Membe kuwania urais 2015...

Sungi

Senior Member
Apr 29, 2009
149
47
Kuna tafrani ya kutupiana maneno kati ya mzee Mudhihiri na Membe kuhusu kujengwa kwa kiwanda cha saruji kilomita 35 kutoka eneo lenye malighafi ambalo ni Mchinga ambapo Mudhihiri ndio Mbunge.

Kitu ambacho kinanishangaza ni hili la kwamba Membe ana nia ya kugombea urais mwaka 2015 (ana haki kama mtanzania kufanya hivyo).

Alipoulizwa (Membe) iwapo anahisi matamshi ya Mudhihir yana msukumo wa maadui wake kisiasa ambao wanahisi anaweza kugombea urais 2015, Membe alisema kwa vyovyote itakuwa hivyo.

Hivi kuwa waziri wa mambo ya nje ndio ticket Tanzania kuwa rais?

(Source: Mwananchi Mwananchi Communications Ltd)
Je anazo qualities zote za kiongozi? Ni zipi? Je ni kweli ana hasira? na itakuwaje watu ambao aliwakosea au walimkosea siku za nyuma? Maana mmoja kati ya sifa kuu za kiongozi ni kuwa mvumilivu ama sivyo itakuwa kila kukicha unanyonga watu.

Je wanaompinga wana mawazo gani kuhusu huyu mheshimiwa? Nazungumzia kuanzia akina Mudhihir mpaka waliopo madarakani juu.

Je tangu aingie Foreign kuna mabadiliko gani makubwa kashafanya?

Nauliza kwa sababu inaonekana kuwa kuna kila dalili anaweza kuwa rais wetu 2015 lakini je watanzania wategemee rais wa namna gani na presidency yake itakuwa ya namna gani?
Membe akiri kuwania urais 2015
*Aelezwa kuiga mbinu alizotumia JK
*Kombora la Mudhihir lamshusha nguvu
*Aelezwa ni nyoka anayemaliza wenzake kwa rais

Na Mwandishi Wetu, Dodoma-UMMA Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Kimataia, Bernard Membe amekuwa ni kiongozi wa kwanza kukiri kuwa ana nia ya kuwania urais mwaka 2015 ikiwa ni siku chache baada ya Mbunge wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir kumtaja kwa mafumbo bungni mjini hapa wiki hii.

Membe alinukuliwa na vyombo vya habari siku moja baada ya Mudhihir kisha kombora lilikuwa likimtaja Waziri mmoja anayetokea mkoa wa Lindi kuwa amekuwa mbinafsi na fisadi kutokana na tabia yake ya kutumia jina la rais Jakaya Kikwete kukwamisha ujenzi wa kiwanda cha saruji katika jimbo la Mudhihir.

Mudhihir ambaye inalezwa kabla ya kutoa kombora hilo aliwasiliana na wabunge wenzake kutoka Lindi, alifafanua kuwa ubinafsi wa waziri huyo ambaye sasa imefahamika wazi kuwa ni Membe, unalenga kumdhohofisha yeye kisiasa kwa kuwa tu, anaonekana kupingana na harakati za Membe kuwania urais mwaka 2015 kwa kutumia mbinu kama alizowahi kuzitumia rais Kikwete miaka zaidi ya kumi iliyopita.

Membe safari hii licha ya kukubali kuwa na nia ya urais anaelezea kuwa, alichokizungumza Mudhihir kinatokana na wabaya wake wasiomtakia mema katika harakati zake za kuutaka urais na kutumia wizara ambayo ilitumiwa na rais Kikwete kupata urais mwaka 2005.

‘Bila shaka, bila shaka. Mudhihir ninayemfahamu asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye, namheshimu sana," alinukuliwa Membe na gazeti moja la kila siku, akifafanua kuhusu dhana ya Mudhihir kutumiwa na watu kumlipua.

