Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Nimesikiliza Channel Ten wamewahoji maafisa walioenda kusaidia uokoaji katika meli ya Mv Skagit wanasema walikuwa wanavizia wajeruhi na maiti waliokuwa wanaelea majini. HAKUNA MZAMIAJI hata mmoja aliyezama chini iliko meli kuangalia kama kuna wananchi wenzetu waliojifungia kwenye vyumba vya meli kujiokoa. Na hata leo hakuna mpango wa kuzamia na kwenda kwenye vyumba. Wakati Mv Spice imezama tuliambiwa pale Nungwi mkondo ni mkali hawawezi kuzamia, sasa nashangaa hata hapa pa jana ambapo maCaptain wanakadiria kina cha mita 30 watu hawazamii kuwatoa majeruhi. Huenda hii ni janja ya serikali kupunguza idadi ya vifo kwa kupata maiti wachache maana hata ukisoma vyombo vya habari kuhusu Mv Spice official death ni 20 huenda wanataka na hii Skagit official death ibakie 31.
Ushauri: watumiaji vyombo vya majini kama chombo kinazama usithubutu kujifungia kwenye vyumba kusubiri kuokolewa kwani uokoaji Tanzania ni janga la kidunia. Ukijifungia kwenye vyumba ndio kaburi lako huko. Nchi haina wazamiaji maskini. Poleni ndugu zetu mliopata maafa.
Ushauri: watumiaji vyombo vya majini kama chombo kinazama usithubutu kujifungia kwenye vyumba kusubiri kuokolewa kwani uokoaji Tanzania ni janga la kidunia. Ukijifungia kwenye vyumba ndio kaburi lako huko. Nchi haina wazamiaji maskini. Poleni ndugu zetu mliopata maafa.