Nchagwa Chacha
Member
- Apr 5, 2011
- 58
- 3
habari zenu wana JF? Yamenibana imenibidi niseme inasikitisha kuona meneja wa Tra border ya sirari anaishi hotel yapata sasa na kwa gharama ya juu kwa hadhi ya hotel hiyo inayojulikana kwa jina la Goldland Tarime mjini. Ninachohitaji kujua huyu mtu anatumia pesa zake binafsi au anatumia kodi za wananchi kwa kulipia gharama za hotel malazi na chakula takriban mwaka sasa ambapo waliomtangulia walifikia kwenye nyumba hiyo hiyo aliyoikataa yeye na kupelekea kuishi hotel. Mimi nashindwa kuielewa serikali kwa kuingia gharama kubwa kwa mtu mmoja pesa ambayo ingetumika hata kuchongea madawati ya watoto wetu shuleni au kujenga madarasa. Naiomba serikali ikemee hili mara moja kwa matumizi mabaya ya kodi za wananchi.