Lakini kombora la Mudhihir linaelezwa kuwa kali kupita yote katika maisha ya kisiasa ya Membe. Maisha ya kisiasa ya Waziri huyu yanaelezwa kuwa yale ya kutumia migongo ya wengine kupandia na mara kadhaa waziri huyu ametazama wapi panaweza kumanyua na kuangusha kila anayedhani anaweza kuwa mwiba kwake.

Watu wengi waloongea na Gazeti hili wamekuwa wakijiuliza hao maadui wa Membe ni kina nani? Amewafanyia nini? Wana chuki gani dhidi yake? Na kwanini yeye ahusishwe na hili? Na ni kipi kilichomfanya ajibu juu ya hoja hii wakati kuna waziri mwingine anayetoka Lindi? Haya na mengine ni maswali ambayo membe anatakiwa kuwajibu watanzania ambao walistushwa na kauli iliyotolewa na Mudhihiri nay eye kuijibu.

Ni katika mbinu za aina hiyo, Waziri huyu anaeleza kumteka Rais Kikwete kwa kuwa ananufaika na kuwa naye katika ziara nyingi za ughaibuni, ziara zinazoelezwa hapa ndani kuwa haziendani na kunyanyua uchumi wananchi na badala yake kuliingiza taifa katika madeni ya siku zijazo.

Waziri Membe anatumia kigezo cha yeye kuwa Mkatoliki kama mtaji wa kisiasa na mbinu hii anaamini ndiyo itakayomnyanyua ili kushinda kiraisi katika uchaguzi ujao. Hata hivyo hivi karibuni inaelezwa kuwa, alijiiingiza katika mgogoro mkubwa na madhehebu ya Kikirstu, baada ya kujiingiza kutetea suala la Tanzania kujiunga na OIC na lile la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

Kujiingiza kwa Membe katika mambo haya tata, kunatafsiriwa kulilenga kumfurahisha rais Kikwete kwa kuwa mambo hayo yameandikwa katika ilani ya uchaguzi na yanaonekana hayatatekelezwa kwa kuwa wakristo wana msimamo mkali.


Pia kuna dhana kuwa, kujiingiza kwa Membe katika mambo haya tata, kuna lengo la kusaka misaada hasa ya kifedha kwa mataifa yenye asili ya Kiarabu, ili kumsaidia katika kampeni zake za kuwania urais mwaka 2015, jambo ambalo yeyeamkuwa akilipinga.

Membe kwa siku za nyuma alikuwa miongoni mwa kundi la Mtandao, kundi linalofahamika katika kumuingiza madarakani rais Kikwete. Inaelezwa sasa baada ya kundi hilo kugawanyika, sasa hivi Membe ameungana na kundi jingine linalojumuisha viongozi wakubwa katika sehemu nyeti kama Bunge na pia wafanyabiashara ambao wara kadhaa wamekuwa akijiibua kama wasemaji wa watanzania.

Hata hivyo, kuna taarifa kuwa, waziri huyu amekuwa akijionesha kuwa ni shushushu wa Uasalama wa Taifa, mbinu anayoitumia kutanua mtandao wake ambao sasa unaonekana kuanza kupata ushindani hasa baada ya Mudhihir kuamua kwa makusudi kuulipua.

Wachunguzi wa mambo ya Kisiasa wamediriki kukubali kauli ya Mudhihiri kuwa Membe ni Nyoka aina ya MDIMU ambae sifa yake kubwa ni ubinafsi na roho mbaya, Membe itakumbukwa kuwa alihusika kwa kiasi kikubwa kumaliza wenzie hata wakati wa awamu ya Tatu aliwamaliza kina Hans Kitine, Malecela, kwa kutumia ushushu wake aliweza kumtokomeza swahiba wake wa Sasa Sitta asipate nafasi baada ya kushindwa 95 huko Urambo, alitumia uzandiki aloutaja Mudhihiri kufanikisha wenzie wanamtandao wasipate nafasi ktk awamu ya kwanza ya Mzee mkapa ambae alimstukia na Kumuondoa na kumpeleka nje ya Nchi.
 
Last edited:
The formula has worked twice before, ndo maana anayeingia kwa hiyo ofisi anaona ashaingia kwa home stretch... Kidogo tungekuwa na Woman President kama Ban Ki Moon asingefanya mambo yake..
 
Huyu Membe either ni shallow thinking au cocky enough.

Hili swali lilikuwa na swali lililojificha, in other words, in not so many words, aliulizwa "ni kweli una nia ya kugombea urais 2015?". Akajibu "Ndiyo".

Kama ana nia ya kugombea urais mtihani wa kwanza kashashindwa.
 
Membe akiri kuwania urais 2015
*Aelezwa kuiga mbinu alizotumia JK .
*Kombora la Mudhihir lamshusha nguvu
*Aelezwa ni nyoka anayemaliza wenzake kwa rais.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma-UMMA Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Kimataia, Bernard Membe amekuwa ni kiongozi wa kwanza kukiri kuwa ana nia ya kuwania urais mwaka 2015 ikiwa ni siku chache baada ya Mbunge wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir kumtaja kwa mafumbo bungni mjini hapa wiki hii.

Membe alinukuliwa na vyombo vya habari siku moja baada ya Mudhihir kisha kombora lilikuwa likimtaja Waziri mmoja anayetokea mkoa wa Lindi kuwa amekuwa mbinafsi na fisadi kutokana na tabia yake ya kutumia jina la rais Jakaya Kikwete kukwamisha ujenzi wa kiwanda cha saruji katika jimbo la Mudhihir.

Mudhihir ambaye inalezwa kabla ya kutoa kombora hilo aliwasiliana na wabunge wenzake kutoka Lindi, alifafanua kuwa ubinafsi wa waziri huyo ambaye sasa imefahamika wazi kuwa ni Membe, unalna kumdhohofisha yeye kisiasa kwa kuwa tu, anaonekana kupingana na harakati za Membe kuwania urais mwaka 2015 kwa kutumia mbinu kama alizowahi kuzitumia rais Kikwete miaka zaidi ya kumi iliyopita.

Membe safari hii licha ya kukubali kuwa na nia ya urais anaelezea kuwa, alichokizungumza Mudhihir kinatokana na wabaya wake wasiomtakia mema katika harakati zake za kuutaka urais na kutumia wizara ambayo ilitumiwa na rais Kikwete kupata urais mwaka 2005.

‘Bila shaka, bila shaka. Mudhihir ninayemfahamu asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye, namheshimu sana,” alinukuliwa Membe na gazeti moja la kila siku, akifafanua kuhusu dhana ya Mudhihir kutumiwa na watu kumlipua.

Lakini kombora la Mudhihir linaelezwa kuwa kali kupita yote katika maisha ya kisiasa ya Membe. Maisha ya kisiasa ya Waziri huyu yanaelezwa kuwa yale ya kutumia migongo ya wengine kupandia na mara kadhaa waziri huyu ametazama wapi panaweza kumanyua na kuangusha kila anayedhani anaweza kuwa mwiba kwake.

Watu wengi waloongea na Gazeti hili wamekuwa wakijiuliza hao maadui wa Membe ni kina nani?amewafanyia nini?wanachuki gain dhidi yake?na kwanini yeye ahusishwe na hili?na nikipi kilichomfanya ajibu juu ya hoja hii wakati kuna waziri mwingine anaetoka Lindi?haya na mengine ni maswali ambayo membe anatakiwa kuwajibu watanzania ambao walistushwa na kauli iliyotolewa na Mudhihiri nay eye kuijibu.

Ni katika mbinu za aina hiyo, Waziri huyu anaeleza kumteka Rais Kikwete kwa kuwa ananufaika na kuwa naye katika ziara nyingi za ughaibuni, ziara zinazoelezwa hapa ndani kuwa haziendani na kunyanyua uchumi wan chi na badala yake kuliingiza taifa katika madeni ya siku zijazo.

Waziri Membe anatumia kigezo cha yeye kuwa Mkatoliki kama mtaji wa kisiasa na mbinu hii anaamini ndiyo itakayomnyanyua ili kushinda kiraisi katika uchaguzi ujao Hata hivyo hivi karibuni inaelezwa kuwa, alijiiingiza katika mgogoro mkubwa na madhehebu ya Kikiristu, baada ya kujiingiza kutetea suala la Tanzania kujiunga na OIC na lile la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi. Kujiingiza kwa Membe katika mambo haya tata, kunatafsliwa kulilenga kumfurahisha rais Kikwete kwa kuwa mambo hayo yameandikwa katika ilani ya uchaguzi na yanaonekana hayatatekelezwa kwa kuwa wakristo wana msimamo mkali.

Pia kuna dhana kuwa, kujiingiza kwa Membe katika mambo haya tata, kuna lengo la kusaka misaada hasa ya kifedha kwa mataifa yenye asili ya Kiarabu, ili kumsaidia katika kampeni zake za kuwania urais mwaka 2015, jambo ambalo yeyeamkuwa akilipinga.

Membe kwa siku za nyuma alikuwa miongoni mwa kundi la Mtandao, kundi linalofahamika katika kumuingiza madarakani rais Kikwete. Inaelezwa sasa baada ya kundi hilo kugawanyika, sasa hivi Membe ameungana na kundi jingine linalojumuisha viongozi wakubwa katika sehemu nyeti kama Bunge na pia wafanyabiashara ambao wara kadhaa wamekuwa akijiibua kama wasemaji wa watanzania.

Hata hivyo, kuna taarifa kuwa, waziri huyu amekuwa akijionesha kuwa ni shushushu wa Uasalama wa Taifa, mbinu anayoitumia kutanua mtandao wake ambao sasa unaonekana kuanza kupata ushindani hasa baada ya Mudhihir kuamua kwa makusudi kuulipua.

Wachunguzi wa mambo ya Kisiasa wamediriki kukubali kauli ya Mudhihiri kuwa Membe ni Nyoka aina ya MDIMU ambae sifa yake kubwa ni ubinafsi na roho mbaya,membe itakumbukwa kuwa alihusika kwa kiasi kikubwa kummaliza wenzie hata wakati wa awamu ya Tatu aliwamaliza kina Hans Kitine,malecela,kwa kutumia ushushu wake aliweza kumtokomeza swahiba wake wa Sasa Sita asipate nafasi baada ya kushindwa 95 huko
Urambo,alitumia uzandiki aloutaja Mudhihiri kufanikisha wenzie wanamtandao wasipate nafasi ktk awamu ya kwanza ya Mzee mkapa ambae alimstukia na Kumuondoa na kumpeleka nje ya Nchi.

 
Wachunguzi wa mambo ya Kisiasa wamediriki kukubali kauli ya Mudhihiri kuwa Membe ni Nyoka aina ya MDIMU ambae sifa yake kubwa ni ubinafsi na roho mbaya, membe itakumbukwa kuwa alihusika kwa kiasi kikubwa kummaliza wenzie hata wakati wa awamu ya Tatu aliwamaliza kina Hans Kitine,malecela,kwa kutumia ushushu wake aliweza kumtokomeza swahiba wake wa Sasa Sita asipate nafasi baada ya kushindwa 95 huko urambo,alitumia uzandiki aloutaja Mudhihiri kufanikisha wenzie wanamtandao wasipate nafasi ktk awamu ya kwanza ya Mzee mkapa ambae alimstukia na Kumuondoa na kumpeleka nje ya Nchi.

Hizo sifa za raisi mtarajiwa? yataka moyo.
 
