Mengi alia na mafisadi; na yeye achunguzwe!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,419
21,244
Mengi alia na mafisadi,adai wanataka kumharibia uhusiano


*Abainisha hana ndoto za kuwa mwanasiasa

Na Mwandishi Wetu


MWENYEKITI Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi, amesema limejitokeza kundi la mafisadi waongo na vibaraka uchwara, wanaomvumishia kuwa anajijengea umaarufu wa kisiasa, tayari kwa kugombea uongozi wa kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao.

Bw. Mengi amesema kundi hilo la watu waovu, wanataka kuharibu uhusiano wake na viongozi wa kisiasa nchini.

"Nia yao ni kuhakikisha kuwa ushupavu na uadilifu wa wale wote wanaomuunga mkono Mhe. Rais katika vita dhidi ya ufisadi, wanadhoofishwa na wakati huo huo mizizi ya ufisadi, inajichimbia zaidi na mafisadi wanajijenga zaidi na kuimarika," alisema Bw.Mengi kupitia katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

Alisema mafisadi hao wanadiriki hata kusema kuwa vyombo vya habari anavyovimiliki na vinavyopiga vita ufisadi, ni adui wa nchi na vinataka isitawalike.

"Sasa tujiulize, adui wa nchi ni yupi, ni yule anayetetea na kulinda mali za nchi yetu au ni yule anayezipora. Je anayetaka nchi yetu isitawalike ni yule anayepora mali ya umma na yule anayepiga vita uporaji wa mali ya umma ?" Alihoji Bw. Mengi.

Aliwaomba wananchi wenye nia njema na nchi yao, wawapuuze mafisadi na waongo, badala yake waongeze nguvu katika vita dhidi ya ufisadi.

Alisema binafsi ameridhika na biashara zake na kwamba anaunga mkono kauli ya Rais kuhusu umuhimu wa kutengenisha shughuli za kibiashara na uongozi wa kisiasa.

"Vile vile naomba ndugu zangu Watanzania waone kwamba heka heka hizi za mafisadi na waongo, zina nia mbaya na ni fitina zenye nia ya kujenga chuki na kuvuruga nchi," alisisitiza ,Bw. Mengi kupitia katika taarifa yake ya kurasa mbili.

Aliwashauri wale aliowaita kuwa ni mafisadi, kuacha fitina za kueneza chuki baada ya kupora mali za umma na kwamba wasitumie nguvu za ufisadi wao kupora amani ya nchi.

"Nawashauri warudishe mali za umma walizopora, waombe ushauri wa viongozi wao wa kiroho, watubu uovu wao na waombe msamaha," alisema.

Alisema litakuwa jambo la kushangaza kuzungumza juu ya kumsamehe yeyote yule wakati mamilioni ya ya fedha yaliyoporwa yamehifadhiwa katika mabenki ndani na nje ya Tanzania wakati wananchi wanakosa fedha za kununulia dawa.
 
Mengi knows once he goes against CCM he is finished.They will bring him down in an instant therefore he knows its best for him if he keeps his political life away from business life.
 
I agree with Bwana Mengi. Some of the people behind the EPA rip off are just big time conmen masqarading as businessmen. In Mengi these so called "succesful " businesmen have found their match. They are "mafisadi" and unpatriotic and will remain so in the hearts and minds of Tanzanians. They have their bodies in Tanzania but their souls in India (or Iran) and keep their money in Europe. Shame and curse be upon them.
 
Wengi wanajua ndiko aelekeako hasa haya mambo ya kijipublicise kwa kila afanyanyacho kwa jamii
 
Mbona kila anayepambana anasema anawajua mafisadi hawataji? Mafisadi noma kila mtu anasemea pembeni na mafisadi wanatisha. Tunajaza thread hapa uwezi ona jina la fisadi, isijekuwa tunajitisha wenyewe? Hata mkuu wa kaya anawaogopa.

