Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,385
Mengi anguruma mkutano wa Madola
Na Jesse Kwayu
30th November 2009
B-pepe
Chapa
Maoni
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amesema kwamba sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kukuza ajira, kushiriki katika vita dhidi ya ufisadi pamoja na kulinda mazingira.
Akizungumza mjini hapa mwishoni mwa wiki katika mkutano wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Madola, Mengi pia alisema nguvu za pamoja kati ya serikali na sekta binafsi ndizo zinaweza kusaidia kuleta mabadiliko ya kweli.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini hapa, Mengi pia alisema tatizo kubwa la kutokuendelea kwa Waafrika si umaskini wa kukosekana kwa rasilimali ila fikra zao ambazo alitaka zibadilike.
Alisema kinachotokea kwa Bara la Afrika kwa sasa ni umaskini unaotokana na watu wake kuwa watumwa wa fikra na ili waondokane na hali hiyo na kuweza kutumia rasilimali zao vizuri, ni lazima kwanza wajikomboe kifikra.
Alisema hakuna maendeleo yanayoweza kufikiwa kama mtu hajajikomboa kifikra.
Alisema mdororo wa kiuchumi duniani unaweza kutumiwa na nchi za Afrika na zile zinazoendelea kwa ujumla kubadili hali zao kwa kuongeza thamani kwenye mazao yao ambayo miaka na miaka wamekuwa wanauza kama mali ghafi kwa mataifa yaliyoendelea. Alisema kitendo cha kuuza mali ghafi kwa mataifa ya magharibi ni sawa na kuwa wafadhili kwa mataifa hayo. Alitaka hali hiyo ibadilike.
Mengi alisema rushwa, maarufu kama ufisadi, ni adui mkubwa wa maendeleo ya uchumi na ni lazima vita dhidi yake ihusishe sekta binafsi na serikali kwa pamoja.
Alitaka sekta binafsi ijikite katika kukuza ajira, kupambana na ufisadi pamoja na kukuza ujuzi wa wananchi ili nchi ifanikiwe kujinasua kutoka kwenye mdororo wa uchumi.
Mengi alikuwa mmoja wa wafanyabiashara maarufu kutoka Jumuiya ya Madola aliyepata fursa ya kuzungumza katika mkutano wa Baraza la Biashara la nchi hizo.
CHANZO: NIPASHE
Na Jesse Kwayu
30th November 2009
B-pepe
Chapa
Maoni
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amesema kwamba sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kukuza ajira, kushiriki katika vita dhidi ya ufisadi pamoja na kulinda mazingira.
Akizungumza mjini hapa mwishoni mwa wiki katika mkutano wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Madola, Mengi pia alisema nguvu za pamoja kati ya serikali na sekta binafsi ndizo zinaweza kusaidia kuleta mabadiliko ya kweli.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini hapa, Mengi pia alisema tatizo kubwa la kutokuendelea kwa Waafrika si umaskini wa kukosekana kwa rasilimali ila fikra zao ambazo alitaka zibadilike.
Alisema kinachotokea kwa Bara la Afrika kwa sasa ni umaskini unaotokana na watu wake kuwa watumwa wa fikra na ili waondokane na hali hiyo na kuweza kutumia rasilimali zao vizuri, ni lazima kwanza wajikomboe kifikra.
Alisema hakuna maendeleo yanayoweza kufikiwa kama mtu hajajikomboa kifikra.
Alisema mdororo wa kiuchumi duniani unaweza kutumiwa na nchi za Afrika na zile zinazoendelea kwa ujumla kubadili hali zao kwa kuongeza thamani kwenye mazao yao ambayo miaka na miaka wamekuwa wanauza kama mali ghafi kwa mataifa yaliyoendelea. Alisema kitendo cha kuuza mali ghafi kwa mataifa ya magharibi ni sawa na kuwa wafadhili kwa mataifa hayo. Alitaka hali hiyo ibadilike.
Mengi alisema rushwa, maarufu kama ufisadi, ni adui mkubwa wa maendeleo ya uchumi na ni lazima vita dhidi yake ihusishe sekta binafsi na serikali kwa pamoja.
Alitaka sekta binafsi ijikite katika kukuza ajira, kupambana na ufisadi pamoja na kukuza ujuzi wa wananchi ili nchi ifanikiwe kujinasua kutoka kwenye mdororo wa uchumi.
Mengi alikuwa mmoja wa wafanyabiashara maarufu kutoka Jumuiya ya Madola aliyepata fursa ya kuzungumza katika mkutano wa Baraza la Biashara la nchi hizo.
CHANZO: NIPASHE