Rwabugiri,
Kwanza tujiulize ni gazeti gani lililochapisha hii makala?
 
Hii habari wala haikukaa sawa zaidi ya kuzungumzia maudhi ya Mudhihir..Kinachonishinda kuelewa ni kwamba Membe pia ni Mbunge wa Mtema huko Lindi iweje awe mtu asiyependa maendeleo ya Lindi?..Hicho kiwanda cha saruji ambacho wanadai Membe anakiwekea ngumu, tuambiwe sababu basi! na kinajengwa na nani na kwa kibali gani hata Membe aweze kuzuia uwekezaji huo..

Ni vizuri tukipata story nzima ya hicho kiwanda ya yanayohusika maanake tunaweza kusema Zitto alikuwa na roho mbaya nyoka mbaya sana tena Koboko! kwa kuzuia mkataba wa Buzwagi.. Wapo kina Adam Malima waliounga mkono na kudai kama Karamagi anaweza kuwaletea wawekezaji kwao afanye kama alivyofanya atapokelewa..Lakini tulipokuja ufahamu ukweli kila mmoja wetu alikubaliana na Zitto..Leo hii huyo Karamagi yuko wapi!.. hivyo Mudhihir pia atuambie huu mkataba wa kiwanda cha sarujji unahusu shirika gani na kwa nini Membe kauzuia hali unajengwa ktk mkoa wake mwenyewe.. Huo Ubinafsi kwani Membe anajenga kiwanda hicho nyumbani kwake?.. Au ubinafsi una maana mbili tofauti!
Kwa hiyo msitegemee sisi wote hapa JF tunawez kuamini yote yanayozungumzwa kwa vishoka maanake habari nzima inajaa FITNA..

Huyo Membe anasifiwa kwa Ukatoliki wake kisha huyo huyo anaelezewa kukubali Tanzania kujiunga na OIC pamoja na Mahakama ya kadhi pia kupata mjisaada toka Arabuni.. Hizi ni chuki kubwa za watu binafsi ambao wanataka kutumia wao dioni kama kigezo cha kuifikisha hoja yao lakini wanadunda..Kwani toka lini bungeni mbunge hukatazwa kutoa maoni yake, akikubaliana na waislaam basi kisha kuwa puppet!..Hee kisha mnadai sisi wote ni Watanzania hali mkitumia maneno ya wakristu wana msimamo mkali kwani nani kasema hamna msimamo ikiwa mtakubaliana na Membe au wazo la OIC..hamuoni nje zaidi ya mipaka ya kanisa utafikiri Ma Ayatollah wa kiafrika.

Kwa mwenye uwezo mzuri wa kufikiri atajua fika mada hii haihusiani na swala la Membe kugombea Urais mwaka 2015 bali ni kuhakikisha fikra zake za kugombea zinapigwa vita..Hizi ni fikra tu kila mtu anaweza kufikiria kugombea na sii kazi ya gazeti wala Mudhihir kuchambua uwezo wa Membe..Yeye huyo Mudhihir tumesikia mangapi?.. hadi watu walisema ajali yake imetokana na kulaaniwa, na aliponea chupuchjupu.... iwe leo Membe kuwa Nyoka!..Basi nasi tutaamini kwamba Mudhihir kweli alilaaniwa kweli maanake kuna mengi alofanya wala hayafurahishi..Kaingia uwaziri wala hakukaa kaingia Ufisadi, Kikwete mshikaji ewenyewe kamtolea nje basi imekuwa Membe ndiye mfitini...Tunajua fika, where Mudhihir anajaribu kuficha ukweli.. gubu limemjaa kuona alipigwa chini bila kutegemea..
Jamani upuuzi huu utakwisha lini..Basi yaonyesha hata kuchaguliwa kwa Asha Rose Migoio UN ni mbinu za Membe ili apate kushika Uwaziri..

Watasema sana lakini sisi wengine tunajua kwamba Membe hakupelekwa nje kwa sabnabu yeye ndiye Mbinafsi..Hapana huyu alikuwa shushushu ambaye alionekana kuwa hatari kwa Mafisadi.. na Mkapa ahakumpenda wala wale shemeji zake waliokuwa Mabalozi Canada hawakumpenda.. Sisi tuliokuwepo hapa tunayajua haya na tumeyaona kwa macho yetu visa na vitimbi alivyokuwa akifanyiwa lakini pamoja na yote hayo Membe alikuwa karibu sana na Watanzania..Naweza kusema hakuna muda au wakati Ubalozi wa canada umekuwa karibu na wananchi wake kama wakati wa Membe, Aziz na mama Chipungahelo.. hawa ni watu ambao wakazi wa Canada kamwe hawatawasahau..Sasa fikirieni tu haya yamekuwa ugenini huyu mtu anaweza kufanya mangapi akiwa ndani Tanzania nchi yake mwenyewe..

Yes Membe anaweza kuwa na mapungufu yake kama kiongozi. Ni utawala wa kiafrika ambao hatutegemei pepo lakini siku kwa siku tunapokuwa nam mtu mwenye moyo na ukaribu na watu haasa ktk madaraka basi bila shaka sisi wananchi ndio waamuzi wa haki na sio hawa wabunge ambao ugonvi baina yao ktk meza kuu na hawajui kinachoendelea ktk maisha ya walalahoi..
I'm for Membe....
 
Last edited:
Here we go, wameshaanza kuchafuana ili mwenye ubavu aweze kulifikia sinia la Pilau 2015... Hakuna anayejadili ukosefu wa maji safi kwa wananchi wala huduma mbovu kwenye vituo vya afya, tunachosikia ni huyu kafanya hivi yule kafanya vile, alimradi siku zipite na wananchi tunabaki kushangilia...

Life Goes On
 
Mkandara,

..kuna Wanigeria wanataka kujenga kiwanda cha saruji Lindi.

..inaelekea malighafi ya kiwanda hicho inapatikana jimbo la Mudhihir--Mchinga.

..Membe anataka kumzidi mahesabu mwenzake kwa kulazimisha kiwanda kijengwe jimboni kwake -- Mtama.

..Mudhihir amekuja juu anadai malighafi haitotoka Mchinga kwenda Mtama, na hatishiki hata kama Membe "nyoka mdimu" akiwa Raisi 2015.

..Membe anautaka Uraisi lakini anakosea anapochanganya masuala ya udini-udini.

..kwanza anatoa matamko premature kwamba Tanzania iko tayari kujiunga na OIC.

..alipoona moto umemwakia akaenda kukutana na Kardinali Pengo, na baada ya hapo kubadili tamko lake la mwanzo kwa kudai kwamba mchakato bado unaendelea.
 
membe kama waziri wa mambo ya nje ndie hasa anaetakiwa kutoa msimamo wa serikali juu ya mambo ya OIC.
sasa kwa membe kufanya kazi yake ghafla kuambiwa anafanya masuala ya kidini dini kwa kweli inashangaza na haiingii akilini hata kidogo
hivi watanazania lini tutajifunza kuangalia mambo kwa mtazamo wa kisiasa na sio dini?
 
gaijin said:
membe kama waziri wa mambo ya nje ndie hasa anaetakiwa kutoa msimamo wa serikali juu ya mambo ya OIC.
sasa kwa membe kufanya kazi yake ghafla kuambiwa anafanya masuala ya kidini dini kwa kweli inashangaza na haiingii akilini hata kidogo
hivi watanazania lini tutajifunza kuangalia mambo kwa mtazamo wa kisiasa na sio dini?

gaijin,

..Membe alitakiwa kutoa msimamo ambao ni final.

..hakutakiwa kutoa matamko kabla ya serikali kufikia uamuzi ktk suala hili.

..sasa Waziri anatoa matamko kuhusu OIC, baadaye anakwenda kuonana na Kardinali, na kurudi na kauli tofauti, kwanini wananchi tusiliangalie suala hili la kisiasa ktk jicho la kidini?

NB:

..kwa mtizamo wangu suala hili ni kubwa kuliko waziri wa mambo ya nje. nadhani uamuzi wa serikali unapaswa kutolewa bungeni na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.
 
Membe kujitokeza kusema kuwa anataka urais hakuna noma, Mimi naona ni vizuri sana kwake kusema na kuweka wazi mipango yake na sisi kama Watanzania watamjua na kusema kuwa anafaa au hafai. Hivyo kuwa mkatoriki siyo sababu kwake na Kwa Watanzania.
 
‘Bila shaka, bila shaka. Mudhihir ninayemfahamu asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye, namheshimu sana," alinukuliwa Membe na gazeti moja la kila siku, akifafanua kuhusu dhana ya Mudhihir kutumiwa na watu kumlipua.
Aaah wapi Dilunga? waandishi wetu hao! direct quote ya Membe inasema jamaa hataki kulumbana na Mudhihir, kichwa cha habari "Membe akiri kuwania Urais 2015"

Ukiisoma kwa umakini mdogo tu hiyo habari hakuna mahala Membe "anakiri" kugombea urais ni maneno yaliyopandikizwa tu na mwandishi kui "sexy up" story.

Huu ni uharibifu mkubwa mwandishi kaunga unga story kwa super glue huku akijichanganya mara ukatoliki, mara OIC mradi kufikia malengo yake ya uharibifu.

Shame on you waandishi uchwara!
 
Membe, anajidanganya kutumia historia ya Jakaya kwenye maisha yake. Hapa duniani kila mtu ana historia yake peke yake. Mfano: Jinsi walivyoingia Ikulu watu kama Julius (RIP), Ali, Benjamin na Jakaya - ni tofauti kabisa.
 
Mwandishi anamaanisha ili mgombea urais afanikiwe lazima awe mkatoliki,je sisi wa KKKT na madhehebu mengine tutaishia katika Upinda tuu?Naomba atuweke wazi ili tusihangaike kuwatafutia nafasi akina Lyatonga,malachela na wengine!
 
Jamani,Membe na mudhihir wote wanajuana..hapa kuna issue moja tu...Kiwanda cement.Membe ana watu wake wanataka kujenga Mtwara mjini hicho kiwanda...Mudhihir nae ana watu wake (TioT)wanataka wajenge Mchinga,ila malighafi iko mchinga.....sasa hapo wanatakiwa kwenda na hoja zao kwenye kamati ya mkoa...sio bungeni.......ila mwaka ujao MM hana lake...ubunge anataka labda atokee hapo....kwenye kiwanda
 
Hao ndio aina ya watu wanaotaka kutuongoza katika nchi hii. Tutaendelea kusema pasipo vitendo hadi kiama. Jamaa kapania kuwa Rais kwa gharama yoyote ile. Lakini tukikataa asiwe Rais nani kwa mtazamo wako unadhani anafaa kuwa Rais wetu ajaye ndani ya CCM.
 
membe kama waziri wa mambo ya nje ndie hasa anaetakiwa kutoa msimamo wa serikali juu ya mambo ya OIC.
sasa kwa membe kufanya kazi yake ghafla kuambiwa anafanya masuala ya kidini dini kwa kweli inashangaza na haiingii akilini hata kidogo
hivi watanazania lini tutajifunza kuangalia mambo kwa mtazamo wa kisiasa na sio dini?

Watanzania hatutakiwi kuangalia mambo kwa mtazamo wowote katika hayo mawili uliyotaja hapo. Tunachotakiwa ni kuangalia mambo kwa mtazamo wa Kiutu na Kimaadili, kwa sababu katika haya, siasa na dini ni sehemu tu ndani yake.
 
Back
Top Bottom