Sasa Mengi nae analalamika! Mengi apunguze kulalamika, si nayeye alichota NBC au wakati huo ufisadi ilikuwa bado. Ifikie wakati mafisadi tuwajue tuchukue hatua wenyewe.
 
unakukumbusha article ya mwanakijiji leo mtanzania daima, imenikumbusha ule wimbo tukiwa wadogo

watoto wangu eh, mimi baba yenu eh
sina nguvu tena eh
kupambana na simba eh

tulikuwa tunaimba tunazunguka kwenye mabalamwezi kijijini kwetu kusiko na umeme, watoto hatukuwa na mipaka, kama mnavyofungia watoto wa mjini kwenye mageti, hata kama mnawafungia kwenye mageti, msisahau kuwaimbisha kama alivyoandika mwanakijiji leo

watanzania wangu eh, mimi rais wenu eh
sina nguvu tena eh, kupambana na m afisadi eh
lowasa kanizidi eh, kaungana nao eh
nikipambana nao eh, nitawapata wapi eh
pesa za kampeni eh,

watoto wangu eh, mimi baba yenu eh
 
Mafisadi wanajulikana kwanza na familia zao, ndugu zao, marafiki zao, vimada wao, mafiasadi wenzao, ofisi zao, wafanyakazi wao, jirani zao, bank zao, hospitali zao, hoteli zao, clubs zao, soko lao, maduka yao; JE serikali hapa haijui bado? Wasitu***** akili zetu bwana!
 
...bora ya Mengi ambaye practically kutokana na biashara zake amesaidia familia nyingi sana through ajira na analipa kodi na kutuletea services nyingi tuu,impact ya Mengi ni kwa maelfu for the better....akifilisika msifikiri he'll go down by himself ni wengi watahangaika sana,i respect mengi kwa anayofanya ingawaje naona mmeanza kumponda eti its all publicity,waulizeni ambao watoto wao wanakula na kwenda shule kwa ajira za mengi ndio mtaelewa,hope tungekuwa na Mengi wengine maelfu tungeendelea sana...heshima mbele kwa watu kama kina Mengi sio wanasiasa uchwara wa CCM ambao ni kulinda maslahi yao tuu na matumbo yao!
 
Ni uhusiano gani anaoongelea hapa? uhusiano na nani, kwani wanafanya biashara pamoja?, anyway, sitaki kuingilia sana hili, lakini nafikiri anajitetea yeye mwenyewe/he is defending his interests, labda kashindwa kupigana nao chini kwa chini akaona bora apige kelele. nimeona leo katoa press release kwenye gazeti la Dairy News, ameongea hivyohivyo.
 
Mengi ni "mtaalam" wa kutafuta HURUMA kwa WaTZ. Na anajua muda na namna ya kuwasilisha "malalamiko" yake! Awataje wanaomuandama ili tulie nao kwa niaba yake?
 
Mimi naona Mengi anajitafutia umaarufu kinamna aseme nani kasema anataka yeye agombee urais??
si amtaje na wapi wameeneza uvumi huo?
Chombo gani kilicho tumika?
Huyu anatafuta umaarufu tu hakuna kitu.
 
Mimi naona Mengi anajitafutia umaarufu kinamna aseme nani kasema anataka yeye agombee urais??
si amtaje na wapi wameeneza uvumi huo?
Chombo gani kilicho tumika?
Huyu anatafuta umaarufu tu hakuna kitu.

Yaani wewe na Wildcard ndio mmepalenga vizuri sana!Mengi thinks simply coz he is good when it comes to charity and seems like it is one of his favorite pasttimes kwamba he is a saint in the eyes of the Tanzanians and when he has a small problem we should all carry it on our shoulders.Guess he is mistaken.Ugomvi wake na manji ulipelekea hadi kuundwa kwa kamati za viongozi wa dini kuutatua ulikuwa exaggerated.masuala yake na Masilingi ambayo yalimfanya Mkapa arejee nchini kuja kuwapatanisha vilevile yalikuwa exggerated.Sasa he wants to create a molell out of anthill then wote tuingie kuomba yaishe!
JK alipokuwa anamtambulisha Mengi Marekani kipindi fulani kabla ya mkutano wa Sullivan alisema he is everything in TZ nadhani its gonna be proved!
 
Wakuu heshima mbele,

Baada ya juzi kupitia taarifa kwa vyombo vya habari amabyo ilitolewa na mmoja wawafanyabiahara maarufu,Bwana Mengi kuhusu watuhumiwa wa ufisadi kwamba wanaeneza fitna dhidi yake, na badala yake kurejesha mapesa ya umma waliyoiba.

Ukiangalia kwa Undani,kuhusu kauli hii ni kuwa inawezekana kabisa Mengi anawafahamu wanoeneza fitina juu yake,kwanini hakuwataja watu hao.Mhe . Mengi amekuwa akitaka huruma toka kwa watanzania bila yeye kuguswa huku ni mmoja wao ambao wamesababisha sisi tuwe hapa.


