Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kauli ya waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa, Bernard Membe, kuwataka vijana wapiganie haki kwa nguvu zote na kulitetea taifa kwa gharama yoyote.
Inaashiria wapo viongozi ndani ya serikali na chama tawala CCM waliochoshwa na kukerwa na hali ya mambo ilivyo sasa hapa nchini.
Membe aliyasema haya jana katika tamasha la Campus Night lililoandaliwa na kanisa la VCC Victory Christian Centre.
Kanisa linaloongozwa na Mchungaji Huruma Nkone. Membe alisema Tamasha linapaswa kutumiwa na vijana kuitetea nchi kwa gharama yoyote pasipo hofu ya kuogopa jambo lolote. Alisema pia, vijana wengi hawana ajira.
Kauli hiyo aliisindikiza na takwimu ambayo inaonyesha ni 10% ya vijana kati ya vijana laki moja ndio wamepata ajira.
Tamasha hilo lilikusanya idadi kubwa ya vijana wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali jijini Dar es salaam. Kwa kauli ya Membe nashawishika moja kwa moja kuwaunga mkono CHADEMA katika harakati zao za kupigania haki ya wanyonge.
Membe ameonyesha kupingana na misimamo ya viongozi wenzie kuwa harakati za CHADEMA hazina tija kwa taifa.
Inaashiria wapo viongozi ndani ya serikali na chama tawala CCM waliochoshwa na kukerwa na hali ya mambo ilivyo sasa hapa nchini.
Membe aliyasema haya jana katika tamasha la Campus Night lililoandaliwa na kanisa la VCC Victory Christian Centre.
Kanisa linaloongozwa na Mchungaji Huruma Nkone. Membe alisema Tamasha linapaswa kutumiwa na vijana kuitetea nchi kwa gharama yoyote pasipo hofu ya kuogopa jambo lolote. Alisema pia, vijana wengi hawana ajira.
Kauli hiyo aliisindikiza na takwimu ambayo inaonyesha ni 10% ya vijana kati ya vijana laki moja ndio wamepata ajira.
Tamasha hilo lilikusanya idadi kubwa ya vijana wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali jijini Dar es salaam. Kwa kauli ya Membe nashawishika moja kwa moja kuwaunga mkono CHADEMA katika harakati zao za kupigania haki ya wanyonge.
Membe ameonyesha kupingana na misimamo ya viongozi wenzie kuwa harakati za CHADEMA hazina tija kwa taifa.