Tatu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2006
- 1,100
- 313
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi mkoani Kagera, imemhukumu Meneja wa Shirika la Posta tawi la Biharamulo mkoani Kagera, Claud Masali (52), kifungo cha miaka 250 baada ya kupatikana na makosa 50.
Hukumu hiyo iliyosomwa kwa zaidi ya saa tatu na kuvuta hisia za wengi, ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Kagera, Wilbard Mashauri, baada ya kuridhika na upande wa mashitaka kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.
Mtuhumiwa huyo alidaiwa kuwa wakati akiwa kazini katika tawi hilo, kwa nafasi yake, alisababisha hasara ya sh milioni 25.
Kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, Mkaguzi wa Polisi, Jumanne Ibrahim na Mrakibu wa Polisi, Obeid Mhandi, walidai mahakamani hapo kuwa mkuu huyo wa Posta, alitenda kosa hilo Septemba 11, mwaka 2004 kwa nyakati tofauti, akiwa mtumishi wa shirika hilo.
Walitaja baadhi ya makosa hayo kuwa ni pamoja na kuingiza mahesabu ya uongo kwenye vitabu vya mahesabu, kughushi na kuiba fedha za shirika kwa kuongeza sifuri mbele pindi mteja alipotumiwa fedha Money Fax.
Walidai kuwa mkuu huyo bila kujali, alitumia wadhifa wake kuliibia shirika lake ambapo kwa kila mteja aliyetumiwa fedha, alikuwa akilazimika kuongeza sifuri mbele na kuonekana ni zaidi, na kiasi kilichokuwa kikibaki, alikuwa akichukua yeye na kuingiza mfukoni mwake.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, kati ya makosa hayo 50, atatumikia kifungo cha miaka mitano kwa kila kosa, hivyo kulazimika kutumikia kifungo cha miaka 250 jela, lakini adhabu hizo zitakwenda pamoja.
Awali kabla ya kusomewa hukumu hiyo, mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa wilayani Misungwi mkoani Mwanza, anadaiwa kuruka dhamana baada ya kuona mwelekeo wa kesi yake unaenda vibaya.
Hata hivyo, alikamatwa Aprili 9 mwaka huu jijini Mwanza, akiwa amejificha na tangu wakati huo alikuwa rumande hadi jana alipohukumiwa kifungo cha miaka 250 jela.
Source: Tanzania Daima
Nafikiri huu ni mfano wa kuigwa na Mahakama zote Tanzania. Ufisadi utapungua kama mahakama na waendesha mashitaka watafanya kazi zao kwa uadilifu.
Hukumu hiyo iliyosomwa kwa zaidi ya saa tatu na kuvuta hisia za wengi, ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Kagera, Wilbard Mashauri, baada ya kuridhika na upande wa mashitaka kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.
Mtuhumiwa huyo alidaiwa kuwa wakati akiwa kazini katika tawi hilo, kwa nafasi yake, alisababisha hasara ya sh milioni 25.
Kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, Mkaguzi wa Polisi, Jumanne Ibrahim na Mrakibu wa Polisi, Obeid Mhandi, walidai mahakamani hapo kuwa mkuu huyo wa Posta, alitenda kosa hilo Septemba 11, mwaka 2004 kwa nyakati tofauti, akiwa mtumishi wa shirika hilo.
Walitaja baadhi ya makosa hayo kuwa ni pamoja na kuingiza mahesabu ya uongo kwenye vitabu vya mahesabu, kughushi na kuiba fedha za shirika kwa kuongeza sifuri mbele pindi mteja alipotumiwa fedha Money Fax.
Walidai kuwa mkuu huyo bila kujali, alitumia wadhifa wake kuliibia shirika lake ambapo kwa kila mteja aliyetumiwa fedha, alikuwa akilazimika kuongeza sifuri mbele na kuonekana ni zaidi, na kiasi kilichokuwa kikibaki, alikuwa akichukua yeye na kuingiza mfukoni mwake.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, kati ya makosa hayo 50, atatumikia kifungo cha miaka mitano kwa kila kosa, hivyo kulazimika kutumikia kifungo cha miaka 250 jela, lakini adhabu hizo zitakwenda pamoja.
Awali kabla ya kusomewa hukumu hiyo, mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa wilayani Misungwi mkoani Mwanza, anadaiwa kuruka dhamana baada ya kuona mwelekeo wa kesi yake unaenda vibaya.
Hata hivyo, alikamatwa Aprili 9 mwaka huu jijini Mwanza, akiwa amejificha na tangu wakati huo alikuwa rumande hadi jana alipohukumiwa kifungo cha miaka 250 jela.
Source: Tanzania Daima
Nafikiri huu ni mfano wa kuigwa na Mahakama zote Tanzania. Ufisadi utapungua kama mahakama na waendesha mashitaka watafanya kazi zao kwa uadilifu.