Naomba ninukuu moja ya maneno ya mengi ni kuwa "Nawaomba ndugu zangu Watanzania waone kwamba hekaheka hizi za mafisadi na waongo zina nia mbaya na ni fitna zenye nia ya kujenga chuki na kuvuruga amani,”.Hii inaonesha ni jinsi ganiMengi anawafahamu hao ambao wanataka kuvuruga amani ya nchi na kwanini asiwapeleke katika Vyombo vya kisheria ili waadhibiwe.Naomba Ahojiwe na watu wa usalama na aeleze umma ni kina nani ambao wanataka kuhatarisha amani ya nchi yetu.

Mengi ameenda mbali zaidi,kwamab wanaharibu mahusiano yake na rais wa nchi,hapa mie nimeshindwa kuelewa faida yake ni ipi kama akiwa karibu na viongozi wa juu wa nchi..Inasaidia nini?Kama ana mpango wa kuwasaidia watanzania siyo lazima kuwa karibu na Rais wa nchi.

Kimsingi nimekereka na taarifa hii,haina manufaa kwa sisi watanzania zaidi ya kuchochea vurugu na kuharibu mwelekeo wa Hotuba aliyoitoa Mhe. Rais Wiki iliyopita.rais aliweza kuziba kelele za muungano na akaongelea mambo muhimu ya nchi yetu hasa suala la mipango iliyopo ya chuo kikuu cha DODOMA.

Watu wanatumia siasa kupata sympath,kama wana gomvi wao wa kibiashara siye hautuhusu.


Kwa hili Mengi ameteleza,na kamwe asipende kutegemea huruma za wananchi,kama anawaju mafisadi na awataje kwa majina ns iyo kuzungumza kwa uhalisia.
 
Kwa hili Mengi ameteleza,na kamwe asipende kutegemea huruma za wananchi,kama anawaju mafisadi na awataje kwa majina ns iyo kuzungumza kwa uhalisia.[/SIZE][/QUOTE]

yamekuwa hayo, kila mtu anazake
 
Kumbe sikuwa peke yangu......!

Au angalau angetujulisha hayo waliyomfanyia hata aseme wanataka kuvuruga amani then we (Tanzanians) ndo tujaji kama ni mbinu za kuvuruga amani au ni personal issues zao yeye na wao. Kuna kilichofichika hapa

Sijui pengine amekisema sikukisikia. mimi huwaga nabadilisha chanel mara awekwapo huyu maana akianza kuhutubia basi wimbo unaanza chanel 5 na kuisha bado akiongea..... anabore sometimes.!
 
Kwa kweli... Huyu mzee anaheshimika lakini amekuwa na tabia fulani ya kutuweka Watanzania upande wake kila akizungumzia matatizo yake na wafanyabiashara wenzake!!! Nakumbuka hata wakati wamepelekana mahakamani na Manji alipohojiwa alikuwa anajiunganisha na Watz kana kwamba tunajua bifu lao. Nimemfuatila kwa muda mrefu ni mtu anayetafuta public sympath siku zote.

Itabidi naye achunguzwe, mbona kodi alizokwepa watu wanaelewa na hawasemi? au tuanike uozo wake hapa Jf? Nadhani hajawa msafi kiasi cha kujiunganisha na watanzania kana kwamba tuna vita moja na yeye!

Sio kweli hata kidogo!!!! Na wewe kwa maana moja au nyingine ni.....
 
mengi sio fisadi magazeti yake yanaandika habari za ufisadi, kwani nyie hamwajui mafisadi mbona sasa tunakuwa kama hatuwajui. walishatajwa na wakatishia kwenda mahakamani labda wameficha ukweli sasa lakini hakun mtanzania mwenye akili timamu asiyewajua mafisadi hapa.ni kama vile kusema hakuna ukimwi tanzania na hakuna mmoja wetu ambae hajakumbwa na janga la ukimwi. linganisha ukimwi na ufisadi.
 
Mengi anashangaza sana kila anapozidiana kete na wenzie yeye hukimbilia kwa wananchi kuomba sympathy. Ch akushangaza hapa imemwaga hilo press realease lake tata na kuweka mafumbo chungu nzima sjui anatagemea nani ategue hicho kitendandawili. Kwanini asiwataje hao watu anaishia kumwaga mafumbo?

Ni usanii kwa kwenda mbele........
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom