Membe akanusha kuitabiria CHADEMA ushindi 2015!!

Kiganyi

JF-Expert Member
Apr 30, 2012
1,242
765
Bernard Membe
Nimefafanua kuhusu uvumi uliotolewa na vyombo vya habari kuhusu kukutana kwangu na vijana wa CHADEMA waliofika nyumbani kwangu jimboni

Bernard Membe

Nimewaeleza kuwa upinzani si uadui na wapinzani si maadui zetu.

Bernard Membe
Sijawahi kuitabiria CHADEMA ushindi kwa kuwa sina kipaji hicho ambacho kinapatikana kwa Synovate, Mtoto wa Sheikh Yahya na TD Joshua

Bernard Membe

Upinzani upo kwa mujibu wa kanuni, sheria na Katiba hivyo hauwezi kuwa uadui. Wapinzani wako ndani ya vyama vyetu wenyewe


Bernard Membe

Nina imani uvumi huu haujaenezwa na CHADEMA bali watu nje ya CHADEMA wenye malengo ya kisiasa haswa kunifitinisha na wana CCM na CHADEMA

Bernard Membe

Kamwe watanzania tusikubali kulishwa kasumba ya kuwa Upinzani wa kisiasa ni uadui. Tusigawanywe kwa itikadi wala dini


Bernard Membe
Nawapenda watanzania wote bila kujali itikadi zao, dini zao, makabila yao na marika yao. Umoja wetu ndio nguvu yetu.



MY TAKE; Nyoka ya MDIMU haiaminiki au Magazeti yalizusha hizo taarifa??


Magamba wengine igeni toka kwa Membe kuwa na political tolerance!
Bahati nzuri mimi nimeshiriki press Conference hii. Mhe. Membe alitumia fursa hiyo kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu Wizara ambayo yamekuwa yakiandikwa na kutangazwa na vyombo vya habari isivyo.

Masuala hayo ni pamoja na taarifa kuhusu uwasilishwaji wa Ripoti ya Tanzania kuhusu Mpango wa Nchi za Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM).

Katika suala hili Mhe. Membe alitoa ufafanuzi kuwa, ni kweli Mhe. Rais hatoweza kuwasilisha ripoti ya tathmini ya Tanzania katika Mkutano ujao wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) unaotarajiwa kufanyika mjini Addis Ababa mwezi Julai, 2012 kwa kuwa Timu ya Umoja wa Afrika chini ya APRM inayopitia ripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi hiyo. Hivyo Tanzania itawasilisha ripoti yake Januari 2013baada ya timu hiyo kuipitia na si kwa sababu Tanzania inadaiwa Dola za Marekani laki nane (800,000) kama mchango wake kwa mpango huo.

"APRM ni chombo kilichoanzishwa na Serikali za Afrika na kwa hapa Tanzania kinaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje, ni chombo cha hiari kwa nchi za Afrika kujitathmini zenyewe kiutawala bora, si kweli kuwa Rais atashindwa kuwasilisha Ripoti ya Tanzania AU kwa sababu hatujalipa deni, bali ni kwa sababu timu inayopitia ripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi yake hivyo tunatarajia kuwasilisha ripoti yetu mwezi Januari 2013 wakati wa kikao kingine cha Wakuu wa nchi wa AU," alisema Mhe. Membe.

Kuhusu suala la fedha zilizotoweka Wizarani, Mhe. Membe alieleza kuwa hakuna fedha zilizopotea isipokuwa Wizara imewasimamisha kazi Watumishi watano waliofanya mchakato wa kuhamisha kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya ziara za Mhe. Rais za Addis Ababa, Geneva,…na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuli yaani Katibu Mkuu ambaye hakuwepo wakati mchakato huo unafanyika.

Aliongeza kuwa, Watumishi hao wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguziunaofanywa na kamati iliyoundwa ili kujiridhisha kama taratibu za kifedha zilifuatwa au kukiukwa katika mchakato huo mzima.

"Tarehe 1 Machi, 2012 wakati mimi sipo Wizarani wala Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Mhasibu Mkuu kuna mchakato wa kuhamisha fedha kiasi cha shilingi bilioni 3.5 ulifanywa kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya safari za Mhe. Rais za Geneva, Addis Ababa,…..na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuli. Timu inayojumuisha watu kutoka TAKUKURU, Usalama wa Taifa, Wizara na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali imeundwa ili kuchunguza suala hilo ili kujua kama taratibu za kifedha zilifuatwa au kukiukwa na uchunguzi ukikamilika tutaweka hadharani hakuna cha kuficha," alisema Mhe. Membe.

Vile vile, Mhe. Membe alipinga uvumi unaoenezwa kuwa amekitabiria ushindi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa kusema kuwa yeye si mtabiri na kwamba yeye ni mwanachama halisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa maneno na kwa matendo.

Mhe. Membe aliongeza kuwa alichokifanya ni ukarimu kwa kuwakaribisha Vijana wa CHADEMA jimboni kwake Mtama mkoani Lindi na kushiriki nao chakula nyumbani kwake.

"Ukarimu hauna udini, rangi wala itikadi, vijana wa CHADEMA walikuja nikawakaribisha kwa chakula nyumbani, na leo nataka niwape somo kidogo, upinzani sio uadui, nchi inayoona upinzani ni uadui haiko salama wala haitaendelea,"alisisitiza Mhe. Membe.
 
watakuja hapa kuweka video yake halafu atakataa kuwa nayo siyo yeye imefanyiwa photoshop tu
 
watakuja hapa kuweka video yake halafu atakaa kuwa nayo siyo yeye imefanyiwa photoshop tu

Asante Membe mtu yeyote anaweza kutabiri maana utabiri na matokeo siyo lazima vilingane ila sasa utabiri wako umeutimiza kwa kusema aliyeeneza uvumi hatoki ndani ya chadema-asante baba
 
Kumbe Membe anatweet! Safi sana.

Ila msimamo na mtazamo wake huu nimeukubali. Wana ccm wangekuwa na mawazo ya aina hii nchi yetu ingekuwa mbali sana. Kwa mtaji huu zile nyimbo za Komba " wapinzani tuwachane chane tuwatupe" zimepitwa na wakati. Kwa mtazamo wangu CHADEMA wanafanya kazi nzuri ya siasa sidhani kama wanasubiria Membe awatabirie ndio waone.

Utimilifu wa kazi yao unaonekana dhahiri kwenye mapokeo ya watu. Nadhani Membe yuko sahihi, sdhani kama CHADEMA ndio wenye kueneza uvumi huu, watakuwa ni wanasiasa ndani ya CCM wenye siasa za maji taka.
 
Mh Membe anaonyesha ni mkomavu ktk siasa, anajiamini, anasimama ktk kweli na kweli inamweka huru, bila kujua dini yake ana hofu ya Mungu anajua mbele ya safari kuna kuulizwa juu ya matendo ya hapa duniani.
 
Hivi anachokanusha hapa Membe ni kitu gani. Vyombo vya Habari vinavyoaminika viliandika na kutangaza maneno ya Membe. Wazi kabisa. Hawakuongeza wala kupunguza. Wangefanya hivyo wangekuwa wanakiuka misingi muhimu ya tasnia muhimu ya uandishi wa habari. Angekuwa na haki ya kuwashtaki (ofcourse MCT).

Kwa mtu yeyote makini hapa kaongeza tu stori nyingine, AMEPINGANA NA PROPAGANDA ZA HOVYO, CHEAP ZA CHAMA CHAKE CCM na wana CCM wenzake. Stori juu ya stori. Asante Membe. Tusubiri kesho watakuandikaje au leo jioni kwenye Tvs zetu.

Ofcoz with the coming back of Andrew Chenge on board and the like wakiendelea kujipatia nguvu katika Kamati za Bunge na sasa wakielekea kuliteka bunge, baada ya kuwa wameishaiteka ikulu, wakaiteka CCM na wameiweka mfukoni serikali ya CCM, watu kama Membe hawana namna sasa hivi isipokuwa kujionesha kuwa wako upande wa wanamabadiliko!

Mtu kama Membe na wenzake ni wa kuazimwa milango yote ya fahamu, kwa tahadhari kubwa hata wanachosema (kwa kuchelewa sana) ni ukweli.

 
Mhe. Membe ni mtu muelewa na mwenye msimamo makini..,anajitambua lakini pia anawatambua wanasiasa wenzake ndani ya Nchi hii. Yuko sahihi akisema kuwa upinzani si uadui. Haina maana kwa watanzania kuwagawa kwa misingi yeyote hata ikiwa ina manufaa ya kisiasa ndani yake.,kwani ubaguzi wa aina yeyote hauna mwisho mwema.
 
Maneno ya membe yana uoga ndani yake. Awe ametabiri au la,kulikuwa na ulazima gani wa kujibu,Kama anajua vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa sheria,nini ubaya wa kukitabiria ushindi chama mojawapo. Na kwanini ameamua kukanusha leo,pengine hilo nalo angetuambia,kwamba alikuwa anatafakari nini hadi leo.

Na kwanini aseme yeye si mpiga ramli wakati tayari amekwisha tuambia kuwa aliyesema maneno hayo si CCM wala CHADEMA,ni nani basi kama si ramli.

Kaka yangu Membe, elewa kuwa wananchi ndio walinzi wa kweli wa mpenda haki,mwalimu Nyerere alikuwa akikisema sana chama cha mapinduzi, lakini haikuwahi kuonekana kama ana hatari ya kufanyiwa jambo baya na chama chake kwani siku zote alilindwa na wananchi. Wewe unaogopa chama kusimamia ukweli.

Mbona hujatuambia jitihada zako za ku-establish mahakama ya kadhi ziliishia wapi,hizo ndo baadhi ya ajenda muhimu za kutuelezea wa-tz na sio whether uliitabiria CDM ushindi au la!
 
Kwa mtu mwenye akili hata hizi kauli ukizichunguza bado unaona zina mwelekeo chanya kuelekea CHADEMA...ameng'ata na kupuliza hapa hamna kupinga wala kuunga mkono
CHEZEA POLITICIANS WEWE........
 
Bahati nzuri mimi nimeshiriki press Conference hii. Mhe. Membe alitumia fursa hiyo kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu Wizara ambayo yamekuwa yakiandikwa na kutangazwa na vyombo vya habari isivyo.

Masuala hayo ni pamoja na taarifa kuhusu uwasilishwaji wa Ripoti ya Tanzania kuhusu Mpango wa Nchi za Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM).

Katika suala hili Mhe. Membe alitoa ufafanuzi kuwa, ni kweli Mhe. Rais hatoweza kuwasilisha ripoti ya tathmini ya Tanzania katika Mkutano ujao wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) unaotarajiwa kufanyika mjini Addis Ababa mwezi Julai, 2012 kwa kuwa Timu ya Umoja wa Afrika chini ya APRM inayopitia ripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi hiyo. Hivyo Tanzania itawasilisha ripoti yake Januari 2013baada ya timu hiyo kuipitia na si kwa sababu Tanzania inadaiwa Dola za Marekani laki nane (800,000) kama mchango wake kwa mpango huo.

"APRM ni chombo kilichoanzishwa na Serikali za Afrika na kwa hapa Tanzania kinaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje, ni chombo cha hiari kwa nchi za Afrika kujitathmini zenyewe kiutawala bora, si kweli kuwa Rais atashindwa kuwasilisha Ripoti ya Tanzania AU kwa sababu hatujalipa deni, bali ni kwa sababu timu inayopitia ripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi yake hivyo tunatarajia kuwasilisha ripoti yetu mwezi Januari 2013 wakati wa kikao kingine cha Wakuu wa nchi wa AU," alisema Mhe. Membe.

Kuhusu suala la fedha zilizotoweka Wizarani, Mhe. Membe alieleza kuwa hakuna fedha zilizopotea isipokuwa Wizara imewasimamisha kazi Watumishi watano waliofanya mchakato wa kuhamisha kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya ziara za Mhe. Rais za Addis Ababa, Geneva,…na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuli yaani Katibu Mkuu ambaye hakuwepo wakati mchakato huo unafanyika.

Aliongeza kuwa, Watumishi hao wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguziunaofanywa na kamati iliyoundwa ili kujiridhisha kama taratibu za kifedha zilifuatwa au kukiukwa katika mchakato huo mzima.

"Tarehe 1 Machi, 2012 wakati mimi sipo Wizarani wala Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Mhasibu Mkuu kuna mchakato wa kuhamisha fedha kiasi cha shilingi bilioni 3.5 ulifanywa kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya safari za Mhe. Rais za Geneva, Addis Ababa,…..na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuli. Timu inayojumuisha watu kutoka TAKUKURU, Usalama wa Taifa, Wizara na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali imeundwa ili kuchunguza suala hilo ili kujua kama taratibu za kifedha zilifuatwa au kukiukwa na uchunguzi ukikamilika tutaweka hadharani hakuna cha kuficha," alisema Mhe. Membe.

Vile vile, Mhe. Membe alipinga uvumi unaoenezwa kuwa amekitabiria ushindi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa kusema kuwa yeye si mtabiri na kwamba yeye ni mwanachama halisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa maneno na kwa matendo.

Mhe. Membe aliongeza kuwa alichokifanya ni ukarimu kwa kuwakaribisha Vijana wa CHADEMA jimboni kwake Mtama mkoani Lindi na kushiriki nao chakula nyumbani kwake.

"Ukarimu hauna udini, rangi wala itikadi, vijana wa CHADEMA walikuja nikawakaribisha kwa chakula nyumbani, na leo nataka niwape somo kidogo, upinzani sio uadui, nchi inayoona upinzani ni uadui haiko salama wala haitaendelea,"alisisitiza Mhe. Membe.
 
Waziri wa mambo ya nje benard membe akana kusema kwamba alikitabiria chama cha chadema pamoja ni vyama vingine kushinda katika chaguzi za mwaka 2015

chanzo :star tv
 
He still adds no value. Ameendelea ku-cement tu yaliyoandikwa. Ok bado APRM hapa tunaipitia, je vipi kuhusu kuwa tunadaiwa Dola Laki 8...?
 
Akane asikane huo ndio ukweli. Hata hivyo kachelewa sana kukanusha! Ni sawa na mtu kuzuia message aliyomaliza kuituma kwenye simu yake, haiwezekani. Message was delivered!!!
 
AMESEMA MTU ATAKAELETA USHAHIDI WA UTABIRI HUO BASI YEYE ATAKUWA TAYARI KUWAJIBIKA. mwenye ushahidi wa kauli kuwa CHADEMA itachukua nchi 2015 aweke tuone uwajibikaji wa mkuu Membe.
 
Back
Top Bottom