MENGI NA IPP WanaHUJUMIWA?

Kachanchabuseta

JF-Expert Member
Mar 8, 2010
7,270
675
WanaJF bado najiuliza kinachoendelea kwa vyombo vya IPP( ITV na Radio one etc) vya mzee mengi. Muda mrefu mzee huyu amekuwa akipambana na mafisadi lakina sasa naona wanatokea mlango wa nyuma na kuanza kuhujumu wafanyakazi wake.

Mimi nahisi TBC na Clouds FM chini ya RA wako behind this, kuna movement kubwa ya wafanyakazi wa IPP kwenda Clouds fm na TBC. Hapa naomba msiangalie kuwa hawa watu kuama ni kwa masilahi yao lakini kuna kitu kiko nyuma yao

Hizi Radio na TV zinatumiwa sana na mafisadi


Denken buiten de doos

Nawakilisha
 
Kings of Kings,

Hilo lisikupe wasi wasi, IPP media inaaminika na Watanzania wengi.

Inawezekana kuna ukweli katika hili lakini watangazaji wazuri wengi watajiunga ITV pia.

Kumbuka watangazaji wengi wanaanzaia IPP.

Vipindi vitaendelea kama kawaida.
 
Hivi wakati ITV inachukua watangazaji wa RTD ilikuwa ni hujuma?
Mengi sio mpinga ufisadi kufikia kuhujumiwa!
 
Bado Watangazaji wengi wazuri wapo mtaani, acha hao waondoke, hautaona pengo Itv na Radio One..
 
hiyo mkuu wala isikupe wasi wasi kama huo yawezakua ni movement of labour just kwa ajili ya maslahi.
Kama makampuni yanapigana vita ya ufisadi then wafanyakazi wanafaidika kwa kuongezewa mishahara ili wahame au wasihame ni jambo nzuri kiuchumi maana vita hii yaboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza idadi ya wafanyakazi and mwishowe uchumi unazidi kukua mkuu.
 
hiyo mkuu wala isikupe wasi wasi kama huo yawezakua ni movement of labour just kwa ajili ya maslahi.
Kama makampuni yanapigana vita ya ufisadi then wafanyakazi wanafaidika kwa kuongezewa mishahara ili wahame au wasihame ni jambo nzuri kiuchumi maana vita hii yaboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza idadi ya wafanyakazi and mwishowe uchumi unazidi kukua mkuu.

Mafisadi wamejaribu kufanya direct attack but now is indirect attack
 
Ni aibu sana vyombo karibu vyote vya habari nchini kumgeuza mjasiriamali Mengi kuwa ndicho chuo chao ambapo mtu akishakufundishwa kazi akaelewa na kuiva, wao wanaenda tu kuvuna sehemu ambako hawakupanda kitu.

Aibu hiyo inakuwa kubwa kwa upande wa serikali ambayo katika soko huria inatakiwa kumsaidi Mengi kwa hali na mali ili aweze kuajiri Wa-Tanzania wengi zaidi lakini badala yake wao ndiyo wa kwanza kupandishia dau wafanyakazi wa mtu binafsi tu anayejihangaikia. Haipendezi hivi wanamvunja moyo na hata wakati mwingine kumkebehi ua hata vitisho kama vya Masilingi..

Kwa kuwa waswahili wengi hatuna nidhamu ya kufanikisha juhudi za kibiashara, wachache wetu kama MMengi wasaidiwe kufikia malengo makubwa zaidi. Kwingineko duniani watu wa aina yake huthainiwa na kusaidiwa mno na serikali husika.

Mhe Nyalandu wewe ulietembea nchi za watu unafahamu sana hili; Mengi na Wa-Tanzania wengine wa aina yake wapate msukumo wa serikali na wala si kuzutwa nyuma shati lake. Wapo akina Mama Lwakatare na kiu ya kukamilisha ndoto ya kutujenge chuo kikuu, Bahresa, Piri Mohamed, Scandinavia bus, SH Amon ...
 
Sidhani kama ni hujuma............. wengi wetu humu JF tushabadirisha makampuni kibao na wala haikuwa hujuma.......... Mimi nadhani ni maslahi tu yanamtoa mtu sehemu moja kwenda nyingine ..................... Inawezekana kuondoka kwa hujuma, lakini silioni hili katika IPP na hao wengine
 
Much as nina-admire juhudi za Mzee Mengi na IPP kuwa kielelezo cha mafanikio ya ujasiriamali wa wazalendo wa Kitanzania, sishawishiki kwamba hama hama hiyo ni hujuma.

Kwanza mtu anahitaji kuelewa hulka ya waandishi kuhama hama kwa matumaini ya kupata nafuu katika vipato vyao, ambavyo kusema ukweli ni vya chini na haviko commensurate na juhudi zao za kutafuta habari, japo mimi nina-question sana weledi wao katika taaluma zao (ukiondoa magwiji wachache).

Hao waliohama IPP ama alitokea sehemu nyingine ndo wakaenda hapo au walianzia hapo lakini na wenyewe wako katika safari ya kutafuta maisha kama wengine. Free movement of labour inataka watu wawe huru kuchagua mazingira wanayodhani ni bora kwa utendaji kazi hata kama hali halisi ni kwamba kule waendako na kwenyewe hakuna chochote kikubwa na cha maana.

Reaction ya IPP inatakiwa kuwa ni kuanziasha sera itakayo ifanya ionekane ni mwajiri bora kwa kutoa mzaingira mazuri na package inayovutia watu kuja na wale waliopo kuendelea kubaki.
 
Ingawa suala la maslahi lina nafasi kubwa katika kuchangia wafanyakazi kuhama kutoka itv kwenda kwingineko mimi mwenyewe nimekumbwa na wasiwasi kwamba huenda kuna mikono ya watu nyuma ya hili. Iko wazi kwamba mzee mengi anao maadui wengi hapa nchini ambao wanajaribu kufanya kila wawezalo kwa nguvu ya pesa jumshusha chini.

Sakata la mchezo mchafu wa dawa za kulevya na kamisha nzowa + others ni kithibitisho tosha. Mbali na RA yule mfadhiri wa yanga Manji naye anafanya kila awezalo kumuangusha adui yake.

Nnacho amini ni kwamba IPP haiwezi kufa kwa kuondokewa na watangazaji wake maana kuna watangazaji wengi sana kwenye vituo vidogo vya dsm na mikoani na wengine wako vyuoni SAUT, SJMC, DSJ na kwingineko ambao wangependa kupata "nationalwide recognition".

Afterall hao watangazaji wanaoondoka sio waanzilishi wa itv/radio one wengi wao waliletwa kuziba nafasi za walioondoka so hata wao wanavyoondoka nafasi zao zinazibwa.

ENDELEA KUPIGA KAZI MZEE MENGI..
 

TBC inapomfuata mfanyakazi mmoja na kumshawishi ajiunge nayo, maana yake hawatamfanyia interview. Je, kumuajiri mtu bila usaili sio ukiukwaji wa taratibu za kuajiri watumishi serikalini? Naombeni ufafanuzi.
 
mada nzuri sana, wandugu reginald mengi sio mzalendo na mpiganaji kiasi wengi wanavyomfikiria. Kwanza ni rafiki kipenzi wa mkwere ambae ni fisadi no 1. Pili bif yake na akina rostam imekaa kimaslahi binafsi zaidi. Janja yake mengi ni kukimbilia kwa wananch ili apate mass suport. Kama angekua mkweli asingekua na kadi ya ccm mpaka leo, na bado ni kada wa ccm na mpambe wa mkwere. Hahujumiwi na mtu yeyote na bado mabaya yake yote yataonekana, kwani mara zote mungu hamfichi mnafiki, waache wa hame tu, hata sylivia nae ataondoka. She is young and very brilliant lawyer. Mengi anapenda umaarufu kwa kujifanya anasaidia sana wakati wafanyakazi wake anawalipa vijisenti. Huo ni unafiki.
 
mada nzuri sana, wandugu reginald mengi sio mzalendo na mpiganaji kiasi wengi wanavyomfikiria. Kwanza ni rafiki kipenzi wa mkwere ambae ni fisadi no 1. Pili bif yake na akina rostam imekaa kimaslahi binafsi zaidi. Janja yake mengi ni kukimbilia kwa wananch ili apate mass suport. Kama angekua mkweli asingekua na kadi ya ccm mpaka leo, na bado ni kada wa ccm na mpambe wa mkwere. Hahujumiwi na mtu yeyote na bado mabaya yake yote yataonekana, kwani mara zote mungu hamfichi mnafiki, waache wa hame tu, hata sylivia nae ataondoka. She is young and very brilliant lawyer. Mengi anapenda umaarufu kwa kujifanya anasaidia sana wakati wafanyakazi wake anawalipa vijisenti. Huo ni unafiki.

Huyu Mengi anayepambwa wengi wetu hatujui upande wake wa pili. ITV/Radio one kuna matatizo ya Uongozi. Wafanyakazi wa idara ya matangazo hawana tarehe maalumu wa kulipwa mishahara, kuna miezi wanalipwa mpaka tarehe 10 ya mwezi unaofuata, sasa katika mazingira kama haya, si ajabu washindani wake kibiashara hata bila hujuma wanaweza kirahisi kabisa kuchukua wafanyakazi.
 
i think ni busara sana kabla ya kumpamba mengi watu wajue mazuri na mabaya yake na msimamo wake upo wapi? Mengi ni mjasiriamali na msingi wake mkubwa ni kutumia mtaji kuwanyonya watu, ili atengeneze faida kubwa zaidi. Hivyo ni lazima ajipendekeze kwa wananchi kwani hiyo ni moja ya marketing strategies zake. Zaidi ya nusu ya watanzania wananunua bidhaa zake kila siku na kumzidishia utajiri. Huyu jamaa sio mtu mzuri ni very fake ndio maana yupo karibu na kikwete ili kulinda biashara zake anamjua kikwete ni mtu wa visasi hivyo anaogopa kufilisiwa na ccm. MENGI NI MNAFIKI SANA ANASTAHILI KUTUBU MADHAMBI YAKE.
 
Itv na radio one wamekosa ubunifu,habari zao si za kina,wavivu wa kutafuta habari.e.g kipindi cha michezo kila siku mashndano ya kuvuta kamba,habari za kimataifa duni...i hate it nowadays.najikuta natizama tbc iliyochakachuliwa.
 
TBC ni chombo kinachojiendesha chenyewe kibiashara baada ya TIDO Mhando kuiua TVT kwa hiyo hatuitegemei tena kama chombo cha taifa ila chombo cha CCM kinachotumika kutangaza mafisadi, Kwa kuaribu vyombo vya Utangazi vya Mengi wanaona sawa kabisa, Walianza na Original Commedy, Maimatha na Ben, Kumbuka Clauds ni rafiki sana na Riz1 na Masha kwa kuwa hata mkurugenzi wao ruge Muta huwa wanachangia madem, ukiangalia hata coment za Kidonde (msema ovyo) utagundua kuwa ni washabiki wa ufisadi hivyo kumhujumu Mengi ni sawa kabisa
 
Mengi si mpambanaji halisi dhidi ya ufisadi. Yuko kimaslahi binafsi zaidi!
I wouldn't therefore sympathise with him.

He should borrow a leaf from a fellow tycoon Sabodo who has even dared to speak vehemently against JK.
We all know whose @...........$ Mengi has always been kissing!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom