ya waandishi wa habari: na kupeleka copy za data fake PCB.
3: Mengi anafungua kesi kwa kusingiziwa data fake: na anataka ataje biashara gani anafanya Tanzania na alinapa kiasi gani cha kodi.

Kwa vile Rostamu ni zezeta kama alivyosema Dr. Mwakyembe ajui huo mchezo ukoje wa kumumaliza kabisa.

Kilichobaki Rostamu kama ana akili ni kukata ticket ya oneway mpaka Irani akasherekee pesa alizoiba Tanzania.

Dunia nzima kama ni mfanya biashara mkubwa lazima ukope sehemu yeyote hile Bank/Ndugu etc. na Kufilisika ni kitu cha kawaida tu kwa mfanya biashara.
 
Last edited:
Ngekewa,
Watanzania wameshoshwa na kauli zinazomuhusisha Rostam Aziz na hujuma kwa maslahi ya Taifa na wangependa kuona anatokea mtu mwenye uwezo wa kutowa ushahidi wa hujuma zake na kumfikisha katika vyombo vya sheria. Hili la kutaka billioni tano na nusu kwa madai ya kukashifiwa na kuacha kile kilichotarajiwa na wananchi ni kitendo cha ubinafsi ambao mtu aliejitangaza kuwa mpiganaji wa ufisadi hakimfai kukifanya.
Mkuu labda hufahamu ya kwamba hakuna ushahidi wowote unaohusiana na kesi yoyote ambao haujapelekwa serikalini. Toka ujenzi wa BoT (twin Tower), wizi wa fedha za EPA, rada, IPTL, Kagoda TISS na mengineyo yote ushahid upo tayari mikononi mwa serikali isipokuwa vyombo hivyo vimeacha kusimnamisha madai ya wananchi.
Alichofanya Mengi ni marudio tu mamba mengi ambayo tayari yamekwisha fahamika sema tu kilichokosekana siku zote ni mtu atakayeweza kuita - Koleo ni Koleo..Na kibaya zaidi wananchi wote tumejikusanya ktk saga hili la Mengi na Rostam kama vile pambano la mieleka..
Nimekwisha sema Mengi kufanya lolote zaidi ya kututaarifu kupitia vyombo vya habari, hawezi kwenda fungua mashtaka mahakamani kwa kosa la Ufisadi wa kiongozi wa nchi wakati viongozi hao ndio wenye ushahidi na wameshindwa kuufanyia kazi...Ushahidi wetu ni wizi uliotokea na uchunguzi umeshafanya sehemu nyingi tu toka mkaguzi wa mahesabu ya serikali hadi vyombo vya uchunguzi..
wakati Mkapa akiwa madarakani tuliingiza mashirika zaidi ya manne nayoyajua kuchunguza Corruption nchini mengine toka Ujarumani na yote yalichota fedha na kukabidhi report zao, nothing happened, labda umesahau hata ile report ya Warioba ilifukiwa mbele ya macho yetu na wapo watu kwa hasira zao walimlgeuka warioba na kumwita Mnafiki kwa sababu hakufanya uchunguzi wake kufikia ngazi za juu..Na haikuwa kweli isipokuwa serikali ilichagua mabangusilo wa kutupwa ndani kama kifumba macho ya wadanganyika.. na tulilala kweli kwani hadi leo hii hakuna mmoja wetu anayeuliza tena kuhusiana na Mafisadi wale..Amina Chifupa hivi majuzi tu alitaka kutoa list ya wauza Unga nchini na aliikabidhi kwa rais ambaye kaamua kukaa kimya..
Sasa kama angekuwa hai na kaiotoa hiyo list tungeuliza ushahidi na bila shaka mwisho wa yote angekuwa mnafiki kwa kushindwa kukusanya ushahidi wakati haikuwa kazi yake.. Matokeo yake ametutoka na kazushiwa mengi magonjwa ya kia aina kuonyesha kwamba AC pia alikuwa mnafiki tu.
Dr. Slaa kazungumza sana kuhusiana na Mafisadi, Zitto Mwakyembe, mama Kilango lakini wote hawa wamekuwa lawamani kila siku kuliko hata hao Mafisadi wenyewe..Na kibaya zaidi watu hawa wamefikia hadi kutishiwa maisha yao, yet sisi Wadanganyika tunawaona kama ni watu wanaotafuta UMAARUFU..
Kwa mtaji huu mkuu wangu hata akija Yesu nadhani mtatafuta mbinu za kumuua tena kama sio kumwita Mnafiki kabla hajatukomboa wengine wenye imani.

Kitendo cha Mengi kushtaki ni swlaa la sheria na msingi mzima wa mtu binafsi anapotaka kusafisha jina lake... hakuna unafiki isipokuwa unafiki ungekuja kama atakubali suluhu nje ya haki..Mengi hana kesi dhidi ya Rostam kuhusiana na Ufisadi, hakuibiwa yeye bali tulioibiwa ni sisi sote wananchi na zaidi ya hapo kumbuka tu kuwa maswala mengi ya Rostam hayupo pekee..Haiwezekani kabisa kuwa kesi zote hizi zimelala ktk filing cabinets za PCCB...
 
Back
Top Bottom