Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Umem discredit Masha based on maneno ya Mengi (umesema kama hizi habari ni kweli basi Masha fisadi) halafu hapo hapo ume kandya maneno ya Mengi kwamba anatatufa populatity. Kama maneno ya Mengi nayo ni discreditable sasa wawezaje kuyatumia kumhukumu Masha ?



Kwanza habari za siku Mwanamke wa Kiafrika, unapotea mno kwenye mapambano na kuibuka siku za ushindi, huna mpango! :)

Mengi amefanya udaku kwa kudokezadokeza identity ya "waziri kijana" akiogopa, akishindwa kujiamini kuanisha anatachotaka kusema. Ndio nilivyomaanisha, aache kuwa wussy na mdaku.

Wote uanza kwa kuita udaku. Clinton & John Edwards na wengine wengi walianza hivyo kwa kusema ni udaku lakini mwisho wakaishia kuja na definition za ajabu ajabu za ubazazi wao.

Naomba ukumbuke dalili ya mvua ni mawingu na panapofuka moshi kuna moto. Unaweza ukawa na data lakini likija suala la technicalities za kortini kuhusu defamation unakuta umebanwa mbavu. Mengi anawanasheria wazuri natumai wameasesi mazingira yote na kuamua atoke kama alivyotoka. Kaa chini fikiri kisha utajua kwamba Mengi anajua analolifanya.

Mwombe radhi Mengi katika hilo!
 
Mkuu FMES, mwambie huyo kijana aache ujinga na achape kazi, mambo mengine yatafuata.

- Sawa sawa, naona maneno meeengi sana na emotions nyingi sana damn! anyways hapo juu naona so far ndio maneno ya maana kuliko mengine mengi wka sababu kuna mengi bado kujulikana kuhusu hii habari, kwa hiyo tutaongea na wote kuanzia na Mzee Mengi, na wengineo wote wanaoshukiwa kuwa ndio watajwa ingawa hayakutajwa majina wazi.

Thanxs Guys na Respect!
 
Alianza kwa kukurupuka na kutishia kulishtaki gazeti la mwanahalisi. Akajisahau kabisa kwamba yeye ni waziri mwenye dhamana ya kumlinda Kubenea na kwamba IMMA ina wakurugenzi na wazungumzaji wake.

Baadae kawatembelea wahalifu mahabusu walioshitakiwa na serikali akasahau technically yeye ni mmoja (tena muhimu sana) ndani ya serikali na ndio walioshitaki

Watuhumiwa wakatolewa mahabusu without removal order hadi kufukuzwa mahakamani na yeye akawa wa kwanza kuitetea magereza kwa kosa hilo la wazi kabisa la kujisahau

Halafu akawakashifu walemavu wa ngozi kwa kuongea maneno ambayo anajaribu kuyaruka kwa utetezi dhaifu ajabu

Na sasa amemtishia Mengi na demokrasia ya vyombo vya habari na kujaribu kutetea ufisadi wazi wazi bila aibu.

Huyu bwana mdogo kwanza kabisa amepwaya kwenye hiyo ministry. Utendaji wake umefikia kikomo (very unfortunately). Nilidhani alivyoponea chupu chupu kule ministry of energy angejifunza; kumbe he has reached the bar!

Siasa za makundi ni utamaduni popote pale duniani. Kama yeye anashindwa kuona upepo na kugundua ni kundi gani he should side with at his young political age, basi amekwisha!

He has to go now. Kwenye siasa aondoke kabisa. Arudi tu kwenye professional yake!
 
"Nionayo na kuyasikia yakifanyika Tanzania yameniacha mdomo wazi, yaani sasa mafisadi tunashughulikiwa? Jamani Ile Tanzania ya wapole, wanyenyekevu, wachovu mko wapi? Hebu ondoeni vuguvugu hili ili sisi mafisadi tuendelee kunyanyasa kama zamani"
Nadhani hiyo ni sehemu ya sala ya mafisadi. HAKI YA NANI MMEKWISHA!
 
Mengi amefanya udaku kwa kudokezadokeza identity ya "waziri kijana" akiogopa, akishindwa kujiamini kuanisha anatachotaka kusema. Ndio nilivyomaanisha, aache kuwa wussy na mdaku.

Asante Kuhani. Ni woga na uchokozi. Alijua fika kauli kama hiyo ingepelekea nini. Hivi Ngeleja kwa mfano sio waziri kijana? No wonder kusemwa Mengi anatafuta popularity. Kama aliona hawezi kutaja jina angetafuta njia nyingine ya kutoa hiyo habari (kama kuwapa GP waichapishe). Ambavyo JF is where people can talk openly, one anaweza kuuita udaku na mwingine akaona sio udaku. Mwisho wa siku tunakubali au kutokukubaliana pale ukweli unapobainika.
 
Mambo ya udaku yametoka wapi tena wakuu? Kwani Mengi naye si ana haki ya kusema chochote kama tulivyo na haki hiyo sisi wengine? Iweje leo aseme kile kinachomkera halafu ashutumiwe kuwa mdaku?

Naomba ndugu zangu tukumbuke kuwa wengi wetu hapa hatuna uwezo au ujasiri wa kuitisha mkutano wa wanahabari na kumsema waziri mmoja wa serikali hii. Ndio maana tunatumia jamvi hili. Hii si mara ya kwanza kwa Mengi kuzungumzia juu ya vitisho anavyopata. Binafsi, nakumbuka mara ya kwanza ilikuwa kwenye miaka ya tisini ambapo alitangaza kuwa kuna wa(m)fanyabiashara wa kiasia (hakutaja jina) waliotishia kumuua. Kama mkuu Kinyambiss alivyosema, sheria ina mkondo wake na wafanyabiashara/viongozi wote wanajua hilo kwani wanaweza kutumia kumshtaki mtu au wanaweza kushtakiwa. Ningependa niwapinge wakuu wanaodai kuwa Mengi anatafuta popularity. Nafikiri kati ya magazeti, redio na TV anavyovimiliki, angeweza kujitangaza bila kumtuhumu waziri wa serikali.

Hivyo basi, kwa vile hatujui kwa ukweli ni waziri gani anayetajwa au ni vitisho gani vilitolewa, tuvute subira na ukweli utatujia. Haisaidii kama tukigeuza jamvi hili kuwa kitovu cha uzushi.
 
Alianza kwa kukurupuka na kutishia kulishtaki gazeti la mwanahalisi. Akajisahau kabisa kwamba yeye ni waziri mwenye dhamana ya kumlinda Kubenea na kwamba IMMA ina wakurugenzi na wazungumzaji wake.

Baadae kawatembelea wahalifu mahabusu walioshitakiwa na serikali akasahau technically yeye ni mmoja (tena muhimu sana) ndani ya serikali na ndio walioshitaki

Watuhumiwa wakatolewa mahabusu without removal order hadi kufukuzwa mahakamani na yeye akawa wa kwanza kuitetea magereza kwa kosa hilo la wazi kabisa la kujisahau

Halafu akawakashifu walemavu wa ngozi kwa kuongea maneno ambayo anajaribu kuyaruka kwa utetezi dhaifu ajabu

Na sasa amemtishia Mengi na demokrasia ya vyombo vya habari na kujaribu kutetea ufisadi wazi wazi bila aibu.

Huyu bwana mdogo kwanza kabisa amepwaya kwenye hiyo ministry. Utendaji wake umefikia kikomo (very unfortunately). Nilidhani alivyoponea chupu chupu kule ministry of energy angejifunza; kumbe he has reached the bar!

Siasa za makundi ni utamaduni popote pale duniani. Kama yeye anashindwa kuona upepo na kugundua ni kundi gani he should side with at his young political age, basi amekwisha!

He has to go now. Kwenye siasa aondoke kabisa. Arudi tu kwenye professional yake!

- Mkuu pole pole, hakuna jina la waziri lililotajwa hapa na Mzee Mengi, au?, so far hiki kitendawili kimeniacha hoi sana kwamba the mighty Mengi anaogopa kutaja jina la waziri anaishia kwenda national kuimba taarabu?

- Mawaziri vijana waliosoma kwenye awamu ya nne wako wangapi? au ni mmoja tu huyu anayetafutwa sana hapa JF? I mean ikigundulika kuwa sio yeye itakuwaje? Wakuu kwanza tutafute facts zote za the ishu kabla ya kuruka na hizi hukumu nzito nzito, hatuwezi kuendesha taifa na mob justice!

With all due respect kwa mzee Mengi ambaye ninamuheshimu sana kwa kulisimamia taifa, kwenye hili hajatusaidia kabisa ila anatugawa as a nation na it is wrong!
 
TAARIFA YA BW. REGINALD A. MENGI, MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LIMITED KWA VYOMBO VYA HABARI


Hivi karibuni waziri mmoja kijana anayeongoza wizara nyeti alipendekeza nibambikiziwe kodi bandia ya kiasi kikubwa nitakachoshindwa kulipa na hatimaye nifilisiwe kama njia pekee ya kuninyamazisha kabisa eti kama alivyofilisiwa tajiri mmoja mkubwa huko Urusi.

Alidai kwamba vyombo vyangu vya habari vimekuwa mno mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.

- Waziri wa mambo ya ndani anaweza kuhusika na kodi? I am missing something here or what?

Hivi kweli wakuu hii thread nzima na matusi yote yaliyorushwa humu kwa waziri ambaye hakutajwa jina, ni kwa sababu tu ya haya maneno juu au kuna mengine yamefutwa?
 
- Waziri wa mambo ya ndani anaweza kuhusika na kodi? I am missing something here or what?

Hivi kweli wakuu hii thread nzima na matusi yote yaliyorushwa humu kwa waziri ambaye hakutajwa jina, ni kwa sababu tu ya haya maneno juu au kuna mengine yamefutwa?

Influence yake ni kubwa hata kama sio waziri wa fedha. Ni waziri wa mambo ya ndani na pia anaweza mfanya haonekane threat kwa national security
 
kwa jinsi mambo yanavyokwenda hata kama masha si waziri mhusika nadhani
ni vyema huyu mheshimiwa akaenda "low profile" na kisha afanyie kazi issue
angalau moja anayoweza "kutoka nayo".
haya maneno (isomeke kashfa) anazohusishwa nazo nadhani zikiendelea
zitamtilia ukungu matamanio yake ya kisiasa.
 
Influence yake ni kubwa hata kama sio waziri wa fedha. Ni waziri wa mambo ya ndani na pia anaweza mfanya haonekane threat kwa national security

- Mkuu ahsante kwa post yako, Mengi ni mtumzima sana na mwenye uzoefu mkubwa sana na serikali, hakutaja jina waziri anayemtisha, sasa eti kuna anayesema kwamba waziri wa jamhuri ajiuzulu kwa sababu Mengi ametoa taarifa kwa taifa bila kutaja jina la waziri, sasa huyu waziri wa ndani ajiuzulu kwa sababu huenda Mengi anamsema yeye, is that so?

- Kweli huo utawala wa kusadikika ndio inapaswa kua muongozo wa taifa letu la kesho? Yaani mimi leo ni kukurupuka na kusema waziri flani kijana ana elimu sana ananifuata fuata, basi ahaaa huyu ni waziri fulani huyu ajiuzulu sasa huyo hafai kabisaa?

- Jamani mweee! hivi kweli Tanzania tumefikia this low?
 
- Mkuu ahsante kwa post yako, Mengi ni mtumzima sana na mwenye uzoefu mkubwa sana na serikali, hakutaja jina waziri anayemtisha, sasa eti kuna anayesema kwamba waziri wa jamhuri ajiuzulu kwa sababu Mengi ametoa taarifa kwa taifa bila kutaja jina la waziri, sasa huyu waziri wa ndani ajiuzulu kwa sababu huenda Mengi anamsema yeye, is that so?

- Kweli huo utawala wa kusadikika ndio inapaswa kua muongozo wa taifa letu la kesho? Yaani mimi leo ni kukurupuka na kusema waziri flani kijana ana elimu sana ananifuata fuata, basi ahaaa huyu ni waziri fulani huyu ajiuzulu sasa huyo hafai kabisaa?

- Jamani mweee! hivi kweli Tanzania tumefikia this low?

Mkuu kweli that is the lowest we can get, it is saddening really. But we should not forget how frustrating this is. We boldly said wazee wamechoka, tunataka vijana a rhetoric which see to have paid some how, look at what we get now from these educated, travelled, rich and visionary young leaders. Nothing. Almost all of hawa viongozi vijana have reduced themselves to zeroes from heroes. I was expecting them to play tough in this corruption scandle, but it seems they have all gone native and are becoming worse than those who have been in the system for decades. Kama Mwanzo wanaonesha ujinga huu, tutegemee nini baadaye??. Kwa hiyo i can understand peoples unguided attacks kwa watu kama hawa.
 
Kwanza habari za siku Mwanamke wa Kiafrika, unapotea mno kwenye mapambano na kuibuka siku za ushindi, huna mpango!

Mhhh,

Mwenzangu, Nilihesabu kuwa wewe ni miongoni wa wale waliodai kuwa mimi naharibu hii forum? What happened? Nikiwa hapa nilikuwa naharibu forum, na nilipotoka ili nisiharibu forum, nikawa msaliti na mkosa mpango?

Mengi amefanya udaku kwa kudokezadokeza identity ya "waziri kijana" akiogopa, akishindwa kujiamini kuanisha anatachotaka kusema. Ndio nilivyomaanisha, aache kuwa wussy na mdaku.

Fair enough,

Swali langu lilikuwa rahisi tu, nilitaka kujua unatafsiri vipi kutojiamini. Asante kwa maelezo mazuri. Kwa tafsiri yako, waweza kumwona Mengi kama wussy na mdaku. Kwa tafsiri yangu, namuona Mengi kama mtu makini kwa kuanza na 45' kabla hajatumia RPG.
 
Wana mtandao mafisadi watajaribu kwa kila wanachoweza kupigana na Mengi kama ambavo wamekuwa wanafanya for a while now. Katika hili, watawasha moto mkubwa sana hapo Tanzania. Alianza Malima, akafuata Manji na sasa wameanza kumtumia huyu kijana wa watu.

Hapa ni Stop..... leave Mengi alone!
 
1.
Mkuu kweli that is the lowest we can get, it is saddening really. But we should not forget how frustrating this is. We boldly said wazee wamechoka, tunataka vijana a rhetoric which see to have paid some how, look at what we get now from these educated, travelled, rich and visionary young leaders. Nothing. Almost all of hawa viongozi vijana have reduced themselves to zeroes from heroes. I was expecting them to play tough in this corruption scandle, but it seems they have all gone native and are becoming worse than those who have been in the system for decades. Kama Mwanzo wanaonesha ujinga huu, tutegemee nini baadaye??. Kwa hiyo i can understand peoples unguided attacks kwa watu kama hawa.

2.
TAARIFA YA BW. REGINALD A. MENGI, MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LIMITED KWA VYOMBO VYA HABARI

Hivi karibuni waziri mmoja kijana anayeongoza wizara nyeti alipendekeza nibambikiziwe kodi bandia ya kiasi kikubwa nitakachoshindwa kulipa na hatimaye nifilisiwe kama njia pekee ya kuninyamazisha kabisa eti kama alivyofilisiwa tajiri mmoja mkubwa huko Urusi.

Alidai kwamba vyombo vyangu vya habari vimekuwa mno mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.

- Mkuu Bongolander, with all due respect eti hizo quotes mbili hapo juu zina uhusiano wowote with each other?

- Halafu eti Mzee Mengi sasa anakubalika na kuaminika ndani ya JF kwamba akisema ni ukweli? Since when? Kweli tukafukue hukumu zote alizowahi kuhukumiwa hapa JF ambazo ni mbaya kuliko hata hizi za Masha? Lakini this time anasema ukweli na ni lazima waziri wa ndani ajiuzulu maana anasema ukweli na anamsema yeye haiwezekani akawa anamsema mwingine, this is Mengi bwana you know he is telling the truth,

- Really? Yale tuliyoambiwa humu ndani ya Mengi kuiba hela za vilema na kukwepa kulipa kodi ya benzi sasa yameisha kwa vile huenda amegusa tunapopataka? Duhh! What a contradictoures!

Sasa Mengi is clean clean, lahaula lakwata!
 
Wana mtandao mafisadi watajaribu kwa kila wanachoweza kupigana na Mengi kama ambavo wamekuwa wanafanya for a while now. Katika hili, watawasha moto mkubwa sana hapo Tanzania. Alianza Malima, akafuata Manji na sasa wameanza kumtumia huyu kijana wa watu.

Hapa ni Stop..... leave Mengi alone!

I agree...they should leave Mengi alone
 
Nafikiri waziri Masha anasikitisha sana.

Ungetegemea ujana wake, kuijua dunia na pia kuwa na pesa za kutosha kungemfanya huyu kijana mwenzetu afanye yale tunayoyaamini wengi, lakini inaelekea ni mjinga kama Watanzania lundo nzima ambao tumekuwa tukigongana nao. Ukiwakuta huku majuu utafikiri watu wa maana, wakirudi nyumbani ni wabaya kuliko hata watu ambao hawana exposure kubwa.

Hii ni aibu kubwa sana kwa vijana wote. Hatuna tofauti na watu kama akina Yona, Ballali, Chenge na wengine.

Kushindwa kwake kushughulikia matatizo ya Albino ni dalili tosha kwamba huyu kijana mwenzetu yuko out of touch na hana jipya zaidi ya ujinga ambao inaelekea mungu ametulundikia sisi watu weusi.
Hivi tuna matatizo gani? Aibu kweli kweli.

Mkuu FMES, mwambie huyo kijana aache ujinga na achape kazi, mambo mengine yatafuata.

Mtanzania,

Hii issue ya ma-albino ilimfuta Masha toka kwenye list yangu ya watu makini. Hii kwangu ilikuwa kubwa kuliko hata ile ya mwanahalisi.

Huu ugomvi wa mafisadi na Mengi unazidi kukua siku hadi siku. Magazeti ya Thisday na Kulikoni yamewaweka pabaya sana mafisadi. Wanamwandama sana Mengi kwa kinachoandikwa kwenye magazeti yake.

Kuna wakati walileta ugomvi wao dhidi ya Mengi hapa JF. Maneno kibao hapa kuwa Mengi ndio anamiliki hii forum, mara kuwa Mengi haguswi nk. Watu hapa wanaona kinachoendelea, na kwa hili, ukichukulia na yale yaliyosemwa hapa na kwenye magazeti nyumbani karibuni kuwa kuna waumini wa dini fulani wana mpango wa kugomea bidhaa za Mengi, wenye kuona kinachoendelea wanaweza kuona hii series inaelekea wapi.


Kuna Mengi sana sikubaliani na Mengi. Najua pia kuwa sio magazeti yote ya IPP yanasakama mafisadi (wtf with nipashe na alasiri) lakini najua kuwa kuna magazeti ya IPP kama Thisday na Kulikoni yameandika mengi sana kuhusu mafisadi na ufisadi wao.
 
Hata hivyo alipotakiwa kufafanua juu ya kauli hiyo Waziri Masha alikanusha kusema hivyo badala yake alifafanua kuwa alieleza Serikali kusikitishwa na mauaji hao na kulaumu tu kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikilikuza suala hilo.

"Sijawahi kuzungumza kitu kama hicho, isipokuwa nilisema kuwa serikali inasikitishwa sana na mauaji hayo na tunafanya juhudi kukomesha, ila baadhi ya waandishi wa habari wanataka kukuza mpaka suala hili kuonekana kuwa ni watanzania wote ndio wanaohusika kitu ambacho si kweli," alisema Bw. Masha.
 
... Halafu msihukumu tu kilichoandikwa hapo kwani waandishi waliokuwepo walipata nafasi ya kuuliza na kuzungumza na Mengi (unless na sisi tumtafute atufafanulie).

Tusubiri magazeti yatakavyoripoti kwani mimi nimepata hard copy to ilivyo na nilisikiliza kidogo ITV kwenye taarifa ya habari ya saa nne usiku. Wakati wakirudia sehemu ya hayo mahojiano.

Mwanakijiji unanishangaza kweli wakati mwingine, yani umeweka habari, umeweka bandiko, ambalo unasema tusicomment based on kile ulichotuandikia kwa sababu hiyo siyo full story. Basi kama ni hivyo chini kabisa ya habari yako ungeandika "hadithi itaendelea gazeti la kesho"!

Hapo ndio tungejua hii hadithi tumesimuliwa nusu tu na kwamba sasa hivi tukalale kama wajukuu wa babu na kesho babu atatumalizia hadithi ya sungura Mengi na paka Masha.

Comments, hukumu, etc. etc. zimekuja based on the information you laid out here, Mr. Mhariri Mtendaji !
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom