Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,144
Meneja wa Shoprite kizimbani kwa kuwafungia chumbani wafanyakazi
RAIA wa Kizungu, ambaye ni Meneja Mkuu wa duka la kuuza bidhaa za kusindika maarufu kama Shoprite, amefikishwa kizimbani kwa tuhuma za kuwafungia katika chumba wafanyakazi wa duka hilo kinyume na sheria.
Mtuhumiwa huyo ni Fredrick Skein [33] ambaye alitokea nchini Afrika ya Kusini, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala ya jijini Dar es Salaam kujibu tuhuma zinazomkabili.
Alisomewa shtaka lake katika Mahakamani hiyo na Inspekta Msaidizi wa Polisi, Denis Mujumba mbele ya Hakimu Janeth Kinyage wa Mahakama hiyo.
Mujumba alidai kuwa, mshitakiwa alitenda kosa hilo Novemba 12, mwaka jana, katika duka hilo lililopo barabara ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
Ilidaiwa kuwa mshitakiwa aliwafungia wafanyakazi hao katika chumba zaidi ya masaa kadhaa kwa sababu ambazo hazikuweza kuelezwa Mahakamani awali hadi kesi itakaposikilizwa.
Wafanyakazi waliofungiwa katika chumba hicho walikuwa watatu na walitambulika kwa jina la Anna Temu, Juma Said na Hassan Kassim.
Hakimu alimwambia mshitakiwa angeweza kuwa nje kwa dhamana kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaoweza kusaini milioni moja kila mmoja na kuwasilisha hati zake za kusafiria mahakamani.
Hata hivyo mshitakiwa alitimiza masharti ya dhamana na kuweza kuwa nje kwa dhamana, na kesi iliahirishwa hadi hapo Machi 3, mwaka huu, itakapotajwa tena.
RAIA wa Kizungu, ambaye ni Meneja Mkuu wa duka la kuuza bidhaa za kusindika maarufu kama Shoprite, amefikishwa kizimbani kwa tuhuma za kuwafungia katika chumba wafanyakazi wa duka hilo kinyume na sheria.
Mtuhumiwa huyo ni Fredrick Skein [33] ambaye alitokea nchini Afrika ya Kusini, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala ya jijini Dar es Salaam kujibu tuhuma zinazomkabili.
Alisomewa shtaka lake katika Mahakamani hiyo na Inspekta Msaidizi wa Polisi, Denis Mujumba mbele ya Hakimu Janeth Kinyage wa Mahakama hiyo.
Mujumba alidai kuwa, mshitakiwa alitenda kosa hilo Novemba 12, mwaka jana, katika duka hilo lililopo barabara ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
Ilidaiwa kuwa mshitakiwa aliwafungia wafanyakazi hao katika chumba zaidi ya masaa kadhaa kwa sababu ambazo hazikuweza kuelezwa Mahakamani awali hadi kesi itakaposikilizwa.
Wafanyakazi waliofungiwa katika chumba hicho walikuwa watatu na walitambulika kwa jina la Anna Temu, Juma Said na Hassan Kassim.
Hakimu alimwambia mshitakiwa angeweza kuwa nje kwa dhamana kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaoweza kusaini milioni moja kila mmoja na kuwasilisha hati zake za kusafiria mahakamani.
Hata hivyo mshitakiwa alitimiza masharti ya dhamana na kuweza kuwa nje kwa dhamana, na kesi iliahirishwa hadi hapo Machi 3, mwaka huu, itakapotajwa tena.